Mtu pekee ambaye angeweza kutamka kauli hizi na nikamwelewa ni mke tu wa Seth Singh, lakini kwa wewe naona kama umetumwa tu.
Sijui kama kuna wakati huwa unafikiria shida za wenzio. Sijui kama unafikiria maumivu ya wenzio wanaoteseka kutokana na wizi wa hawa unaowatetea.
Nitajitolea kukutembeza uijue Tanzania. Nitarudi February ukiwa tayari niPM.
Ova
Shida yako shida yangu. Ukweli ubaki kuwa ukweli.
Tulikuwa na shida ya umeme na hawahawa mnaosema leo hii ni wezi ndiyo waliokuja kuwekeza wakati tuna shida.
Huyo Sethi ni mwekezaji kutokea Iringa, kama hakuwekeza Tanzania atawekeza kwingine, hakuanza leo, toka enzi za Nyerere wazee wake walikuwa na kampuni Iringa ya ukandarasi ikiitwa Ruaha Concrete Company RCC.
Ni mtu wa kawaida sana wala kilemba na ndev zake sisikutishe hiyo ni imani yake. Na hana wizi huyu, ni mfanya biashara, alikuta urithi wa wazee wake kauendeleza sasa umekuwa wa Kimataifa, ni faraja kubwa sana kwa Tanzania kwa kijana mfanya biashara kutokea Iringa kuikuza biashara na kuwa wa Kimataifa. Inabidi tujivunie. Na kampuni yake imeinunuwa Mechmar na VIP kwa makubaliano maalum na wamewalipa.
Nilidhani Watanzania tungejivunia kuwa kijana wetu wa Kitanzania kaweza kujitutumuwa, kutumia akili, kukopa, kuhangaika na kuweza kuinunuwa hiyo mitambo ambayo tulishindwa kama taifa kuinunuwa wenyewe wakati wa shida.
Kainunuwa, katutowa kwenye janaga la kuwa mitambo ya watu wa nje, kaahidi kuwa anaibadilisha kuifanya ya gas mwaka huu huu unaokuja kesho kutwa 2015 na kuufanya umemem ushuke hadi kufikia senti 8. tena si kwa maneno kwa maandishi na miakataba amabapo hakuna kampuni nyingine yeyeote iliyowahi kufanya hivyo hadi hii leo.
Leo anakuja mtu kuwajaza ujinga kuwa huyu ni mwizi na wewe bila kufikiri hata chembe unakubali tu.
Sethi alikuibia nini wewe?
Ile mitambo pale Tegeta ni yako? uliinunuwa wewe? au iliinunuwa Serikali yako?
Huyu Sethi ni wakusaidiwa, huyu si wa kusakamwa, katutoa kwenye shimo kwa kuinunuwa hiyo mitambo kutoka kwa wawekezaji ambao hawana uchungu na hii nchi hata chembe na kakubali kushusha bei ya umeme na kakuballi kubeba madeni yote yatakayojitokeza.
Huyu ni mzalendo huyu, huyu ni wa kubebwa na kuenziwa na kupewa kila msaada anaouhitaji si wakunyanyaswa hata kidogo.
Dhambi ya Sethi ni nini?