ITV, Mengi to be dealt with soon

ITV, Mengi to be dealt with soon

Mwenye taarifa aniambie kama huyu Nkoma alishakubalika kwamba ni M-Tanzania.

Prof. Nkoma haionyeshwi alizaliwa wapi lakini tangu alipoletwa nchini kutoka huko Botswana, ilieleweka yeye ni raia wa Malawi. Kusoma hapa na kuajiliwa hapa ilikuwa ni makosa ya ujamaa wa enzi hizo. Ano ndugu pia walioko nchini bila uraia wetu na wanaishi maeneo ya Kunduchi.

Pamoja na suala hilo kuzimwa na ikulu, je alishakuwa M-Tz? Isije ikawa tunasumbuliwa na raia wa nchi jirani.

Wakuu,
Kama kuna MewanaJF mwenye details zaidi kuhusu huyu jamaa Nkoma na atupe data hapa ili tuzifanyie kazi mapema please,
Nawakilisha
 
Watanzania vita hii si ya Mengi pekee yake, hii ni vita ya watanzania didi ya mafia waliojificha kwenye nembo ya mtandao.Mhusika mkuu ni Mh.Kikwete hana jinsi anavyo weza kukwepa lawama hizi za kuiuza nchi.

Hawa wahindi miaka yote hawakujiingiza kwenye siasa maana ikulu ya wakati huo haikuwa pango la wanyanga'anyi,tangu wanyang'anyi waingie ikulu imekuwa kimbilio lao.Wahindi hawa si wa kuaminika mnamkumbuka bwana Amir Jamal mhindi aliyekabidhiwa hazina mnakumbuka alipo kufa alizikwa wapi? familia yake hadi sasa iko Canada je hakuwa na raia mbili au tatu,mhindi gani aliye na uchungu na nchi hii ya Tanzania nilibahatika wakati fulani kutembelea Machester Uingereza wahindi wote walio hamisha wazungu kwa kununua nyumba zao ni kutoka Tanzania maana wale wa Uganda Amin ali wa "time".Wakikujua wewe ni mtanzania wanakwambia wanatoka Uganda ukienda kesho yake ukajitambulisha wewe ni mganda mhindi huyohuyo wa jana anakwambia ni mtanzania,sasa leo hii tumekufa maana wameingia Ikulu wanatawala nchi kwa sababu ya kuwa na viongozi wadhaifu na waroho wa mali.

Hawa wahindi hawawezi kutoa shs milioni 400. eti kusaidia vijana wa CCM bure mbona hawawapi mdawati watoto wanaosoma wakiwa wamekaa chini?.

Watu tulio wapa dhamana ya kulinda katiba wameshindwa leo hii inadhihilisha wazi ni jinsi gani hatuna uongozi dhabiti hivyo nidhahili vita hivi si vya Mengi ni vyetu na imefika mahala sasa pa kukomboa nchi kwani Tanzania haijawa huru ilikombolewa toka kwa wazungu na kuingizwa kwa mamuluki weusi ndo maana Tangu enzi na enzi hakuna mtanzania amewahi kuchagua Rais au kiongozi wa nchi mara zote kikundi kidogo cha watu kimekuwa kikiwaletea watanzania mtu wao na sisi tunampigia kura ya maoni "referendum" Je nani alimpendekeza Kikwete,Mkapa,au Mwinyi?
Si haohao tulio waamini kumbe ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo?

Leo hii wanamiliki kila mradi kuanzia madini mpaka stendi za mabasi.

Ni wakati wetu wa kufunguka macho maana mkuu wa nchi amekuwa Vasco Da Gama wa karne ya leo, hana uchungu na nchi alipewa naye atawapa wengine lakini hatima ya yote wananchi ndo mnaopata cha moto.

Tufunguke sasa tuchuje makapi.

toka nimejiunga hapa JF nimepata ufahamu ambao sikuwahi kuhupata sehemu yoyote hile.Napata uchungu sana na nchi yangu Tanzania hasa ninapo ona viongozi wetu tulio wachangua kwa kuamini wata badilisha maisha yetu na kutuletea maendeleo kiujumla,kinyume chake wao ndio wamekuwa vinara wa kutuangamiza kwa masilahi yao binafsi.

Ndugu zangu wanaJF hii vita ni ngumu sana,tusi subiri mtu au kiongozi aje atusaidie kwenye vita hii bali mimi na wewe! tuna paswa kupambana na huu uaramia unaofanya na watu wa chache kwa manufaa yao na familia zao.
 
Mkuu Mtumishi,

Nimeziona hoja zako lakini labda nikueleze kuwa hoja hizi zinatiririka kwa kadri matukio yanavyobadilika au hoja za nyongeza zinapojitokeza.
Kwa mfano hoja yangu ya kwanza niliitoa wakati thread hii haikuwa na mwelekeo wowote au kitu thabiti cha kutufanya tujiingize katika details. Baada ya kuunganishwa kwa hizo barua hapo juu sitegemei hali ya uchangiaji itabaki kuwa ni ileile la hasha, kuanzia hapo tunajadili yale mapya yaliyojitokeza ambayo hayakuwepo hapo mwanzo. Bahati nzuri maelezo ya kwenye barua yanajieleza kuwa yanayotokea yanaweza kutokea kwenye taasisi yeyote ile. Kutakiwa Mengi?ITV kutoa maelezo ya uvunjaji wa taratibu au sheria si kitu kigeni.
Kwa faida yako na wachangiaji wengine kuwa, hata Mengi alipokuwa mwenyekiti wa baraza la mazingira la taifa (NEMC) aliwahi kuongoza harakati kadhaa ambazo tulionyeshwa kupitia ITV akiamuru viwanda kadhaa kufungwa kwa kukiuka taratibu na sheria zinazohusu utunzaji wa mazingira. Kwa hiyo hili si jambo geni ni la kawaida huzikuta taasisi au kampuni yeyote ile. Kuna watu ambao walikuwa wanalalamika kuwa Mengi anakwenda kufanya kazi kiutendaji ambazo zilitakiwa kufanywa na Mkurugenzi wa NEMC lakini wengine waliona sawa tu ili mradi ametekeleza kazi za NEMC.
Mwisho, sh*t si tusi.

i399_180pxUturn.svg.png
 
A wrong move at the wrong time....trust me, it could be a blessing in disguise for RM. Serikalini kuna baadhi ya watu wameamua kupumzika kufikiri. Hawasomi public mood
 
Hivi hao jamaa walipotuma hizo barua walikuwa wanajua kuna kesi mahakamani? au wanafikiri wao wanaishi kwenye parallel universe; au dhana ya subjudice hawaifahamu? Maana, kulikuwa pia na kikao cha kamati ndogo ya ulinzi na usalama ambayo nayo ilitaka maelezo na ushahidi kutoka kwa Mengi kwa sababu za kiusalama wa taifa! siku mbili baada ya hii barua kutolewa..
 
Maana, kulikuwa pia na kikao cha kamati ndogo ya ulinzi na usalama ambayo nayo ilitaka maelezo na ushahidi kutoka kwa Mengi kwa sababu za kiusalama wa taifa! siku mbili baada ya hii barua kutolewa..
Na Mengi alienda? Ningekuwa mshauri wake ningemzuia...!
 
Mkuu, wacha ubaguzi 🙁

Theoretically, Yes!
In Practice, kila nchi ina ubaguzi ktk mambo ya aina fulani. Wa-Asia kaka hata siku moja hawatakupa nafasi kama hiyo.

Uliza Uambiwe jinsi Wasidi wanavyoishi India.
 
Pundamilia,
Naona wikiendi uliianza toka jana, ....

Niko gado na ninakataa isuue.

Hupendelea kungalia maswala in 3D.

Hili jamvi halinogi bila ya changamoto.

Unakumbuka enzi za midahalo shuleni?

Endelea kufurahia mapumziko yako ya mwisho wa juma.
 
Punda, achana na mawazo ya "Kipundapunda" na badala yake jadili issue. Sasa kama yamekushinda kabisa kwanini usim PM robot Invisible ili aweze kukujulisha kuwa amezipataje kama una mind kwa sana? Huwezi kuwa hapa JF unajadili hoja halafu unalaumu kuwa nini kimewekwa hapa na moderators,kama kuna shida nadhani unaweza kwenda kule kwenye malalamiko ili ufikishe yale yanayokusibu.

Wanasema if its too hot why stay in a kitchen mkuu,joto likizidi unajiondoa jikoni,kuna forums nyingi tu kama michezo,hoja mchanganyiko na hata muziki wa gospel na kizazi kipya mkuu.

Kwa kifupi ni kwamba huna haki ya kuuliza kwanini habari flani ama document flani imewekwa hapa,hiyo ni kazi ya moderators,wewe ni kujadili ama kuwa msomaji,unless ni posting unayohisi ni disrespectful ama unlawful,ni options mbili ambazo zinakupa uhuru wa kutosha kabisa wewe kama mwanadamu,na si kama "Punda"

Na wewe mkuu achana na Punda jadili hoja za Punda.

Huna haki ya kuhoji kwanini Punda anahoji.

Mimi na wewe tuko huru kujieleza, kama hukubaliani na hoja zangu hujalazimishwa kuzijibu.

Ni nini motive ya Mengi kuanika barua hadharani?
 
Mkuu yamekuwa hayo tena,umepiga bonge la U-Turn,polepole tutafika tu na ukweli siku zote utasimama

Hoja hujibiwa na hoja.

Maelezo yangu yapo sawa kabisa, kama kuna mahali hujaelewa, tafadhali nijulishe.
 
Wakuu naomba niulize, TCRA (serikali) wamemlima Mengi barua kwa sababu na makosa waliyoyaona wao, sasa je kwa kitendo ambacho Habari corporation ilikifanya cha kuchapisha matoleo mawili ya RAI kwa tarehe moja na namba zilezile, hivi serikali imechukua hatua gani kwa Kampuni hiyo na mmiliki wake? Au ndo mambo ya kulindana na kumuonea mnyonge???
 
Wakuu naomba niulize, TCRA (serikali) wamemlima Mengi barua kwa sababu na makosa waliyoyaona wao, sasa je kwa kitendo ambacho Habari corporation ilikifanya cha kuchapisha matoleo mawili ya RAI kwa tarehe moja na namba zilezile, hivi serikali imechukua hatua gani kwa Kampuni hiyo na mmiliki wake? Au ndo mambo ya kulindana na kumuonea mnyonge???


Mkuu je wadaganyika wametoa malalamioko yao kuhusu suhala hili kwenye vyombo husuka??
 
Na wewe mkuu achana na Punda jadili hoja za Punda.

Huna haki ya kuhoji kwanini Punda anahoji.

Mimi na wewe tuko huru kujieleza, kama hukubaliani na hoja zangu hujalazimishwa kuzijibu.

Ni nini motive ya Mengi kuanika barua hadharani?

nani kakuambia ni Mengi ndiyo ameanika hiyo barua? Umeona nakala zimetumwa kwa watu wangapi? Umeona maelekezo ya barua ya kwanza kuhusu nakala? Unless kuna unachojua kuwa ni yeye ndiye aliyeanika hadharani maana hapa imewekwa na Invisible ambaye kwa kadiri ninavyojua siyo Mengi!
 
Mimi nadhani watu humu tunatumia emotions bila kuangalia mambo kwa undani . Mengi amekosea katika hili, huwezi kutumia vyombo vyako vya habari kumuattack mtu mwingine. Nakubalina kile anachosimamia vita vya mafisadi , lakini kitu alichofanya ni kosa. Tuache ushabiki usio na msingi tuangalie hiko kipengele cha 22 kilichotajwa hapo juu kinasemaje .

Hivi itakuwaje kama kesho na mimi nitaanzisha TV yangu na kuanza kusema watu fulani ni mafisadi . SO where are we going to draw a line. Hili ni tatizo , na ninaishukuru bodi ya utangazaji kwa kum-summon Mengi.
 
nani kakuambia ni Mengi ndiyo ameanika hiyo barua? Umeona nakala zimetumwa kwa watu wangapi? Umeona maelekezo ya barua ya kwanza kuhusu nakala? Unless kuna unachojua kuwa ni yeye ndiye aliyeanika hadharani maana hapa imewekwa na Invisible ambaye kwa kadiri ninavyojua siyo Mengi!

Nimeambiwa na Mengi

Uliza swali jingine.
 
Wakuu naomba niulize, TCRA (serikali) wamemlima Mengi barua kwa sababu na makosa waliyoyaona wao, sasa je kwa kitendo ambacho Habari corporation ilikifanya cha kuchapisha matoleo mawili ya RAI kwa tarehe moja na namba zilezile, hivi serikali imechukua hatua gani kwa Kampuni hiyo na mmiliki wake? Au ndo mambo ya kulindana na kumuonea mnyonge???

Mkuu tena habari nyingine ya kushambualia watu vile vile? Nakwambia bongo tusiponyanyua mawe tukatoana meno ili adabu ichukue mkondo wake, tutaendelea kuburuzwa tu!
 
Nimeambiwa na Mengi

Uliza swali jingine.



Mtoto wa kuumeni kuwa mpole punguza taharuki, si wewe uliyesema hoja inajibiwa kwa hoja kwenye post yako hapo juu au?? sasa mbona unaleta mambo ya akina khadija kopa??? Mipasho kwa kwenda mbeleee, i wish mods wangeanzisha kundi la taarabu hapa nafikiri tungekuwa na waimbaji wazuri sana.. hahaha
 
Serikali hii imejaa vilaza wengi, wao wanafikiri kwa kuifungia ITV ndio wanamkomoa Mengi kumbe unknowingly ndio wanamjenga! Wananchi sasa wanajua kua watoto wao wanasoma kwenye mchanga bila madawati kwa sababu wajanja wengi ambao ndio hao mafisadi wamekuwa wakiibia nchi hii toka enzi ya mzee RUKSA ; kuanzia kwenye mpango wa DEBT conversion ambayo baadae ikezaa EPA; sasa mapesa waliokomba hawa watwana yangeliweza kutupatia dawa kwenye zahanati zetu na maman na dada zetu wasingekuwa wanazalia barabarani au kulala wawili wawili huko kwenye maternity wards.Hivyo basi mtu yeyote atakayekuwa upande wa mafisadi na kuwapiga vita wapinga ufisadi [akiwamo Reginald Mengi] atakuwa anapambana na nguvu ya umma!!
 
I have no doubt kuwa Mengi ndiye anayehusika na hizi barua kufika hapa, je motive yake ni nini ikiwa tayari mawakili wake wana shughulikia hili swala?

So far mambo yako katika hatua za mwanzo, Mengi ana wasiwasi gani gani hadi kutofika kuwaamini mawakili wake?

Je, hawa mawakili wana mshauri vizuri mteja wao?

Mkuu Pundamilia, kwanza naomba nitambue uhuru wako wa kikatiba wa kutoa maoni. Pili naomba niungane na Kapinga, Mzee MM na wengine juu ya yale waliyochangia. Pia nami nikuulize hapa:

  1. Unauhakika gani kuwa Mengi ndiye anayezifikisha docs hapa JF?Kama ni Mengi then ni Mengi pia kakwambia kuwa hawaamini maAdvocates wake?Asingewaamini angewapa hiyo kazi?
  2. Unaona Ubaya gani kwa Watanzania kupata info kama hizo za kwenye barua za Sakata la M na TCRA humu mtandaoni?Do u have good intentions na JF au nawe ni walewale mamluki tu?


Kuhusu Mengi kutaka kuonewa huruma na Wananchi, kwa mtizamo wangu, sidhani kama biashara za Mengi na mambo yake mengine yanahitaji huruma ya Watanzania ili kufanikiwa. Ila hayo ya Mafisadi kwa sasa yatahitaji huruma ya Wananchi, kama ambavyo tumekuwa na huruma hata wakaendelea kutunyanyasa na kutunyonya ndani ya ThiThiEm.


Let it be so said
 
Back
Top Bottom