Luca Paguro
JF-Expert Member
- Mar 26, 2023
- 478
- 1,068
- Thread starter
- #81
Umasikini sio lazima uwe na njaa au ukose ng’ombe, hata ukosefu wa uwezo wa kuchagua maisha bora zaidi ni umasikini. Unaweza kuwa na magunia ya mazao lakini bado ukose maji safi, elimu bora au huduma za afya, nyumba yako mbaya. Hapo bado ni umasikini wa miundombinu, sio wa chakula tu.mtu anaishi nyumba ya nyasi,ana gunia 200 za mpunga ndani,ana gunia 150 za mahindi,ana ng'ombe 300 wengine kawapeleka sehemu nyingine malishoni huyo mtu unaweza kumweka kundi gani. Wengi wanaongelea mtu masikini ni yule hana nyumba nzuri ya kuishi,lakini ukweli ni kwamba wanajidanganya, mleta mada huwa anapita tu vijijini anachungulia dirishani na kuona nyumba zilizoezekwa kwa makuti na kutoa picha ya jamii yote ni maskini,hataki kujifunza tamaduni na mwenendo mnzima wa maisha ya watu. Naweza kuta mtu amejenga nyumba nzuri lakini life style yake haiko sawa,nyumba hiyo ameiweka bond,hana kitu zaidi ya kufanya biashara ya mkopo, unamlinganishaje mtu huyo na mfugaji,mwenye mashamba,mkulima aliyeamua kujenga nyumba zilizoezekwa kwa makutu? Lazima unapoleta mada yako ufanye na utafiti kidogo ufuatilie life style za watu hao unaowazungumzia. Afya bora,mavazi si kipimo cha umas
Hata hivyo Watanzania wengi maisha yao hayapo hivyo. Wengi chakula walicho nacho ni cha kula wao tu sio kwamba wanauza ili wapate hela ndefu. Hapana
Na ukitaka kujua hao watu ni masikini, subiri uone wakishaanza kuumwa magonjwa ambayo ukienda hospitali unahitaji hela kutibiwa, hapo ndio utaona bila kuomba kuchangiwa hatoboi. Watu wengi hata uwezo wa kumsomesha tu mtoto kwa hela zao wenyewe hadi chuo kikuu hapa Tanzania hawawezi. Kwa ulimwengu wa sasa huo ni umasikini. How can you convince me that watu wanaoishi kwenye nyumba nilizoziona sio masikini? Unaongea porojo tu