Ilikuwa ni lazima Masogange afe?

Ilikuwa ni lazima Masogange afe?

Mungu amrehemu tu kwa kweli,ukweli anaujua yeye na Muumba wake,ila inasikitisha sana vijana wadogo tunavyofutika! Pumzika kwa amani Didi.
 
Kwa awamu hii ...wauza nganda na watumiaji sugu..nakwambia wana "go" mmoja mmoja tena pole pole kama hivi...
Hakuna njia mbadala wa kuondoa hili tatizo.....pameharibika sana....
Wale ma manju waliomo kule "ndani" ujuwe ni mda tu unavutiwa.....washapewa vya kuondokea mdogo mdogo..
Safari lazima......."punju" huwa haidanganyi....ni mda tu!
 
Alivyohamishiwa MNH baada ya kufariki ni kwamba mama ngoma hawana mortuary?
 
JamiiForums naomba msiunganishe uzi huu na zile nyingine nyingi zilizoripoti kifo cha Agnes Masogange... Maudhui yake ni tofauti kabisa

Kuna kitu kinaendelea lakini bado hakijawa wazi sana... Ngoja mshtuko wa habari za kifo utulie... Kuna mengi yatajitokeza......
Wiki iliyopita kuna binti aliuawa gesti Chalinze... ALINYONGWA.... Lakini muda mchache kabla ya mauaji kufanyika alipigiwa simu na ndugu yake wakati wauaji wakiwa tayari chumbani kwake... Akiwasiliana kilugha na huyo ndugu yake alimwambia kuna wanawake wanne wamemvamia chumbani lakini watatu anawafahamu
Baada ya hapo simu zake hazikupatikana tena! Maiti yake iligundulika siku ya pili... Katika kufuatilia undani wake ikaonekana alikuwa kwenye mtandao wa biashara ya madawa ya kulevya... Na kulikuwa na tatizo kati yake na hao wauaji wake... Hii ilitokana na mawasiliano yaliyofumwa kwenye simu yake
Mchana wa siku aliyouliwa kulikuwa na majibizano kwa njia ya maandishi
Yeye aliandika kuwa kwakuwa wao wamemwaga mboga basi yeye atatoboa sufuria kabisa... Naye akajibiwa kuwa.. Hatasubiri afanye hivyo... Watamfuata huko huko juu.....

Baada ya mazishi kaka yake mmoja akapigiwa simu kupewa pole na kuambiwa kila kilichotokea pale msibani mpaka kuzika... (Kwahiyo wauaji walikuwepo msibani) kisha akaambiwa kuwa MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI
Baada ya kama siku tatu za mauti yake binti mwingine akakutwa kauliwa kwa kuchomwa visu mwili mzima (alikuja Kutambuliwa kama mmojawapo aliyeshiriki mauaji ya kwanza), na mwingine naye akaponea chupuchupu akiwa keshakula visu vya kutosha na sasa hajulikani alipo
Scenario nzima inaonesha ni mauaji ya visasi kati ya makundi mawili na kuna kitu kikubwa kinafichwa!!!!
Ni vigumu kwasasa kulink kifo cha Agnes na hayo mauaji mengine lakini tayari kuna watu wameshaanza kutuhumiwa. ..
Agnes Masogange amekuja kuwa maarufu zaidi baada ya kuja kuhusishwa na biashara ya madawa ya kulevya... Tuhuma dhidi ya madawa ya kulevya zilipelekea akamatwe na kufunguliwa kesi... Ni juzi tu hapa mwezi uliopita alikutwa na hatia na kuhukumiwa kulipa faini au kifungo... Alinusurika kifungo kwa kulipa faini iliyolalamikiwa na wengi
Mabush lawyer wengi walisema kuwa kesi kama ile kama huna watu wazito nyuma yako unaondoka na maji...

Kwanini kifo chake kimeacha mashaka!?
Mitandao ya hizi biashara haramu., haipatani kabisa na kitu kinaitwa polisi... Kwa baadhi ya nchi watuhumiwa hufuatwa na kuuliwa huko huko jela au mahabusu
Masogange akiwa tayari kwenye spotlight ya polisi... Nini ingekuwa future yake!? Kumbuka ni vigumu tena kumtumia kwenye hiyo biashara.. Tayari ana file.. Hivyo keshakuwa ndege mweupe!
Lakini je anafahamu mangapi!? Je hawezi kuropoka?!?
Je ni nani aliyekuwa tayari kugharamia maisha yake ya anasa wakati sasa hawezi tena kuzalisha!?
Risk ni zipi akiachwa hai?
Risk ni zipi akinyamazishwa!!?
Je baada ya kesi kwisha alikuwa na madai kwa washirika wake kibiashara!?
Kifo hupangwa na Mungu kwa wale waamini.. Lakini nyuma yake kuna sababu za kifo... Naamini siku moja ukweli utajulikana
RIP Agnes!
. Mkuu endeleza hii movie. Inaita sana
 
yaani alichokiandika kaka yangu mshana sijaelewa kabisa nimetoka kapa kabisa labda nimpate mtu anieleweshe kidogo ndo nitaelewa
Unajua msingi wa mada umemezwa na ishu ya Agnes.. Yani mjadala sasa Sio nilichoandika mwanzoni bali kilichofuatia mwishoni
 
Wewe mwanamke acha ujinga kwenye mambo ya msingi masuala ya maandamano hapa tena yanatoka wapi.

Na kwa taarifa yako hayo maandamano sidhani kama mtaweza kuyafanyaaa naaapa kabisaaa hayatoweza kufanyika na wewe utakuwa shahidi hapa kuwa dottoz aliandika.

Nakuambia tenaaa maandamano hayatafanyika na hata yakifanyika mtakijua nini kitatokea mtavunjwa miguu na mimi nitasupport mvunjwe miguuu woteeeeeee hata muuliwe tu maana mtaharbu amani ya Tanzania yetu.

Asante na meseji sent and delivery....
Ujinga ni hulka ya kibinadamu...karibu Coca.
Tutaona kama kuna atakaye andamana na unafiki wenu.
 
Anko nimekusoma japo hayo maswali ya mwisho magumu sana
 
Haya basi,Kufa ni lazima.
Its the most certain thing a human being can be sure of.Alafu alilazwa siku nyingi.Amefariki kwa Typhoid.Just a natural death.Sidhani kama alikuwa na madhara tena kwenye biashara ile.Alidrop akaanza kujisogeza karibu na ibada.She was targeted alipokamatwa south.So hakuwa mtu sahihi tena kumpa kazi.
Typhoid! unauhakika? Pumu! (Steve Nyerere) ina uhusiano na typhoid? Hapana, mwanzo ilikuwa upungufu wa damu!
 
Acha kuzuga
Hakuna typhoid inaua mtu siku hizi
Kama umeamua kutaja cause of death ....wewe sema ukweli tu
Haf this time mkidanganya nitaanika data zote wazi
Ustake ncheke.
bye
 
Back
Top Bottom