nusuhela
JF-Expert Member
- Jan 26, 2014
- 6,474
- 8,139
Mikopo ya 10% ni uongo, porojo, ulaghai na propaganda za siasa za CCM, Wewe inawezekana ni kada wa chama.
[/QUOTE
Kada kivipi?
Mikopo ya 10% ni uongo, porojo, ulaghai na propaganda za siasa za CCM, Wewe inawezekana ni kada wa chama.
[/QUOTE
Kada kivipi?
Unasema nyumba na majengo hazipimi umasikini halafu chini unaniwekea picha ya jengo zuri kijijini kuonesha kuwa umasikini upo chiniUkitaka kujua utamu wa dafu hadi uchokonoe ndani.
Huwezi kupita ukiwa ndani ya basi uka judge umasikini au utajiri wa sehemu.
Definition ya utajiri au umasikini ina vigezo vingi mno hata Marekani tunasema ni taifa lililoendelea lakini kuna sehemu ukipita vijijini hata baadhi ya miji kama Memphis unaweza sema afadhali Dar Tandale.
Nikupe mfano kuna sehemu ukienda Zambia unaweza kuta nyumba za majani ila unakuta nje kuna VX Limepaki nje la milioni250.Ukienda Tabora unaweza kuta vijijini vingine nyumba za majani lakini madirisha ya vioo tinted a dish nje la mitandao.Kwa vigezo vyako hao huwezi kuwaita ni watu masikini ni utamaduni wao.
Je mtu kama ana uhakika wa kula kwa mwaka mzima chakula kizuri cha afya ila nyumba yake ni ya majani huwezi kumuweka huyo mtu kwenye kundi la umasikini.Usipime vigezo vya umasikini na utajiri kwa mijengo peke yake yapo mambo mengi ya kuangalia.
Mtu wa kijijini ana magunia 300 ya mahindi na 300 ya mchele 100 ya mtama.Na hayo magunia ni ajili yake tu kula na familia yake.Mifugo kadhaa ya kuku na ng'ombe 300 wako porini machungani.Ana tractor na analima chakula chake na cha kuuza cha ziada nyumba yake ni ya majani kulingana na jadi yao.Ana tractor la kulimia huyu utamuita masikini?.
Mwingine anaishi mjini ana nyumba ya ghorofa moja ila kajenga kwa mkopo na nyumba iko kwenye bondi.Madali wa Majembe auction mart wanakwepana anadaiwa kati ya mtu huyu na huyo mwenye nyumba ya majani ni nani tajiri na nani masikini?
Hata huko Lindi na Ruangwa unakokuongelea ukipita barabarani kwa vigezo vyako utaona ni masikini lakini ukiingia ndani ndani unaweza kuta watu wana maendeleo ya ajabu.Mara nyingi matajiri hawapendi kukaa sehemu zenye misongamano nenda hata Marekani ma Celebrity uone wanapoweka mijengo yao wanakuwa na hadi viwanja vyao vya ndege binafsi
Hata Kilimanjaro wanasifiwa wameendelea lakini mji wa Moshi wenyewe ukiuona utaona wa kawaida.Ukipita sehemu za wapare utaona mpauko na kama nusu jangwa.
Sasa kwa kilimanjaro na upareni kwa ujumla maendeleo hayako unavoona ukiwa kwenye basi panda kule juu milimani uone matusi yao.
Kule unakuta mtu ana umri wa miaka 65 amezaliwa amekuta bomba la maji nyumbani kwao hawajui kitu kinaitwa kuteka maji kichwani na kuna mijengo ya hatari maendeleo ya shule na vyuo ndio usiseme.Wajerumani walifika kule mapema sana wakajenga makanisa na shule za misheni hata Ndanda Mtwara.
Nenda kwa kina Nshomile utakuta hali kama ya Kilimanjaro na Mbeya
Usi judge maendeleo ya watu ukiwa umekaa kwenye basi pata muda teremka ingia ndani ndani.
Nimekuwekea picha moja chini nilikwenda siku moja Upareni acha pale chini Mwanga palipokauka ukame nilipanda sehemu moja inaitwa Usangi milimani kabisa juu hadi kule ni lami na ni kijani kibichi tulikwenda.
kwenye msiba nikaona nyumba kama hiyo hapo unaweza sehemu hao wapare ni masikini hawana maendeleo?.Cha ajabu sijakutana na nyumba ya majani hata moja achilia angalau iliyopigiliwa mabati ya madebe.
Tembea ujione usingoje kuambiwa aliimba marehemu Dr Remmy Ongala.
Matajiri wa kweli wapo bana sio kweli na wanaogombea udiwani ni wangapi bwashee mpaka useme matajiri hakuna aisee mtu anunue Ford Raptor la 2023 kodi Tsh 46m harafu useme wananunua kuficha umasikini sio kweli aisee.Tanzania matajiri wa kweli WACHACHE sana, wengi wapigaji tu na 10% za udalali wa kila kitu, pamoja na Rushwa. Na ndo maana huwezi kuona impact sana ya hao wanaojiita so matajiri.Hauoni kila mtu anakimbilia kwenye siasa, awe mbunge, sasa hivi hadi Udiwani watu wanataka kutoana macho -ni ujanja ujanja.
Middle class hapo imejaa mikopo na madeni sio mchezo....
Hii bongo watu wamechoka sana, na usishtushwe na magari sijui nyumba, hivyo vinaficha umaskini na hofu ya maisha kwa walio wengi.
hili nalijua sana na najua nilichofanyaUnasema nyumba na majengo hazipimi umasikini halafu chini unaniwekea picha ya jengo zuri kijijini kuonesha kuwa umasikini upo chini
Make it make sense please
Sawa mkuu nimekuelewa. Nitafanya utafiti lakini hili suala tunasoma hata shuleni na vyuoni kuwa umasikini Tanzania upo kwa kiwango kikubwa na ni moja ya nchi zenye masikini wengi zaidi Africa (takribani milioni 28) meaning kila utafiti unaofanyika unaleta matokeo yaleyalehili nalijua sana na najua nilichofanya
Nia yangu nikukuonyesha kuwa usipite kwenye basi tu unaona nyumba za ajabu uka conclude umasikini wa nchi nzima.
Tembea interior zaidi
Hata kwenye statistics utafiti wako haujakaa sawa ulichofanya ni random sampling
Na inategemea wakati unafanya hiyo sampling ulipita maeneo gani.
Collect enough data to make a conclusion.
Hata hivyo ndugu yangu nikupongeze na nisikukatishe tamaa umefanya vizuri kutuamsha kwa kweli kazi yako nzuri
Halafu upande mwingine wa shillingi ni ajabu kwa kweli halafu moja ya nchi zenye utajiri mkubwa wa mali asili ni Tanzania.Sawa mkuu nimekuelewa. Nitafanya utafiti lakini hili suala tunasoma hata shuleni na vyuoni kuwa umasikini Tanzania upo kwa kiwango kikubwa na ni moja ya nchi zenye masikini wengi zaidi Africa (takribani milioni 28) meaning kila utafiti unaofanyika unaleta matokeo yaleyale
Mimi nilisafiri kwenda Kilimanjaro 2023.Hivi ni mimi peke yangu naliona hili?
Mbona nchi yetu masikini jamani. Mimi nimezaliwa Ruangwa huku Lindi mara nyingi nimeona watu wakipakandia Lindi kwa umasikini hususani mitandaoni, mimi nikadhani ni huku tu hali ni mbaya, mpaka nilivyopata exposure. Maeneo mengi nilizunguka zamani utotoni nikawa sipakumbuki ila miaka ya karibuni nimezunguka sana. So nilikuwa na observe, nione kwa nini watu wanasema Lindi masikini, huenda mikoa mingine ni tajiri
Advance nimesoma Mbeya, nikawa napita njia ya Ruangwa-Masasi-Songea-Mbeya
Kuanzia hapa Ruangwa ukiwa unaenda Songea, hapa kati watu wanaishi maporini kwenye nyumba za matope, nyingine wameezeka nyasi, mabati yana kutu maeneo mengine unaona kabisa hata huduma za msingi hawazipati. Yani kitu kizuri kuangalia ni nature tu, mazingira ya asili kweli Tanzania imebarikiwa
Ukifika Songea sasa, vijiji vyake udongo mwekundu halafu nyumba mbaya yani ukipaangalia kama Uganda. Bora Songea mjini pale kumeendelea halafu nyumba sio mbaya sana. Issue ipo kutoka Ruvuma kwenda Mbeya sasa, vijiji vyote humu kati vimejaa umasikini (bora hata Makambako niliona pana nyumba nzuri) ila nilipofika Mbeya nilibaki mdomo wazi, nikawa najiuliza hili ni jiji? Khaaa
Yani nyumba za matope zimetapakaa milimani kote mji umechafuka kila kona nikiangalia naona umasikini tu.
Sikuipenda hii njia, nikaanza kutumia route ya Dar, natoka home naenda Dar nakaa siku 2 au 3 hivi halafu ndo naenda Mbeya. Dar nilikuwa nafikia Kimara kwa bro, ana nyumba nzuri na mtaa wao mzuri ila umepoa sana. Nikawa natoka asubuhi naenda kuzurura maeneo mengine ya Dar. Aisee kumbe nako ni umasikini tu umejaa. Ila Dar bora kuna miundombinu ambayo inapendeza lakini kuna mitaa nilipita ina nyumba zina kutu, nyumba zimebanana yani hovyohovyo. Nikawa najiuliza ina maana ni mimi tu ndo naona hii nchi haiko sawa? Kutoka Dar hadi Mbeya nako nilisafiri mchana ili nione mazingira nako hivyohivyo tu ni umasikini, sikupenda hata nikawa nasafiri route za usiku
Mwezi May mwaka huu tulisafiri kwenda Kigoma. Jamani hii njia ndo niliona umasikini funga kazi, bora Lindi kwa kweli 🙌
Kuna vijiji vipo Morogoro huku mmh, utafikiri bado wanatawaliwa na mfalme. Tena bora Morogoro, Dodoma kuna vijiji niliona vijiji nyumba watu wamejenga na matofali ya kuchoma halafu juu wameegesha tu bati halafu juu ya bati wameweka matofali ili bati lisiezuliwe na upepo. Aisee, nilishangaa sana, Tabora kuna vijiji tumepita nikaona nyumba zimejengwa style kama nyumba za Kiafrika za nyasi ila tu zenyewe zimejengwa na bati kuanzia juu mpaka chini, zipo nyingi halafu zimekaa kama kambi za wakimbizi. Uzuri nilisafiri na treni, niliona kila kitu vizuri. Kutoka Dar to Kigoma kuna li ardhi likubwa tu limeachwa hamna hata mashamba, wala nini yani nchi kubwa ila hatujui kutumia ukubwa wetu. Nimefika Kigoma nako umasikini wa kutisha
Hata form 4 tulienda study tour Zanzibar, nako ni overrated. Ukitoa pale Stone Town, kuna maeneo ni mabaya. Mji umechoka mbaya, mabati yana kutu. Kuna sehemu Zenji ya masista inaitwa Machui ndo tulipata hostel za kulala sisi wanafunzi, yani hata internet shida, kubaya af ni dakika 30 tu kutoka Stone town. Pako kama Nachingwea. Network inasumbua, migomba mingi kama Bukoba yani pabaya tu.
Tulitoka Stone Town kwenda Nungwi, hapa kati yani nako ilikuwa ni umasikini mtupu. Nilichopenda Zanzibar ni beach ya Nungwi, bei ya vitu pale Darajani, na Forodhani wakati wa usiku kulikuwa na vyakula vya kutosha na watu wa kila race, ila walivyokuwa wanatuzungusha kwenye ma historical site huko nilikuwa naona mabaya tu. Hayavutii. Kamji kamejichokea kinoma
Hadi nimerudi mkoani kwetu Lindi, huku nako ni kubaya. Nyumba mbaya. Yani naona nchi yetu masikini tu kuanzia bara hadi visiwani
Hadi sasa mikoa ambayo sijafika ni Songwe, Rukwa, Mwanza, Kagera, Mara, Simiyu, Shinyanga, Geita, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga. Labda mikoa hii itakuwa tofauti ila sijafika.
Lakini naona vita dhidi ya umasikini tumeishindwa kabisa. Nchi kubwa, resources nyingi ila inasikitisha. Tushukuru Mungu Bongo wananchi wake wavumilivu, wengi wanaonekana kuwa na furaha tu
Kubwa mno mkuu..Kuna gepu kubwa sana kati ya tajiri na masikini Tanzania. Kubwa sana.
Hiyo ni 1% watanzania ni maskini walioridhika.Kuna gepu kubwa sana kati ya tajiri na masikini Tanzania. Kubwa sana.
Ni kweli umasikini ni mkubwa sana na viongozi wetu hawaoni hilo kwasababu ndio mazingira waliyozaliwa na kukulia tena wanasema vijana wa siku hizi hamuujui umaskini, miaka ya 60 hadi 90 kulikuwa na umaskini kweli kweli.Hadi sasa mikoa ambayo sijafika ni Songwe, Rukwa, Mwanza, Kagera, Mara, Simiyu, Shinyanga, Geita, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga. Labda mikoa hii itakuwa tofauti ila sijafika.