Issue ya RC wa Dar imefanikiwa kuzimwa

Issue ya RC wa Dar imefanikiwa kuzimwa

aliyekudanganya nani
[HASHTAG]#bashitebringyourcertificates[/HASHTAG]
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Watu wanamsubiria tu azungukeee weee ila hawatasaau kamwe!!! Lazima lazima amtoe asipomtoa halitaisha
 
Suala halijazimwa, au kama limezimwa basi kwa nje tu, lakini kwa ndani, kwenye mioyo ya watu bado linafukuta. Kuna siku litalipuka upya. Ukitaka ujue kama limezimwa hebu wawekee wabongo sanduku la kupiga kura mbele yao leo, ndipo utagundua kwa hawataki uji....!
 
Mjadala wa Bashite ulitawala kwa muda zaidi kwenye vyombo vya habari lakini mh rais amefanya jitihada mbalimbali ili kutuondoa watanzania katika mjadala wa vyeti vya bashite
Kwa hili rais amefanikiwa!
Kwani vyeti sasa vimezoeleka na hakuna tena mjadala unaoshinikiza vyeti

Hata mkuu wa mkoa mwenyewe hasikiki tena sijui ndio lile azimio la wa hariri liko kazini

Mkuu wa nchi kafanikiwa sana kuzima mjadala uliomhusu mkuu wa mkoa kwa asilimia zote
Hao wahariri pia wamesaidia mjadala kufungwa.

Asenteni sana wahariri.
 
Na mkiendelea kupiga kelele anatumbuliwa Mwigulu Chemba ili swala la Bashite lizimwe. Bashite ndiye kipenzi cha Mukulu
na mkiendelea nyinyi kidomodomo ndio mtatumbuliwa kwanza. hata mungu anawaona ushetani wenu kumuandama paulo kwa chuki zenu.
 
Jinai haifi na isitoshe hana kinga.Anaemlinda hamsaidii bali anampa kiburi cha muda.

Hili ni donda ndugu kwa mkulu na yeye mwenyewe.

Mkulu anaelinda majambazi hafai mbinguni na duniani.
Yaani siku huyo baba yake anayemkingia kifua anaachia madaraka tu, pingu zitamhusu fasta.
 
Mkuu kazima nini sasa mbona mnakuwa mazezeta sema mmeongea mpk baadae mkajiona wapuuzi tu wenywe ...wanaume mnakua km wanawake
 
Si ameshitakiwa tume ya maadili na meya wa Kinondoni kwa tiketi ya chadema, au mmesahau?

Tunangoja tusikie hilo shauri likiamuliwa na tume.
 
Kapunguza mjadala, hajatatua chanzo cha mjadala.
Vitu vyote viko pale pale.
Kwa kifupi ameahirisha mjadala.
Kwa wenye akili hili jambo liko pale pale kama ambavyo bado yuko kwenye ofisi ile ile ujinga unaendelea kuwa mkubwa kwao wote wawili ney kawagonga sasa
 
Nitajie mtu mmoja alieshtakiwa sababu ya vyeti

Kuna nurse amepigwa Mvua Saba week tatu zilizokwisha.Pole kama husomi Magazeti.

Ya yule nurse imewezekana kushtakiwa na kufungua sababu hana Pesa,mnyonge.Vibarua tu.Lakini hawa wenye pesa zao na Wenye wa kuwabeba wanapata tu.

Kuna wengine wawili kesi zao zimepelekwa Mahakama kuu Arusha. Hao wanaoshtakiqa hawana wa kuwabeba.Ati tuna Tume ya Katiba,Sheria na Haki za Binadamu.

Binadamu kwa Tanzania ni Watawala tu,wengine ni viatu.
 
Back
Top Bottom