Superman
R I P
- Mar 31, 2007
- 5,693
- 1,707
Masikini Vijana wa Tanzania, kwa nini lakini?
Serikali ya CHADEMA na sura mpya ya Vijana wa Tanzania
- Vijana, wasichana na wavulana ni sehemu kubwa ya Taifa zaidi ya nusu ya Watanzania wote.
- Vijana bado wanaonekana ni Taifa la kesho.
- Vijana wanatumiwa kama washabiki katika siasa - ushiriki wao katika uongozi ni finyu.
- Ukosefu wa ajira kwa vijana unazidi kuongezeka Hasa vijana wa kike hawana ajira na kujikuta wanajiingiza katika vitendo vya biashara ya ngono.
- Vijana wenye vipaji wametelekezwa vipaji vya vijana haviendelezwi.
- Vijana wengi ni hohehahe vijana wako duni zaidi kiuchumi.
- Vijana wanabugudhiwa wanakamatwa kwa uzururaji, wafanyabiashara ndogondogo wanatimuliwa!
- Vijana wanateketea kwa UKIMWI na madawa ya kulevya.
- Michezo imepuuzwa na vijana hawana cha kufanya hivo kujiingiza katika uhalifu.
Serikali ya CHADEMA na sura mpya ya Vijana wa Tanzania
- Tunaamini kwa vitendo kuwa kijana ni Taifa la Leo.
- Tutatoa fursa na kuwezesha kizazi kipya kuwa mstari wa mbele katika siasa, uchumi na sekta nyingine.
- Tutaweka mazingira ya kuundwa kwa Baraza Huru la Vijana Tanzania.
- Tutawezesha vijana wa kike na wa kiume kumiliki ardhi na rasilimali nyingine kwa kutenga maeneo kadhaa ya biashara kwa vijana tu.
- Tutaweka kipaumbele katika kukuza ajira kwa vijana kupitia vipaji vyao katika nyanja mbalimbali tutazielekeza halmashauri kuanzisha mifuko ya ukuzaji vipaji vya Vijana.
- Tutaweka mazingira ya kuboreshwa kwa malezi ya Vijana katika familia na mashuleni ili kukabiliana na UKIMWI na madawa ya kulevya.
- Tutatoa leseni za bure na likizo ya kodi kwa Vijana wafanyabiashara ndogondogo na Vijana wanayojishughulisha na uzalishaji mali.
- Muziki wa kizazi kipya utapewa kipaumbele ili soko la muziki huu litakuzwa nje ya Tanzania.