Ni kweli maambukizi na vifo vinavyotokana na corona, kwa mataifa mengi vimepungua sana kutokana na hatua mbalimbali walizochukua. Mataifa kama US, UK, Israel wamefanikiwa sana kupunguza vifo, japo cumulative number ukiangalia utaona inazidi kupanda. Lakini vifo na maambukizi kwa siku vimepungua kwa kiwango kikubwa sana. Marekani vifo vinapungua kwa wastani wa 40% kwa wiki, UK wamepunguza wastani wa cases 28 kwa siku, Israel wamepunguza vifo kwa 94%. Haya Ni mafanikio makubwa sana.
Lakini kinachowasaidia sana ni ukusanyaji wa taarifa. Huu utaratibu wa kwetu wa kutoakupima na kutoa takwimu ni wa kijinga, kishamba na kimbumbumbu kabisa. Takwimu ni muhimu sana katika jambo lolote. Ndiyo zinakupa picha ya ukubwa wa tatizo, ndizo zinakuongoza kuona kama mbinu zako zinafanya kazi au hapana.
Kutokupima na kutokutoa takwimu, kwa kweli kunafanya elimu ya Rais Magufuli kutiliwa mashaka makubwa sana. Ni mwanasayansi gani hajui umuhimu wa utafiti na takwimu? Labda alisoma tu masomo ya sayansi lakini hajui sayansi.