Umenikumbusha kisanga cha Saddam Hussein wakati wa vita ya Ghuba kwa bahati mbaya hata Saddam alikuwa victim wa crafty Russian Military baada ya Rais Bush jr kumuomba mlevi Boris Yeltsin Rais wa Urusi wakati huo kwamba wawapatie jeshi la Merikani CODE za Iraq's integrated air defense systems, Boris Yeltsin akampatia Rais Bush jr secret codes za ADS zilizo nunuliwa na Saddam kutoka Urusi, kilicho fuata ni ADS zote za Iraq zikawa jammed kwa kutumia specialized air force bombers kutoka US Airforce baada ya kutekeleza operation hiyo, ndio baadae zikatumwa squadrons za jetfighters kushambulia jeshi la Saddam Hussein pamoja critical infrastructures za nchni Iraq!!
Nafikiri baada ya Iran kukumbuka tukio la Iraq ndio maana Iran ili-decline offer ya URUSI kunatokana na kusalitiwa na Urusi during Gulf WAR.
Wakati wa utawala wa Yeltsin hali hii ingeweza kueleweka, lakini kufikia mwaka 2008 chini ya uongozi wa Putin na Medvedev Russia ilipaswa kuwa na msimamo thabiti zaidi wa kuimarisha washirika wake, jambo ambalo pia lingekuwa faida ya moja kwa moja kwa ulinzi wao wenyewe.
Mfano halisi ni Iran, tangu mwaka 2007 walikuwa wameingia mkataba wa kupata S-300, lakini kutokana na shinikizo la Marekani na Israel, Russia ilisita hadi 2016 kupeleka mfumo huo, na Iran wakaweka rasmi kazini mwaka 2017.
Hata hivyo, leo hii Iran ndiyo anayetoa msaada wa moja kwa moja kwa Russia kupitia teknolojia ya droni za Shahed, ambazo zimegeuza mwelekeo wa vita na hata Warusi wenyewe wanazitambua kama game changer.
Hii ni picha ya kijasusi na kisiasa yenye tafsiri moja kuu , kwa muda mrefu Russia ilijaribu kutafuta usawa na NATO na Israel, lakini sasa inajikuta inategemea mshirika ambaye waliwahi kumcheleweshea msaada na kum dis appoint , Russia inarudi nyuma na kutafakari kwenye laiti ingesimama thabiti kwa Libya, Iraq, Syria, Iran n.k basi hii vita angekuwa na nguvu zaidi....
Na ndio maana wakati huu wamekuwa haraka sana kupeleka S400 kwa Iran...
Russia ilijiamini kwamba NATO inamugopa na hawawezi siku moja kuthubutu kuivamia Russia au kuisaidia direct Ukraine, tazama sasa NATO wanamtishia kuingiza askari ndani ya Russia....
Kama methali ya Kiswahili isemavyo ,
“Akufaaye kwenye dhiki ndiye rafiki wa kweli.”..