Israel imebomoa majumba na kuua Gaza; Hamas imeporomosha uchumi wa Israel. Kumbe vikundi vinavyokwenda Israel ni vya watumwa

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,194
10,929
Kwa kiwango kikubwa Israel yote inalishwa na shughuli za kilimo na ufugaji zinazofanyika kusini ya nchi hiyo na mpakani na Gaza ambazo asili ya ardhi hizo zenye rutuba zilitwaliwa na wayahudi waliovamia mpaka kufikia 1948. Na hata mashamba ya mitende ya kaskazini ya Israel yapo kwenye maeneo ya mabedui wa kiarabu waliozingirwa na uvamizi huo.

Kabla ya mwaka 1990 matajiri wa kiyahudi walitumia nguvu kazi kutoka Gaza kwa shughuli zote za mashambani. Pale wapalestina hao walipojuwa wanatumikishwa kwenye ardhi walizofukuzwa wazazi wao na kuanza mapambano ndipo Israel ilipoanza kuwawekea vikwazo na vizuizi vya ukaguzi na pia kuanza kufikiria kutafuta wafanyakazi kutoka mataifa mengine.

Kwa ujumla Israel inahitaji watu 300,000 kufanya kazi kwa gharama ndogo kwenye mashamba hayo.Zaidi ya nusu bado waliendelea kuwa ni wapalestina maskini kutoka Gaza ambao kila asubuhi huingia eneo hilo kwa vikwazo vingi na ukaguzi wa hali ya juu wakienda kujitafutia riziki zao.

Pamoja na wapalestina hao Israel imeweza kuwashawishi raia wengi kutoka nchi maskini kwenda nchini humo kufanya kazi za shambani kwa gharama za chini sana.Moja ya taifa lenye idadi kubwa ya wafanyakazi wa mashambani ni Thailand.

Wataiand pamoja na kukubali kufanya kazi kwa gharama ndogo lakini husaini mikataba ya muda mfupi inayowakataz kufanya mahusiano yoyote ya kimapenzi na wenyeji au kuanzisha familia nchini Israel.
Kutokana na kukua kwa uchumi wa viwanda wa Israel idadi kubwa ya raia wake wamekuwa wakiingia kufanya kazi za kiofisi na kupanua zaidi hitajio la wafanyakazi kutoka mataifa maskini.Hali hiyo imepelekea Israel kufikiria kupata raia wa mataifa mengine ya kiafrika kwa bei rahisi kwa kisingizio cha kwend kuchukua mafunzo ya kilimo.

Baada ya shambulio la kushtukiza la Hamas hapo oktoba 7 mwaka huu 2023 idadi kubwa ya wafanyakazi wa mashambani wa Thailand waliathiriwa kwa kuimizwa,wengine kufariki dunia na waliobaki hai kuamua kurudi kwao wakiazimia kutokurudi tena kwa shughuli za kilimo huko Israel.

Pengo la wafanyakazi hao lingezibwa na vibarua kutoka Gaza ambao wanapakana na maeneo hayo lakini Israel imeingiwa na hofu na watu hao wote na hivyo kuamua kuwarudisha makwao pamoja na vipigo na fedheha na bila ya hata kuwalipa ujira wao waliokwisha kuutumikia.

Hali hiyo imesababisha mashamba kutokupata huduma na hivyo mazao kuharibika na magugu kuota nafasi yake.Kwa vile mazao hayo hulisha karibu Israel yote kutokupata huduma kumepelekea kuzuka kwa hofu ya njaa nchini humo.

Mabanda ya mifugo ambayo ni moja ya nguzo za uchumi wa Israel yamebaki na ngombe wasiokuwa na watu wa kuwakatia majani na kuwalisha pamoja na kuwapa matunzo yake. Wale wachache waliobaki wamekuwa wakitoa maziwa mara mbili tu kwa siku badala ya mara tatu kabla ya oktoba saba.

Kwa kujua athari za kiuchumi za kukimbia na kufukuzwa kwa wafanyakazi wa bei rahisi,vikundi vya raia vimekuwa vikihamasishana kufanya kazi hizo bila mafanikio kwani wengi wao hawana nguvu na ari ya kufanya kazi hizo ngumu za mashambani.

Israel’s farms need foreign labourers. The Hamas attacks triggered an exodus

1701064592279.png

1701064666406.png
 
Imeporomosha uchumi kidogo sana

Nakupa taarifa ya kwamba pato la taifa la Israel pamoja na udogo wake kwa mwaka huu pekee ni Trilioni elfu moja na mia nne, hata uunganishe nchi zote za Afrika Mashariki hazifikii.
Kwamsaada wa Usaid
 
Imeporomosha uchumi kidogo sana

Nakupa taarifa ya kwamba pato la taifa la Israel pamoja na udogo wake kwa mwaka huu pekee ni Trilioni elfu moja na mia nne, hata uunganishe nchi zote za Afrika Mashariki hazifikii.
Takwimu za kabla ya vita.
umeambiwa baada ya vita hali ni mbaya sana.
 
triloni 7 wanazopewa za msaada si chochote kwenye uchumi wq Israel
Huo uchumi ulikuwa unategemea pamoja na mambo mengine kwenye Kilimo.Kama vita havitaisha mapema kuna hatari ya kutaka kuomba misaada ya vyakula kutoka nje mbali na ngano ambazo walikuwa wakichukua kutoka Ukraine.
 
Sasa wakija huku kutafuta watumwa wa mashambani wasitudanganye kuwa wametoa sholarshipi za masomo ya kilimo.
Na serikali iwe makini na hadaa za mayahudi kutupeleka kwenye mashamba yaliyoporwa kutoka kwa wapalestina.Mwishowe vijana wetu wanapata madhara bure.
Umeongea vzr, jamaa kanifungua macho kuona vijana wetu wa SUA wakipelekwa huko ,eti mafunzoni.

Chikwera, Present of Malawi kalaumiwa pia kupeleka lundo la vijana huko.
 
Umeongea vzr, jamaa kanifungua macho kuona vijana wetu wa SUA wakipelekwa huko ,eti mafunzoni.

Chikwera, Present of Malawi kalaumiwa pia kupeleka lundo la vijana huko.
Hamtaki kujifunza kwa waliofanikiwa? Israel ata watanzania wasipokwenda kujifunza raia wa nchi nyingine zinazojitambua watakwenda kwa manufaa yao...bakini na siasa zenu uchwara.
 
Hamtaki kujifunza kwa waliofanikiwa? Israel ata watanzania wasipokwenda kujifunza raia wa nchi nyingine zinazojitambua watakwenda kwa manufaa yao...bakini na siasa zenu uchwara.
Kujifunza nini?

Tangu wanafunzi hao walipo anza kupelekwa huko wamejifunza nini kilicho leta mabadiliko makubwa nchini?

Wanaenda kutumikishwa mashambani kwa kisingizio eti ni field practical.
 
Israel anao uzoefu mkubwa wa mambo ya vita na hii vita ni ndogo sana kwa Israel na kamwe usifikiri kuwa itamtingisha kiuchumi.

Kama jlikuwa hujui ni kwamba Israel inamatajiri wakubwa wanaoishi nje ya nchi yao pamoja na nchi nyingi marafiki ambao ni tamaduni kwao kutoa michango ili kuisaidia Israel kuendesha vita.

Ungejiuliza kuhusu athari za vita kiuchumi kwa upande wa Palestina, sababu Palestina hatoweza kuisimamisha nchi yake baada ya vita pasipo kupewa misaada
 
Kwa hiyo hata huyo mtanzania aliyefia mikononi mwa Hamas, alienda kutumikishwa katika mashamba ya Kilimo Israel?
Maana tuliambiwa kuwa alikuwa miongoni mwa watanzania walioenda kuchukua mafunzo ya Kilimo!
 
Kujifunza nini?

Tangu wanafunzi hao walipo anza kupelekwa huko wamejifunza nini kilicho leta mabadiliko makubwa nchini?

Wanaenda kutumikishwa mashambani kwa kisingizio eti ni field practical.
Sasa mabadiliko utaona kwa sampuli ya watu 200 kati ya watu 50miloni?
 
Hamtaki kujifunza kwa waliofanikiwa? Israel ata watanzania wasipokwenda kujifunza raia wa nchi nyingine zinazojitambua watakwenda kwa manufaa yao...bakini na siasa zenu uchwara.
Kuwa na staha na maoni ya watu.

"Uchwara" ni kauli hizo.
 
Kujifunza nini?

Tangu wanafunzi hao walipo anza kupelekwa huko wamejifunza nini kilicho leta mabadiliko makubwa nchini?

Wanaenda kutumikishwa mashambani kwa kisingizio eti ni field practical.
Siri kubwa imefichuka.
Wanalazwa kwenye mabanda kama mifugo na kazi ngumu sana za kulisha ng'ombe na kulima
Kwani sisi hatuna ardhi za kufanya hizo kazi.
Tatizo kubwa mpaka vita vya Gaza vimeanza serikali yetu wala Israel hawakuwahi kusema ukweli kuhusu madhumuni ya vikundi vikubwa kama vile kwenda Israel.
 
Huwezi kuona kwa sababu hao ni vibarua wanaenda kutumikishwa mashambani huko wala hawarudi na chochote cha kusaidia nchi.
Ni vibarua wa bei rahisi.
Watailand walionusurika kifo wamesema hawarudi tena.
Yule hayati Clement aliyekufa angekuwa yuko chuo chochote rasmi cha kielimu basi tungepata salamu za maombolezo kutoka chuoni kwake au kwa wanafunzi wenzake.Lakini kwa kuwa wenzake ni wale watailand ambao nao wameponea kutekwa hakuna hata mmoja aliyemlilia
 
Back
Top Bottom