Itakuwa sahihi CHADEMA kushiriki mazungumzo na Rais Samia huku Mwenyekiti wake akiwa ndani kwa kesi ya kubambikiziwa?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.
 
Ni vyema Makamu Wenyeviti na viongozi wengine washiriki ili wapate nafasi ya kutoa malalamiko yao kuhusu Mbowe na mambo mengine kwenye faragha na Mother! Sometimes mazungumzo ya faragha yana nguvu kuliko haya ya kwenye press ambako kutunishiana misuli ni kwingi
 
MTOA MADA umeandika kishabiki sana ungetaka maoni ungeandika kwa kubalance story sasa unasema kesi ya kubambika wewe ndiyo haklimu unayetoa maamuzi? kwanini unaingilia kesi ambayo iko mahakamani?

Je, akikutwa na kesiya kujibu utasemaje tena? CHADEMA inatakiwa ijiendeshe kama taasisi siyo kama inavyofanya sasa hivi kuwa sipokuwepo mbowe basi hakuna kinachoendelea ndani ya chama.
 
Sio kukuziba mdomo tu, bali anakutesa pia.
Pia mazungumzo hayoyatakuwa na dhamira ya kuendelea kukididimiza chama kilicholengwa na serikali kwa kuhalalisha sababu ya kumbambikiza mwenyekiti, na kuvijenga vyama washirika wa mfukoni mwa chama tawala.
 
Ni vyema Makamu Wenyeviti na viongozi wengine washiriki ili wapate nafasi ya kutoa malalamiko yao kuhusu Mbowe na mambo mengine kwenye faragha na Mother! Sometimes mazungumzo ya faragha yana nguvu kuliko haya ya kwenye press ambako kutunishiana misuli ni kwingi
Kwani kuna kitu hakijui kuhusu Mbowe?
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.
Kwanza lazima ujue dhamira njema ipo au ni ghiliba. Kumbuka mtu unayetaka kuzungumza naye alitamka anataka kuliponya taifa,kujenga mshikammano na upendo, akakataa watu kubambikiwa kesi. Iweje leo abadili msimamo wake? Lazima kuwa mwangalifu si kwa kuwa mtu kasema?
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.



Nawasilisha.
Kwa kweli nitashangaa mshangao wa kunitoa roho.
CHADEMA watashiriki vipi huku wamefungwa pingu mikono, miguu na kufungwa kutambaa machoni?
CHONDE CHONDE CHADEMA msituue kwa pressure.
 
Kwa kweli nitashangaa mshangao wa kunitoa roho.
CHADEMA watashiriki vipi huku wamefungwa pingu mikono, miguu na kufungwa kutambaa machoni?
CHONDE CHONDE CHADEMA msituue kwa pressure.
Hamna kushiriki na hila hapo na gilba
 
Hakuna umuhimu wowote wa kukutana na wa KUDEMKA wakati Mbowe akiwa lupango kwa kesi FEKI. Chadema wasifanye hayo makosa hasa ukitilia maanani Chadema ndicho chama pekee kilichoandika barua kwa wa KUDEMKA kuomba mazungumzo naye.
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.
 
Mtoa mada wewe ni fala kama mafala wengine, kwahy chama cha siasa ni chadema tuu.? Nyie nyie mnasema polisi wanaingilia kazi za mahakama halafu tena nyie nyie wanachadema mnasema mbowe amebambikiwa kesi sasa hapo napo sio kuingilia mahakama.?
Natamani huo mkutano uwepo hata Leo ili tuone wanaume mkisusa kama wanawake, makamu mwenyekiti c yupo bc yeye aje.
 
Baadhi ya wakati ni vyema wapinzani kukaa pamoja na rais na kueleza haki yao kwenye nchi yao. Kuwepo kwa Mbowe mahabusu sio kuwepo mahabusu kwa Chadema.


Lunatic
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.

Sioni haja yoyote ya cdm kushiriki kwenye kikao na wahuni. Waende vyama washirika wa ccm ili wakajadili.
 
Ukipewa wito na mfalme sharti utii.Ni fursa muhimu kwa CDM kushiriki Wana agenda nyingi muhimu za kitaifa zaidi ya Mbowe binafsi, japo mfuga mbwa akiridhia kwa mapungufu Katiba yetu! Mbowe anaweza tolewa ndani ya dk 15.
 
Hiyo ndio nafasi nzuri uso uso mnayafikisha na mnamsikilizana inajulikana mbivu na mbichi.
Kukutana wanaweza kukutana, ila cha msingi na iwepo dhamira ya kweli ya kutafuta suluhu katika kupata katiba mpya na mambo mengine ya msingi kama uhuru wa kufanya mikutano ya kisiasa pasipo kuingiliwa na vyombo vya dola.
 
Teyari tumesikia taarifa juu ya Rais Samia kukutana na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini katika siku na tarehe ambayo bado haijawekwa wazi kwa umma huku mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bwana Freeman Mbowe akiwa mahabusu kwa kesi inayolalamikiwa kuwa ni ya kubambikiziwa.

Kwa hali ilivyo, ni wazi mkutano huo utafanyika huku Mwenyekiti huyo wa CHADEMA ndani kwani si rahisi atoke mapema unless kuwe na maahikinikizo makubwa ya ndani na nje ya nchi kwani danadana za kesi yake tayari zimeshaanza na bila shaka zitaendelea.

Swali ni je, katika mazingira haya, itakuwa sahihi kwa CHADEMA kushiriki katika hayo mazungumzo huko mwenyekiti akiwa ndani kwa kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa?

Au itakuwa ni busara kwa CHADEMA kugomea mazungumzo hayo kama shinikizo la kutaka Mbowe atendewe haki katika hiyo kesi au kwa sharit la kutakai kes hiyo ifutwe kama haiwezi kuendesha.kwa haki?

Binafsi naamini kitendo cha Mbowe kuongoza harakati za kudai katiba mpya pamoja na yeye kufunguliwa hii kesi inayopingwa Karibu kila kona ya hii dunia, ni moja ya mambo yaliyoisukuma serikali kukutana na wapinzani katika harakati za kujisafisha mbele ya.umma wa watanzania na dunia kwa ujumla, hivyo ushirika wa CHADEMA katika mazungumzo haya ni muhimu sana.

Sasa narudia swali langu hili:
Je, CHADEMA washiriki hayo mazungumzo wakiwa na agenda ya kutaka Mbowe afutiwe hiyo kesi inayodaiwa kuwa ni ya kubambikiziwa au wasishiriki kabisa kama shinikizo la kutaka Mbowe aachiwe au atendewe haki katika hiyo kesi?

Nawasilisha.

Inategemea format ya mazungumzo yenyewe. Kama yatakuwa ya vyama vyote kwa jumla chini ya uongozi wa Shibuda na Msajili wa Vyama ni bora wasiudhurie maana hawatapata nafasi ya kutoa dukuduku zao kwa kikamilifu. Aidha, wataipa serikali kisingizio cha kusema kuwa pamekuwa na mazungumzo na wapinzani.

Kama format itakuwa ya wao peke yao na serikali au wao pamoja na vyama vya ACT Wazalendo, CUF, NCCR Mageuzi ( pengine na CHAUMMA)mazungumzo yatakuwa na tija zaidi na hivyo itakuwa busara wakihudhuria.

Amandla...
 
Back
Top Bottom