Ilani ya CHADEMA 2010-2015

Ilani ya CHADEMA 2010-2015

..nimeshtushwa na ilani kwamba Chadema wanamipango ya kujenga reli itakayopita Serengeti!!
 
Katika ilani ya CHADEMA mambo ya fungu maalum yamejitokeza haya. Mengi katika haya ni blah blah! Mf kuhusu elimu wanasema kuwa; halmashauri za miji na wilaya zitakuwa na fungu maalum ambalo litakalo kuwa linashughulikia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu tofauti na chombo chao watakachokianzisha MAALUM kwa ajili ya wale wa daraja la 1 na 2. Pia kwenye suala la afya ukr 27-28 wanasema hivi:

"Huduma ya bima afya itakuwa hitaji la lazima kwa kila Mtanzania, bila kujali kama ni mfanyakazi wa serikali au la. Ili kuwawezesha wananchi vijijini na wale wasio na ajira katika mfumo rasmi, Serikali ya CHADEMA itaanzisha utaratibu wa bima ya afya ya jamii (Community Health Insurance) ambapo kila familia itakuwa na fungu maalumu la matibabu litakaloratibiwa na Halmashauri ya Mji/Wilaya husika".

Huu ni muendelezo wa sera zisizotekelezeka. Kwanza wanazungumza afya itakuwa hitajio la lazima au la msingi kwa kila Mtanzania, then wanazungumzia insurance kwenye issue za afya. Sasa insurance inatakiwa kucover nini hapa? Halafu hii mifuko maalum mbona mingi saana. Yaani pale ambapo wanakuwa hawana means ya kuclarify au kusema watafanyaje wao wanakimbilia kwenye MAALUM,
 
Sina hakika kama idadi ya watu inafahamika na watu wa CHADEMA.
Ukurasa wa 33, wanasema hivi,

"Inakadiriwa kuwa Tanzania ina watu wenye ulemavu wasiopungua milioni nne, ambayo ni takribani asilimia nne ya watu wote nchini."

Ukikokotoa kwa mujibu wao, inamaana kuwa Tanzania inawatu takribani 100. Hili kosa ni very basic. Yaani hata idadi ya watu haieleweki. Utapangaje maendeleo bila kufaham una wananchi wangapi??
 
Anfaal,
Mkuu nimekusoma lakini nachoshindwa kuelewa ni kwamba wewe unapinga mengi kwa sababu imani yako kiitikadi inatofautiana na hiyo ya Chadema. Hivyo huwakosoi kwa kujali itikadi bali unakosoa kwa kufikiria ni makosa yamefanyika. Binafsi yapo mengi ambayo sikubaliani nayo kiitikadi lakini nawaelewa wanachokusudia kwani matatizo ya Tanzania leo hii sio mahitaji isipokuwa ni kutoka ktk matatizo ya Umaskini..

Hapa nikiwa na maana kwamba Tanzania ni kama taifa gonjwa na kinachotakiwa ni TIBA kwanza kabla hujafikiria kumbebesha mgonjwa majukumu ya kuendeleza Taifa letu. Huwezi kufikiria matatizo yetu yapangiwe ilani sawa na ya Marekani au Uingereza ambao hawana matatizo ya kijamii (social walfare) isipookuwa wana mahitaji ya kijamii.

Tanzania leo wanawake wanakufa kwa mimba, nusu ya watoto wa kike hawamalizi elimu ya secondary, Maradhi kama malaria yanaua watoto wasiopungua millioni kila mwaka na kadhalika. Hivyo itazame ilani ya Chadema kwa mengo ya ponya kwanza kabla hujafikiria mbele. Na ndio maana wapo wengi wanaopinga hata Ufisadi kuwa agenda kuu ya Chadema hali wanashindwa kuelewa kwamba huwezi kuweka ahadi ya ELIMU hali nusu ya billioni utakazo allocate zitapotea mifukoni mwa watalawa.

Labda kwa kifupi tu, nizungumzie nilichokielewa mimi:-
Chadema wanapompigia sifa Nyerere ni ktk kukumbuka fikra zake ktk kulijenga Taifa letu. Ni sawa na kusifia architecture blueprint ya nyumba unayotaka kujenga kwa ajili ya familia yako. Sasa makosa ya mwalimu yalikuja ktk Ujenzi wake ambapo tunaweza kusema aliweza kutupa ramani nzuri sana lakini jinsi alivyopanga ku raise fedha za ujenzi wa hilo jengo ndipo tulipokwama..Lakini hii haina maana mpango mzima wa ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa na makosa.

Binafsi siku zote natumia mfano wa makao makuu ya Dodoma, Tutapingana sana humu janvini lakini binafsi naamini kabisa maamuzi ya kupeleka makao makuu Dodoma was a perfect idea isipokuwa tu ndio hivyo tuli fail kama tulivyofail kiuchumi na tunaendelea ku fail kwa sababu tumeshindwa kurudi nyuma na kutazama malengo ya mwalimu japokuwa alishindwa hata yeye kukamilisha.

Halafu ktk hoja yako ya kuendelea umeshindwa kuelewa kwamba kuendelea kunakozungumziwa ni makuzi ya Kitaifa.. Nchi inaweza kuendelea kwa kusuasua haina maana bado ni mbaya na remote kuliko ilivyokuwa miaka 50 iliyopita, hapana kila nchi duniani inaendelea kwa kiasi fulani hata huko Haiti au Guinea Biissau wanaendelea ukilinganisha na miaka 50 iliyopita isipokuwa tunapowaweka ktk mzani wanabakia masiokini wa wisho na ndio tunasema ni maendeleo ya kusuasua.

Maswala mengine ya Elimu na Afya nadhani Chadema wako karibu na jamii zaidi yangu mimi na wewe hivyo siwezi kuwapinga zaidi ya kuwasikiliza wananchi wapiga kura. Nimeona watu wakipinga kabisa elimu na Afya ya bure, lakini nchi nyingi zilizoendelea zimetokea huko. Hawakuvamia elimu na afya ya kulipia wakati wakiwa ndani ya matatizo tena basi hizo shule na Hospital za makanisa ndizo zilikuwa bure zamani kupinga mfumo wa kulipia baada ya nchi nyingi za Ulaya ku adapt system ya kulipia.

Hivyo utakuta kwamba sisi tumerukia na kudandia hili treni la kulipia wakati sisi bado ni Wajinga wengi kuliko wasomi, maskini wasiokuwa na uwezo kuliko wenye uwezo tena kwa asilmia zaidi ya 70..Nusu ya wananchi wetu wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi kutokana na kutokuwa na elimu..Na hata wale waliosoma wamesoma ili wapatiwe ajira ambazo ni adimu badala ya kuwa wao kuwa wabunifu wa vifaa ambavyo vitakidhi mahitaji yetu na nje.

Kwa hiyo tuna kila sababu ya kuomba maendeleo ya haraka ktk sekta ambazo ni muhimu sana hasa Elimu, Afya na Ajira. Na hivi vitu haviwezi kupatikana pasipo kuweka malengo ya juu zaidi kiasi kwamba hata nusu yake ikifanikiwa basi tutakuwa tumepiga hatua zaidi ya kusuasua..
 
Anfaal,
Mkuu nimekusoma lakini nachoshindwa kuelewa ni kwamba wewe unapinga mengi kwa sababu imani yako kiitikadi inatofautiana na hiyo ya Chadema. Hivyo huwakosoi kwa kujali itikadi bali unakosoa kwa kufikiria ni makosa yamefanyika. Binafsi yapo mengi ambayo sikubaliani nayo kiitikadi lakini nawaelewa wanachokusudia kwani matatizo ya Tanzania leo hii sio mahitaji isipokuwa ni kutoka ktk matatizo ya Umaskini.. QUOTE]

Mkandara, kwenye post yangu ya mwanzo ya ilani ya CHADEMA nilisema wazi kuwa tunaanza na ya CHADEMA then itafuata ya vyama vingine taratibu. Kimsingi ilani ndio ainisho kuu la nini tutegemee kutoka kwa wanasiasa. Tujifunze kuwapima hawa wanasiasa kutokana na yale waliyoandika badala ya majukwaani. Uzoefu unaonyesha kuwa, hawa wanasiasa wanatabia ya kuyakana ya jukwaani. Sasa km CHADEMA wameainisha watafanya nini basi tuanzie hapo waliyosema na wakibahatika kuchukua nchi tuwahoji kwa yale waliyoahidi. Na hata kama hawatabahatika basi itabidi watambue wazi kuwa maandiko yao yanasomwa. Pia ni kweli hitaji kuu la nchi ni umasikini, lakini means ya kujikwamua kutoka kwenye huo umasikini ikiainishwa kiusanii lazima tuseme na tuzungumze na katika siasa changamoto kama hizi haziepukiki.
Hapa nikiwa na maana kwamba Tanzania ni kama taifa gonjwa na kinachotakiwa ni TIBA kwanza kabla hujafikiria kumbebesha mgonjwa majukumu ya kuendeleza Taifa letu. Huwezi kufikiria matatizo yetu yapangiwe ilani sawa na ya Marekani au Uingereza ambao hawana matatizo ya kijamii (social walfare) isipookuwa wana mahitaji ya kijamii.QUOTE]

Mkuu Mkandara, ukisema kwamba matatizo yetu hayawezi kupangiwa ilani sawa na ile ya Marekani, hapa wewe mwenyewe unakinzana na ilani ya CHADEMA maana mf mmoja wapo wanaoutolea katika mshahara wanasema watatumia mfumo wa Italy kuhakikisha mshahara unapanda kulingana na mfumuko wa bei. Hili nimeliweka kando sijalizungumza kwanza nikisoma issues zao kwenye uchumi na hili pia nitalijadili. Hawa wanasiasa wanafaa kutambua kuwa tunasoma wanayoandika. Kwenye mikutano yao wamesema elimu hadi kidato cha sita itakuwa bure lakini kwenye ilani wanasema mpaka kidato cha nne. Nina mashaka makubwa kama hata wenyewe wanajua ilani yao imeandika nini.

Tanzania leo wanawake wanakufa kwa mimba, nusu ya watoto wa kike hawamalizi elimu ya secondary, Maradhi kama malaria yanaua watoto wasiopungua millioni kila mwaka na kadhalika. Hivyo itazame ilani ya Chadema kwa mengo ya ponya kwanza kabla hujafikiria mbele. Na ndio maana wapo wengi wanaopinga hata Ufisadi kuwa agenda kuu ya Chadema hali wanashindwa kuelewa kwamba huwezi kuweka ahadi ya ELIMU hali nusu ya billioni utakazo allocate zitapotea mifukoni mwa watalawa.

Labda kwa kifupi tu, nizungumzie nilichokielewa mimi:-
Chadema wanapompigia sifa Nyerere ni ktk kukumbuka fikra zake ktk kulijenga Taifa letu. Ni sawa na kusifia architecture blueprint ya nyumba unayotaka kujenga kwa ajili ya familia yako. Sasa makosa ya mwalimu yalikuja ktk Ujenzi wake ambapo tunaweza kusema aliweza kutupa ramani nzuri sana lakini jinsi alivyopanga ku raise fedha za ujenzi wa hilo jengo ndipo tulipokwama..Lakini hii haina maana mpango mzima wa ujenzi wa nyumba hiyo ulikuwa na makosa. QUOTE]

Hili ni tatizo jingine. Haiwezekani uandike kuwa miaka 50 ya CCM (kwa mujibu wa CHADEMA) na ukumbuke nusu ya miaka hiyo Nyerere ndiyo alikuwa kiongozi eti Tanzania imeendelea kuwa katika lindi la umasikini. Halafu mbeleni unasema kuwa aliweka misingi imara. Kamwe haiwezi kuwa misingi imara km haijatufikisha tulipokusudia. Misingi imara ni pamoja uongozi bora. Sasa utaona wanajichanganya. Upande mwingine quotes za Nyerere zinawekwa na upande wa pili anaonekana na yeye kaifikisha nchi hapa tulipo
Binafsi siku zote natumia mfano wa makao makuu ya Dodoma, Tutapingana sana humu janvini lakini binafsi naamini kabisa maamuzi ya kupeleka makao makuu Dodoma was a perfect idea isipokuwa tu ndio hivyo tuli fail kama tulivyofail kiuchumi na tunaendelea ku fail kwa sababu tumeshindwa kurudi nyuma na kutazama malengo ya mwalimu japokuwa alishindwa hata yeye kukamilisha.

Halafu ktk hoja yako ya kuendelea umeshindwa kuelewa kwamba kuendelea kunakozungumziwa ni makuzi ya Kitaifa.. Nchi inaweza kuendelea kwa kusuasua haina maana bado ni mbaya na remote kuliko ilivyokuwa miaka 50 iliyopita, hapana kila nchi duniani inaendelea kwa kiasi fulani hata huko Haiti au Guinea Biissau wanaendelea ukilinganisha na miaka 50 iliyopita isipokuwa tunapowaweka ktk mzani wanabakia masiokini wa wisho na ndio tunasema ni maendeleo ya kusuasua.QUOTE]

Mkandara nakushauri kwa hili ujipe fursa uipitie ilani km hujafanya hivyo. Maana wanasema kuwa masikini wameongezeka kutoka mil 10-13. Yaani wanaosihi chini ya dola 1 kwa siku. Upande mwingine wanasema wanataka waongeze kasi ya maendeleo kutoka taratibu kwenda kwa kasi. Hapo unatetea nini sasa. The arguments are typical contradictory.
Maswala mengine ya Elimu na Afya nadhani Chadema wako karibu na jamii zaidi yangu mimi na wewe hivyo siwezi kuwapinga zaidi ya kuwasikiliza wananchi wapiga kura. Nimeona watu wakipinga kabisa elimu na Afya ya bure, lakini nchi nyingi zilizoendelea zimetokea huko. Hawakuvamia elimu na afya ya kulipia wakati wakiwa ndani ya matatizo tena basi hizo shule na Hospital za makanisa ndizo zilikuwa bure zamani kupinga mfumo wa kulipia baada ya nchi nyingi za Ulaya ku adapt system ya kulipia.

Hivyo utakuta kwamba sisi tumerukia na kudandia hili treni la kulipia wakati sisi bado ni Wajinga wengi kuliko wasomi, maskini wasiokuwa na uwezo kuliko wenye uwezo tena kwa asilmia zaidi ya 70..Nusu ya wananchi wetu wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi kutokana na kutokuwa na elimu..Na hata wale waliosoma wamesoma ili wapatiwe ajira ambazo ni adimu badala ya kuwa wao kuwa wabunifu wa vifaa ambavyo vitakidhi mahitaji yetu na nje.

Kwa hiyo tuna kila sababu ya kuomba maendeleo ya haraka ktk sekta ambazo ni muhimu sana hasa Elimu, Afya na Ajira. Na hivi vitu haviwezi kupatikana pasipo kuweka malengo ya juu zaidi kiasi kwamba hata nusu yake ikifanikiwa basi tutakuwa tumepiga hatua zaidi ya kusuasua.QUOTE]

Mwisho nakubaliana na wewe, Watanzania wanayahitaji saana maendeleo kuliko kipindi kingine chochote ambayo pia yanaweza kuainishwa kiuhalisia na kiukweli.
 
Nimefanikiwa kupata Ilani ya CHADEMA muda si mrefu. Japokuwa ndio kwanza nimeisoma kwa 70% (bado naendelea), nimependa jinsi walivyoainisha vipengele muhimu ambavyo kama kweli vikifanyiwa kazi, ni dhahiri Taifa litasonga mbele kwa kasi.

Ilani hiyo iko very objective, na measurable. Sijui kama watu wengi wameweza kuipata na kuisoma. Mimi imenifanya niamini kuwa chama hiki kiko serious sana.

Japokuwa sio mwanachama wa hiki chama, nimeamua kukiunga mkono.

 
Hata mimi sio mwanachama ila naiunga muko ni nzuri
 
Sura ya tano ya Ilani ya CHADEMA inazungumzia hali ya UCHUMI na kuweka mikakati km watachaguliwa kuingia madarakani nini watafanya. Km nilivyosema mwanzoni, wao kujifanya wanaita mpango kazi huu si ukweli kabisa maana ni ahadi ndio zilizojazana.
Sura ya tano inaanza kwa kuonyesha dhamira ya serikali kujitegemea na kujikita kwenye kuongeza uwigo wa makusanyo ya kodi. Mf ukurasa wa 49 unasema hivi;

"Kupanua wigo wa mapato yatokanayo na kodi, ikiwemo kufuta misamaha holela ya kodi isiyolenga katika kuboresha na kukuza uchumi. Kodi zote za bidhaa na huduma zitakazotozwa nchini zitakuwa na lengo moja kubwa nalo ni kuipatia serikali mapato"

  • Lakini kwa ujumla sura nzima kwa kiasi kikubwa ni vague. Mfano kwenye quotation hiyo hapo juu, CHADEMA hawapo specific wanaposema wataangalia upya misamaha ya kodi , wanalenga misamaha ipi???
  • Pia licha ya kuzungumzia spending cuts ili kuendana na makusanyo, serikali yao huenda ndio ikaongeza expenditures kutokana na malengo yao ya kurejesha usafiri wa "warranty" kwa wanafunzi ambao wao wameahidi kuulipia. Pia wamesema wataanzisha mamlaka mbalimbali, km mamlaka itakayojikita kwenye kilimo, mikopo ya wanafunzi nk. hizi pia ni gharama kwahiyo dhana ya spending cuts inakinzana na yale yaliyoainishwa katika ilani yao.
  • Katika sura hii, tatizo la mfumuko wa bei halijapewa ufafanunuzi na ukizingatiwa kuwa hili ni tatizo kubwa saana kwa wananchi wa kipato kidogo.
  • Suala la riba, limeachwa lina hang km uzungumziaji/uendelezaji/uimarishaji wa SACCOS ulivyoachwa.
  • Masoko ya dhamana/hisa/fedha na yenyewe hayajatajwa kabisa.
Kwa ujumla kwenye dhana ya uchumi, ilani imepwaya zaidi na kujikuta ikirudiarudia yale yaliyoanishwa kwenye kilimo.
 
Wakuu nimeamua kuweka ilani za vyama vyetu vikuu hapa maana uchaguzi umekaribia na slaa anawez kutangazwa kama raisi kabla wafuasi wake hatujasoma ilani ,tafadhali chukua muda kidogo uzipitie kisha tujadiliane.nionavyo chadema wamejipanga sana hata kwenye maandalizi ya ilani ila wenzetu ahadi nyingi na fake statistics na mambo mengi wamerudia ilani ya 2005-2010 yaani ni wavivu kweli wamekopi na kupest,du sijui kama wanaweza kuwa viongozi bora
 
Haya wadau Pateni copy ya Ilani ya Uchaguzi ya Chadema..najua wachambuzi wa siasa mnaleta Hoja zenu kwenye hii ILANI
 

Attachments

Ilani ya uchaguzi CHADEMA inaleta matumaini. Ni muda dhahiri kwa CCm kujiandaa kuondoka madarakani. Si vyema kuifanyia nchi majaribio, lakini kila jambo la heri huja na heri, na jambo jipya na la manufaa, mwanzo wake ni watu wapya na wachache. Tujitokeze tarehe 31.10.10 tupige kura za ndiyo kwa CHADEMA and vote out CCM!
 
Wanajamii,
Najua, inawezekana kuna thread kuhusu sera za Chadema juu ya Elimu na 'teknolojia'. Kuanzia ya chini hadi Elimu ya juu. Naomba nipewe link tafadhali.

Kama hamna, naomba wenyewe wanifupishie kidogo hapa tafadhali.
 
SERA ZA CHADEMA ZITALETA MAISHA BORA KWA WATANZANIA WOTE.

TATIZO INACHUKUWA MUDA WANANCHI KUZIELEWA NA KUZIAMINI. CHA KUFANYA NI WAGOMBEA UDIWANI NA UBUNGE KUELEZA MARA NYINGI NA KUFAFANUA.

'LETS DIVIDE THE NATIONAL CAKE TO ALL TANZANIANS'

Pia tuwaambie Sera Kali 3 za CHADEMA:

-Elimu Bureeeee

- Afya Bureeeeee

-Vifaaa vya ujenzi kushushwa bei mfano Cement, mabati, n.k

- Maisha yatakuwa nafuu. Kwa mfano bidhaa muhimu kwa mwananchi wa kawaida masikini wa kule kijijini zitapunguzwa kodi. Kwa maana hiyo zitashuka Bei. Mf Sukari, Mafuta ya kupikia, mkate, soda and what have you.

Jazia na mengine.

DK SLAA IS A KING
 
Asante Mpadmire. Tuna muda wa kutosha kuwaelimisha ndugu zetu kuwa CCM sio dini. Na pia kwamba Chadema imedhamiria kuleta mabadiliko mwaka huu
 
Back
Top Bottom