Israel yalegeza masharti kuwezesha kupatikana mateka wake 40 kati ya wale wanaoendelea kushikiliwa na vikundi vya wapiganaji Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,192
10,926
Matumaini ya kupatikana nafuu kwa wapalestina karibia milioni 2 na nusu wanaoangamia kwa vita na njaa yameanza kupatikana.

Katika mazungumzo ya kusitisha vita baina ya Israel na Hamas kila upande umelegeza masharti yake ili kufikiwa kwa lengo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa zinazovuja kutoka kikao cha upatanishi huko Doha nchini Qattar,kimsingi Israel imekubali sharti la Hamas la kuachiwa wafungwa wa kipalestina baina ya 700 mpaka 800 kati ya maelfu walioko kwenye magereza ya Israel.

Sharti jengine muhimu la Hamas la kuruhusiwa kurudi watu kwenye maeneo yao hasa Gaza ya kaskazini nalo limekubaliwa.

Hata hivyo huenda Israel ikaunganisha na kikwazo cha umri na jinsia za hao watakaoruhusiwa kurudi maeneo kwa hofu ya kuruhusu wapiganaji watakaotia nguvu wenzao ambao bado Israel inaendelea kupambana nao.

Kwa upande wa Hamas nao wamelegeza sharti la kutaka Israel iondoshe majeshi yake yote kutoka Gaza.

Israel open to civilian return to north Gaza in truce talks

 
Vita sio nzuri.
Nyakati hizi sio za kupigana Bali za kufanya mazungumzo.

Ieleweke kuwa Dola la Kiislamu haliwezi kufanikiwa kutawala Dunia ya Leo.

Kuna wajahidina wanasema watapigana hadi kila nyumba na kila Tenti liwe na Waislamu tu na hawakubaliani na chochote kile Hadi ndoto yao itimie.
Hilo ndio tatizo.
 
Ulichoandika ni kweli! Nimesoma habari hii RT news!
Hata hivyo nionavyo makubaliano hayo hayatakuwa na maana yo yote wakati Ukanda wa Gaza umeharibiwa vibaya mno na wapalestina wengi wameuawa,na wengine kuachwa majaruhi.
Lakini pia Israel ikiona lengo lake limefanikiwa la kuachiliwa mateka wake,itaendeleza vita na Hamas,itakamata maelfu ya Wapalestina kuwarudisha magerezani!
 
Back
Top Bottom