Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Inasikitisha sana: TTCL Yafilisika Rasmi

Toka awamu ya Alli Hassan Mwiny iliamuliwa kuwa shirika la umma lisiloweza kujiendesha lenyewe halitopewa ruzuku.

Wizi, Uzembe, Uvivu, Uongo ndiyo unayapeekea mashirika yote ya umma kufa.

Ukiona lipo ujuwe hilo amma linajiendesha lenyewe au linapewa ruzuku kwa kuwa hakuna mbadala wa mashirika binafsi, mfano TANESCO, kama si kusaidiwa na Serikali lingeshakufilia mbali zamani sana.

Sishangai.

Kuna uwezekano sera ya ubinafsishaji wa mashirika ya umma ni moja ya chachu ya kufilisika na kufa kabisa kwa taasisi hizi...

Wajanja wanatumia mwanya huo kuyumbisha taasisi hizi walau zionekane hazina mchango kwa pato la taifa, baada ya hapo shirika linauzwa bei chee kwa wajanja...
 
Mark Mwandosya ndo ameiua TTCL,haya yanayotokea sasa TTCL hayana tofauti na kisa cha TANESCO/IPTL
 
Mark Mwandosya ndo ameiua TTCL,haya yanayotokea sasa TTCL hayana tofauti na kisa cha TANESCO/IPTL

IPTL/TANESCO NI MAUZAUZA YA KIKWETE,
BHARTI/TTCL NI MAKANDOKANDO YA MARK MWANDOSYA.
 
Tatizo kuu hapo ni mikataba tu, hawa wahuni walifanya ujanja wa kununua hisa TTCL ili kutumia miundombinu yake kwa kuikuza Celtel.
Fikiria walitumia minara ya TCCL na kuwafanya wapatikane nchi nzima, na ofisi zao zikawekwa kwenye kiwanja cha TTCL.
Sasa wameshakuza Simu zao za mkononi na wanajitegemea hawataki tena TCCL ifufuke kwa sababu wanajua itakuwa mshindani wao mkubwa kibiashara.
Inasikitisha sana kuona mali za umma zinafanywa ni shamba la bibi na hawa raia wa kigeni kwa kuwatumia viongozi tuliowapa dhamana ya nchi yetu.
Ova
 
Dr. Kazaura alileta matumaini hapa mwishomwisho, lakini naona kuna maradhi ya kimsingi hapo ambayo hayawezi kubadilishwa na mtu mmoja hata awe na ujuzi gani.

Bahati mbaya hili litakuwa kwenye rekodi yake kama CEO aliyeipitisha TTCL kwenye kuwa mufilisi.
 
Nimesikitika sana kwa shirika hili kufilisika.

Nimekuwa mteja mwaminifu wa TTCL kwa muda mrefu. Ila hapa mwishoni kwa kweli nili-notice kitu. Huduma ya internet broadband ikawa inasumbua sana, mpaka nimeiacha jumla.
 
Kampuni za serikali zote hazina faida zaidi ya kuchukua pesa za wananchi na kunufaisha wachache ni bora kampuni zote za serikali NHC, ATC etc zifungwe na wananchi wa kawaida wauziwe hisa au pesa irudishwe hazina. Wakiziuza wasiuze nyumba badala yake nyumba wapewe wafanyakazi wa serikali ziwe nyumba za serikali. NHC inaongeza bei ya nyumba kinyemela wanapata maeneo ya bure lakini wanauza Apt ya vyumba viwili milioni 250 pale Morocco! wakati gharama ya kutengeneza ni milioni 30-40 inafanya soko liaribike
 
Tanzania sijui tuna laana kutoka kwa nani...., yaani ukifanya biashara na Serikali lazima uwe tajiri kuliko serikali yenyewe,....Watanzania wote bila kujali itikadi zetu tuanze kujikomboa kifkra then tutajua tujitawale vipi, zaidi ya hapo nikukaa mkao wa kuliwa tu kila kukicha.
 
Tumechoka na taasisi ya urais kuwa na mwekezaji mzawa, sasa tuanze kufikiria kutafuta mwekezaji mgeni ashike taasisi hii ya urais nchi isonge mbele. Makampuni ya serikali ni hasara tu na kufilisika hakuna inayoendeshwa kwa faida. TRL mmh. Tutafute mwekezaji
 
Dr. Kazaura alileta matumaini hapa mwishomwisho, lakini naona kuna maradhi ya kimsingi hapo ambayo hayawezi kubadilishwa na mtu mmoja hata awe na ujuzi gani.

Bahati mbaya hili litakuwa kwenye rekodi yake kama CEO aliyeipitisha TTCL kwenye kuwa mufilisi.
Mkuu take it from me. TTCL haijafilisika na sasa wako kwenye mkakati kuanzia April kuvamia soko la GSM badala la hili la sasa la CDMA. Tuliza ball endelea kuwa na imani na Kamu.Haya mengine mbona hakuna jipya? Kwani kufilisika kwa TTCL kumeanza kutajwa leo? Juzi juzi hapa wakati Zitto ana mgogoro na chama chake walienda kina Filikunjombe. Nao wakaja na porojo hizi hizi. Hatujui walienda kuiambia nini serikali. Zitto nae anakuja na yake....TTCL is there to stay. Misukosuko iliyoipata ni mizito ingeshakuwa marehemu kitambo.
 
For the most part it is the problems everywhere in governmet owned business
  • Shirika alijawekeza kwa muda mrefu kuboresha mitambo na huduma ili kushindana; iwe aiport, bandari au kwengine
  • Taasisi zingine za serikari azilipi madeni yake kwakutumia huduma
  • Shirika alijaweza adapt mazingira ya ushindani na subtitute services za hudama za simu au watu kutua uwanja mwengine wa ndege
  • Shirika alina mikakati thabiti ya marketing and pricing inataka serikari iwawekee sera favourable ili kushindana
  • Shirika alijaweza ji-position sawa sawa sokoni na huduma zao
  • Serikari imelamba kitengo cha faida cha TTCL on the 40 percent ya hisa za Certel Tanzania hivyo kuinyima faida/kipato za kuboresha shirika ilhali serikari inachukua kodi bado TTCL

To name a few of mentioned problems tatizo sio serikari pekee tatizo ni management for the most part, sera za serikari na jinsi tunavyoendesha mambo ya kibiashara. Hata sijui biashara watu wamesoma wapi lakini ni kwamba wafanya biashara wengi na biashara nyingi Tanzania hazina ubunifu zaidi ya sector ya kampuni binafsi kwenye simu but then this are owned by other international conglomerates.

Kikwetu people look at the existing opportunities and aim to exploit the easiest strategy of entry sasa basi muwekee ushindani utasikia serikari lazima idhibiti bei za fulani, serikari lazima inikopeshe, serikari inipe ardhi bure etc to do with nagging the government lakini huwezi kusikia wakilaumu ukosefu wa mbinu za kibiashara.

Maana hata hapo serikari ikitoa hizo hela inahakikishiwa vipi TTCL kuweza kushindana huko baadae kwenye soko ambalo kuna established players already na wamejishusha sana bei kutokana na ushindani ilihali menejiment TTCL ndio kwanza inaomba wateja wawasaidie kununua bidhaa zao hata kama ni gharama zaidi isn't that wierd and this man still holds his postion: only in Tanzania.
 
Katika nchi yetu kuna matatizo ya utendaji na utaalamu binafsi wa watendaji,
Si vibaya kwa mashirika yetu kama haya tukatafuta wataalam wazoefu toka nje ili kuyainua na kusimamia kwa kipindi maalum, rais Moi wa kenya aliweza fanikiwa kwa kuifufua benki ya taifa ya biashshara (KCB) illiyokuwa imependekezwa kufirisiwa kwa kumkabidhi mtendaji mkuu aliyemnunua toka barclays jukumu hilo na sasa kcb hiko kila mahali ndani ya east africa.
 
Katika nchi yetu kuna matatizo ya utendaji na utaalamu binafsi wa watendaji,
Si vibaya kwa mashirika yetu kama haya tukatafuta wataalam wazoefu toka nje ili kuyainua na kusimamia kwa kipindi maalum, rais Moi wa kenya aliweza fanikiwa kwa kuifufua benki ya taifa ya biashshara (KCB) illiyokuwa imependekezwa kufirisiwa kwa kumkabidhi mtendaji mkuu aliyemnunua toka barclays jukumu hilo na sasa kcb hiko kila mahali ndani ya east africa.
Mkuu labda tukodishe na viongozi wa serikari pia maana wote wanahusika kwa uzembe uliopo.

Serikari kwa kutokuja na sera mbadala za mashirika yake na kutokujua purpose ya mashirika yake hili iimize wananchi kupata huduma zile zinazolengwa na faida za muda mrefu.

Halafu kuna swala la kuteuliwa bila ya usaili sahihi, hivi kweli hadi tukodieshe mgeni kuona washindani wanafanya nini?
Mbona marketing mix ya private hiko wazi, kuna swala la aina tofauti ya bundle kufikia wateja tofauti, price plans tofauti, intorduction of new lines of businesses kama money tranferm, maduka ya simu na bidhaa zingine za sector yote kwenye kuongeza faida zaidi ya kutegemea hela ya huduma za simu ambapo kuna ushindani mkubwa tayari.

Sasa wewe miaka yote hupo na strategy hile hile ya 'catch-all' na mazingira ya biashara yana badilika mbele ya macho yako uoni wenzio wanachofanya, kwa maana hiyo wataalamu wa biashara wapo hapo hapo bongo. isipokuwa serikari aina dira na miradi yake na wala aijali inaendeshwa vipi, kufikia malengo gani ndio maana yeyote anaweza jiendeshea kampuni la serikari ya Tanzania ni uozo simply from the owner; watakwambia tunataka yajiendeshe kwa faida na yalipe kodi kubwa kuongeza pato la tiafa bila ya kujali athari za raia wao.

I tell you nchi hii inahitaji raisi kijana changamoto kubwa ni uzalendo wa taifa naona kama vile wanapwaya vijana wote ulikilinganisha na wazee viewpoint zao katika mchakato wa katiba umetoa mashaka. Binafsi nina imani na wasira, lowassa, sitta, membe na wazee wengine wa CCM kwa standpoint zao kuliko vijana walizozionyesha pale misingi ya taifa ilipochokozwa, but then they lack creativity something which is much needed at the moment and way forward.
 
Tatizo kuu hapo ni mikataba tu, hawa wahuni walifanya ujanja wa kununua hisa TTCL ili kutumia miundombinu yake kwa kuikuza Celtel.
Fikiria walitumia minara ya TCCL na kuwafanya wapatikane nchi nzima, na ofisi zao zikawekwa kwenye kiwanja cha TTCL.
Sasa wameshakuza Simu zao za mkononi na wanajitegemea hawataki tena TCCL ifufuke kwa sababu wanajua itakuwa mshindani wao mkubwa kibiashara.
Inasikitisha sana kuona mali za umma zinafanywa ni shamba la bibi na hawa raia wa kigeni kwa kuwatumia viongozi tuliowapa dhamana ya nchi yetu.
Ova

Wameua viwanda vyetu vyote, sasa wamehamia kwenye mashirika ya umma! Wameua TANZANIA RAILWAYS CORPORATION ambalo lilikuwa mkombozi kwa ajirga za watanzania, wakawapa Magabachori! Wakaua AIR TANZANIA CORPORATIONI na ndege zake hazijulikani walikozipeleka, sijui zilikumbwa na tufani ya chuma chakavu! Nazikumbuka vizuri zile Boeing737 Serengeti, Kilimanjaro na Boeing737 Ngorongoro hizi zote hazijulikani zilipo kutokana na sera mbovu za CCM!
 
Reli liko hai wakati usafirishaji wa mizigo umeshuka toka tani zaidi ya milioni moja miaka kabla ya 2007 hadi tani 150,000 sasa??!!

Hebu tuambie ni kazi gani zinaendelea?!

usiseme imekufa sema imepungua utendaji. kilichokufa hakiwezi hata kupumua.
lkn kwa sasa TRL ule uwezo wake wa zamani umeshatafutiwa ufumbuzi. nimpongeze DR. MWAKYEMBE kwa juhudi na moyo wa UZALENDO aliofanya kuliokoa shirika letu.
matatizo ya nchi hii yanasababishwa na uzembe mkubwa wa utawala dhaifu wa CCM. ispokuwa kuna baadhi ya viongozi wachache wenye uchungu na nchi hii ndio angalao wanaonyesha ujasiri wa kuthubutu kutenda yale ambayo CCM chini ya SERIKALI YAKE inaleta udhaifu wake haswa kwenye maslahi muhimu ya wananchi wa TZ.
 
Dr. Kazaura alileta matumaini hapa mwishomwisho, lakini naona kuna maradhi ya kimsingi hapo ambayo hayawezi kubadilishwa na mtu mmoja hata awe na ujuzi gani.

Bahati mbaya hili litakuwa kwenye rekodi yake kama CEO aliyeipitisha TTCL kwenye kuwa mufilisi.

Kama una heshima yako duniani CCM na serikali yake strictly ni sehemu ya kustaafia. Unless ukubali kusimama peke yako.
 
Back
Top Bottom