Itakuwa sahihi CHADEMA kushiriki mazungumzo na Rais Samia huku Mwenyekiti wake akiwa ndani kwa kesi ya kubambikiziwa?

Huo ni mkutano wa Wenyeviti wa vyama vya siasa. Yeye akiwa M/kit wa CCM ambacho ni chama tawala. Je kwa Chadema kitakuwaje ambacho ni chama kikuu cha upinzani??
 
Inategemea format ya mazungumzo yenyewe. Kama yatakuwa ya vyama vyote kwajumla chini ya uongozi wa Shibuda na Msajili wa Vyama ni bora wasiudhurie maana hawatapata nafasi ya kutoa dukuduku zao kwa kikamilifu. Aidha, wataipa serikali kisingizio cha kusema kuwa pamekuwa na mazungumzo na wapinzani.

Kama format itakuwa ya wao peke yao na serikali au wao pamoja na vyama vya ACT Wazalendo, CUF, NCCR Mageuzi ( pengine na CHAUMMA)mazungumzo yatakuwa na tija zaidi na hivyo itakuwa busara wakihudhuria.

Amandla...
Utaratibu uliopangwa inaonekana watakutana kupitia umoja wa vyama chini ya Shibuda.
 
Utaratibu uliopangwa inaonekana watakutana kupitia umoja wa vyama chini ya Shibuda.
Bora wasihudhurie. Mkutano utageuka wa wakina TLP, TADEA, ADC n.k. kuonyesha jinsi wasivyokubaliana na agenda za Chadema. Itakuwa ni kupoteza muda kama ilivyokuwa kushiriki katika uchaguzi wowote chini ya mfumo tulionao sasa hivi. Vichwa vya habari vitakuwa " wapinzani wasema kuwa Katiba Mpya sio priority na serikali isiingilie uhuru wa Mahakama".

Amandla...
 
Bora wasihudhurie. Mkutano utageuka wa wakina TLP, TADEA, ADC n.k. kuonyesha jinsi wasivyokubaliana na agenda za Chadema. Itakuwa ni kupoteza muda kama ilivyokuwa kushiriki katika uchaguzi wowote chini ya mfumo tulionao sasa hivi. Vichwa vya habari vitakuwa " wapinzani wasema kuwa Katiba Mpya sio priority na serikali isiingilie uhuru wa Mahakama".

Amandla...
Umeona mbali!
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.
Hakuna mazungumzo ya chadema yanaweza fanyika Ili Hali Mwenyekiti yupo ndani,
 
Wewe jamaa huwa nakushangaa sana!Dikteta Samia akisema kuwa anataka akutane na vyama vya upinzani huwa anamaanisha kuwa anataka akutana na vile vyama ambavyo ni mapandikizi ya CCM na vyama rafiki wa CCM kama vile ACT wazalendo,TLP,CUF na kadhalika na siyo chama pendwa cha wananchi-chadema.

Kwani hukumsikia hata alipokuwa anahojiwa na Kikeke kule BBC aliiponda sana chadema?
 
Wewe jamaa huwa nakushangaa sana!Dikteta Samia akisema kuwa anataka akutane na vyama vya upinzani huwa anamaanisha kuwa anataka akutana na vile vyama ambavyo ni mapandikizi ya CCM na vyama rafiki wa CCM kama vile ACT wazalendo,TLP,CUF na kadhalika na siyo chama pendwa cha wananchi-chadema.

Kwani hukumsikia hata alipokuwa anahojiwa na Kikeke kule BBC aliiponda sana chadema?
Huo mkutano wao utapuuzwa tu maana CHADEMA ndio wanaoaminika zaidi kama wapinzani
 
Ni vyema Makamu Wenyeviti na viongozi wengine washiriki ili wapate nafasi ya kutoa malalamiko yao kuhusu Mbowe na mambo mengine kwenye faragha na Mother! Sometimes mazungumzo ya faragha yana nguvu kuliko haya ya kwenye press ambako kutunishiana misuli ni kwingi
Ili wakamwombe msamaha au,kwani hajui kuwa hawatendei haki wapinzani?
KUSHIRIKI MAZUNGUMZO HAYO NI UWOGA

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
MTOA MADA umeandika kishabiki sana ungetaka maoni ungeandika kwa kubalance story sasa unasema kesi ya kubambika wewe ndiyo haklimu unayetoa maamuzi? kwanini unaingilia kesi ambayo iko mahakamani?

Je, akikutwa na kesiya kujibu utasemaje tena? CHADEMA inatakiwa ijiendeshe kama taasisi siyo kama inavyofanya sasa hivi kuwa sipokuwepo mbowe basi hakuna kinachoendelea ndani ya chama.
Wewe umeandika utopolo,kishabiki,kiccm,kidikteta

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.
Tutatuma barua kwenye kikao hicho kwamba Mjumbe wetu kwenye mazungumzo hayo ni Freeman Mbowe , sasa kwa vile yuko jela basi hatutakuwa na mwakilishi , FULL STOP
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.
Hii ni pasua kichwa,hapa kinachohitajika ni busara na hekima ili kulimaliza jambo hili,bila hekima hili jambo haliwezi kuisha kwa sababu CHADEMA hawana dola na waone matukio ya uonevu kutoka chama tawala yanavyoiandama chadema kama vile kufungwa bila sababu,kupigwa risasi Tundu Lissu na kuvuliwa ubunge,kutekwa tekwa ovyo na kubambikiziwa kesi,kunyang'anywa wabunge na kuwaapisha kupitia Ndugai,hivyo inabidi busara ya hali ya juu na hekima vitumike.
Kukutana na rais wakati mheshimiwa Mbowe akiwa ndani haipendezi hata kidogo,lakini kwa namna ya kipekee ni jambo jema kufumba macho na kuziba masikio ili kukutana na rais ili kueleza yote bayana na kutafuta ufumbuzi wa maswala haya yanayosumbua siasa za Tanzania,ili kuleta na kujenga umoja na mshikamano pamoja na upendo wa dhati kwa Watanzania wote.
 
Kwa kweli nitashangaa mshangao wa kunitoa roho.
CHADEMA watashiriki vipi huku wamefungwa pingu mikono, miguu na kufungwa kutambaa machoni?
CHONDE CHONDE CHADEMA msituue kwa pressure.
Sikiliza hasira hasara kumbuka ccm hawana cha kupoteza wenye shida ni sisi hivyo inabidi tujishushe tuwasikilize na tujadiliane nao hasa kesi ya Mbowe na wale Wabunge kumi na tisa,busara itumike kumaliza hii changamoto.
 
Inategemea format ya mazungumzo yenyewe. Kama yatakuwa ya vyama vyote kwa jumla chini ya uongozi wa Shibuda na Msajili wa Vyama ni bora wasiudhurie maana hawatapata nafasi ya kutoa dukuduku zao kwa kikamilifu. Aidha, wataipa serikali kisingizio cha kusema kuwa pamekuwa na mazungumzo na wapinzani.

Kama format itakuwa ya wao peke yao na serikali au wao pamoja na vyama vya ACT Wazalendo, CUF, NCCR Mageuzi ( pengine na CHAUMMA)mazungumzo yatakuwa na tija zaidi na hivyo itakuwa busara wakihudhuria.

Amandla...
Safi sana hapo nimekuelewa mkuu.
 
Sikiliza hasira hasara kumbuka ccm hawana cha kupoteza wenye shida ni sisi hivyo inabidi tujishushe tuwasikilize na tujadiliane nao hasa kesi ya Mbowe na wale Wabunge kumi na tisa,busara itumike kumaliza hii changamoto.
Unajadilia nao nini sasa kwa mfano?
Kama polisi wanatumika kuvunja sheria na katiba si bora kushughulika na hao mapolisi?
 
Back
Top Bottom