ITV Live: Lipumba anamshukia Kikwete ESCROW

ITV Live: Lipumba anamshukia Kikwete ESCROW

Kila kikicha LIPUMBA anakuwa mwepesi wa siasa. Haya maneno ya dalali, mara usanii yamekuwa yakitumiwa sana kwenye sakata la ESCROW kutaka kumsafisha REGINALD MENGI kuwa dalali wa vitalu. LIPUMBA naye anaondoka nayo kama yalivyo.
Kikwete ni mbongo flavor..... HII NDO POINT ELEWA HILO mpuuz mkubwa wewe
 
amesema rais ni fully msanii...nchi hii hatuna rais tuna mbongo flavor hata wenzetu wanatushangaaa....
Ni kweli na wanahaki ya kutushangaa.huwezi kuwa na Rais mwizi na asiye jiheshimu still akipita barabarani wadanganyika mnajipanga kumpigia makofi
 
Si bora eo unaweza kusema wamekosa panadol, tuliamnishwa wakatimwa Nyerere kuwa Aspro mbili kwa magonjwa 20. Na sisi tumo tu. Kumbe yote tunadanganywa tukiumwa tusiulize dawa tujikandamizze na Aspro mbili kwa magonjwa ishirini.

Leo uansema "wansima " chini ya mbuyu, Neema kubwa hiyo. Wakati huo wa Nyerere chini ya mbuyu unakwenda kuokota mabuyu ufanye lunch.

Hicho ni kizaramo au mihemko imekutawala?
 
Hayo yalikuwa wakati wa Nkapa, wala alikuwa hajali Wazanzibari wakiuwana, ana uchungu nao upi? lakini mwenye uchungu nao alipoingia madarakani, tukaona amani imeingia Zanzibar, waliokuwa wanauwana na kuwekeana mavi sasa wanaongoza Zanzibar kwa pamoja, raha mustarehe.

Au huyajuwi hayo?

Nasikitika sana unavyomtetea jk ccm ni walewale, hakuna kipindi ambacho watz wengi wameuawa na serikali kama cha jk, arusha nadhani unakumbuka, mtwara huko nako ndo usiseme ndo maana uchaguzi serikali za mitaa tandahimba ccm hamujapata ujumbe, wala kiti chochote na hiyo ni salamu
 
Si bora eo unaweza kusema wamekosa panadol, tuliamnishwa wakatimwa Nyerere kuwa Aspro mbili kwa magonjwa 20. Na sisi tumo tu. Kumbe yote tunadanganywa tukiumwa tusiulize dawa tujikandamizze na Aspro mbili kwa magonjwa ishirini.

Leo uansema "wansima " chini ya mbuyu, Neema kubwa hiyo. Wakati huo wa Nyerere chini ya mbuyu unakwenda kuokota mabuyu ufanye lunch.

Mama wa kuhororoja umeingiliwa account? unaandika hovyohovyo leo
 
Hao wezi ni akina nani? unabwabwaja na kuhororoja bila mpango.

Kikwete kapelekewa maazimio manane na yote kayafanyia kazi, kinachokuuma ni nini?
Hakuna mwizi.sasa hayo maazimio aliyofanyia kazi yanahusu nini?
 
Heshima pekee kwa Nyerere na Familia yake hawakuwa Mafisadi.Hakuogopa kumwajibisha Fisadi yeyote na alitetea mali ya Umma kwa nguvu zake zote.Daima tutamkumbuka baba yetu wa Taifa la Tanzania.

Alimwajibisha nani? Njaa mtindo mmoja. Si yeye wala familia yake wala mawaziri wake na familia zao hatukupata kuwaona wala kusikia kuwa hata siku moja walikaa kwenye foleni ya sukari au mchele. Kama si ufisadi huo ni nini?

Familia yake, kuna mmoja alikuwa tapeli. Usitake kulianzisha hapa saa hizi.
 
Hebu acheni kuzunguka mbuyu bhana ile pesa ilikuwa haijalipwa kwa IPTL, ilikuwa bado kuandikiwa vocha na hundi ya kumlipa IPTL kile anachostahili sasa hapo pesa si ya umma? hivi kwa kuwa wakandarasi na wazabuni mbalimbali wanaidai serikali tutasema mapesa yote yaliyoko kwenye akaunti za serikali ni mali ya wazabuni na wakandarasi? enyi watanzania nani kawaloga? Wizara fulani ikwa na madeni na madai mbalimbali ya suppliers akaunti yote inakuwa ni mali ya suppliers? kuna upumbavu na ujinga tunaolishwa kwa kuwa inajulikana watanzania ni wajinga.
Mkuu umemaliza.watanzania si wajinga kihivyo though watawala wanafikiri sisi wote bado ni wajinga,la hasha na wajinga wachache wamebaki tu huko ccm
 
Hayo yalikuwa wakati wa Nkapa, wala alikuwa hajali Wazanzibari wakiuwana, ana uchungu nao upi? lakini mwenye uchungu nao alipoingia madarakani, tukaona amani imeingia Zanzibar, waliokuwa wanauwana na kuwekeana mavi sasa wanaongoza Zanzibar kwa pamoja, raha mustarehe.

Au huyajuwi hayo?

Wewe nawe huishi vituko! Sasa unashangaa nini Lipumba kuwa na uhusiano au kupongezwa na Chadema?
 
Kuna maazimio manane na hakuna hata moja lilionesha kuna wizi au wezi. Kama lipo tuoneshe. link hii hapa:
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Tovuti Rasmi ya Ikulu
Azimio la nane: "Bunge linaazimia kwamba Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Ardhi na Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO wawajibishwe kwa kuishauri mamlaka ya uteuzi kutengua uteuzi wao.
Azimio hili ndilo Azimio ambalo limevuta hisia za watu wengi, na pengine ndilo ambalo utekelezaji wake unasubiriwa kwa hamu. Utekeelzaji wake umeanza. Kwanza, ni kuhusu Bodi ya TANESCO, tumeanza mchakato wa kuunda Bodi mpya kwani iliyopo imemaliza muda wake. Kuhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, kwa vile ni mtumishi wa umma anatawaliwa na Sheria na Kanuni za Utumishi wa umma, hivyo nimeshaelekeza Mamlaka kuchunguza tuhuma zake na hatimaye ikibainika ana makosa hatua za kinidhamu zitachukuliwa. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameshajiuzulu. Tumelitafakari suala la Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi la kupokea fedha kutoka VIP Engineering and Marketing ambazo kwa maelezo yake ni kwa ajili ya shule anayoimiliki na kuiendesha. Mwenyewe ameeleza wazi kupitia vyombo vya habari. Pamoja na hayo yapo mambo ya msingi kimaadili ambayo hayakuzingatiwa, hivyo tumemwomba atupishe tuteue mwingine. Kuhusu Prof. Muhongo nimemuweka kiporo, kuna uchunguzi niliagiza ufanywe na vyombo vyetu bado nasubiri taarifa hiyo ili nifanye uamuzi ndani ya siku chache zijazo.


Pukupuku langu, hawa walitakiwa na wamewajibishwa kwa kosa gani?
 
Alimwajibisha nani? Njaa mtindo mmoja. Si yeye wala familia yake wala mawaziri wake na familia zao hatukupata kuwaona wala kusikia kuwa hata siku moja walikaa kwenye foleni ya sukari au mchele. Kama si ufisadi huo ni nini?

Familia yake, kuna mmoja alikuwa tapeli. Usitake kulianzisha hapa saa hizi.

Ha ha ha FF! Hukumbuki kwa jinsi alivyokuwa anaichukia rushwa kidogo Chief Fundikira alambwe Hamsa wa Ishirini akiwa waziri wa sheria kwa kupokea rushwa? Siku hizi siku hizi mpokea rushwa ndio mjanja.
 
Lipumba ana stress, uchaguzi unakaribia na anajua hawezi kushika hata nafasi ya tatu
sio stress tu, hata kama ana kichaa, ukweli lazima usemwe, ukweli wenyewe ni kuwa, Mr.Kikwete ni muhujumu uchumi na mwizi namba moja.
tanzania imeingizwa kwenye ukata wa hali ya juu na rais kilaza mwizi hana huruma.
 
usiniambie wakati wa nyerere sikuwepo
mimi nimeshuhudia ccm ikila nchi bila huruma huku wananchi wake wakiwa na hali mbaya

na wakati wa nyerere mapato yatokanayo na kodi hayakua makubwa kama siku hizi
kulikuwa hakuna wizi wa bilion 300 kama siku hizi ila wa benja na kikwete yote tumeyashuhudia bora mwinyi alijitahidi kwa kiwango chake

Aufahamu kuhusu sakata la utoroshwaji wa nyara za serikali lililomkumba mke wa mzee mwinyi? Maccm wezi
 
Back
Top Bottom