IPTL yazua Kizaazaa Mahakamani

Nilipo ona kuwa boss wa IPTL kasema mkurugenzi wa TRA akamatwe mara moja machozi yalinitoka! Ila baada ya kuoma ameenda mahakamani nikajipa tumaini kuwa hata ikitoka hukumu ya kukamatwa, itakuwa imetolewa na sehemu sahihi,maana kwa upeo wangu mkurugenzi wa TRA ni mteule wa Rais, mtu binafsi kutoa agizo la kumukamata, maana yake ni kuwa wewe una nguvu kuliko Rais,Mungu Inusuru Tanzania
 
Ukisikia serikali kuwekwa mfukoni ndo huko, yaani mshataki anaamua mpaka hukumu ya mshatikiwa wake, only in tanzania.
 
Dah yaani mwizi wa kuku anachomwa moto halafu huyu anaachwa anazurura mpaka anakimbilia mahakamani.....upuuzi wa serikali dhaifu. Hakuna wa kuchukua hatua,wote wezi
 
Mhehe mwenye asili ya Asia aiweka Serikali ya Tanzania mfukoni.
JK kawekwa mfukoni na mhehe ndiyo maana hana say yoyote.
Akimwaga mboga mhehe anamwaga ugali, kwahiyo mpaka sasa mhehe ndiyo Rais wa nchi hii.
 
Tutamuelewa tu Mwalimu Nyerere aliposema kuwa Kiongozi wa umma hatakiwi kuwa Mfanyabiashara. Matokeo yake ndo haya, Wafanyabiashara wenzake hawalipi kodi na pia wanatishia uhai wa Serikali kwa kuwafunga jela watendaji wa Serikali yenyewe.
 
Singa singa alishausoma uwezo na ulafi wa viongozi wa tanzaina siku nyingi, wote kawaweka mfukoni, mkuu wa nchi yupo kimya tangu hii kashfa iibuliwe. Kwa nchi makini wote wahusika wangekalishwa pembeni kupisha uchunguzi kama kasfa zinawahusu au hapana., lakini yeye kimya na wauhumiwa wanapisha air port kwenda kupumzika nchi za watu na kuweka vyema maswala yao, halafu unasema unaongoza nchi. Nchi inaongozwa na matapeli na wezi ikulu ni rubber stamp tu.
 
Singasinga amepeleka madai mahakamani akitaka Mkurugenzi wa TRA akamatwe na kufunguliwa mashtaka na ikibidi afungwe jela miaka mingi sana. Hii imetokea baada ya Mkurugenzi huyo kukusudia kufuta hati ya mauzo ya hisa ya IPTL. Ndipo Singasinga akakimbilia mahakamani kuweka zuio; pamoja na kutaka bosi huyo wa TRA akamatwe mara moja.

Vyanzo: Mwananchi & Mtanzania.

MAONI YANGU
Tutasikia mengi mwaka huu. Tukumbuke kwamba Singasinga aliinunua IPTL kitapeli kwa kutumia nyaraka za kugushi. Ujinga huu unawezekana kwa Tanzania tu--kwamba tapeli na fisadi mkubwa anaweza kuja akatapeli na kuiba mabilioni ya fedha za umma halafu akaiweka serikali mfukoni mwake.

Baba Nyerere uone watawala uliowaacha wanavyotishwa na mafisadi.
:israel:

aliinunua kwa nani kwa njia za kitapeli? mbona hao walioibiwa hawalalamiki badala yake alalamike zitto? Kuna kesi yoyote TANZANIA unayoijua iliyofunguliwa na hao walioibiwa kampuni ya IPTL?
 
inasikitisha sana Raisi kukaa kimya na huyu singasinga anawatisha bure hawezi chochote hii nchi kweli imewekwa mfukoni,angelikuwepo Baba wa taifu huyu angepewa masaa 24 awe ameondoka nchini.kweli sijui serikali ya ccm inakwenda wapi jamani kwa nini tusiamke tufanye kitu?
 
Nadhani kwa utawala wa sheria ambao nchi hii inaufuata Bw. Singh ana haki ya kufungua madai yake mahakamani pale anapohisi kuwa amenyimwa haki zake. Na ndani ya mfumo huo mtu yoyote anakuwa hana hatia mpaka mahakama zinaposema vinginevyo. Hivyo huyo bwana Singh hana hatia kwa sasa mpaka hapo mahakama itakaposema vinginevyo.
 
Namkumbuka sana Nyerere na ile kauli yake ya tajiri moja kuweka serikali mfukoni, ndio haya ya huyu Singasinga wakuu.
Exactly na mimi pia lately nimekuwa nikikumbuka tukio la yule Mgiriki aliyeiambia serikali ya Nyerere kwamba ameiweka mfukoni. Yani ndio exactly walichofanya Rugemalila na Singasinga, wamemwaga mpunga kwa kila waliyedhani ataleta kokolo, kuanzia makatibu wa Rais mpaka makarani wa benki, daaaaah, inasikitisha.
 
Anatoa agizo la mkurugenzi TRA kukamatwa yeye ni nani? Inaoneka kaiweka ikulu mfukoni mwake huyu si bure.
 
Wakuu naomba hizi Hasira tuzihamishie 2015 na mfano uwe s's katika chaguzi za serikali za mitaa.......tumeshalalamika sana khs hiking Chama kilichowekwa mfukoni na Singa Singa s's inabidi tuchukue hatua,atoke Singa Singa na Chama chake.
 
Huyu singasinga ni shida kwa kweli yani anatoa tamko la kukamatwa kwa afisa na yeye mwenyewe kutoa hukumu eti afungwe miaka mingi.......akati mwenyewe amenunua company kimagumashi....
 
Hata ingekua mahakama ya the hague,mahakamani hakunaga siasa,kama hamkujiandaa vyema singasinga lazima awaache keepleft.

Sio kuachwa keepleft tu. Nakuhakikishia IPTL watakapoibuka na kudai bado wao ni wamiliki halali wa hisa za IPTL ni lazima serikali ya nchi hii izirudishe kwake au wazinunue toka kwake kwa hela atakayoitaka yeye. Hisa za kampuni yoyote lazima ziandikishwe nchini kisheria. Sing wa PAP hisa zake hazikusajiliwa hivyo inaonekana hela zililipwa kwa mtu asie husika. Lazima IPTL kisheria ashinde kesi hiyo iwe imefunguliwa mahakama za hapa nchini au za kimataifa.
 
Bosi wa IPTL anakuwa na kibuli kiasi cha kumdharau mkuu wa taasisi ya umma kiasi hiki, Mawaziri na makatibu wanakuwa na kiburi hata kukataa kujiuzuru wakidai mkuu wao ndiye anajua walichokuwa wanafanya na ndiye aweza kuwafukuza!

Je, kuna nini hapa na ni nani kinawapa watu hawa hii jeuri!?

Pengine alishiiriki uteuzi utajuaje??
 
Back
Top Bottom