Jaji Mkuu (Chande) amedanganya umri?

Jaji Mkuu (Chande) amedanganya umri?

Nimeona alikuwa darasa moja na PM Mizengo Kayanza Pinda. Hivi PM wetu ana umri gani? We can start from there kufanya estimation ya umri HALISI wa CJ Omari Chande.

Haya mambo ya kugushi UMRI na ELIMU imeyalea CCM na inaonekana haijali kabisa unless someone has steped on their toes ndiyo utasikia sio RAIA (Ulimwengu, Bashe case). ame-forge Umri (Masauni, Nape case).

Mimi najua Omary Chande na Mdogo wake Othman Chande (boss wa TISS) wanasoma sana JF. Kwanini basi Chande asijitokeze hadharani hata kama sio JF aka clear the air kuhusu UMRI wake halisi? Hang on a little bit, nimesahau kwamba hii ni Tanzania chini ya CCM, ni Upepo tu utapita! You can forge everything with impunity.

Hebu angalia nchi za wenzetu makini, kama the MOST POWERFUL MAN ON EARTH, Barak Obama President of the USA alituhumiwa na mwananchi wa kawaida tu kwamba sio RAIA wa Marekani, lakini IKULU ya Marekani ikachukua liberty ya ku prove kwamba ni raia kwa kuonesha LIVE kwenye TV vyeti vya kuzaliwa vya Obama vinavyoonesha alizaliwa USA na ni Raia halali wa Marekani. Iweje Omary Chande au mahakama yenyewe ishindwe kufanya hivyo?!

Kama Chande ataendelea kuzika kichwa chake mchangani (style ya mbuni) ili hali kiwiliwili chake chote kikiwa nje, basi sisi wananchi tutaamini kwamba kweli amegushi UMRI wa kuzalia kwa KUOGOPA kustaafu mapema na hii itakuwa kashifa nyingine kwa mhimili huu wa kutoa HAKI.
umeongea vizuri mkuu lakini tatizo hapa sio ccm bali ni Watanzania (yaani sisi). Hivi fikiria kidogo: Ukija kupanda ndege alafu ukapata ushuhuda wa wazi kuwa rubani hana uwezo wa kutosha unafanyaje? ...au chukulia unaenda kituo cha basi alafu unaona dereva amelewa chakali si unachagua gari nyingine na hata kama umeshalipa si angalau unaonyesha ujasiri wa kudai kurudishiwa nauli yako!?
Sasa sisi tumeshawajua hawa watu na hatufanyi maamuzi yoyote.
Nakumbuka issue ya akliyekuwa mbunge wa Temeke (Kihiyo) ilianza kama masihara lakini ikaishia kujulikana kuwa hakuwahi kusoma DIT/Dar Tech

 
Kuna kila dalili za ukweli kuhusu hili.
Kuna jamaa wa TISS kanitonya hiyo issue ipo na Usalama wa taifa walikuwa wanatafuta namna ya kuificha sana tangu Lissu alipoanza kufumua uozo wa baadhi ya majaji.
iyo ishu mbona wakina Lisu walishaiendea chimbo kitambo sana kabla hata hajawalipua wengine bungeni lakini wakaamua kuipotezea .......inasemekana umri huo ni mdogo ukilinganisha na umri wa mdogo wake
 
Alikuwa Tambaza High ,mwaka mmoja mbele yangu. Tulikuwa tunakaa wote Tambaza Hostel,na katika zile cubicle za watu wawili,mimi nilikuwa nakaa na huyu Jaji,hajadanganya umri,amedanganya jina. But he is a good mankwa maoni ya wengi. Yeye ni Mohamed Chande.
 
kuna jitu linaleta ubishi wa kijinga eti halinatabia ya kudandia uzi wa watu na uzi huu siyo wake..kama hunapoint za kumtetea huyo mme wako baki msomaji maana unaandika maelezo mengi halafu ni kinyesi kitupu na jina lako kinyesi kitupu..

Hahaha.kakukera.ehhh..nimeona.na.mimi
 
suala siyo majina, mbona hata mtoa mada kasema mwaka aliomaliza? Yeye yawezekana alitafuta data za umri aloingia nao chuoni maana ndo kiini cha mada yake. Anahitaji umri halisi wa cj.

Kama mtu anadiriki kudanganya wazi kuwa habari za darasa zima Kitivo cha Sheria mwaka 1974 hazipatikani wakati zinapatikana mpaka online, utamwamini huko anakodai kuwa jaji mkuu kadanganya umri?

Kama anadai kuwa h
abari za darasa zima Kitivo cha Sheria mwaka 1974 hazipatikani, hizi habari kuwa J. Msofe, Jaji Masati, jaji B. Luanda, R. Sheikh, na V.K. Lyimu walisoma darasa moja na jaji mkuu amezipata wapi?

Hata kama amezipata kwenye source nyingine sidhani kama
J. Msofe, Jaji Masati, jaji B. Luanda na V.K. Lyimu wamesoma darasa moja na jaji mkuu.

Tatizo la wabongo mkiambiwa kitu mnaitikia ndiyo tuu. Ham-reason kabisa.

 
  • Thanks
Reactions: Ame
Alikuwa Tambaza High ,mwaka mmoja mbele yangu. Tulikuwa tunakaa wote Tambaza Hostel,na katika zile cubicle za watu wawili,mimi nilikuwa nakaa na huyu Jaji,hajadanganya umri,amedanganya jina. But he is a good mankwa maoni ya wengi. Yeye ni Mohamed Chande.

Mkuu Ganesh

Jaji Mkuu anaitwa Mohamed Othaman Chande.

Amedanganya jina vipi?

Hebu tufafanulie kidogo
 
Kama mtu anadiriki kudanganya wazi kuwa habari za darasa zima Kitivo cha Sheria mwaka 1974 hazipatikani wakati zinapatikana mpaka online, utamwamini huko anakodai kuwa jaji mkuu kadanganya umri?

Kama anadai kuwa h
abari za darasa zima Kitivo cha Sheria mwaka 1974 hazipatikani, hizi habari kuwa J. Msofe, Jaji Masati, jaji B. Luanda, R. Sheikh, na V.K. Lyimu walisoma darasa moja na jaji mkuu amezipata wapi?

Hata kama amezipata kwenye source nyingine sidhani kama
J. Msofe, Jaji Masati, jaji B. Luanda na V.K. Lyimu wamesoma darasa moja na jaji mkuu.

Tatizo la wabongo mkiambiwa kitu mnaitikia ndiyo tuu. Ham-reason kabisa.


Mtu anakwambia labda iwe alianza darasa la kwanza akiwa na miaka minne as if its the only option iliyopo, wakati enzi za zamani watu walikuwa wanarukishwa madarasa kama mchezo!
 
Alikuwa Tambaza High ,mwaka mmoja mbele yangu. Tulikuwa tunakaa wote Tambaza Hostel,na katika zile cubicle za watu wawili,mimi nilikuwa nakaa na huyu Jaji,hajadanganya umri,amedanganya jina. But he is a good mankwa maoni ya wengi. Yeye ni Mohamed Chande.

mkuu, unataka kuniambia Chande Othamn si jina lake halisi?!
 
Kamanda Lissu atumwagie ukweli wote maana anawajua majaji wote in and out!
 
Mtu anakwambia labda iwe alianza darasa la kwanza akiwa na miaka minne as if its the only option iliyopo, wakati enzi za zamani watu walikuwa wanarukishwa madarasa kama mchezo!

Si umeiona diversion hiyo? Sasa siyo tena kadanganya umri, bali ni jina.

Hakyanani kuna mtu hapa ata-doubt his sexuality. Subiri.
 
Nina wasi wasi kama ww ni gthinker au kama unajua maana ya mitandao ya kijamii otherwise ungeenda kusoma magazeti tu, acha uvivu wa kufikiri, hv mm nikiweka cheti cha kuzaliwa cha jaji mkuu hapa utakataa kwa kuwa mm sie nilieanzisha topic? Think, reason, conclude.
Kama unafikia kujisifia(qualify) wewe mwenyewe kuwa ndiyo greater thinker sina sababu ya kubishana na wewe, lakini kumbuka self qualification is no qualification. Ungeacha jamii, kutokana na mchango wako wasema wewe ni nani.
 
Suala la mtoto mdogo wa miaka 4 kuanza darasa la kwanza kidogo linawezekana miaka hii,ila kwa miaka ya nyuma hilo jambo lilikuwa gumu kweli kweli.
Hivi,uadilifu wetu kama taifa u wapi?
Kama mtendaji mkuu wa idara ya kutoa haki kisheria anadanganya umri,our destiny is at stake.

Mkuu Eliah G Kamwela, unaweza kunitajia mtu maarufu kwa Tanzania ambae hajawahi kudanganya.
 
Alikuwa Tambaza High ,mwaka mmoja mbele yangu. Tulikuwa tunakaa wote Tambaza Hostel,na katika zile cubicle za watu wawili,mimi nilikuwa nakaa na huyu Jaji,hajadanganya umri,amedanganya jina. But he is a good mankwa maoni ya wengi. Yeye ni Mohamed Chande.


Mzee Nyerere, asante kwa kutuweka sawa.
 
Au kwa sababu hiyo ndiyo maana kaamua kujitoa kwenye kesi ya Lema asije akachimbuliwa zaidi?just thinking aloud
 
Mtu anakwambia labda iwe alianza darasa la kwanza akiwa na miaka minne as if its the only option iliyopo, wakati enzi za zamani watu walikuwa wanarukishwa madarasa kama mchezo!

Kama unamtetea Jaji mkuu kudanganya umri ni haki yako lakini si kwa staili hii ndugu yangu.
Kama aliruka madarasa basi isemwe hapa kwamba aliruka kutoka darasa la kwanza hadi la tano, na ilikuwa lini, i mean mwaka gani, sio maneno matupu kama haya unayoandika hapa, muhimu ni kuweka ushahidi tu wa hilo.

Mwalimu Nyerere alipata bahati hiyo ya kuruka madarasa na wengine wapo waliopta bahati hiyo. Kinachotafutwa hapa ni ukweli wa umri wake na si kutafuta njia nyingine yeyote nyepesi nyepesi na za uongo uongo ya kujustfy utetezi wako juu ya tuhuma hizi za kughushi umri.
 
Namba 47 kumbe Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda ni classmate wa Jaji Mkuu, Othman Chande.

Hivi Mizengo Pinda si ameshastaafu kazi serikalini(TISS) ndipo akaenda kuwania ubunge? ama aliingia katika siasa kabla ya kuretire?
 
Back
Top Bottom