Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Hapana si kweli, viwanda na mashirika ya umma kunzishwa kwake ilikuwa ni uongozi mbovu wa Nyerere, unaanzisha kiwanda unampa mtu kukiendesha kiwanda hajawahi kuedesha kiwanda hana asili na kiwanda hana asili na mashirika, kwao njaa tupu, ashaum si matusi hata choo kajan kukionea alivyookuja Dar chuoni. Unafikiri kuna kitu kitafanyika hapo?

Alipkuja Mwinyi akasema hakuna tena kutoa ruzuku, haya diyo masali ya huo uozo wa Marehemu Nyerere.

CCM inaongozwa na watu na watu wa awali waliweka misingi mibovu, sasa ule ujamaa wa kuwa kila shirika ni la umma kila kiwanda ni cha umma hakuna tena, au hujamsikia Kikwete?

Hivyo vilivyobaki kuwepo mpaka leo ni maajabu.

kwa maelezo yako haya nyerere pia alikuwa fisadi na mlimbikizaji Mali za umma kisirisiri?
 
aulizwe Jaji Warioba yeye bado yumo ndani ya bodi ya TTCL,kwani yeye ndiye anasimamia share za Salim A Salim. na huyu Omar issa wa BRN kwa kushilikiana na Mo Ibrahim ndio waliazisha celtel na kununua TTCL kwa bei poa
 
Nikiwakumbuka marehemu roho inaniuma sana! Tulikuwa na marehemu aitwaye TANZANIA RAIRWAYS CORPORATION alikuwa na watoto wengi kama Mv Liemba, Mv Mwongozo, Mv Umoja, Mv Victoria na Mv Bukoba! Huyu Mv Bukoba alipoteza maisha yake akitokea Bandari ya KemondoBay May21st,1996 akielekea Mwanza Mjini, na huo ukawa ndio mwisho wake! Pia tulikuwa na watoto 8821-Fullpower aliyetokea CANADA, baadaye akaja mwenzake 8901 kumuongezea nguvu akitokea GERMANY! Huyu 8901 alikuwa na uwezo wa kupandisha Mlima wa Saranda-Manyoni na mabehewa 24 ya abiria peke yake bila kuhitaji msaada wa mwenzake! Mara ya mwisho kumtia machoni alisababisha ajali Igandu-Msagali Juni24th, 2002 akielekea Dodoma! Pia kulikuwa na marehemu aitwaye AIR TANZANIA CORPORATION alikuwa na watoto wengi kama Boeing 737 Serengeti, Kilimanjaro na bila kusahau Boeing 737 Ngorongoro! Huyu Ngorongoro mara ya mwisho kumtia machoni alikuja na jeneza la Baba wa Taifa, Mwalimu J.K.Nyerere akitokea St Thomas, London! Marehemu wote hawa wameuliwa kwa juhudi kubwa na CCM!

oooooh kweli inauma sana kwa chozi LA damu,
 
moja ya tatizo kuu lililokuwa linaitesa hii TRL ni ukwasi uliotawala kutoka kwa viongozi wazembe waliopewa nafasi kuendesha wizara ya mawasiliano na uchukuzi akiwemo prof MWANDOSYA na wengineo waliomtangulia. hawa hawakuwa na uthubutu kama aliouonyesha Dr. Mwakyembe.
mfano hai ni jinsi alivyoweza kuhakikisha shirika linatoka katika usanii wa wawekezaji kutoka india na hatimaye shirika limerudi mikononi mwa wazawa.
na pili ameweza kutekeleza ahadi yake ya kuliinua kwa kuliwezesha shirika kutengeneza miundo mbinu ikiwemo ubadilishaji wa njia ya reli ya zamani na kuweka njia mpya yenye viwango vinavyoendana na wakati.
pia amweza kufanikisha kuingiza locomotive mpya 10 na kukarabati 8 zilizopo kwa kufunga engine mpya. pia ameweza kuingiza behewa za mizigo zisizopungua 40 hivyo kuwezesha sasa shirika kurudi katika hali tunayoitarajia kwa siku chache zijazo. pia amewezesha kuingiza behewa za abiria mpya zisizopungua 20 hii itasaidia sasa kufanya usafiri wa abiria kutoka dar kwenda mikoani kuwa na uhakika na kufika kwa uhakika zaidi.
nadhani kama wewe ndg ni muelewa basi kwa haya aliyoyafanya mwakyembe ni uthubutu aliokuwa nao ndio umewezesha kulikwamua shirika hili.
kuna mengi ameweza kuyashughulikia na kuleta matumaini ikiwemo pia masuala ya bandari zetu hili nalo tumpongeze kwa uthubutu wake wa kushughulikia ufisadi uliolundikana tangu enzi hapo bandarini. tuwe na imani nae tu kwa aliyoweza kuyafanya. tofauti na walio mtangulia hapo awali je unaweza kuniambia ni kipi kilichowazuia wao wasiweze kufanya aliyofanya mwakyembe? kama c uzembe na ubinafsi.

nilimeliona hili mwezi October tanga reli imefanyiwa ukarabati pamoja na garimoshi zake ila headquarters za mkoa ptuuuu mungu atuepushe na hii aibu
 
kwa maelezo yako haya nyerere pia alikuwa fisadi na mlimbikizaji Mali za umma kisirisiri?

Cha kujiuliza ni kwanini alimpeleka waziri wa fedha Amir Jamal (Mhindi wa Morogoro) Uswisi kuwa balozi huko kabla ya kustaafu kwake.

Benki kuu ikachomwa moto na fedha yote ya kigeni humo ndani "ikayeyuka".

Kuna mengi sana ya kujiuliza na kufayiwa utafiti wakati huu wa uwazi.
 
Cha kujiuliza ni kwanini alimpeleka waziri wa fedha Amir Jamal (Mhindi wa Morogoro) Uswisi kuwa balozi huko kabla ya kustaafu kwake.

Benki kuu ikachomwa moto na fedha yote ya kigeni humo ndani "ikayeyuka".

Kuna mengi sana ya kujiuliza na kufayiwa utafiti wakati huu wa uwazi.


Hati nini? Aisee , embu tupe link tusome yasije kuwa ya kusadikika, Kha! kama ni kweli Tanzania hakuna mtu mwema.
 
Serikali iache kujibebesha mizigo isiyo na maana. Kwa kizazi cha Tanzania tulicho nacho leo, aina ya uongozi na sera zinazoongoza nchi hii, haiwezekani, na haitawezekana biashara ya mawasiliano ya simu ifanywe na shirika la serikali... Tunazo kampuni binafsi ambazo zinafanya majukumu yake relatively vyema, ni bora serikali ikajipa fursa ya kushughulikia maeneo mengine muhimu kama elimu, kilimo, afya, nishati na upatikanaji wa maji safi na salama...
Nimelazimika nikucheke :sorry: na kukushangaa. Wewe ni mmoja wa wale wale waharibifu wa mashirika yetu kwa manufaa yako.
Hivi uko Tanzania kweli au asia? maana vyote ulivyovitaja pia vimebinafsishwa wewe vipi? bila shaka wamekubinafsisha na wewe ndio maana wasema kauli tata!
 
Mwalimu aliwaachia Watanzania mambo mengi ya maana ya kuwafanya wasonge mbele kimaendeleo. Kazi zote nzuri zilizofanywa na waasisi wetu zimeuawa, na sasa kuna wanafiki kila siku wanasema hao wazee hawakuifanyia la maana nchi hii.
 
Cha kujiuliza ni kwanini alimpeleka waziri wa fedha Amir Jamal (Mhindi wa Morogoro) Uswisi kuwa balozi huko kabla ya kustaafu kwake.

Benki kuu ikachomwa moto na fedha yote ya kigeni humo ndani "ikayeyuka".

Kuna mengi sana ya kujiuliza na kufayiwa utafiti wakati huu wa uwazi.

Wewe shida yako udini tu!
 
aulizwe Jaji Warioba yeye bado yumo ndani ya bodi ya TTCL,kwani yeye ndiye anasimamia share za Salim A Salim. na huyu Omar issa wa BRN kwa kushilikiana na Mo Ibrahim ndio waliazisha celtel na kununua TTCL kwa bei poa
Ndugu yangu hii mada imekuibua. Tangu mwaka 2007 hadi leo, umeingia hapa na kupost mara 25 hivi. Hii mada, bila shaka imekugusa mno.
 
http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/29397-wafanyakazi-ttcl-wadai-mwajiri-bil-7-8

Tembelea ukurasa hapo juu,TTCL inadaiwa mpaka na wafanyakazi wake mweeeh!!!


ADUI MKUBWA WA TTCL NI AIRTEL
1.tangu aingie ttcl hajawahi kuwekeza hata s
hilingi moja
2.pesa aliyonunua hisa alilipa nusu halafu akarudishiwa na kuanzia celtel kama mali ya ttcl(baada ya muda mafisadi wakaiondosha celtel na kugawana hisa ttcl akabaki yatima na hazina akachukua 40% na celtel 60% huku ttcl ikiambulia malipo kiduchu
3.airtel wamezuia muda mrefu ttcl isikopeshwe ati atakuwa mpinzani wakati airtel ana hisa 35%.wakati ttcl ilikuwa inakopesheka
4.aitel hataki kuondoka mpaka alipwe!! je alipwe nini wakati hakuwekeza hata shilingi!!!!?

Zitto na Makamba kazi kwenu!!!!!!


LOCAL NEWS


TTCL-Airtel blame game takes new twist



TWEET



Details Published on Thursday, 20 November 2014 02:28 Written by SHARIFAH AKIDA of MUM Hits: 816


THE long-drawn-out blame game between Tanzania Telecommunications Company Ltd (TTCL) and Bharti Airtel over shares has taken a new twist with the Telecommunication Services Workers' Union (TEWUTA), threatening to drag the company to the court of law should it fail to abide to the contract they had signed.Bharti Airtel has 35 per cent shares in TTCL while the remaining 65 are owned by the government. TEWUTA also threatened to engage the general public to push Airtel to voluntarily pull out its shares, as it has alleged that company's failure to adhere to the terms of their contracts crippled TTCL's ability to compete.The union's Secretary General, Mr Junus Ndaro, told reporters in Dar es Salaam yesterday that due to the Airtel's breach of contract, TTCL has been underperforming and operating at a loss margin.Mr Ndaro asserted that Bharti Airtel has failed to inject working capital and improve TTCL's operation as it was agreed in their contract signed in 2001 thus making the company's operation even worse."Airtel failed to sufficiently invest in TTCL. It is not even providing opportunity for the company to access loans from financial institutions, all these make the company operate under very minimal capital thus making it fail to stand in the market, which is now marred with stiff competition," he explained.He noted that TTCL does not benefit from this joint venture as it was previously expected. He noted that the deadlock pitting the two sides, which has lasted for more than a year, has stalled TTCL's efforts to implement major business plan or to look for new investors to revive the ailing state-owned telecommunications firm.Mr Ndora, who was flanked with National TEWUTA Chairman Pius Makuke, affirmed that Airtel's failure to pull out its shares from TTCL was a clear indication of sabotage because the former had already issued withdrawal notice since 2012."Since then, Airtel, despite having a small share, has been delaying the talks without genuine reason; this is like sabotage to our company," he charged.Mr Ndaro explained that on February 23, 2001, TTCL sold 35 per cent of its shares to SMI/Detecon.Later on, the company, which was a partnership between the Netherlands-based Mobile System International and DETECON of Germany, used the TTCL business licence to set up Celtel Tanzania.Airtel Public Relations Officer Jackson Mmbando declined comment when contacted on Wednesday.
 
Jinni unalijuwa au unalisikia tu?

Kila ninapojaribu kufikiria kuhusu wewe hata sipati picha,!! Usalama wa taifa,ikulu,takukuru,polisi kijana wa nape(propaganda). Anyway ni mambo ya mtandao ila una walakini kichwani mwako!!! au unafanya makusudi ili kupotosha!!
 
Si huko kwenye ibada zenu kila mtu lazima awe nalo la mahaba na blood suckers(isis, boko haram, Al caeda)

Kila siku tunaona mkitoana mapepo kwenye ibada zenu makanisani, ( mnasukumiwa hapo hapo mapepo halafu mnadanganywa yanatolewa) unafikiri siku hizi mtatudanganya na ma tv yanaonesha kila siku.

Misikitini hatuna upuuzi huo, kwanza utathubutu kuingia huyo jinni muovu? Maawe.
 
Back
Top Bottom