Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,503
- 51,098
Nastaajabu kuona chama cha CHADEMA ambacho kinajinasibu kuja kushika dola kinashindwa kuipa shinikizo ENDELEVU serikali ya CCM ifanye uchunguzi kujua ni kitu gani kilimsibu kada wao Ben Saanane. Hili linastaajabisha kwa sababu Ben Saanane alikuwa ni mwanachama, tena kada nguli wa chama, na si hivyo tu bali masaidizi wa Mwenyekiti.
Ukimya huu wa Chadema unatuma meseji kwa wanachama na wananchi kuwa "Unaweza kutumikia chama, lakiniyakikufika, unabaki peki yako na chama wala hakitakusemea, wala kukupigania".
Haiwezekani chama makini kikaliacha hili jambo hivihivi. Liko wapi shinikizola chama kutaka kuundwa tume kuhusu makada wao walipotezwa na kuuawa mpaka sasa?.
Kuna yule kada wa Chamdema kiongozi wa Kata ya Hananasif, bwana Michael. Iko wapi Zeal ya chama kutaka kujua ni maswahibu gani yamewafika makada wao?.
CHADEMA INAO WAJIBU WA KULISHIKIA BANGO SUALA LA BEN SAANANE. La sivyo kitawezaje kupigania watanzania wote wakati kinashindwa kumpigania kada wake?
Ukimya huu wa Chadema unatuma meseji kwa wanachama na wananchi kuwa "Unaweza kutumikia chama, lakiniyakikufika, unabaki peki yako na chama wala hakitakusemea, wala kukupigania".
Haiwezekani chama makini kikaliacha hili jambo hivihivi. Liko wapi shinikizola chama kutaka kuundwa tume kuhusu makada wao walipotezwa na kuuawa mpaka sasa?.
Kuna yule kada wa Chamdema kiongozi wa Kata ya Hananasif, bwana Michael. Iko wapi Zeal ya chama kutaka kujua ni maswahibu gani yamewafika makada wao?.
CHADEMA INAO WAJIBU WA KULISHIKIA BANGO SUALA LA BEN SAANANE. La sivyo kitawezaje kupigania watanzania wote wakati kinashindwa kumpigania kada wake?