Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Umeongea ukweli.kuna majinga yanatunisha kifua eti tuna madini wakati hayo madini yenyewe ili yaweze kua na manufaa na thamani lazima tuwauzie hao hao mabeberu.Tatizo liko kwenye akili zetu namna yakupiga hatua zetu uku kila mmoja akinufaika ipasavyo.Kwahiyo kushindwa kwetu kunatufanya tuwachukie mabeberu waliotumia rasilimali tulizowapa vizuri uki sisi kile tulichokipata kutoka kwao tuneshindwa kukitumia ipasavyo.
 
Hivi ni afrika tu ndiyo inayotakiwa kudidimizwa na wakubwa wa dunia?.Mbona ziko nchi nyingi tu uko asia zimepiga hatua kubwa ya maendeleo na hatuwasikii hao wakubwa wa dunia wakiangaika nao.Mimi bado naamini tatizo liko kwetu wenyewe.Tungekua tunajielewa kwakuacha ujinga tulipaswa tuwe mbali sana na wala hakuna ambaye angeweza kutuzuia.Tunajiona tunadidimizwa kwasababu akili zetu bado hazijataka kua huru kuanzia kwenye kufikiri hadi kutenda.
 
Umeandika kama una harisha huku point ikiwa 0

Hebu weka takwimu hapa tuone kiwango cha umasikini wakati wa Mkapa, JK, Magufuli na sasa Samia ili tuone kama hao wengine wameendeleza sana nchi kisha Magu ndio akaiporomosha.

Sikia bwana mdogo, nmefuatilia viongozi wote tangu Mkapa, JK Magufuli na sasa hivi bado naendelea kufuatilia awamu ya Samia.

Hakuna popote unaweza kuthibitisha kwamba nchi hii iliwahi kuwa tajiri sana ikafika kipindi ikawa masikini ikafika kipindi tena ikawa tajiri kulingana na viongozi wake!

Kiufupi hakuna takataka yeyote anaweza kunishawishi kwa chochote kila kitu naona mwenyewe.!
 
Kwani dhalimu alifanya nini, au zile brainwash za kwenye TV ndio uliona kapatia? Zile $192 alizoongopa tunawadai Barrick mlilipwa. Kile kushika uchumba cha $300m kimeshalipwa chote?
Dhalimu wako alijaribu kuwazindua watz ila vibaraka kama wale walioenda kuolewa na amsterdam wakaanza kuturudisha nyuma
 
Ukisema ukweli na kulishauri taifa unaonekana Msaliti, ukiipinga na kuikosoa serikali unaonekana CHADEMA, na adui wa Nchi.

Ukiisifia na kuipongeza SERIKALI Kwa mazuri unaonekana kuwa wewe ni CCM.
 
Dhalimu wako alijaribu kuwazindua watz ila vibaraka kama wale walioenda kuolewa na amsterdam wakaanza kuturudisha nyuma

Hamna mshamba anaweza kumzindua mtu. Yeye ndio alizinduliwa kwa kupewa urais akaanza ulimbukeni wa madaraka. Matokeo yake saa hii amekaa kwa kutulia wanaume wanaendelea na yao.
 
Hongera kwa makala nzuri ambayo umeiandika kwa uzalendo mkubwa kwa Nchi yako .Lakini kwa Sasa hivi hatuna viongozi wenye uweledi wa kulipeleka mbele Taifa letu. Ukitaka kuona Hilo ebu cheki kesi ya Mbowe ndo utaamini aina gani ya viongozi tulionao.Hata hivo kiunabii Tanzania ipo gizani na hiki kipindi kitapita ili aje atakaetuoeleka mbele.Tafuta ukweli kuhusu utawala wa Tanzania utaelewa nini kinaendelea kwenye nchi yetu.Hivi vitu wanavijua wachache.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu Malcom, in all honesty, taja machache (notable) kati ya hayo mengi sana Magufuli aliyofanya vizuri.
 
Una mawazo mazuri lakini still hujumuelewa vizuri mwamba " Malcolm'' kuhusu diplomasia uwezo wa kidiplomasia ambao kama nchi ilikuwa ni tunu yetu ya Taifa. Mtoa mada yuko very clear kwamba nchi yetu ilikuwa isolated na jinsi dunia invyokwenda kwa sababu ya uhafidhina(conservative)wa kiongozi aliepita
Unajinasibu kwa kuwa muelewa lakini bado una mihemko tu kaa mtoto mdogo anaeweka kila kitu mdomoni akizani ni chakula. Unaweza kuita wenzako takataka kumbe wewe mwenyewe unaishi dampo. Jifunze kuna nchi na taifa, huwezi kujenga nchi huku taifa likigawika, maendeleo sio magorofa wala kelele na kibuli alichokuwa nacho mshamba flani hivi ila maendeleo ni Maisha ya watu
 
Bwana Heriel. Usitake kurahisisha mambo. Hakuna tatizo la “UCHADEMA” wala “UCCM” wala “uchama”. Kuna tatizo la kusimama kwenye UKWELI na kwenye UONGO. Ukisema UBINAFSI sawa.

Wako wengi sana wanaonufaika na uongo. Hivyo ukweli unapigwa vita kwa kila nyenzo. Tena kauli yako kuwa tatizo ni “uchama” wanaipenda sana. Ndio hao wakizidiwa hoja hudai “maendeleo hayana chama”, “maendeleo hayataki siasa bali vitendo tu”, “usiwaamini wanasiasa”, “achana na itikadi; uzalendo kwa nchi tu”.

Serikali yetu (ya CCM) kwa kiwango kikubwa husimama kwenye uongo na propaganda. Wakijitokeza watanzania kukosoa, kutoa taarifa sahihi na ushauri bora huitwa “wapinzani”, “ wasaliti”, “pinga pinga”, CHADEMA”, “wachaga”.

Wako pia wanaounga mkono upinzani/CHADEMA hata katika mapungufu ya msingi. Wanabishia ukweli na wakati mwingine kuukalia kimya. Lakini hawana athari sana kwenye nchi zaidi ya vyama vyao.

Wanaotoa matamko ya kuiunga mkono serikali hata katika makosa wengi ni wanapropaganda na wasaka fursa ndio maana wanaitwa “CCM”. Vile vile wako mashabiki wa watu binafsi wasioangalia ukweli bali propaganda kama “MATAGA”, “sukuma gang”, “msoga gang”, “wakojani”, n.k.

Tatizola Tanzania ni jamii iliyojengeka kusaka fursa za ulaji tu. Hakuna cha siasa makini, vyama makini, wala uongozi bora.
 
Mfano mlijitoa mahakama ya haki za binadamu Africa, mlijitoa Open Governance Initiative ambayo ina advocate uwazi na uwajibikaji serikalini n.k. let alone influence yetu kidiplomasia AU,SADC, na EAC ilishuka sana hatukua power brokers/Regional Kingpins kama enzi zile za 70s-90s.

Nakumbuka hadi Kuna sheria iliundwa ikitaka arbitration eti zisikiliswe humu humu nchini kwa mahakama za ndani?? Kuna mindset mbovu ilijengeka kwamba tunaweza fika mbali bila input ya dunia.

Weird!
 
Ndio maana wanataka Nchi ifanyiwe format ili kila mwenye uwezo apewe nafasi
 
Akili za Kabudi hizo. Yaani ukitaka kuteseka mpe masikini cheo na hela.
Alikuwa akinywa sharubati na kutafuna korosho kwenye vikao vya baraza la mawaziri huku anapigwa na kiyoyozi anasahau matatizo yoye anaiona Tanzania ipo sawa na USA anaanza kuwakemea masponsa wake 😁
 
Alikuwa akinywa sharubati na kutafuna korosho kwenye vikao vya baraza la mawaziri huku anapigwa na kiyoyozi anasahau matatizo yoye anaiona Tanzania ipo sawa na USA anaanza kuwakemea masponsa wake 😁
Kumuamini binadamu ni kazi sana. Halafu nilichogundua yule Mzee hanaga aibu.
 
Hakuna wakumuogopa ila ukweli lazima tuwe makini. Kwani nani ambae hajui kuwa wale watu hawataki nyie mpate? Ukitaka kuwa rafiki mzuri wa nchi za Kimaghalibi linda maslahi yao basi hapo umemaliza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoa mada ametoa mfano wa baadhi ya nchi zilikuwa kwenye lindi la umaskini lakini wakaweza kujiposition ndani ya system na wakatoka kiuchumi. Je, hao wazungu wasiotaka tuendelee hawakuwepo wakati nchi hizo sijapiga hatua?

Mtoa mada bila shaka hakuzitaja nchi hizo kwa bahati mbaya bali ni kuleta fikra kwamba inawezekana kutengeneza good cooperation framework ya kuweza kuendelea. Je, hujaona kipengele hicho?
 
Mkuu kwanini unambana Magufuli kwenye angle moja tu(diplomacy)?

Je nchi haiwezi kuendelea bila diplomacy?

Kipindi cha kikwete tulikua vizuri sana kwenye diplomasia na uhusiano wa kimataifa, lakini tuliambulia nini kama taifa?

Magufuli hakua vizuri kwenye diplomasia lakini ni kweli hakufanya kitu kama tunavyoaminishwa?
 
MImi sikatai kuwa jamaa aliharibu diplomasia ila mtoa uzi katumia point moja ya diplomasia kumponda kabisa jiwe kuonesha hafai kabisa na katumia point hiyohiyo kuwapaisha baadhi ya watu.

Madhaifu ya jpm ya kidiplomasia yanerekebishika lakini madhaifu ya wanadiplomasia anaowataja mtoa maada yakina nape na January makamba huo sio udhaifu Bali ni msiba wa vizazi na vizazi mtu anawaza kubinafsisha Tanesco, juzi juzi kaulizwa kwanini umeme unakatika alichokijibu anakijua mwenyewe.

Mtoa maada angeweza kutoa maada yake kwa kuangalia pande mbili angeanisha magufuli alichokosea na angesema Nini viongozi wabebe kutoka kwa magufuli. Kwa maana alichokuanacho magufuli ni kikubwa kawazidi Cha hao madiplomasia
 
Jakaya Kikwete naye alikosea na tukamsema, uzuri alikuwa ni mtu ambaye anapenda kusikiliza ushauri wa kitaalamu, kufuata kanuni taratibu na aliheshimu sheria za kimataifa: Ndiyo maana hata aliposhindana na baadhi ya mataifa alikuwa kwenye upande salama kwasababu alifahamu fika kwamba hakuna nchi inayoweza kuendelea duniani bila diplomasia.

Sasa Raisi Magufuli tukisema kwamba alikuwa haheshimu kanuni na taratibu, na alikuwa ni mtu ambaye hataki ushauri hata kwenye mambo nyeti mbona mnakasirika wakati ushahidi uko mwingi tu. Mimi ninayezungumza na wewe nakwambia ukweli kwa yake ambaye nimeyaona kama mwanasheria. Nimekaa na watu ambao ni walikuwa washauri wa karibu wa Raisi Magufuli, na wanasema kweli alivurunda. Mengine hatuwezi kuyaweka wazi tu,....

Nikuulize labda hivi unafahamu kwanini tulikuwa tunawinda sana na mabeberu hadi wakakamata ndege zetu, ambazo tukawa tunaogopa hata zisiruke nje ??? Tanzania tuna Bilateral Investment Agreements (BIT's) na nchi zisizopungua 30. Sasa Raisi Magufuli hali akifahamu kwamba kuna utaratibu maalumu wa kufuata unapotaka kuwashughulikia mabeberu, yeye akaamua kufanya kama anavyoshughulika na BAVICHA.

Nchi ikawa inaingia kwenye taharuki zisizo na msingi kisa tabia yake ya kutopenda kusikiliza na kujifanya anajua kila kitu. AU haya nayo umeyasahau mkuu ???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…