Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,194
- 10,929
Kinachoendelea pale Gaza ni kama walimwengu wameamua waiache Israel ishinde vita vyake vya kuwamaliza Hamas na kuitawala Palestina.
Kundi jengine la walimwengu ni kama wale wapenzi wa filamu za vita ambao wameamua waachwe wafaidi uhondo wa vita vya kweli badala ya kila siku kuangalia maigizo.
Mpaka sasa hakuna hata taifa moja lilloamua kutoa msaada wa dhati kwa Hamas au angalau kwa wapalestina wengine wanaouliwa na kupiga mayowe mwisho wa sauti zao kuomba msaada.
Na kundi moja pekee lililojitokeza kusaidia kivitendo na kwa juhudi za kweli nalo ni Houth ambao kutokana na unyonge wa hali zao na uduni wa silaha walizonazo msaada wao haujafika kikamilifu kuwasaidia wale walaiozimia kuwafikishia msaada wao.
Hizbollah kikubwa anachokifanya ni kujilinda nafsi yake dhidi ya uchokozi wa Israel.Hawa nao sifa wanayopaswa kupewa ni kwamba hawakubali kukaa kimya au kukimbia wakichokozwa.
Iran nayo imepatwa na hofuj sana na vita hivi kubwa wakiamua kutokwenda mbali ili kulinda rasilimali zao wanazozikuza kwa kasi hasa katika teknolojia za kivita.Na hata wale wanaotamani kuipiga Iran wanaiogopa kwa hilo kwamba wakiamua kupiga ina uwezo wa kujibu.
Ukiacha hapo ni kuwa mataifa mengine ama yameamua kwa makusudi kuiacha Israel ishinde au wamepata uwanja tu wa kuangalia mapambano ya kivita.
Kinachofanya tuseme hivyo ni kuwa katika hali zote basi watu wa Gaza walistahiki kupewa msaada ili wasiendelee kuuliwa na Israel isingeachwa ikapiga na kuua na kugaragaza kila siku iwe ni kwa sababu yoyote ile iliyowaingiza vitani.
Hata kama imekwenda Gaza kulipiza kisasi kwa kuvamiwa oktoba 7,2023 basi ikiwa haiwezi kuonesha aliyewapiga haipaswi kupiga kila mtu na kuua bla kushikwa mikono.Ubindadamu kama huo huwa unafanyika nje ya uwanja wa vita huku mitaani tunakoishi.Tukiona watu wanapigana na kuleta fujo sana ama sisi au polisi huingia kati na kuwazuia wasiendelee kupigana.Na kama kuna mmoja amekaliwa juu karibu ya kuuliwa huwa tunamshika yule aliyejuu na kumsukuma huko ili asifanye anachoelekea kukifanya na wala hatumuulizi maswali katika hali hiyo.
Kwa Palestina kuna diplomasia nyingi za kinafiki kutoka mataifa ya magharibi ambazo tafsiri halisi ni kuvuta muda ili Israel ikamilishe malengo yake ambayo yamewekwa wazi na Netanyahu kuwa ni mpaka watakapopata ushindi dhidi ya Hamas.
Kila njia moja ya kutafuta ushindi ikishindikana ,Israel imekuwa huru sana kuchagua njia nyengine ipendayo kutafuta ushindi.Baada ya moto wa angani na ardhini ilifuatiwa na njaa na kiu na sasa wanafikiria kutumia mafuriko ya bahari.
Nchi jirani na Palestina zinaweza zikapewa sifa zote mbaya kwa binadamu.Kwanza wamekuwa waoga sana bila sababu za maana.Ni wanafiki kwa upande wa kidini na sifa yoyote nyengine mbaya inayojulikana ni sifa yao. Na hata huo ubindadamu pia umewatka na wameanza kuchukua sifa z kinyama.
Wamewaachia watu wa Gaza wafe kwa njaa na bila ya kushinikiza kupeleka misaada.Huruma na kelele za kutaka misaada isikatishwe kutokana na hali mbaya ya Gaza tunazsikia kutoka kwa watu kama katibu mkuu wa UN na wenzake.
Cha kushangaza ni kwanini Israel haishindi pamoja na kupewa nafasi yote hiyo ya kushinda ikiwemo kupewa nguvu ya kuua kwa njaa.
Kinachofanya Israel isishinde ni rehma za Mwenyezi Mungu pekee.Katika hili kuna ujumbe ambao utawafikia walimwengu baadae.
Kundi jengine la walimwengu ni kama wale wapenzi wa filamu za vita ambao wameamua waachwe wafaidi uhondo wa vita vya kweli badala ya kila siku kuangalia maigizo.
Mpaka sasa hakuna hata taifa moja lilloamua kutoa msaada wa dhati kwa Hamas au angalau kwa wapalestina wengine wanaouliwa na kupiga mayowe mwisho wa sauti zao kuomba msaada.
Na kundi moja pekee lililojitokeza kusaidia kivitendo na kwa juhudi za kweli nalo ni Houth ambao kutokana na unyonge wa hali zao na uduni wa silaha walizonazo msaada wao haujafika kikamilifu kuwasaidia wale walaiozimia kuwafikishia msaada wao.
Hizbollah kikubwa anachokifanya ni kujilinda nafsi yake dhidi ya uchokozi wa Israel.Hawa nao sifa wanayopaswa kupewa ni kwamba hawakubali kukaa kimya au kukimbia wakichokozwa.
Iran nayo imepatwa na hofuj sana na vita hivi kubwa wakiamua kutokwenda mbali ili kulinda rasilimali zao wanazozikuza kwa kasi hasa katika teknolojia za kivita.Na hata wale wanaotamani kuipiga Iran wanaiogopa kwa hilo kwamba wakiamua kupiga ina uwezo wa kujibu.
Ukiacha hapo ni kuwa mataifa mengine ama yameamua kwa makusudi kuiacha Israel ishinde au wamepata uwanja tu wa kuangalia mapambano ya kivita.
Kinachofanya tuseme hivyo ni kuwa katika hali zote basi watu wa Gaza walistahiki kupewa msaada ili wasiendelee kuuliwa na Israel isingeachwa ikapiga na kuua na kugaragaza kila siku iwe ni kwa sababu yoyote ile iliyowaingiza vitani.
Hata kama imekwenda Gaza kulipiza kisasi kwa kuvamiwa oktoba 7,2023 basi ikiwa haiwezi kuonesha aliyewapiga haipaswi kupiga kila mtu na kuua bla kushikwa mikono.Ubindadamu kama huo huwa unafanyika nje ya uwanja wa vita huku mitaani tunakoishi.Tukiona watu wanapigana na kuleta fujo sana ama sisi au polisi huingia kati na kuwazuia wasiendelee kupigana.Na kama kuna mmoja amekaliwa juu karibu ya kuuliwa huwa tunamshika yule aliyejuu na kumsukuma huko ili asifanye anachoelekea kukifanya na wala hatumuulizi maswali katika hali hiyo.
Kwa Palestina kuna diplomasia nyingi za kinafiki kutoka mataifa ya magharibi ambazo tafsiri halisi ni kuvuta muda ili Israel ikamilishe malengo yake ambayo yamewekwa wazi na Netanyahu kuwa ni mpaka watakapopata ushindi dhidi ya Hamas.
Kila njia moja ya kutafuta ushindi ikishindikana ,Israel imekuwa huru sana kuchagua njia nyengine ipendayo kutafuta ushindi.Baada ya moto wa angani na ardhini ilifuatiwa na njaa na kiu na sasa wanafikiria kutumia mafuriko ya bahari.
Nchi jirani na Palestina zinaweza zikapewa sifa zote mbaya kwa binadamu.Kwanza wamekuwa waoga sana bila sababu za maana.Ni wanafiki kwa upande wa kidini na sifa yoyote nyengine mbaya inayojulikana ni sifa yao. Na hata huo ubindadamu pia umewatka na wameanza kuchukua sifa z kinyama.
Wamewaachia watu wa Gaza wafe kwa njaa na bila ya kushinikiza kupeleka misaada.Huruma na kelele za kutaka misaada isikatishwe kutokana na hali mbaya ya Gaza tunazsikia kutoka kwa watu kama katibu mkuu wa UN na wenzake.
Cha kushangaza ni kwanini Israel haishindi pamoja na kupewa nafasi yote hiyo ya kushinda ikiwemo kupewa nguvu ya kuua kwa njaa.
Kinachofanya Israel isishinde ni rehma za Mwenyezi Mungu pekee.Katika hili kuna ujumbe ambao utawafikia walimwengu baadae.