Ilani ya CHADEMA 2010-2015

Source: Sera ya Ardhi ya CHADEMA

Sera ya Ardhi
Hali katika sekta ya ardhi ikoje?

  1. Watanzania wote ni wapangaji katika ardhi yao – sheria za ardhi hazitoi mamlaka ya kumiliki ardhi kama mtu binafsi ama vikundi.
  2. Sheria hizi zinampa mgeni mamlaka makubwa juu ya ardhi kuliko mwananchi.
  3. Mfumo dume umetawala katika kumiliki ardhi – wanawake na vijana hawajapata fursa ya kumiliki au ‘kukodisha’ ardhi.
  4. Wageni wanauziwa ardhi kama khanga.
  5. Mfumo mbaya wa ugawaji na umiliki wa ardhi pamoja na rushwa imesababisha utitiri wa migogoro ya ardhi.
  6. Wananchi wanaporwa ardhi zao kwa visingizio vya kuendeleza maslahi ya Taifa.
  7. Utaratibu uliyopo wa milki ya ardhi hautoi uhakika kwa wanyonge na maskini kumiliki ardhi yao.
  8. Kuna urasimu mkubwa unaoshawishi rushwa katika kutoa haki za kumiliki ardhi.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini ili kumilikisha Ardhi kwa Watanzania?
  1. Tutarejesha mamlaka ya asili ya wananchi kumiliki ardhi.
  2. Hatima ya ardhi ya kijiji itaachwa mikononi wa mamlaka ya Serikali ya kijiji.
  3. Rais hatokuwa na mamlaka ya kuhamisha ardhi kutoka kundi moja hadi jingine.
  4. Wageni watapatiwa ardhi kwa masharti yafuatayo - kutoimiliki, kutoiuza, kutoipora rasilimali na kutoitumia kwa namna itakayoharibu mazingira.
  5. Umilikaji wa ardhi kwa wanawake haitakuwa suala la mjadala tena. Mfumo dume wa kumiliki ardhi utatokomezwa na kufanywa historia.
  6. Utawekwa utaratibu wa kisheria utakaowawezesha wanawake kumiliki ardhi bila bughudha wala hofu ya kuporwa.
  7. Itaimarisha mabaraza ya ardhi ya vijiji na wilaya na kuhakikisha yanatoa haki kwa wananchi.
  8. Utawekwa utaratibu wa serikali kuwawekea mawakili wananchi wasio na uwezo katika mashauri ya ardhi katika ngazi ya mahakama kuu na mahakama ya rufaa.
  9. Tutatunga na kusimamia sheria zitakazo shughulikia uvamizi na ujenzi holela.
  10. Itatoa maelekezo kwa halmashauri kuendesha mipango ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu za wananchi.
  11. Itarejesha nyumba zote za serikali zilizouzwa kwa upendeleo.
  12. Tutaunda baraza la Taifa la ardhi litakalowajibika kwa Bunge.
  13. Mahitaji ya ardhi kwa jamii za vijijini yatapewa kipaumbele kuliko mahitaji ya wengine.
  14. Tutalinda ardhi za vijiji dhini ya umegaji mkubwa ili kuepuka matatizo ya kijamii.
  15. Itahakikisha vijiji vinakuwa ni vitengo vinavyojiendesha na kujitawala vyenyewe na tutawezesha wanavijiji kushiriki kikamilifu kuendesha masuala yote ya ardhi kupitia vikao vya mkutano mkuu wa kijiji.
  16. Tutahakikisha wanyonge na maskini wanamiliki ardhi ya nchi yao bila ubaguzi wa jinsi wala umri.
  17. Madaraka ya kutoa haki za kumiliki ardhi yatakuwa chini ya mikoa (majimbo).
 
Source: Sera ya Biashara ya CHADEMA

Sera ya Biashara
Kwa nini Tanzania inafanya biashara ya uchuuzi?

  1. Mitaji bado ni ndoto kwa wafanyabiashara na hasa wanawake na vijana kutoka familia za kimasikini.
  2. Kutishwa mzigo wa kodi kubwa.
  3. Ushindani usio sawa – Wafanyabiashara wa nje wanakandamiza wa ndani na wafanyabiashara wakubwa wanakandamiza wadogo.
  4. Bidhaa zenye ubora hafifu.
  5. Ukosefu wa soko la nje.
  6. Rushwa na Upendeleo kwa makusudi ya kisiasa.
  7. Wafanyabiashara wachuuzi.
  8. Wafanyabiashara wadogowadogo, Machinga, wananyanyaswa.
  9. Ushiriki hafifu katika mashirika ya kibiashara kama Jumuiya ya Afrika Mashariki.
  10. Serikali kujitoa COMESA bila kujali maoni ya wafanya biashara wa ndani na matokeo yake kusababisha hasara kubwa kwa nchi.
  11. Mikataba mibovu ya kimataifa bila kushirikisha wananchi.


Serikali ya CHADEMA itafanyaje kuimarisha biashara?
  1. Tutaimarisha upatikanaji wa mitaji .
  2. Tutaondoa kodi zisizo za lazima hususan kwa wafanyabiashara wazawa.
  3. Tutatekeleza sheria ya ushindani sawa wa kibiashara.
  4. Tutaimarisha utendaji wa shirika la viwango la Tanzania ili kuongeza ubora wa bidhaa zetu.
  5. Tutaimarisha na kutoa nguvu zaidi za kifedha kwa shirika la SIDO ili liwezeshe vijana kujiajiri kwa kuanzisha biashara na viwanda vidogo.
  6. Tutaziagiza balozi zetu kuwa vituo vya biashara.
  7. Tutakomesha rushwa za aina zote katika utoaji wa leseni, zabuni na misamaha ya kodi.
  8. Itakuwa mwiko kwa wanasiasa kuingilia shughuli za wafanyabiashara.
  9. Tutarasimisha na kuwezesha Wamachinga kufanya biashara zao kwa uhuru.
  10. Tutaimarisha mashirika kama TCCIA, Chamber of Mines, CTI na mengineyo ili kuwa sauti ya sekta binafsi.
  11. Tanzania itajiunga tena COMESA kwa kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki kama chombo kikuu cha kujadiliana masuala ya kibiashara na mashirika mengine. Lakini Tanzania haitajitoa SADC ili kuimarisha ushirikiano wa kindugu na rafiki zetu nchi za Kusini mwa Afrika.
  12. Tanzania itafanya mashauriano ya kibiashara na Umoja wa Ulaya (EPA) kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki kama sehemu ya COMESA.
  13. Majadiliano yote ya kibiashara yatawashirikisha wananchi kupitia Asasi Zisizo za Kiserikali na Asasi binafsi kama TANGO, TCCIA na CTI ili kuweka mbele masilahi ya nchi.
 
Source: Sera ya Demokrasia ya CHADEMA

Sera ya Demokrasia
Hali ikoje?

  1. Nchi inaongozwa kiimla.
  2. Mfumo wa vyama vingi umegubikwa na mizengwe.
  3. Chama kimoja kimehodhi kila kitu.
  4. Sheria zinagandamiza uhuru na ukweli.
  5. Upeo mdogo wa wananchi katika masuala ya demokrasia.
  6. Vyombo vya uwakilishi kama Bunge na Baraza la madiwani havina meno.
  7. Mfumo mbaya wa uchaguzi usiothamini kila kura ya mwananchi.


Serikali ya CHADEMA itafanyaje?
  1. Tutashirikisha wananchi wote kuandika Katiba upya.
  2. Tutaongoza kwa misingi ya sheria na haki za binadamu.
  3. Tutatoa fursa ya vyama vya siasa kujiimarisha.
  4. Tutabadili mfumo wa uchaguzi na kuwa na mfumo mchanyato wa uwiano wa kura na tulio nao sasa ili kuongeza usawa wa kijinsia katika Bunge na pia kuimarisha vyama vya siasa kama asasi muhimu katika ujenzi wa nchi. Chini ya mfumo mpya wa uchaguzi wagombea binafsi wataruhusiwa bila bugudha yeyote.
  5. Tutatenganisha bayana wajibu na mamlaka ya mihimili mitatu ya uendeshaji wa nchi – Bunge, Mahakama na Dola. Wabunge hawatakuwa mawaziri.
  6. Tutafuta sheria zinazobana Asasi za Serikali kufanya kazi zake.
  7. Tutaimarisha Asasi zisizo za kiserikali ili zifanye kazi zake kwa ufanisi na kwa uwajibikaji mkubwa.
 
Source: Sera ya Kilimo ya CHADEMA

Sera ya Kilimo
Kilimo chetu kidemorora, kwa nini?

  1. Watanzania wengi bado wanalima kwa kutumia jembe la mkono.
  2. Kilimo bado kinategemea huruma ya mwenyezi Mungu kupata mvua.
  3. Soko finyu la mazao ya kilimo – Mengi yanaozea shambani, au kuuzwa kwa bei ya kutupa.
  4. Mifumo mibovu ya kuhifadhi na kusindika mazao ya kilimo.
  5. Sera potofu za soko holela zimeua kabisa motisha ya wakulima wa mazao ya chakula na yale ya biashara.
  6. Bado tunategemea mazao ya biashara tuliyorithi kutoka kwa wakoloni.
  7. Barabara hazifiki vijijini na hivyo mazao ya wakulima kuoza kabla ya kufika sokoni.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini kurejesha hadhi ya kilimo na Wakulima?
  1. Kodi zote za pembejeo za kilimo zitafutwa ikiwemo VAT.
  2. Itatilia mkazo wa kipekee barabara zingiazo vijijini.
  3. Tutatumia mabonde yote, mito na maziwa katika kilimo cha umwagiliaji maji.
  4. Tutarejesha vyama huru vya ushirika na mali zake.
  5. Serikali itadhibiti ya soko holela ya mazao ya kilimo.
  6. Tutatoa ruzuku kwa wakulima wetu ili wazalishe chakula cha kutosha na pia kupambana na ushindani wa bidhaa hafifu kutoka nje.
  7. Tutatoa motisha kwa wakulima kuzalisha mazao mbadala ya biashara km maua, viungo, mboga.
  8. Tutatoa motisha katika sekta ya usindikaji ya mazao ya kilimo – maelekezo kwa halmashauri ya wilaya kuweka mazingira ya uwekezaji katika usindikaji wa mazao yapatikanayo ndani ya wilaya.
  9. Serikali itashirikiana na nchi zingine zinazoendelea kushinikiza nchi zilizoendelea kulegeza masharti ya kuuza bidha zetu za kilimo katika masoko yao.
  10. Tutalinda soko la ndani la bidha zetu.
  11. Tutatafsiri kilimo sio tu kuishia katika kulima na kuvuna bali kwenye kuzindika na kuongeza thamani ya bidhaa.
 
Source: Sera ya Madini ya CHADEMA

Sera ya Madini
Hali ikoje katika utajiri wetu wa madini?

  1. Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali.
  2. Katika kila shilingi mia inayopatikana kwenye madini Tanzania inapata shilingi tatu tu!
  3. Mapato yanoyopatikana kutokana na madini bado hayamfikii wala kumnufaisha Mtanzania
  4. Mikataba ya uchimbaji wa madini imetawaliwa na usiri mkubwa na inanuka rushwa.
  5. Vijana wa Kitanzania wafanyao kazi kwenye migodi ya wageni ni sawa na manamba na watumwa ndani ya nchi yao.
  6. Wachimbaji wadogowadogo wanafukuzwa na kunyimwa fursa ya kumiliki migodi.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini Tanzania ifaidi utajiri wa Madini?
  1. Si chini ya asilimia thelathini ya mapato yatokanayo na madini yatabaki nchini.
  2. Mikataba yote ya uchimbaji itapitiwa upya na kuwekwa wazi kwa wananchi.
  3. Kuwekwa sheria na utaratibu zitakazowalinda Watanzania wanaojishughulisha na uchimbaji wa madini hususan wachimbaji wadogowadogo.
  4. Kugawa maeneo ya uchimbaji kulingana na mahitaji halisi ya wananchi ili kuzuia migogoro iliyopo hivi sasa.
  5. Kutoa mikopo na ushauri wa kitaalamu kwa wachimbaji wadogo na kujihusisha na utafutaji wa teknolojia ya kisasa ya uchimbaji.
  6. Wanawake wafanyao biashara za madini watajengewa uwezo zaidi ili kulinda biashara zao dhidi ya utapeli na pia kuwawezesha kujiendeleza zaidi na kupata masoko ya biashara zao.
  7. Wachimbaji wadogo wadogo wa Kitanzania watawezeshwa kumiliki maeneo ya uchimbaji kama mbinu ya kuzalisha ajira kutokana na sekta ya madini.
  8. Mamlaka za serikali za Mitaa ambayo migodi ya madini au visima vya mafuta vipo zitashiriki kwa kiasi kikubwa katika kuandaa mikataba ya uchimbaji wa madini na mafuta.
  9. Mapato yanayotokana na madini yatatumika katika kuwekeza katika elimu kwa vijana wa Kitanzania.
  10. Usafishaji wa madini angalau kwa hatua za awali ni lazima ufanyike Tanzania ili kutoa ajira na pia kuchangia ukuaji wa uchumi na pato la wananchi.
  11. Tenda zote za ugavi kwa makampuni ya madini kwa bidhaa zinazoweza kupatikana Tanzania zitatolewa kwa Watanzania tu. Makampuni ya kigeni hayataruhusiwa kufanya ugamvi wa vitu kama vyakula, kwa mfano!
 
Source: Sera ya Maji ya CHADEMA

Sera ya Maji
Hali ikoje?
  1. Tanzania ni nchi ya maji
  2. – imezungukwa na maziwa makuu, bahari, mito, chemchem na maji ya mvua.
  3. Asilimia 95% ya wananchi hawapati maji safi, salama na kwa uhakika.
  4. Wananchi hawa, hususan wanawake, hutumia nguvu na muda wao mwingi kuyatafuta maji
  5. Kumekuwa na ahadi hewa za upatikanaji wa maji – Kwa miaka zaidi ya 30 wananchi wote wameahidiwa maji bila mafanikio!


Serikali ya CHADEMA itafanya nini?
  1. Itawekeza katika uvunaji wa maji ya mito, maziwa, chemchem na mvua.
  2. Mamlaka ya Usambazaji ya maji itakuwa chini ya halmashauri za manispaa, miji na wilaya
  3. Itawezesha vijiji kutunza vyanzo vya maji ili visiharibiwe.
  4. Upatikanaji wa Maji kwa Wananchi itakuwa ni kipaumbele muhimu cha serikali ya CHADEMA.
  5. Itaingiza kwenye mitaala kuanzia shule ya msingi hadi sekondari dhana ya utumiaji na utunzaji wa maji.
  6. Tutaboresha na kukarabati miundombinu ya maji iliyopo ili kuzuia upoteaji wa maji.
  7. Tutahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama katika kipindi kifupi iwezekanavyo.
  8. Hatutabinafsisha sekta ya Maji na makampuni yote yaliyobinafsishwa yatarejeshwa chini ya mamlaka za Maji katika Halmashauri za Wilaya. CHADEMA haitaweka MAJI chini ya mikono ya Makampuni ya kigeni, ni hatari kwa usalama wa Nchi.
 
Source: Sera ya Mazingira ya CHADEMA

Sera ya Mazingira
Hali ikoje kwa mazingira yetu?
  1. Mazingira ya mijini ni machafu sana – huduma za uzoaji taka na usafishaji miji ni hafifu, miundombinu ya maji taka haifai.
  2. Jangwa lazidi kujongea na mvua sio za uhakika tena.
  3. Wawekezaji hususan wa maeneo ya madini na viwanda, wanaharibu mazingira.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini kuboresha mazingira?
  1. Itaanzisha mashindano ya usafi wa mazingira na bustani za mapumziko kwa halmashauri za wilaya.
  2. Itahamasisha kila Mtanzania apande na kulea mti mmoja kila mwaka.
  3. Sheria zatatungwa kulazimisha wawekezaji kutunza mazingira hususan, maeneo ya machimbo ya madini
  4. Utunzaji wa mazingira itakuwa ni jukumu la serikali za Mitaa na serikali kuu itashughulikia sera na kusimamia utekelezaji wa sera tu.
 
Source: Sera ya Michezo ya CHADEMA

Sera ya Michezo
Hali ikoje?
  1. Kuna ukosefu wa viwanja vya michezo - Viwanja vya michezo vimetelekezwa na viko katika hali mbaya.
  2. Viwango vya michezo ni duni na wenye vipaji hawaendelezwi.
  3. Tanzania tumepotea katika ramani michezo duniani - Hakuna mchezo wowote kama nchi tunaojivunia kufanya vizuri.
  4. Michezo mingi imeachwa chini ya viongozi matapeli – wananchi wamebakia kuwa washabiki.
  5. Mashindano ya mashule yamefutwa na michezo imeondolewa katika ratiba za kawaida za shule.


Serikali ya CHADEMA itafanyaje?
  1. Tutaziagiza halmashauri kuweka mazingira ya kujengwa vituo vya michezo vyenye viwanja katika kila wilaya.
  2. Tuboresha muundo wa Baraza la Michezo (BMT) nchini ili kuwa na uwakilishi mpaka katika ngazi ya wilaya.
  3. Tutarejesha viwanja vilivyotaifishwa na kuviweka chini uangalizi wa BMT kwa kusudio la kuweza kuviendeleza.
  4. Vilabu vya mpira wa mguu vitatakiwa kuendeshwa kibiashara.
  5. Itahamasisha uwekezaji katika vituo vya vijana (yoso) wenye vipaji, hususan kandanda na riadha ili kuwaendeleza mpaka kufikia kiwango cha kuliwakilisha taifa letu kimaatifa.
  6. Tutarejesha na kuhimiza michezo katika mashule na vyuo – michezo itaingizwa katika ratiba na mitaala, mashindano ya shule na vyuo yatarejeshwa na kupewa mkazo.
  7. Itaanzisha siku ya michezo nchini itakayofanyika kitaifa na katika ngazi ya wilaya.
 
Source: Sera ya Mifugo ya CHADEMA

Sera ya Mifugo
Mifugo yetu imesahaulika?
  1. Tanzania ni nchi ya tatu kwa wingi wa mifugo barani Afrika.
  2. Makabila ya wafugaji hayasaidiwi kuwa wafugaji wa kisasa.
  3. Mchango wa ufugaji katika pato la Taifa bado ni mdogo mno.
  4. Watalaam wa mifugo wanaozalishwa na vyuo vyetu hawakidhi haja na waliopo hawatumiki ipasavyo.
  5. Maeneo ya wafugaji yametelekezwa – hakuna huduma za kijamii kama maji, shule.
  6. Sekta ya usindikaji ya mazao ya mifugo imeuwawa.
  7. Uuzaji wa mazao ya mifugo nje ya nchi umedorora.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini kuboresha maisha ya wafugaji?
  1. Tutarejesha viwanda vyote vya usindikaji wa mazao ya mifugo – mfano Tangayika Packers.
  2. Tutafufua soko la nje la mazao yatokanayo na mifugo.
  3. Tutatoa motisha kwa watalaamu wa mifugo.
  4. Tutaboresha huduma za jamii katika maeneo ya mifugo.
  5. Tutaelekeza halmashauri za wilaya kujenga majosho.
  6. Tutatoa chanjo za mifugo bure.
  7. Tutaimarishaji uzalishaji wa kuku wa kienyeji katika mikoa ya kanda ya kati kukidhi hususan haja ya soko la utalii.
 
Source: Sera ya Miundombinu ya CHADEMA

Sera ya Miundombinu
Nchi yetu ina maeneo mbalimbali yenye bidhaa, neema na utajiri wa rasilimali tele zinazohitajika sana maeneo mengine. Karibu kila kitu kinapatikana hapa hapa nchini kwa ajili ya maisha yetu na ya wengine.

Lakini kutokana na kukosekana kwa miundombinu, maeneo mengi nchini yanakosa bidhaa kutoka maeneo mengine, na kisha kuathiri ukuaji wa soko la ndani na kuwafanya wananchi wakose mahitaji muhimu. Tunashuhudia watu wakiwa na njaa maeneo fulani ya nchi huku wengine wakiharibikiwa na mazao. Katika hali hii, uchumi wa nchi umekuwa ukidorora kwasababu ya kukosa miundombinu ya uhakika na kusababisha watu wengi kushindwa kuendelea.
  1. Miundombinu inayotakiwa kujengwa, kuimarishwa na kupanuliwa katika nchi kavu ni barabara, reli na mabomba. Hivyo basi, wahandisi na makandarasi wa barabara na reli, watapewa zabuni za ujenzi kwa usimamizi wa vyombo vya kuchaguliwa na wananchi, yaani Bunge na halmashauri. Pia washindi wa zabuni watapitishwa na Bunge na Halmashauri kwa uwazi.
  2. Hivi sasa upo mpango wa kujenga barabara kuu muhimu katika kiwango cha lami ambao utagharimiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAM). CHADEMA haitasubiri mpaka nchi tatu ziafikiane, ila itahakikisha kwamba barabara zote kuu zinaounganisha mikoa na kanda zinajengwa katika kiwango cha lami.
  3. Sheria ya Usalama barabarani (Road Traffic Act 1973) itakuwa chini ya Wizara mpya ya Miundombinu badala ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Usalama wa barabara na magari utatofautishwa na usalama wa raia. Wahandisi wa magari na barabara ndiyo watahusika na ukaguzi wa magari na barabara badala ya askari polisi.
  4. Kwenye miji mikubwa, na hususan Dar es Salaam, ujenzi wa barabara zinazopita juu (flying roads) utaanzishwa maramoja ili kupunguza msongamano wa magari na uchelewaji kazini.
  5. Matumizi na ujengaji wa reli utaendelezwa pamoja na kurudishia reli iliyong’olewa ya Mtwara hadi Nachingwea. Njia nyingine mpya za reli zitatafitiwa, kupimwa na kujengwa. Maeneo ambayo yanafaa kujengwa reli haraka ni Mtwara hadi Songea kupitia Nachingwea na Tunduru; Makambako hadi Mbambabay kupitia Mbinga; Arusha hadi Musoma kupitia Serengeti; na Tunduma hadi Mpanda kupitia Sumbawanga.

    Pia CHADEMA itaweka utaratibu wa kupanua reli ya kati kutoka Shinyanga hadi Bukoba kupitia Nyakanazi na Biharamulo; na Dodoma hadi Tanga kupitia Kondoa, Kiteto na Handeni. Maeneo mengine yanayohitaji reli ni Singida hadi Arusha kupitia Katesh; Tabora hadi Mbeya kupitia Chunya; Iringa hadi Singida kupitia Manyoni; Ifakara hadi Tunduru kupitia Mahenge na Liwale; na Dar es Salaam hadi Mtwara kupitia Lindi.
  6. CHADEMA itaanzisha utaratibu wa kusafirisha mafuta kutokea Dar es Salaam au sehemu zenye mafuta kwenda mikoa iliyo mbali kama Kagera, Mwanza, Arusha, Musoma, Ruvuma, Tabora, Manyara, Rukwa, Singida na Kigoma kwa kutumia mabomba ya mafuta ili kuondoa gharama za kutumia usafiri aghali wa barabara au reli na hivyo kupunguza bei ya mafuta mikoani.
  7. Serikali ya CHADEMA itaweka jitihada za makusudi kwa wafanyabiashara wazawa zitakazowawezesha au kuwapa nguvu za kuimudu biashara ya uchukuzi na usafirishaji majini.

    Uwezo wa wazawa kuendesha bandari umejionyesha katika kitengo cha upakiaji na upakuaji katika bandari ya Dar es Salaam ambacho kilikuwa kinaleta faida ya shilingi bilioni 10 kwa mwaka tofauti na sasa ambapo kimeshuka hadi kufikia bilioni 0.4 baada ya kubinafsishwa na wageni.
  8. Sera ya CHADEMA itakazania katika ujenzi wa viwanja vya ndege utakaoendana na kutangaza utalii na vivutio vya kitaifa. Serikali ya CHADEMA pia itanunua ndege kwa ajili ya kuwakodishia au kuwakopesha wafanyabiashara wazalendo ili kuwapa uwezo wa uendeshaji na ushindani katika usafiri wa uchukuzi wa anga.
 
Source: Sera ya Rasilimali ya CHADEMA

Sera ya Rasilimali
Tanzania ni moja kati ya nchi zilizojaliwa utajiri wa maliasili. Ni nchi yenye mito, mabonde, maziwa, vito vya thamani, wanyamapori, milima, misitu na vingine vingi ambavyo kama vitatumika vizuri vinaweza kuliletea taifa letu maendeleo ya haraka katika sekta karibu zote.

Lengo kuu la sera hii ni kurudisha rasilimali za nchi mikononi mwa wananchi wenyewe ili wawe na wajibu na haki katika matumizi, ugawaji na utunzaji wa rasilimali zilizopo kwa manufaa ya Taifa letu.

Kimsingi sera hii ya maliasili inalenga sekta kuu sita:
1. Sekta ya Wanyapori
  1. Kuhimizwa kwa wananchi wenye nia na uwezo wa kuwekeza katika maeneo yafuatayo: Ufugaji wanyamapori; Kuendesha shughuli za safari za uwindaji; Kuendesha shughuli za upigaji wa picha za wanyamapori kitalii; and Kujihusisha na biashara ya bidhaa zitokanazo na wanyamapori.
  2. Kuwapa kipaumbele wazalendo katika kujifunza na kufanya utafiti wa wanyamapori.
  3. Itakuwa ni marufuku kwa wageni kusafirisha au kuhamisha wanyama walio hai, badala yake kazi hiyo itafanywa na wananchi wenyewe.
2. Sekta ya Uvuvi
  1. Kuwawezesha wawekezaji wazalendo kupata teknolojia ya kisasa ili kuongeza pato la Taifa kwa kuongeza kiasi cha mazao ya uvuvi.
  2. Kuweka mkakati utakaowawezesha wavuvi wadogowadogo kuwa na uhakika wa soko la mazao yao. Aidha Kuweka sheria itakayowalazimu wavuvi wakubwa hasa wenye viwanda vya usindikaji kununua toka kwa wavuvi wadogo wadogo.
3. Sekta ya Ufugaji wa Nyuki
  1. Lengo la sera hii ni kufanya ufugaji wa nyuki kuendeshwa kibiashara zaidi, na hii inatokana na kwamba mazao yatokanayo na nyuki bado hayajapatiwa soko la uhakika ukizingatia kwamba aina ya nyuki wanaopatikana katika nchi yetu ndiyo wanaoongoza kwa utoaji wa asali nzuri katika soko la dunia.
  2. Kutolewa kwa elimu muafaka juu ya ufugaji mzuri wa nyuki kibiashara.
  3. Kuongeza juhudi za kutafuta soko la nje na kuchukua jitihada za makusudi katika kuitangaza asali yetu.
4. Sekta ya Misitu
  1. Kufuta utaratibu holela wa uvunaji wa misitu iliyopo hivi sasa.
  2. Kuweka upendeleo kwa wananchi kuvuna na kuuza mazao ya misitu.
  3. Kuhimiza uwepo wa misitu ya kupandwa.
5. Sekta ya Nishati
  1. Kufanywa kwa utafiti wa kina zaidi juu ya matumizi ya kuni vijijini ili kupata nishati mbadala na isiyo aghali, ili kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na kukatwa kwa miti.
  2. Kuwekeza katika utafutaji wa mafuta katika mwambao wa nchi yetu na kuendesha uchimbaji wake iwapo itathibitika kwamba uchimbaji wake unaweza kufanyika kwa manufaa ya Taifa na wananchi wake.
  3. Kuchukuliwa kwa hatua za makusudi ili kupunguza bei ya umeme. Na hili litawezekana iwapo tutakuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika.
  4. Sehemu za vijijini ambako umeme haujafika, CHADEMA kitaweka utaratibu maalum wa kusambaza vifaa vya kutumia nishati ya jua kwa gharama nafuu ili wananchi waweze kulitumia kama nishati mbadala.
6. Sekta ya Utalii
  1. Kuchukua hatua za makusudi ili kuimarisha miundombinu yote inayoelekea sehemu za kitalii.
  2. Kuhakikisha kwamba moja kati ya kazi za balozi zetu ni kutangaza vivutio vyetu vya utalii.
  3. Kuboresha na kuimarisha vituo vya utalii wa mambo ya kale, ili kuinua mapato yanayotokana na eneo hilo.
  4. Wananchi waishio katika maeneo yazungukayo sehemu za kitalii washirikishwe katika mipango yote ihusuyo maeneo hayo. Aidha mipaka ya sehemu zilizotengwa kwa ajili ya utalii ni lazima ikubalike na wananchi hao.
 
Source: Sera ya Maji ya CHADEMA

Sera ya Maji



Serikali ya CHADEMA itafanya nini?

  1. Itawekeza katika uvunaji wa maji ya mito, maziwa, chemchem na mvua.
  2. Mamlaka ya Usambazaji ya maji itakuwa chini ya halmashauri za manispaa, miji na wilaya
  3. Itawezesha vijiji kutunza vyanzo vya maji ili visiharibiwe.
  4. Upatikanaji wa Maji kwa Wananchi itakuwa ni kipaumbele muhimu cha serikali ya CHADEMA.
  5. Itaingiza kwenye mitaala kuanzia shule ya msingi hadi sekondari dhana ya utumiaji na utunzaji wa maji.
  6. Tutaboresha na kukarabati miundombinu ya maji iliyopo ili kuzuia upoteaji wa maji.
  7. Tutahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama katika kipindi kifupi iwezekanavyo.
  8. Hatutabinafsisha sekta ya Maji na makampuni yote yaliyobinafsishwa yatarejeshwa chini ya mamlaka za Maji katika Halmashauri za Wilaya. CHADEMA haitaweka MAJI chini ya mikono ya Makampuni ya kigeni, ni hatari kwa usalama wa Nchi.

Yale yale....... this is just another wishful thinking. Eg Itawezesha vijiji kutunza vyanzo vya maji, tutahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama katika kipindi kifupi etc. How this wishes could be made practical? Mtafanya nini kivitendo?
 
Source: Sera ya Uchumi ya CHADEMA

Sera Ya Uchumi​

Uchumi wa Takwimu, Umasikini kibao, kwa nini?
  1. Uchumi umekuwa kwa matajiri na wageni. Kwa Watanzania walio wengi uchumi unazidi kudorora.
  2. Bei za bidhaa zinapanda kifalaki kila mwaka-Petroli ilikuwa shilingi 450 mwaka 1995, mwaka 2005 imefikia shilingi 1,100 na inazidi kupanda.
  3. Pesa imepotea mifukoni mwa wananchi wakati maisha yanazidi kuwa ghali.
  4. Sekta zinazokuwa kwa kasi ni madini, utalii na utoaji huduma ambazo zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na wageni - ugenishaji
  5. Umaskini umezidi kuongezeka - asilimia 60 ya Watanzania wote maisha yao ya kiuchumi ni duni kuliko 1992.
  6. Kati ya Watanzania mia moja ni arobaini na nne tu wana uhakika wa mlo MMOJA kwa siku.
  7. Tofauti kati ya wenye kipato na wasicho nacho inazidi kuwa kubwa.
  8. Tumegeuzwa soko (dampo) la bidhaa hafifu za nje.
  9. Gharama ya kulipia mikopo holela kutoka nje inazidi kuwa kubwa – mikopo ya miradi isiyotekelezeka na miradi hewa iliyotafunwa na wajanja.
  10. Serikali ya awamu ya tatu imesambaratisha thamani ya shilingi ya Tanzania - Shilingi 575 iliweza kununua dola moja mwaka 1995, mwaka huu utahitaji takriban shilingi 1,200.
  11. Uchumi wa nchi unashikiliwa na wanaume wachache na wanawake kuwekwa pembezoni kabisa katika umiliki wa uchumi. Walio masikini zaidi katika Tanzania ni wanawake na hasa wa vijijini.
  12. Mchango wa wanawake wa Tanzania katika kukuza uchumi hauthaminishwi, mfano mchango wa kukaa nyumbani na kulea watoto na kutunza nyumba haupewi thamani ya kifedha katika kukokotoa pato la Taifa.
  13. Uchumi unakua mjini ilhali vijijini unazidi kuzorota. Umasikini wa Tanzania una sura ya Kijiji.
  14. Masharti ya mikopo ya mabenki kwa wanawake ni magumu sana.
  15. Serikali imepuuza kilimo ilihali kinachangia asilimia 44% ya pato la Taifa na 80% ya ajira.
  16. Bajeti zinapendelea walionacho - mfano kufutiwa kodi mafuta ya ndege


CHADEMA itafanyaje WATANZANIA WOTE wafaidi matunda ya kukua kwa uchumi?
  1. Tutatunga na kutekeleza sera za uchumi zinazojali watu maskini (pro-poor economic policies).
  2. Tutahakikisha kuwa tunatoa kipaumbele kwa sekta zinazotengeneza ajira kwa watu wengi mfano kilimo.
  3. Tutatunga na kutekeleza sera ambazo zitaweka mazingira bora kwa Watanzania kufanya biashara na hasa biashara ya kimataifa ili kuongeza ajira na kukuza pato la mtu binafsi na pato la Taifa.
  4. Tutaweka mazingira ya Watanzania kumiliki uchumi wao wenyewe na kuwezesha wanawake kushiriki katika kumiliki uchumi wa nchi yao kwa kuwapa fursa zaidi na mafunzo bora na ya kisasa zaidi.
  5. Tutafuta misamaha ya kodi kwa wawekezaji wageni isipokuwa kwenye sekta ya kilimo na mifugo tu.
  6. Tutaimarisha benki ya rasilimali (Tanzania Investment Bank) ili itoe mikopo kwa Watanzania kwa masharti na gharama nafuu na hasa kuzingatia umuhimu wa mikopo kwa wanawake ili masharti yalingane na uwezo wa wanawake na vijana katika kulipa.
  7. Tutajenga miundo mbinu ya barabara ili kurahisisha kukua kwa uchumi kwa mikoa ya pembezoni. Barabara za kuunganisha mikoa ya Rukwa, Mbeya, Tabora, Shinyanga na Kigoma zitajengwa ili kuunganisha mikoa hii na nchi nzima.
  8. Tutaelekeza halmashauri za wilaya kuanzisha benki za jumuiya pamoja vikundi vya kuweka na kukopa.
  9. Mikopo ya nje itakuwa ni kwa ruhusa ya Bunge ili kuthibiti ukopaji usio wa lazima.
  10. Kuanzisha mfumo utakaomwezesha kila Mtanzania kumiliki mali bila mizengwe- ikiwamo mali za vipaji.
  11. Sheria zote za umiliki wa mali ikiwemo ardhi zitapitiwa kwa lengo la kuhakikisha haki ya kumiliki mali hasa kwa wanawake na vijana inalindwa kisheria na kufuta sheria au kanuni zote za ubaguzi katika kumiliki mali.
  12. Tutathamini mchango wa Wanawake katika kukuza uchumi kwa kutoa vipaumbele kwa wanawake katika elimu na nafasi za kazi kama ujira wa kazi wasiolipwa ya kulea Taifa.
 
Source: Sera ya Kodi ya CHADEMA

Sera ya Uchumi - Sekta ya Kodi​

Kodi nyingi na za kificho, hali gani hii?
  1. Kodi nyingi ni za kificho au kinyemela – mfano sukari yaweza kuwa na bei ndogo sana iwapo kodi kadhaa katika bidhaa zitaondolewa au kupunguzwa.
  2. Viwango vya Kodi anazotozwa mwananchi ni kubwa mno.
  3. Mfumo mbovu wa kodi unaosababisha mianya mingi ya ukwepaji kodi.
  4. Wageni wanapewa misamaha ya kodi kiholela na kiupendeleo.
  5. Kiwango cha VAT kipo juu sana na mzigo kwa wananchi wengi hasa VAT katika vifaa muhimu vya afya na hasa kwa akina mama.


Serikali ya CHADEMA itafanya yafuatayo kuboresha mfumo wetu wa kodi.
  1. Itaweka wazi kodi zote zinazotozwa – mwananchi lazima ajue kodi anayotozwa.
  2. Tutapunguza VAT ili iendana na viwango vya nchi nyingine za Afrika Mashariki.
  3. Tutaziba mianya ya ukwepaji kodi na kutoa misamaha pale tu itakapobidi na lazima iidhinishwe na bunge.
  4. Tutapanua wigo wa kukusanya kodi.
  5. Tutafuta kodi katika bidhaa zote muhimu kwa akina mama wajawazito na watoto wao na pia vifaa vya elimu na vyakula vinavyozalishwa ndani ya nchi.
 
Source: Sera ya Ulinzi ya CHADEMA

Sera ya Ulinzi

Majeshi yetu tumeyarithi kutoka kwa mkoloni na kwa bahati mbaya baadhi yao bado yana ule mfumo wa utiifu (blind obedience) aliyekuwa anatarajia mkoloni kutoka kwao! Hisia za wananchi kwa baadhi ya vyombo hivi hasa Polisi na Magereza zimebaki kama ilivyokuwa kabla ya uhuru kwamba vyombo hivyo ni adui wa raia! Wananchi wanashambuliwa na polisi kwa maagizo ya wakubwa wao wa kazi wanaopokea amri zenye mnuko wa kisiasa kuliko ule wa kisheria.

Sera ya CHADEMA inajaribu kubadilisha imani, mwelekeo na maadili ya vyombo hivi ili imani ya wananchi irudi kuwa vyombo hivi vipo kwa manufaa yao na siyo kwa sababu tu ya kuwasumbua, kuwaumiza na kuwaswaga kifungoni kila wapendapo au wanapoamriwa. Vilevile inakusudia kuboresha hali duni ya wafanyakazi wa vyomho hivi. Afisa mwenye njaa kali hataacha kutumia cheo na wadhifa wake kudai na kupata rushwa kutoka kwa mwananchi. Vipi basi mwananchi huyu ataamini kuwa Afisa huyo na jeshi lake ni RAFIKI WA RAIA?
 
Source: Sera ya Ushirikiano wa Mataifa

Sera ya Ushirikiano
Utangulizi
  1. Historia yetu kuhusu ushirikiano wa mataifa inaanza tangu awamu ya kwanza tulipopata uhuru kama Tanganyika hadi awamu ya sasa tukiitwa Tanzania.
  2. Ili kurahisisha maelezo yetu, tatatumia jina la Tanzania kwa vipindi vyote kurahisisha mtiririko wa historia ya Taifa kuhusu swala hili muhimu.
  3. Kwa kifupi historia yetu ya Uuhirikiano wa mtaifa mengine ni ile ya kuyumbayumba. Tukianza na uhusiano wetu na majirani zetu, kwanza tulishirikiana nao vizuri kiuchumi na kisiasa. Kwenye hatua ya pili, tukivuruga uhusiano wetu kiuchumi kutokana na kutofautiana kisiasa. Tatu, tukashirikiana kwa msingi wa urafiki baina ya viongozi wa nchi.
  4. Kuhusu ushirikiano wetu na nchi nyingine zisizo jirani, hapa vile vile mwenendo wetu ukawa ni ule ule wa kuyumbayumba. Mwanzoni tulikuwa kwenye kambi ya siasa za mwelekeo wa magharibi (PRO-WEST) na kuwa marafiki na viongozi wa kambi hiyo yaani Uingereza na Marekani. Haikuchukua muda tukajitoa hapo na kuingia kwenye NON-ALIGNED STATES na wakati huo huo tukinyemelea USOSHALISTI na hivyo kuwa marafiki na nchi za COMMUNIST BLOCK zikiwemo Urusi, China, Cuba n.k.
  5. Hakika hii ya mwisho ilishamiri pale Tanzkania ilipong’amua kuwa nchi hizo za kisoshalisti ndizo zitakazoisaidia Tanzania katika azma yake kuu ya kuwa mkombozi na mleta uhuru nchi zote za Africa ambazo hazikuwa huru. Hii inatokana na kuwa nchi nyingi za Africa zilikuwa koloni za Western Block ya Uingereza, America, Ufaransa, Ureno n.k.
  6. Kutokana na juhudi zetu za kupigania uhuru wa nchi nyingi za Afrika, hatungeweza kusemwa kuwa tulikuwa na ushirikiano na mataifa yaliyozifanya nchi hizo koloni zao. Serikali za kikoloni za Africa Kusini, Zimbabwe, Zambia, Malawi, Mozambique, Lesotho, Namibia, Swaziland zilituona kuwa ni maadui na wengine walidiriki haa kuishambulia nchi yetu.
  7. Tusichanganye basi swala la juhudi zetu za kupigania uhuru wa Africa na ushirikiano wetu na mataifa yaliyokuwa yanatawala sehemu hizo za Africa.
  8. Swala la ushirikiano wetu na mataifka sasa na ushirikiano pamoja na mataifa yale ambayo kwa njia moja au nyingine tulihusika kazipatia uhuru ndio msingi wa sera za CHADEMA kuhusu ushirikiano wa mataifa kwa ujumla.


Sera ya Ushirikiano wa Mataifa
  1. CHADEMA tunaamini kuwa nchi yetu imekuwa tegemezi kwa mataifa na mashirika ya nje kwa muda mrefu na kushindwa kujitegemea kiuchumi na sasa, hata kisiasa.
  2. Hali hii ya kuwa nchi tegemezi imedumaza Taifa letu na sasa hatuna ari wala shauku ya kujikwamua wenyewe. Fikira zetu sasa, ubunifu na uvumbuzi unaelezwa tu kwenye utaalam wa kuandika miradi ya OMBA OMBA kwa wafadhili mbalimbali ambao tunawaona kama miungu.
  3. CHADEMA tunaona kuwa hali hii sasa inahatarisha hata kiwango cha uhuru wetu kwani ni lazima tufuate masharti ya wafadhili ili tupate kile tunacho omba.
  4. CHADEMA tunadai kuwa uhuru wetu wa jujiwekea falsafa na itikadi inayotufaa sisi, uhuru wetu wa kujiwekea dira ya maendeleo yetu, uhuru wetu wa kufanya maanuzi kuhusu maendeleo yetu na mwishowe uhuru wetu wa kujiwekea mipango na mikakati ya kuendeleza Taifa lektu – UHURU HUU URUDI MIKONONI MWA WATANZANIA MARA MOJA.
  5. CHADEMA tunachoshwa tunapona kuwa MAKABURU tuliokuwa tukiwapinga juzi sasa ndio wanaoteka njia zetu zote za kiuchumi kama viwanda, taasisi za fedha, usafiri na hata kudiriki kufanya madini ya Tanzanite yanyopatikana nchini tu kutokuwa na thamani hadi iwe na muhuri wa utambulisho wa kampuni yao! Bidhaa zetu haziendi Africa Kusini na hata hapa kwenye viwanda vyao wanakataa kupokea shayiri yetu na kuwakosesha wakulima wetu soko la ndani ya nchi yao. Hali kadhalika matunda yetu yanaozaa shambani ambayo yale ya Africa Kusini yamejaa madukani na magengeni.
  6. Tanzania imejivunia sana juhudi zake za kuleta uhuru nchi nyingi za Africa. Juhudi hizi zilifkanywka kwa gharama kubwa ya kutukosesha sisi maendeleo na wakati mwingine hata damu zetu kumwagika.
  7. CHADEMA hatuna ugomvi na hiyo. Tunayokuwa na ugomvi nayo ni ile kiherehere cha serikali za awamu zote zilizotangulia cha kuingilia siasa za nchi hizo kwa kuzitaka nazo zifuate mfumo wa siasa yetu. Hali hii imetukosesha ushirikiano na nchi nyingi na hasa zile tulizoshiriki kikamilifu kuzikomboa.
  8. Serikali imekuwa kama mfano wa baba anayemwosa mtoto wake wa kiume na halafu kumfuata fuata kijana huyo na kumwelekeza jinsi ya kuishi na mkewe.
  9. Ushirikiano wa mataifa tunaoutaka CHADEMA na ule unaojengeka kwa misingi ifuatayo:-
    • Ushirikikano wa msingi wa UJIRANI MWEMA ni lazima na sio OPTIONAL.
    • Ushirikiano wa kiuchumi kikanda barani Africa ndio uendelezwe.
    • Ushirikiano onaojengeka kutokana na utetezi wa Haki za Binadamu na Utawala Bora unakubalika.
    • Ushirikiano unaojengeke kutokana na imani kuwa uhuru wetu, mategemeo yetu na dira zetu za kujiendeleza zinaheshimika na wengine una msingi mzuri.
  10. Chombo kikuu cha kuanzisha, kuendeleza na kustawisha ushirikiano wa mataifa ni balozi za nchi. Balozi za nchi zinaendjeshwa na mabalozi na maafisa wa Balozi hizo wengi wao wakipewa vyeo hivyo kama tuzo (PATRONAGE) au fadhila za kisiasa.
  11. CHADEMA tunataka ianzishwe mara moja mfumo wa kuwateua mabalozi na maafisa balozi ambao ni PROFESSIONAL na sio vibaraka wa viongozi wengine.
  12. Tunakusudia hivi kwa kuwa tunataka mabalozi wawajibike na yafuatayo:-
    • Kuitangaza nchi yetu kibishara, kiutawala na kiutendaji.
    • Kutujengea uhusiano wa kibiashara na kiuchumi.
    • Kutupatia taarifa sahihi za nchi wanazotuwakilisha ili uhusiano ujengeke kadri utakavyoonekana.

    Nguzo hizo ndizo zitakuwa kipimo cha kuwepo au kutokuwepo kwa ubalozi baina ya nchi yejtu na nyingine.
  13. Makusudi makuu ya sera hizi ni kuwajibisha jamii na siyo kiongozi mmoja mmoja kama ilivyokuwa awali na maamuzi na mamlaka ya nchi juu ya ushirikiano na mataifka mengine. Maamuzi haya yasitokane na shinikizo la wafadhili, wahisani, IMF au Benki ya Dunia n.k.
 
Source: Sera ya Utamaduni ya CHADEMA

Sera ya Utamaduni
Hali ikoje?
  1. Utamaduni wetu wa asili unadharauliwa na kuharibiwa na tamaduni za kigeni.
  2. Mapato yatokanayo na kazi za kisanii hayalindwi ipasavyo na sheria.
  3. Watanzania wengi hawajui kuzungumza kiswahili fasaha – Kiswahili kama lugha ya Taifa hakipewi mkazo unaostahili.


Serikali ya CHADEMA itafanyaje?
  1. Sheria za hatimiliki zitaboreshwa - adhabu kali zitatolewa kwa wakiukaji na fidia kubwa kwa waliodhulumiwa.
  2. Itaagiza kila halmashauri ya wilaya kuanzisha maeneo ya makumbusho ya mila na desturi zetu.
  3. Itaagiza balozi zetu kuendesha shughuli za kukuza kiswahili na kuonyesha utamaduni wetu wa asili kama kivutio kwa watalii.
  4. Baraza la Sanaa la Taifa litapatiwa majukumu na uwezo wa kuendesha mashindano ya ngoma zetu za jadi kitaifa kila mwaka.
  5. Itaweka mkazo wa kipekee kwenye lugha ya Kiswahili - Uswahili ndiyo umoja wetu na ndiyo utambulisho ulio wazi wa Watanzania.
  6. BAKITA itaimarishwa kwa kupewa nyenzo za kazi na wataalamu zaidi.
  7. Tutafungua mjadala wa kuona jinsi ya kutumia kiswahili katika kutoa elimu kwa Watanzania.
 
Source: Sera ya Utawala ya CHADEMA

Sera Ya Utawala​

Utawala wa Ukiritimba na Urasimu, ukoje?
  1. Serikali kuu inaingilia mamlaka ya Serikali za mitaa. Katiba haipo wazi juu ya mamlaka ya serikali za mitaa.
  2. Serikali ni kubwa mno na haina ufanisi.
  3. Halmashauri za Wilaya zimebanwa, hazina uhuru wa kutosha na zinaingiliwa na watawala kutoka Serikali kuu.
  4. Wakuu wa wilaya wanaingilia utendaji wa halmashauri za wilaya na kudhoofisha demokrasia.
  5. Mikoa ni mingi sana na haina ufanisi kiutawala na kiuchumi.
  6. Mfumo wa Muungano ni tata na hautoi nafasi kwa Muungano mkubwa zaidi wa shirikisho la Afrika Mashariki.


Serikali ya CHADEMA itaondoa ukiritimba na urasimu kwa kufanya yafuatayo.
  1. Cheo cha Mkuu wa Wilaya kitafutwa na kazi zote za Ofisi ya Mkuu wa Wilaya zitajuimshwa na Kazi za Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya/Mji/Manispaa/Jiji pamoja na Meya.
  2. Halmashauri za Wilaya zitapewa mamlaka na uhuru zaidi kwa mujibu wa Katiba Mpya itakayotungwa kwa ushiriki wa wananchi.
  3. Mfumo wa serikali za mitaa utaimarishwa kwa kuimarisha serikali ya Kijiji kama chombo cha msingi cha uongozi (governance).
  4. Mameya watachaguliwa na wananchi moja kwa moja na watakuwa na majukumu ya utendaji pia.
  5. Mikoa ya sasa itaunganishwa na kuwa na mikoa kumi tu ili kuwezesha ufanisi wa kazi na pia kuleta ushindani wa kiuchumi miongoni mwa mikoa ndani ya nchi.
  6. Mikoa itakayoundwa itakuwa na mabunge yao na kuchagua viongozi wao kidemokrasia.
  7. Tutarekebisha mfumo wa Muungano ili kuiweka nchi tayari kwa shirikisho la Afrika Mashariki bila kuathiri uhuru na dola ya Zanzibar na Tanganyika.
  8. Mabadiliko yote ya mfumo wa Utawala wa nchi yatafanywa kufuatia zoezi la kutunga katiba mpya nchi kufuatia
  9. Mkutano Mkubwa wa Katiba utakaoshirikisha wananchi wote.
  10. Nafasi za uongozi wa serikali zitakuwa na mtazamo mkubwa wa kijinsia.
  11. Serikali itakayoongozwa na CHADEMA itahakikisha nafasi za Mawaziri, Manaibu Mawaziri na Makatibu Wakuu zinashikiliwa na idadi ya kutosha ya Wanawake ili kuweka uwiano wa kijinsia katika utawala wa nchi.
  12. Serikali ya CHADEMA itahakikisha kunakuwa na usawa wa kijinsia katika nafasi za uongozi katika Mahakama na
  13. Bunge kwa kutoa kipaumbele kwa wanawake wengi zaidi kusomea sheria na kuajiriwa kuwa mahakimu wa mwanzo, wa wilaya na mahakimu wakazi na baadae kuwa Majaji.
 
Source: Sera ya Utawala Bora ya CHADEMA

Sera ya Utawala Bora
Hali ikoje?

  1. Rushwa na upendeleo vimekithiri katika nyanja zote - Rushwa sasa imekuwa utamaduni.
  2. Shughuli za vyama vya siasa zinafanywa na vyombo vya dola.
  3. Matumizi ya anasa ya viongozi ilhali wananchi wamezamishwa kwenye umaskini uliokithiri.
  4. Viongozi kutowajibika mbele ya wananchi.
  5. Wizi wa mali ya umma, ubinafsishaji holela na ufisadi.
  6. Uuzaji wa nyumba za Serikali kwa viongozi kiupendeleo.
  7. Mamlaka ya Umma imeporwa na tabaka la watu wachache.
  8. Ukosefu wa maadili ya Taifa.
  9. Viongozi wabovu wasiokuwa na dira.
  10. Viongozi wanakula njama na wageni kuhujumu rasilimali zetu.
  11. Hakuna morali.
  12. Ubinafsi umetawala.
  13. Uzembe umekithiri.
  14. Viongozi wasiojali nchi na watu wake.
  15. Mwizi ni yule anayekamatwa, asiyekamatwa ruksa.


Serikali ya CHADEMA itafanyaje?
  1. Itafuta PCB na kuunda upya idara ya kupambana na rushwa chini ya idara ya Mkurugenzi wa makosa ya jinai.
  2. Idara ya Usalama wa Taifa itafanyiwa marekebisho makubwa ili ilinde maslahi ya nchi na sio ya wakubwa wachache.
  3. Tutaita Mkutano wa Katiba ndani ya mwaka mmoja wa utawala wa CHADEMA.
  4. Katiba kuwa na kipengele kitakacho ruhusu wananchi kuwawajibisha madiwani, wabunge na wawakilishi “recalling clause”.
  5. Itapiga marufuku uuzaji wa nyumba za Serikali na kurejesha zilizokwisha uzwa kiupendeleo.
  6. Matumizi yote ya gharama kubwa bila stahili kusimamishwa mara moja.
  7. Tutakomesha rushwa na atakayetoa au kupokea rushwa atahukumiwa adhabu kali.
  8. Upendeleo utapigwa vita.
  9. Viongozi wa CHADEMA watajali nchi na watu wake.
  10. Tutahamasisha maadili ya Taifa.
 
Ukiziunganisha zote itakuwa mukide sana,
Zote sera zingekaa pamoja hapo juu.
 
Back
Top Bottom