I'm Confused, Niolewe ama niendelee kumsubiri?

I'm Confused, Niolewe ama niendelee kumsubiri?

kikubwa kilichopo huyu dada hamuamini huyo anetaka wazae, na mm ntamshauri tu akae chin amchunguze akiemkubali kuolewa nae akiridhika sawa aolewe zinaa s nzuri ukiendekeza kama anajiona anastahili kua mke wa mtu aolewe hata hivo maisha yajayo hatujui yatakavokua anaweza wakataa wote wanaomposa kesho na kesho kutwa akose hata wa kumdanganyia kumuoa yote kwa yote yanawezekana
Ila sijamshauri aolewe na mtu aloibuka tuu huko na kuleta posa!
Ndoa nyingi tunazoona zina migogoro na kuvunjika ni sababu ya wadada kuwa desperate kuolewa!
Tusijisahau kiasi hicho, kwamba kuvaa gauni jeupe ndo fahari! Kuna zaidi ya gauni.

Kama Mungu kampangia mume wake yupo tuu! Miaka 23 sio ya kumfanya aolewe na mtu ni mtu!
 
Salaam wakuu, moja kwa moja kwenye mada, naomba msaada wa kimawazo juu ya hili nalopitia wana jamvi wenzangu. Mm ni msichana miaka 23, nimekuwa kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa, (Boyfriend & Girlfriend, kwa maana kwamba sio mahusiano rasmi). Kiukweli nampenda sana huyu mkaka, ananipenda pia anavosema. Lakini tatizo linakuja kwenye Commitment. Mwenzangu anatamani mtoto kabla ya ndoa na mm nataka tupite njia za halali Nusra (Ndoa) kwanza ndo mengine yafuate. Wamekuja vijana watatu kwetu kuniposa sikuwakubalia nikiamini ninae wangu ambae ndo yeye, habari hizo anazijua lakini bado hakutilia maanani,

Sababu ya kutaka ushauri ni kwamba amejitokeza kijana mwingine mwenye nia ya kunioa, nilivompa taarifa kwamba nmeamua nakubali kuolewa kwasabb ya yeye kutonionesha ushirikiano, ananilaumu kwamba nimechukua maamuzi kwaharaka kwanini nisimvumilie. Kiukweli I'm confused, naomba ushauri nimkatae na huyu ili niendelee kumsubiria Boyfriend au ni Move on? Karibuni.

NB: New ID for a Reason. Please don't doubt.



Sent using Jamii Forums mobile app
Olewa fasta. Utakuja kujilaumu baadaye ooh. Wanaume hatuaminiki sana.
 
We mdada unatabia ya uhuni/hujatulia kabisa, Akuna mwanaume(kijana) yupo tayari kuleta posa bila kuwa na mausiano naye na kwa Dunia ya leo inabidi akutafune kwanza, sasa akishanogewa utamu ndo analeta posa kwenu ajimilikishe mazima.
Kuhusu uyo mpenzi wako ni kwamba keshakujua tabia zako vzr na kaona wewe utampasua Kichwa ndo mana hataki kukuoa na kinachobaki ni kukuletea sababu zenye vigezo na masharti kwamba mzae kwanza mara Ooooh subiri kidogo, muoaji hanaga hizo pigo isitoshe angeshakuchukua hata mkae wote uku taratibu za ndoa zikifanyika taratibu kama kweli kigezo ni gharama za harusi.
 
Shida mwanaume kamjibu kua wazae kabla ya haimake sense mtu atake azae lakini ndoa imshinde,so kua baba anaweza kua mume hawezi,huyo dada aolewe kama moyo wake umemruhusu na akili yake ikakubali aolewe tu ya mbele anajua Allah
We dont need to judge ila wanawake huwa mnakasumba kubwa sana ya kulazimisha ndoa mkidhani kupata ndoa tu ndiyo heshima pekee katika jamii, ila ndoa ina vitu vingi sana sana na lazima utayari uwepo pande zote mbili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida mwanaume kamjibu kua wazae kabla ya haimake sense mtu atake azae lakini ndoa imshinde,so kua baba anaweza kua mume hawezi,huyo dada aolewe kama moyo wake umemruhusu na akili yake ikakubali aolewe tu ya mbele anajua Allah
Mshauri kwa makini maisha yake ya ndoa yakianza kwenda hovyo hutakuwepo wakati huo, ushauri uzingatia wakati huu na wa baadae pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama huyo muoaji umeridhika nae olewa tu, ila sio unaolew alafu unaendeleza mahusiano na huyo boyfriend wako utakuwa unazingua na wewe... ndoa ingia mzima mzima kama umeamua uoelewe na huyo basi mwambie boyfriend wako hali halisi na mwambie mnaachana rasmi na namba zenu mzifute kwa kila mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kikubwa kilichopo huyu dada hamuamini huyo anetaka wazae, na mm ntamshauri tu akae chin amchunguze akiemkubali kuolewa nae akiridhika sawa aolewe zinaa s nzuri ukiendekeza kama anajiona anastahili kua mke wa mtu aolewe hata hivo maisha yajayo hatujui yatakavokua anaweza wakataa wote wanaomposa kesho na kesho kutwa akose hata wa kumdanganyia kumuoa yote kwa yote yanawezekana
Kesho tulete posa kwenu?
 
Yaani kama kuna mtu anataka uzae naye kabla ya ndoa basi kama una sumu karibu muwekee tu hana faida kwako, kama kweli ana nia njema na wewe muambie utasubiri huku akiwa amefunga zipu yake.
Kwa aliyekuja kukuposa kama kweli moyo wako umeridhia na umejihakikishia ni mtu mwema kwa uchunguzi wako basi olewa acha hilo jangili liendelee kusubir wa kuzaa naye kabla ya ndoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ya ndoa ni zaidi ya tunavyo fikiria na kufahamu ndoa inaitaji nidhamu, hekima, uvumilivu Upendo, utayari na utimamu wa moyo na akili
Hivyo sishauri mtu kuoa au kuolewa sababu ya kigezo cha umri kwenda au wenzako wameolewa hapana subiri muda muafaka ufike ndipo ufanye maamuzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom