Israel yakasirishwa na Uhispania na Ubelgiji baada ya nchi hizo mbili kusema zitatambua rasmi nchi huru ya Palestina

Malaria 2

JF-Expert Member
Oct 17, 2023
2,646
3,936

Nov 25, 2023 11:03 UTC

1700927639160.png

  • Netanyahu na mawaziri wakuu wa Uhispania na Ubelgiji
Mvutano umepamba moto kati ya utawala haramu wa Israel na Uhispania na Ubelgiji, nchi mbili za Ulaya ambazo mawaziri wake wakuu wamelaani mashambulizi yaliyosababisha uharibifu mkubwa ya utawala huo dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza na kuitaka Tel Aviv na jamii ya kimataifa kulitambua rasmi taifa huru la Palestina
Ofisi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Eli Cohen, imesema katika taarifa yake kwamba waziri huyo amewaita mabalozi wa Uhispania na Ubelgiji kufanya "mazungumzo ya kukemea," akilaani kile alichokitaja kuwa madai ya uwongo ya Mawaziri Wakuu wa Uhispania na Ubelgiji ambayo amesema yanaunga mkono ugaidi.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania, Jose Manuel Albares amejibu madai hayo ya Israel na kutangaza kupitia televisheni ya taifa jana jioni, Ijumaa, kwamba amemwita balozi wa Israel mjini Madrid ili kutoa ufafanuzi wa shutuma za serikali ya Tel Aviv, ambazo amezitaja kuwa "uongo na zisizokubalika."
Ameongeza kuwa: "Suluhisho la sasa la mgogoro wa Gaza halitoshi," na kusisitiza kwamba Israel lazima iwe ya kwanza kuchukua "mkakati wa kina" wa kutatua mzozo wa Israel na Palestina, ikiwa ni pamoja na Ukingo wa Magharibi na Quds Mashariki.
Waziri Mkuu wa Uhispania pia ameitaka jamii ya kimataifa na Israel kutambua rasmi taifa la Palestina.
Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Ubelgiji amesisitiza kuwa Israel lazima iheshimu sheria ya kimataifa ya kibinadamu, na kwamba "mauaji ya raia lazima yakome
 
Niko upande wao. Maana hii ndiyo suluhu pekee na ya uhakika, ya kumaliza huu mgogoro kati ya hao wanaojiita Waisrael, na Wapalestina.
 
Uzi wa kichoko uliojaa chuki sasa utawala Israel una uharamu gani? Wakati umechaguliwa kidemocrasia hayo mataifa yaliyoingia kimapinduzi kama Iran ndio utawala haramu

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
We unakurupuka ka umekunywa gongo,, hayo matusi ya nini,, kwanini hapa inazungumziwa demokrasia ya ndani ya Israel au namna gani taifa hilo kanjanja lilivyopachikwa pale mashariki ya kati,,
 
Back
Top Bottom