Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Baadhi ya yaliyosemwa na TTCL huko Twitter: "TTCL was essentially discriminated in 2002 when its GSM,spectrum,shares were given to Celtel. We are now fixing this unfavorable decision."
 
Tweet nyingine ya TTCL: " TTCL is technically solvent as goverment her main debtor.If Govt wipes TTCL debt and turn it to equity,the balance sheet will look healthier"
 
Another one: "Government has given back TTCL's GSM spectrum similar to that taken over by Celtel."
 
Conclusion: TTCL ni mhanga wa mbinu chafu za makampuni ya simu na watu wasio waaminifu serikalini. Inaonekana bosi Wa TTCL amechoka na ameamua kufunguka. Ila amechelewa mno kuweka mambo wazi.
 
Nani aliingia mkataba na hao bhat airtell? Sijarlewa vizuri ila hii mikataba mingine hii. Kuna watu wananufaika kabla hawajaingia

Wawakilishi wetu, na kama hujajuwa wenye shares hapo Bharti Airtel wamo mpaka nyota wa sasa Warioba, Salim A Salim na wengine wengi mno!!
 
Kampeni zimeshaanza rasmi

ZIle negative campaigns zimeruhusiwa naona
 
Wawakilishi wetu, na kama hujajuwa wenye shares hapo Bharti Airtel wamo mpaka nyota wa sasa Warioba, Salim A Salim na wengine wengi mno!!

Kuhusu hili naweza kukubaliana na ww kwa asilimia zote maana Mzee waryoba ndiye mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TTCL
 
Toka awamu ya Alli Hassan Mwiny iliamuliwa kuwa shirika la umma lisiloweza kujiendesha lenyewe halitopewa ruzuku.

Wizi, Uzembe, Uvivu, Uongo ndiyo unayapeekea mashirika yote ya umma kufa.

Ukiona lipo ujuwe hilo amma linajiendesha lenyewe au linapewa ruzuku kwa kuwa hakuna mbadala wa mashirika binafsi, mfano TANESCO, kama si kusaidiwa na Serikali lingeshakufilia mbali zamani sana.

Sishangai.

Ni kweli bila ruzuku mashirika mengi yangelishakufa kwa sababu yameingiliwa sana na wakubwa serikalini kuhakikisha yanakufa ili yale yao yanawili. Mbona leo NHC ambalo nalo lilikuwa hoi liko safi? Umesahau tu kusema wanayaua mabwana wakubwa wa ccm. Na hili litaendelea kuwa gumu kwenu kulitamka.
Hivi kwani ni siri kwamba watu walipigia kelele ujinga huu? Hata kule kukubali serikali kutoa mikono kwenye mashirika iliyoanzisha yenyewe ilikuwa ni wazo la kipumbavu.
Nenda nchi zilizoendelea uone kama serikali ujitoa kuendesha mashirika yaliyo na direct effect kwenye social services! Likiyumba tu tayari hua inaingilia! kwetu wakina Mwandosya walihakikisha watoto wao wanapewa scholarship na wezi wale ili wawauzie shirika kitapeli. Serikali haiwezi kujivua kwa hili.
 
Ni kweli bila ruzuku mashirika mengi yangelishakufa kwa sababu yameingiliwa sana na wakubwa serikalini kuhakikisha yanakufa ili yale yao yanawili. Mbona leo NHC ambalo nalo lilikuwa hoi liko safi? Umesahau tu kusema wanayaua mabwana wakubwa wa ccm. Na hili litaendelea kuwa gumu kwenu kulitamka.
Hivi kwani ni siri kwamba watu walipigia kelele ujinga huu? Hata kule kukubali serikali kutoa mikono kwenye mashirika iliyoanzisha yenyewe ilikuwa ni wazo la kipumbavu.
Nenda nchi zilizoendelea uone kama serikali ujitoa kuendesha mashirika yaliyo na direct effect kwenye social services! Likiyumba tu tayari hua inaingilia! kwetu wakina Mwandosya walihakikisha watoto wao wanapewa scholarship na wezi wale ili wawauzie shirika kitapeli. Serikali haiwezi kujivua kwa hili.


= Yanawiri

Hiyo benki uliyoyaja imenawiri baada ya kubinafsishwa ilikuwa hohe-hahe.

Umeshasema nchi zilizoendelea, Tanzania ni nchi iliyoendelea?
 
= Yanawiri

Hiyo benki uliyoyaja imenawiri baada ya kubinafsishwa ilikuwa hohe-hahe.

Umeshasema nchi zilizoendelea, Tanzania ni nchi iliyoendelea?
asante kwa sahihisho. Nimesema NHC sio NBC
Hata hivyo nbc haiendi vizuri kama ilivyokuwa! Ipo ipo tu
 
Kuhusu hili naweza kukubaliana na ww kwa asilimia zote maana Mzee waryoba ndiye mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi TTCL


7098613_orig.jpg images.jpg
 
usiseme imekufa sema imepungua utendaji. kilichokufa hakiwezi hata kupumua.
lkn kwa sasa TRL ule uwezo wake wa zamani umeshatafutiwa ufumbuzi. nimpongeze DR. MWAKYEMBE kwa juhudi na moyo wa UZALENDO aliofanya kuliokoa shirika letu.
matatizo ya nchi hii yanasababishwa na uzembe mkubwa wa utawala dhaifu wa CCM. ispokuwa kuna baadhi ya viongozi wachache wenye uchungu na nchi hii ndio angalao wanaonyesha ujasiri wa kuthubutu kutenda yale ambayo CCM chini ya SERIKALI YAKE inaleta udhaifu wake haswa kwenye maslahi muhimu ya wananchi wa TZ.

Mkuu fafanua vizuri hapo kwenye nyekundu; usiongee kisiasa.

Mwenyewe umekiri kuwa matatizo yanasababishwa na uzembe mkubwa wa utawala dhaifu wa CCM. Sasa unategemea Mwakyembe ambaye pia ni Kada wa CCM afanye miujiza gani kuondoa matatizo ya shirika??!!
 
Conclusion: TTCL ni mhanga wa mbinu chafu za makampuni ya simu na watu wasio waaminifu serikalini. Inaonekana bosi Wa TTCL amechoka na ameamua kufunguka. Ila amechelewa mno kuweka mambo wazi.


Mkuu ni kweli tupu inaelekea management imechoka na izi danadana za airtel imeamua kufunguka uma ujue kinachoendelea hata hii kusema imefilisika ni janja inaelekea ili uma ujue hasa nn kinaendeleaana hapo wimbo mkubwanni airtel atoke na airtel hajawaiwekeza chochote iweje adai ela ili atoke
 
Mkuu ni kweli tupu inaelekea management imechoka na izi danadana za airtel imeamua kufunguka uma ujue kinachoendelea hata hii kusema imefilisika ni janja inaelekea ili uma ujue hasa nn kinaendeleaana hapo wimbo mkubwanni airtel atoke na airtel hajawaiwekeza chochote iweje adai ela ili atoke
Ndio ujinga wa chief magunga akila anakula na mbegu mashirika yote wameyatafuna na kupunguza uwezo wa kuajiri na kukuza uchumi wa nchi badala yake tunatoa ajira na kukuza uchumi wa wengine nyumba za serikali tumeuza za mashirika hivyo hivyo Mpaka kuia tanesco Kama ilivyo TTCL , tbl , tanganyika packers e.t.c
 
Huyu anayeutaka Uraisi ambaye kitabu chake kimetoka juzi, ameshindwa kuifufua hii kampuni ambayo iko direct chini ya wizara yake ni utendaji upi sasa aliofanikiwa mpaka tumkabidhi nchi, wakati TTCL Shirika la kizalendo kashindwa kulifufua linakufa chini yake. Only in Tanzania where mtu anashindwa kabisa kiutendaji halafu anataka tumpromote mpaka Urais. Mafisadi wamefanikisha azma yao ya kuua shirika la kizalendo lilokuwa na mtandao nchi nzima na branch Ofisi karibia kila mkoa na ilikuwa inaajiri watanzania wengi. Inasikitisha sana!!


Source:Habari Leo

Tatizo letu watanzania tunawashirikisha wawekezaji hadi ktk mambo ya msingi na muhimu kwetu,wachina wao hawajawahi binafsisha mashirika yao ya simu hata kuingia ubia na mtu yeyote yule,angalia CHINA MOBILE na CHINA UNICOM hakuna mwekezaji ktk hayo mashirika,hata shirika la reli hawakukaribisha wawekezaji na wamefanya hivyo kutokana na umuhimu wa mashirika hayo ktk usalama wa nchi.sisi watanzania wala hatuoni hayo
 
Serikali iache kujibebesha mizigo isiyo na maana. Kwa kizazi cha Tanzania tulicho nacho leo, aina ya uongozi na sera zinazoongoza nchi hii, haiwezekani, na haitawezekana biashara ya mawasiliano ya simu ifanywe na shirika la serikali... Tunazo kampuni binafsi ambazo zinafanya majukumu yake relatively vyema, ni bora serikali ikajipa fursa ya kushughulikia maeneo mengine muhimu kama elimu, kilimo, afya, nishati na upatikanaji wa maji safi na salama...
 
= Yanawiri

Hiyo benki uliyoyaja imenawiri baada ya kubinafsishwa ilikuwa hohe-hahe.

Umeshasema nchi zilizoendelea, Tanzania ni nchi iliyoendelea?

uliyoyaja ndiyo nini na wewe???
uko bize kurekebisha wengine halafu na wewe unaandika makosa
 
Wawakilishi wetu, na kama hujajuwa wenye shares hapo Bharti Airtel wamo mpaka nyota wa sasa Warioba, Salim A Salim na wengine wengi mno!!
Ni kweli kabisa Celtel,Zain,Airtel ni mali Salim Ahmed Salim anayebisha abishe tuu.Link urafiki wa Mo Ibrahim na Salim
 
Mkuu fafanua vizuri hapo kwenye nyekundu; usiongee kisiasa.

Mwenyewe umekiri kuwa matatizo yanasababishwa na uzembe mkubwa wa utawala dhaifu wa CCM. Sasa unategemea Mwakyembe ambaye pia ni Kada wa CCM afanye miujiza gani kuondoa matatizo ya shirika??!!

moja ya tatizo kuu lililokuwa linaitesa hii TRL ni ukwasi uliotawala kutoka kwa viongozi wazembe waliopewa nafasi kuendesha wizara ya mawasiliano na uchukuzi akiwemo prof MWANDOSYA na wengineo waliomtangulia. hawa hawakuwa na uthubutu kama aliouonyesha Dr. Mwakyembe.
mfano hai ni jinsi alivyoweza kuhakikisha shirika linatoka katika usanii wa wawekezaji kutoka india na hatimaye shirika limerudi mikononi mwa wazawa.
na pili ameweza kutekeleza ahadi yake ya kuliinua kwa kuliwezesha shirika kutengeneza miundo mbinu ikiwemo ubadilishaji wa njia ya reli ya zamani na kuweka njia mpya yenye viwango vinavyoendana na wakati.
pia amweza kufanikisha kuingiza locomotive mpya 10 na kukarabati 8 zilizopo kwa kufunga engine mpya. pia ameweza kuingiza behewa za mizigo zisizopungua 40 hivyo kuwezesha sasa shirika kurudi katika hali tunayoitarajia kwa siku chache zijazo. pia amewezesha kuingiza behewa za abiria mpya zisizopungua 20 hii itasaidia sasa kufanya usafiri wa abiria kutoka dar kwenda mikoani kuwa na uhakika na kufika kwa uhakika zaidi.
nadhani kama wewe ndg ni muelewa basi kwa haya aliyoyafanya mwakyembe ni uthubutu aliokuwa nao ndio umewezesha kulikwamua shirika hili.
kuna mengi ameweza kuyashughulikia na kuleta matumaini ikiwemo pia masuala ya bandari zetu hili nalo tumpongeze kwa uthubutu wake wa kushughulikia ufisadi uliolundikana tangu enzi hapo bandarini. tuwe na imani nae tu kwa aliyoweza kuyafanya. tofauti na walio mtangulia hapo awali je unaweza kuniambia ni kipi kilichowazuia wao wasiweze kufanya aliyofanya mwakyembe? kama c uzembe na ubinafsi.
 
..bila kumsahau Waziri William Kusila.

..Mzee Ole Kambainei[director tcra] alipinga kuuzwa kwa TTCL, matokeo yake akafukuzwa kazi na William Kusila.

cc Sangarara, Kimweri

Kwe kweli shirika hili liniuma sana kwani tulipoteza vibarua vingi kwa kupigwa chini na wazungu ambao walijifanya wanaliendeleza kumbe wanaliaribu, kama unakumbuka enzi za Director of Information systems alikuwa Katakweba kitengo hicho alikiweza sana alikishirikiana na mama Mmari hawa viongozi walipigana chini juu hisa siziuzwe Celtel Dr. Kilimbe akagoma na kuwazawadia hizo hisa ambazo nazo serikali ilizichukua, kundi hili la mkapa lilkuwa hatari sana ni mfilisi wa nchi kwa ngongo wa ubinafsishaji, mimi nikisika mtu anamsifia Mkapa nataka hata nimrushie vima anuke mwili mzima kwa aibu. Ukitafuta Gazeti la MBIU la TTCL mwaka 2002 utaona mazambi mengi ya kujiuzia majengo ya TTCL na Celtel kutumia majengo ya TTCL na baadhi ya mitambo, hata sasa hivi walikuwa bado wanatumia nguzo za minara ya TTCL.
 
Back
Top Bottom