Ila maisha

Ila maisha

Habari zenu wakuu,

Nimekaa hapa natafakari nikagundua kuna situations kama hazijakukuta huwezi ukaelewa ukisikia mtu analalama

zamani nilikua nikisikia mtu analalamika hana hata mia naona kama anazingua haiwezekani but now i know na naelewa kumbe ni kawaida tu

Nimeamka tangu asubuhi sina hata mia na siku inaisha hivyo aisee.
View attachment 2874679
Kama unaona maisha ni magumu achana nayo, fanya kitu kingine.
 
In life,unatakiwa kuwa na rafiki Mmoja anayeweza kubeba shida zako,,huyo rafiki anaweza kuwa mmeshare blood labda sister au cousin lakini pia inawezekana akawa rafiki tu wa kawaida...
Bibie,ilikuwa. Kwa sasa, rafiki wa kiume lazima akuchabange,wa kike lazima anufaike kwa namna moja ama nyingine,au na yeye atataka tu naniliyu.
Sema tu utabaki kujiuliza wa kumuamini ni nani?
Miaka ya nyuma,ulikuwa unaweza kukaa kwa rafiki hata mwaka mzima,watu walikuwa waelewa. Sasa hivi,watu walishakuwa wahuni. Atafanyaje mambo yake huku amebanwa?
Je,miaka kama 10 huko mbele,itakuwaje!
Leo hii kuna wajinga atakuja akulilie,hata laki utampa. Ila sasa wewe pata shida,ndo utajua kumbe we mjinga. Utajiona takataka,huku ulijua unamkimbilia aliekukimbilia.
Mara mia uwe na rafiki asiyejiweza,hata asipokupa utajua hana. Kuliko wanaojiona wanaweza,lakini hawana lolote.
 
Back
Top Bottom