Ila maisha

Ila maisha

dah! kukosa mia leo tu, mbona naona kama afadhalli...

kuna mwingine mwaka wa 4 sasa analala kituo cha daladala ana box lake la kulalia, ambalo saiv limeloa na mvua na hajui atapata wap lingine lini..
Mwenyezi Mungu atafanyie wepesi na atujaalie Moyo wa kutokukata Tamaa...

amin insha’allah
 
mimi ni miongoni mwa wale mtu akinililia shida natoa nipate shida mimi sasa nikawalilie walionililia mweeee ni huzuni
Af cha ajabu unajua ni nini?! Hapo hapo unaapa kutorudia kusaidia tena. Lakini,huwezi kama ndo umezaliwa hivyo,ni hivo hivo.
Sema tu,uzuri hakuna kisichokuwa na mwisho duniani humu. Unajinyima kumsitili mtu,kesho anakuona takataka.
Kikubwa tu ni kwa mba hakuna mfu anaekosa wa kumzika, we tenda wema uende zako. Uzuri anaekupotezea kesho hawezi kuja kwako tena.
 
Kuna wakati uhitaji wako inaweza isiwe kitu chochote cha thamani sana bali hata chakula tu ukipata unaweza kushukuru sana.

Niliwahi enda msibani nikala chakula kizuri nikapata na chupa moja ya maji nikaondoka, nilishukuru sana mana mlo wangu nilikuwa sijui nitaupata wapi.
 
Emungu asante sijawai lala na njaa hata siku moja ila nimewah kukaa siku tatu nikishindia maganda ya miogo nilikuwa naenda kwa wachoma chips za viaz makaba kusanya maganda naenda kuosha nayakata upya tena kama kachumbali nayakula ndani ya siku tatu,, leo hy nikikumbuka najiona fala na hakuna kitu kwenye maisha yang nakisamin kama kula,
 
Mimi kwa miguu yangu nilienda kwa mama muuza maandazi, nikanunua matatu, nikala moja asubuh moja mchana moja usiku, mwendo wa maji tu, nilifanya hivyo wiki nzima, maisha muda mwingine yanatufundisha kwa namna ya pekee kabisa kiasi kwamba mtu akisema kuna hili huwezi kuamini mpaka uwe umepitia hiyo situation
Mkuu kwel.... ñimecheka!
 
Habari zenu wakuu,

Nimekaa hapa natafakari nikagundua kuna situations kama hazijakukuta huwezi ukaelewa ukisikia mtu analalama

zamani nilikua nikisikia mtu analalamika hana hata mia naona kama anazingua haiwezekani but now i know na naelewa kumbe ni kawaida tu

Nimeamka tangu asubuhi sina hata mia na siku inaisha hivyo aisee.
View attachment 2874679
Bora wewe umeamka mpaka siku inaisha hauna hela!

Vipi ukiamka ukute mashine hamna! Haipo!... Utajiskiaje!... Ama utatumia ule mlango wa uwani!?
 
Back
Top Bottom