Immanuel Mung'ong'o For BOT GOVERNOR.

Kukamata pabaya anamaanisha JF,

Nia ya Mushi hapa ni kutaka JF iwe matatizoni INGAWA tayari wana JF makini wamemgundua na kumkemea vikali. Yeye amekuja hapa kuvuruga mada za JF kwa floodings na pia kuitisha kuwa watu waingie msituni ili kumwaga damu TZ.

Hii ni plant toka kwa mafisadi wasioitakia Tanzania na JF mema. Amekuja hapa ili kuleta uchochezi na baadaye hii JF ionekane ya watu wanaotaka kumwaga damu Tanzania.

Sisi hatutaki vita Tanzania na Mushi haongei kwa niaba ya JF. Usishangae maneno makali anayotumia.. Huyu ni mtu anayetaka kumwaga damu na wana JF inabidi wamkwepe kama ugonjwa hatari usio na tiba.

Badala ya kumwaga damu...MAFISADI WAKAMATWE NA WAZALENDO WAPEWE NAFASI.
Ni maoni tu.
Wewe unatetea watu ambao ni MAFISADI..Unafikiri watanzania hawaoni hilo?
Ulijaribu jana kule kwenye kamati ya madini.
Na mimi nasema ni heri uwaombe mods wakufungulie ile thread kwani naona sasa ishakuwa VURUGU NA kusabotage maoni na uchambuzi wangu!
Kujaribu kuniingiza matatizoni ili nifungiwe..Na wewe uendeleze propaganda za Killango!
 
Hakuna mambo ya kuchochea vita Tanzania, kama hii ndio nia yako basi hutakiwi hapa JF na Tanzania. Watu kama wewe inabidi mshitakiwe kwenye mahakama za kimataifa kwa kuchochea vita ambazo zimedumaza bara letu la Afrika

Shame on you.

Mkiishiwa na hoja...MWK unajushushia hadi kama hujui...Trust me!
 
Najua misha yake ni safi, msomi, asiyependa MAKUU!
Nina uhakika kuwa hakukubali mambo ya UFISADI..TENA KITENGO ALICHOFANYA KAZI WAKATI WA UFISADI NI KITENGO KILICHOAHUSIKA MOJA KWA MOJA KWENYE EPA!
Huyu bwana HAKUHUSIKA!

Ndullu,Ballali,Body of Directors,DDDD,DF NA wengineo wengi ni watuhumiwa ambao wanataka kusafishwa kwa style ambayo kina IDDI SIMBA WALIVYOSAFISHWA KWA KUCHANGANYWA NA Zitto, NA LOWASSA KWA KUAMBIWA YEYE NI SAFI NA HATA HAKUTAKIWA AJIUZULU!

Hii nchi ina wenyewe huh?

UCHUNGUZI WA WATOTO WA VIGOGO HUKO BOT NAO UWEKWE WAZI...Mapambano yanaendelea!

Alihusika kwa sababu aliona watu wanaiba na yeye akakaa kimya tu.Kwa maana nyingine ni mtu anayekubaliana na wizi. Watu wa namna hii hawtuwataki. Kama we unamuona anakufaa mwambie aendelee kukufundisha hiyo Maths.
 
apart from all that.... jamaa yawezekana ana matatizo makubwa kiakili
kwa sababu hasikilizi, unasema hivi.. anaruka na kile....yeye ana maoni yake na hataki kusikia mtu mwingine anasemaje which is bad.... na character ya aina hiyo yani ni bure kubishana nae kwani hataki kujifunza.... inaelekea he is on one of those episodes. tumsamehe
 
apart from all that.... jamaa yawezekana ana matatizo makubwa kiakili
kwa sababu hasikilizi, unasema hivi.. anaruka na kile....yeye ana maoni yake na hataki kusikia mtu mwingine anasemaje which is bad.... na character ya aina hiyo yani ni bure kubishana nae kwani hataki kujifunza.... inaelekea he is on one of those episodes. tumsamehe

Huyu ni mtu yuko kwenye mission ya kuharibu hili jamvi na mada zinazoendelea hapa kabla ya kufikia nia yake ya kutaka kuitia JF na Tanzania kwenye matatizo.

Mambo ya kuitisha watu kuingia msituni na kumwaga damu ni mambo ambayo anafanya kwa makusudi kabisa huku akijua matokeo yake.

Mtu kama huyu ni wa kuogopwa kabisa na akemewe kwa sauti kali.
 
Huyu ni mtu yuko kwenye mission ya kuharibu hili jamvi na mada zinazoendelea hapa kabla ya kufikia nia yake ya kutaka kuitia JF na Tanzania kwenye matatizo.

Mambo ya kuitisha watu kuingia msituni na kumwaga damu ni mambo ambayo anafanya kwa makusudi kabisa huku akijua matokeo yake.

Mtu kama huyu ni wa kuogopwa kabisa na akemewe kwa sauti kali.

kwa kweli kuna shida hapo... TZ yetu tumezoea amani na huyu anaweza kutuharibia kabisa if we are not careful. Nilikuwa busy na sikuingia JF kwa muda.. nakuja kukuta amefungiwa na the way alivyokuwa anajitia hajui sababu i felt sorry.

He is a good pretender too, kwani hakuhitaji awe refreshed kwa nini amefungiwa alijua, na atafanya tena kwa sababu inaonekana ana mpango wake ambao he will fight to win. mimi sioni sababu ya mabishano in this thread kwa sababu kama yeye alivomfeel jamaa hapo kila mtu ana mtu wake anaemfeel zaidi.... afterall hiyo post anachagua Rais tu na to his knowledge the current BOT boss is the man.. and he shall stay
 
Alihusika kwa sababu aliona watu wanaiba na yeye akakaa kimya tu.Kwa maana nyingine ni mtu anayekubaliana na wizi. Watu wa namna hii hawtuwataki. Kama we unamuona anakufaa mwambie aendelee kukufundisha hiyo Maths.

Kwi kwi kwi,

Nyangumi, hiyo kali kabisa mwanawane....... I love JF
 
kwa kweli kuna shida hapo... TZ yetu tumezoea amani na huyu anaweza kutuharibia kabisa if we are not careful. Nilikuwa busy na sikuingia JF kwa muda.. nakuja kukuta amefungiwa na the way alivyokuwa anajitia hajui sababu i felt sorry.

He is a good pretender too, kwani hakuhitaji awe refreshed kwa nini amefungiwa alijua, na atafanya tena kwa sababu inaonekana ana mpango wake ambao he will fight to win. mimi sioni sababu ya mabishano in this thread kwa sababu kama yeye alivomfeel jamaa hapo kila mtu ana mtu wake anaemfeel zaidi.... afterall hiyo post anachagua Rais tu na to his knowledge the current BOT boss is the man.. and he shall stay

Huyu anafanya makusudi kabisa, nia yake hapa ni kujifanya mpinzani ili aonekane mzalendo (kama anavyojiita) kumbe ni mtu mwenye chuki na nia mbaya kabisa kwa mtandao wa JF na watanzania kwa ujumla.

Mimi namlinganisha Mushi na Charles Taylor wa Liberia kwa jinsi alivyojivika ngozi ya kondoo ili apate upresident na kisha akavuruga west afrika yote kwa vita.

Watu kama hawa ni wakukememewa na kuogopwa kabisa. Hana simile na ya wenzake. Ukisema kitu kidogo yeye anakimbilia kwenye vitisho.. gooooshi!
 
Huyu ni mtu yuko kwenye mission ya kuharibu hili jamvi na mada zinazoendelea hapa kabla ya kufikia nia yake ya kutaka kuitia JF na Tanzania kwenye matatizo.

Mambo ya kuitisha watu kuingia msituni na kumwaga damu ni mambo ambayo anafanya kwa makusudi kabisa huku akijua matokeo yake.

Mtu kama huyu ni wa kuogopwa kabisa na akemewe kwa sauti kali.

Yuko kwenye mission ya kuingiza Tanzania kwenye matatizo kivipi? Kwenye hii thread ni wapi jmushi amesema watu waingie msituni? Acheni kuchanganya ishu! Pia kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake, kama maoni yake hayana kichwa yatakufa yenyewe hakuna u-dictatorship hapa.
 
Wale wasipamini kuwa kuna mbinu za kuufuta ushahidi wa EPA na kusafishana wasome hii...


Mafisadi EPA wafanya vikao

2008-06-23 12:26:48
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Siku chache baada ya Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Bi. Anne Kilango Malecela, kuwaasa wabunge wenzake kuwa kitu kimoja katika kuwabana mafisadi waliochota fedha za Benki Kuu Tanzania (BoT), kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), kuna taarifa kwamba, watuhumiwa hao wa ufisadi nao kwa upande wao, wamekuwa wakikutana kupanga mikakati ya pamoja ya namna ya kulizima suala hilo, Nipashe imebaini.

Habari za uhakika ambazo gazeti hili limezipata kutoka vyanzo mbalimbali vya kuaminika zimeeleza kwamba, mafisadi hao wamekuwa wakikutana mara kwa mara katika moja ya hoteli maarufu mjini hapa ambapo pamoja na mambo mengine, hupanga namna ya kujinasua na kadhia hiyo.

Kwa mujibu wa habari hizo, mafisadi hao wamekuwa wakionekana nyakati za usiku baada ya vikao vya Bunge katika hoteli hiyo ili kujadili masuala mbalimbali lakini kubwa likiwa ni suala la wao kuhusishwa na tuhuma za kuchota Sh. bilioni 133 za EPA pamoja na kashfa ya zabuni ya kampuni ya Richmond.

``Mara kwa mara wamekuwa wakikutana katika hoteli hiyo, kwa ujumla huonekana wakijadili masuala mazito mno, bila shaka ni la wao kuhusishwa na ufisadi,`` kilibainisha chanzo hicho ambacho pia hupendelea kufika katika hoteli hiyo ya kifahari kwa lengo la kujipatia chakula na vinywaji.

Chanzo hicho kilifafanua kuwa, kuhusishwa kwao na kuzungumzia sakata la ufisadi, kunatokana na ukweli kwamba, vigogo hao ni miongoni mwa watuhumiwa wakubwa wa suala hilo.

``Hapana shaka kwamba vigogo hao hujadiliana suala la ufisadi kwani ni miongoni mwa watuhumiwa wa sakata hilo na hupenda kukutana wao tu na kila anayewaona, kwa kweli huwatilia mashaka wanachokijadili,`` chanzo hicho kilizidi kueleza.

Wiki iliyopita wakati akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 kama ilivyowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mustafa Mkulo, Mbunge wa Same Mashariki, Bi. Kilango alitoa wito kwa wabunge wenzake kutokuwa waoga katika kuwakemea mafisadi wanaotuhumiwa kuchota fedha za EPA.

Mbunge huyo machachari, alisema yeye binafsi yuko tayari kufa akitetea ukweli na haki na kujifananisha na mwanafalsafa wa Kigiriki, Socrates ambaye alisema pia alipoteza maisha kutokana na kusimamia ukweli na haki.

Siku iliyofuata, Mbunge wa CCM (Viti Maalum), Bi. Anna Abdallah kwa kile kilichotafsiriwa na baadhi ya wachunguzi wa masuala ya siasa, kuwa ni kujibu kauli ya mbunge mwenzake, alisema kimsingi hakuna mbunge yeyote anayeogopa kulijadili suala hilo.

Bi. Abdallah alisema kila mbunge yuko tayari kupigia kelele uovu huo isipokuwa wanachotofautiana na namna ya kuwasilisha ujumbe huo ndani ya Bunge.

``Baadhi ya wengine wanalisema kwa madoido lakini wengine tunalisema kwa upole, lakini lengo letu sote ni moja na hakuna anayeogopa,`` alisema.

Lakini, akihitimisha mjadala wa wabunge kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya serikali, Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mkulo alisema fedha za EPA hazikuwa za serikali wala BoT bali zilikuwa za wafanyabiashara mbalimbali.

Bw. Mkulo alisema hata hivyo, wafanyabiashara hao kwa sasa ama wamekufa au wako nje ya nchi.

Kauli hiyo ya Waziri, ilionekana kuwashtua baadhi ya wabunge hasa wa kambi ya upinzani ambao pia imedaiwa kwamba, wanajipanga kikamilifu kulizungumzia suala hilo bungeni kwa mapana zaidi katika hotuba ya Waziri Mkuu inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni leo.

Kikao cha Bunge la Bajeti kinaendelea tena leo mjini hapa baada ya mapumziko ya mwishoni mwa wiki.

Baada ya wabunge kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2008/09 Ijumaa iliyopita, leo asubuhi, kitaanza kipindi cha maswali na majibu na baadaye kufuatiwa na hotuba ya Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake kwa mwaka ujao wa fedha wa 2008/09.

Kama ilivyokuwa kwa hotuba ya Waziri wa Fedha na Uchumi, pia hotuba ya Waziri Mkuu itajadiliwa kwa siku tano kuanzia leo hadi Ijumaa ijayo.

Wakati huo huo, Simon Mhina anaripoti kuwa Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amedai kwamba kwa kushirikiana na baadhi ya wabunge, wanajiandaa kutaja hadharani majina ya mafisadi waliochota fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Alidai kuwa wengi wao ni vigogo wanaokiunga mkono Chama Cha Mapinduzi.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Nipashe mwishoni mwa wiki iliyopita, mwanasiasa huyo alisema wanachosubiri sasa ni kuipa serikali muda wa kuweka bayana watu wanaodaiwa kurejesha fedha hizo.

Hata hivyo, Mchungaji Mtikila alidai kwamba hakuna mtu yeyote aliyerejesha fedha hizo, kama serikali inavyotangaza.

``Hakuna fedha yoyote ya EPA ambayo imesharudishwa, maneno ya Waziri wa Fedha na Uchumi kwamba watu wanarejesha fedha, ilikuwa ni aina nyingine ya ufisadi wenye lengo la kuwalinda,`` alidai.

Alizidi kudai kwamba kwa mujibu wa orodha aliyonayo ya waliochota fedha za EPA kinara wao wamemgundua kuwa ana hati mbili za kusafiria.

Alisema fisadi huyo ambaye ni miongoni mwa vigogo matajiri wanaoisaidia CCM, licha ya kumiliki hati ya kusafiria inayomuonyesha kwamba ni Mtanzania, lakini anayo nyingine inayomtambulisha kwamba yeye ni raia wa Iran.

Alisema kigogo huyo mwenye asili ya Kiasia licha ya kwamba anajitapa kuwa ni Mtanzania, lakini wazazi wake wote wawili, hadi sasa wanaishi Iran.

``Ngoja tuangalie kwamba kwa siku mbili hizi serikali itasemaje, vinginevyo sisi tumejiandaa kutaja hadharani majina yote ya wahusika wa EPA, hakuna atakayesitirika wala wasijidanganye,`` alidai Mchungaji Mtikila.

Mwanasiasa huyo alisema moto aliouwasha Mbunge wa Same Mashariki, Bi. Anne Kilango Malecela, hauwezi kuzimika kwa hoja nyepesi za vigogo wa CCM ama kwa vitisho vya wabunge wenzake.

Mchungaji Mtikila alisema kauli za Bw. Mkulo kwamba fedha za EPA sio za serikali na kwamba wanajiuliza kuwa watazifanyia nini, inasikitisha na inalenga kuwatetea waliozipora.
  • SOURCE: Nipashe
Tuma Maoni Yako
 
Yuko kwenye mission ya kuingiza Tanzania kwenye matatizo kivipi? Kwenye hii thread ni wapi jmushi amesema watu waingie msituni? Acheni kuchanganya ishu! Pia kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake, kama maoni yake hayana kichwa yatakufa yenyewe hakuna u-dictatorship hapa.

Kwa hiyo na wewe unataka kuniamulia mimi cha kusema hapa? Mimi nimesema yale ambayo Mushi ameyasema hapa JF. Je una tatizo na hilo mkuu?
 
Hapa JF ni kama kokoro.Utakuta kila aina ya watu.Tunasoma na tunaelewa .Kwenye kokoro hilo kuna watu kila namna wenye mentality tofauti.

Katika kupekecha ndipo unapoweza kujua nani hapa kama Charles Taylor na nani kama Kingunge...

Nimefurahi na Mkuu mmoja aliyetaja kuwa anaye appoint Governor ni Rais.Sasa hizi campaign za nini?
 
mushi unakosea kumpigia mtu kampeni wakati hakuna hata nafasi wazi huko bot.
nafikiri ungefanya kazi ya kumuainisha gavana wa sasa ana ubaya gani na kwasababu gani na gani ili shinikizo la kumfanya aondolewe kwenye wadhifa huo.
 
Kwa hiyo na wewe unataka kuniamulia mimi cha kusema hapa? Mimi nimesema yale ambayo Mushi ameyasema hapa JF. Je una tatizo na hilo mkuu?

Sina muda wa kukuamulia nini useme mkuu. Ila tu nilidhani unachanganya ishu. Kwenye hii Thread jmushi hakuchochea watu waende msituni. That is my point!
 
Kama alikaa kimya wakati wizi unatokea na kuendelea BOT naye ni fisadi tuu...Na kusema kuwa alikaa kwenye position ambayo angeweza kuiba who knows labda naye alikuwa mmojawapo ya waidhinishaji
 
Kama alikaa kimya wakati wizi unatokea na kuendelea BOT naye ni fisadi tuu...Na kusema kuwa alikaa kwenye position ambayo angeweza kuiba who knows labda naye alikuwa mmojawapo ya waidhinishaji

Mkuu, hili ni swali ambalo limeulizwa hapa na kwa jinsi majibu yanavyotolewa na mtoa hoja, sioni kama litajibiwa.
 
Kwa kweli Mushi nashindwa hata kuelewa hii topic ya Ugavana umeifikiriaje...! Kani uteuzi wa gavana wa sasa umetenguliwa kama ilivofanyika kwa Balali? au kuna tangazo la kazi ya gavana limetoka? mi naona hoja yako ni very premature, inconceived and irrelevant at this moment.

By the way vigezo ya mtu kuteuliwa gavana ni hivi hapa: Kutoka sheria ya Bank of tanzania Act, 2006

8.–(1) There shall be appointed by the President a Governor who
shall, unless he dies or resigns or vacates or is removed from his office
for good cause or is disqualified, hold office for a period of five years and
shall be eligible for a re-appointment.
(2) No person shall qualify to be appointed as a Governor unless he–
(a) holds a university degree;
(b) has not less than fifteen years experience in the fields of economics,
banking, accountancy or finance or law;
(c) has been in senior managerial positions in the government
departments or institutions, private institutions or international
organizations; and
(d) has not been appointed and served as the Governor for two
Consecutive term.
(3) There shall be appointed by the President three Deputy Governors
who shall, unless one dies, resigns, vacates or is removed from office for
good cause or is disqualified, hold office for a period of five years and be
eligible for re-appointment for a further term of five years only.
(4) The appointment of the Deputy Governors shall be made on the
basis that at least one of the appointees hails from either side of the
United Republic.



Kwanye hicho kifungu hamna mahali panapotaja ucha mungu wala uwezo wa kidini. Lasivyo tungeteua maaskofu na mashehe wawe magavana.

Pili, swala la kwamba kasoma Cambridge is irrelevant, inamaaninisha waliosoma vyuo vingine digree zao hazitambuliki ili kuopewa madaraka serikalini? Hivi unahabari Mheshimiwa Chenge amesoma sheria Harvard University? unaona amelifanyia nini Taifa?

Bwana Mushi think twice before you put ana argument in this forum kaka
 
Its all about religion. Thats what I see here. Guys prove me wrong, anyway ni mtazamo tu

Ni kweli sasa wameigeuzia udini!
Sasa kuwa na dini flani ama flani kama kuna determine nafasi zetu za kazi na wala si qualifications...Basi tuna shida!
 
Viongozi Wa Juu Wa Taasisi Zetu Nyeti Za Taifa Walishiriki Kimamilifu Kuiuza Nchi...hawafai!
Ushahidi Upo!
Washughulikiwe...na Nchi Ipewe Wananchi!
 
Back
Top Bottom