Ila jamani nchi yetu ni masikini, khaa

Ila jamani nchi yetu ni masikini, khaa

Nchi nzima inanuka umasikini. Unakuta barabarani hapo pana ghorofa nzuri zimepaa hewani, Sasa zunguka mtaa wa pili tu hapo watu wamebanana kwenye vijumba wanaume na vitaulo vyao wanapishana kwenye korido za chumba kimoja na seble na watoto 6 wakubwa unajiuliza Hadi unachoka.
Nyama tunawaachia wengine sisi tunakula miguu ya kuku.
 
Ukitaka kujua utamu wa dafu hadi uchokonoe ndani.

Huwezi kupita ukiwa ndani ya basi uka judge umasikini au utajiri wa sehemu.
Definition ya utajiri au umasikini ina vigezo vingi mno hata Marekani tunasema ni taifa lililoendelea lakini kuna sehemu ukipita vijijini hata baadhi ya miji kama Memphis unaweza sema afadhali Dar Tandale.

Nikupe mfano kuna sehemu ukienda Zambia unaweza kuta nyumba za majani ila unakuta nje kuna VX Limepaki nje la milioni250.Ukienda Tabora unaweza kuta vijijini vingine nyumba za majani lakini madirisha ya vioo tinted a dish nje la mitandao.Kwa vigezo vyako hao huwezi kuwaita ni watu masikini ni utamaduni wao.
Je mtu kama ana uhakika wa kula kwa mwaka mzima chakula kizuri cha afya ila nyumba yake ni ya majani huwezi kumuweka huyo mtu kwenye kundi la umasikini.Usipime vigezo vya umasikini na utajiri kwa mijengo peke yake yapo mambo mengi ya kuangalia.

Mtu wa kijijini ana magunia 300 ya mahindi na 300 ya mchele 100 ya mtama.Na hayo magunia ni ajili yake tu kula na familia yake.Mifugo kadhaa ya kuku na ng'ombe 300 wako porini machungani.Ana tractor na analima chakula chake na cha kuuza cha ziada nyumba yake ni ya majani kulingana na jadi yao.Ana tractor la kulimia huyu utamuita masikini?.
Mwingine anaishi mjini ana nyumba ya ghorofa moja ila kajenga kwa mkopo na nyumba iko kwenye bondi.Madali wa Majembe auction mart wanakwepana anadaiwa kati ya mtu huyu na huyo mwenye nyumba ya majani ni nani tajiri na nani masikini?

Hata huko Lindi na Ruangwa unakokuongelea ukipita barabarani kwa vigezo vyako utaona ni masikini lakini ukiingia ndani ndani unaweza kuta watu wana maendeleo ya ajabu.Mara nyingi matajiri hawapendi kukaa sehemu zenye misongamano nenda hata Marekani ma Celebrity uone wanapoweka mijengo yao wanakuwa na hadi viwanja vyao vya ndege binafsi

Hata Kilimanjaro wanasifiwa wameendelea lakini mji wa Moshi wenyewe ukiuona utaona wa kawaida.Ukipita sehemu za wapare utaona mpauko na kama nusu jangwa.
Sasa kwa kilimanjaro na upareni kwa ujumla maendeleo hayako unavoona ukiwa kwenye basi panda kule juu milimani uone matusi yao.
Kule unakuta mtu ana umri wa miaka 65 amezaliwa amekuta bomba la maji nyumbani kwao hawajui kitu kinaitwa kuteka maji kichwani na kuna mijengo ya hatari maendeleo ya shule na vyuo ndio usiseme.Wajerumani walifika kule mapema sana wakajenga makanisa na shule za misheni hata Ndanda Mtwara.

Nenda kwa kina Nshomile utakuta hali kama ya Kilimanjaro na Mbeya
Usi judge maendeleo ya watu ukiwa umekaa kwenye basi pata muda teremka ingia ndani ndani.

Nimekuwekea picha moja chini nilikwenda siku moja Upareni acha pale chini Mwanga palipokauka ukame nilipanda sehemu moja inaitwa Usangi milimani kabisa juu hadi kule ni lami na ni kijani kibichi tulikwenda.
kwenye msiba nikaona nyumba kama hiyo hapo unaweza sehemu hao wapare ni masikini hawana maendeleo?.Cha ajabu sijakutana na nyumba ya majani hata moja achilia angalau iliyopigiliwa mabati ya madebe.
Tembea ujione usingoje kuambiwa aliimba marehemu Dr Remmy Ongala.
 

Attachments

  • uparekijijini.jpg
    uparekijijini.jpg
    207.1 KB · Views: 8
Ukitaka kujua utamu wa dafu hadi uchokonoe ndani.

Huwezi kupita ukiwa ndani ya basi uka judge umasikini au utajiri wa sehemu.
Definition ya utajiri au umasikini ina vigezo vingi mno hata Marekani tunasema ni taifa lililoendelea lakini kuna sehemu ukipita vijijini hata baadhi ya miji kama Memphis unaweza sema afadhali Dar Tandale.

Nikupe mfano kuna sehemu ukienda Zambia unaweza kuta nyumba za majani ila unakuta nje kuna VX Limepaki nje la milioni250.Ukienda Tabora unaweza kuta vijijini vingine nyumba za majani lakini madirisha ya vioo tinted a dish nje la mitandao.Kwa vigezo vyako hao huwezi kuwaita ni watu masikini ni utamaduni wao.
Je mtu kama ana uhakika wa kula kwa mwaka mzima chakula kizuri cha afya ila nyumba yake ni ya majani huwezi kumuweka huyo mtu kwenye kundi la umasikini.Usipime vigezo vya umasikini na utajiri kwa mijengo peke yake yapo mambo mengi ya kuangalia.

Mtu wa kijijini ana magunia 300 ya mahindi na 300 ya mchele 100 ya mtama.Na hayo magunia ni ajili yake tu kula na familia yake.Mifugo kadhaa ya kuku na ng'ombe 300 wako porini machungani.Ana tractor na analima chakula chake na cha kuuza cha ziada nyumba yake ni ya majani kulingana na jadi yao.Ana tractor la kulimia huyu utamuita masikini?.
Mwingine anaishi mjini ana nyumba ya ghorofa moja ila kajenga kwa mkopo na nyumba iko kwenye bondi.Madali wa Majembe auction mart wanakwepana anadaiwa kati ya mtu huyu na huyo mwenye nyumba ya majani ni nani tajiri na nani masikini?

Hata huko Lindi na Ruangwa unakokuongelea ukipita barabarani kwa vigezo vyako utaona ni masikini lakini ukiingia ndani ndani unaweza kuta watu wana maendeleo ya ajabu.Mara nyingi matajiri hawapendi kukaa sehemu zenye misongamano nenda hata Marekani ma Celebrity uone wanapoweka mijengo yao wanakuwa na hadi viwanja vyao vya ndege binafsi

Hata Kilimanjaro wanasifiwa wameendelea lakini mji wa Moshi wenyewe ukiuona utaona wa kawaida.Ukipita sehemu za wapare utaona mpauko na kama nusu jangwa.
Sasa kwa kilimanjaro na upareni kwa ujumla maendeleo hayako unavoona ukiwa kwenye basi panda kule juu milimani uone matusi yao.
Kule unakuta mtu ana umri wa miaka 65 amezaliwa amekuta bomba la maji nyumbani kwao hawajui kitu kinaitwa kuteka maji kichwani na kuna mijengo ya hatari maendeleo ya shule na vyuo ndio usiseme.Wajerumani walifika kule mapema sana wakajenga makanisa na shule za misheni hata Ndanda Mtwara.

Nenda kwa kina Nshomile utakuta hali kama ya Kilimanjaro na Mbeya
Usi judge maendeleo ya watu ukiwa umekaa kwenye basi pata muda teremka ingia ndani ndani.

Nimekuwekea picha moja chini nilikwenda siku moja Upareni acha pale chini Mwanga palipokauka ukame nilipanda sehemu moja inaitwa Usangi milimani kabisa juu hadi kule ni lami na ni kijani kibichi tulikwenda.
kwenye msiba nikaona nyumba kama hiyo hapo unaweza sehemu hao wapare ni masikini hawana maendeleo?.Cha ajabu sijakutana na nyumba ya majani hata moja achilia angalau iliyopigiliwa mabati ya madebe.
Tembea ujione usingoje kuambiwa aliimba marehemu Dr Remmy Ongala.
Unasema nyumba na majengo hazipimi umasikini halafu chini unaniwekea picha ya jengo zuri kijijini kuonesha kuwa umasikini upo chini
Make it make sense please
 
Tanzania matajiri wa kweli WACHACHE sana, wengi wapigaji tu na 10% za udalali wa kila kitu, pamoja na Rushwa. Na ndo maana huwezi kuona impact sana ya hao wanaojiita so matajiri.Hauoni kila mtu anakimbilia kwenye siasa, awe mbunge, sasa hivi hadi Udiwani watu wanataka kutoana macho -ni ujanja ujanja.
Middle class hapo imejaa mikopo na madeni sio mchezo....
Hii bongo watu wamechoka sana, na usishtushwe na magari sijui nyumba, hivyo vinaficha umaskini na hofu ya maisha kwa walio wengi.
Matajiri wa kweli wapo bana sio kweli na wanaogombea udiwani ni wangapi bwashee mpaka useme matajiri hakuna aisee mtu anunue Ford Raptor la 2023 kodi Tsh 46m harafu useme wananunua kuficha umasikini sio kweli aisee.
 
Unasema nyumba na majengo hazipimi umasikini halafu chini unaniwekea picha ya jengo zuri kijijini kuonesha kuwa umasikini upo chini
Make it make sense please
hili nalijua sana na najua nilichofanya
Nia yangu nikukuonyesha kuwa usipite kwenye basi tu unaona nyumba za ajabu uka conclude umasikini wa nchi nzima.
Tembea interior zaidi
Hata kwenye statistics utafiti wako haujakaa sawa ulichofanya ni random sampling
Na inategemea wakati unafanya hiyo sampling ulipita maeneo gani.
Collect enough data to make a conclusion.
Hata hivyo ndugu yangu nikupongeze na nisikukatishe tamaa umefanya vizuri kutuamsha kwa kweli kazi yako nzuri
 
hili nalijua sana na najua nilichofanya
Nia yangu nikukuonyesha kuwa usipite kwenye basi tu unaona nyumba za ajabu uka conclude umasikini wa nchi nzima.
Tembea interior zaidi
Hata kwenye statistics utafiti wako haujakaa sawa ulichofanya ni random sampling
Na inategemea wakati unafanya hiyo sampling ulipita maeneo gani.
Collect enough data to make a conclusion.
Hata hivyo ndugu yangu nikupongeze na nisikukatishe tamaa umefanya vizuri kutuamsha kwa kweli kazi yako nzuri
Sawa mkuu nimekuelewa. Nitafanya utafiti lakini hili suala tunasoma hata shuleni na vyuoni kuwa umasikini Tanzania upo kwa kiwango kikubwa na ni moja ya nchi zenye masikini wengi zaidi Africa (takribani milioni 28) meaning kila utafiti unaofanyika unaleta matokeo yaleyale
 
Sawa mkuu nimekuelewa. Nitafanya utafiti lakini hili suala tunasoma hata shuleni na vyuoni kuwa umasikini Tanzania upo kwa kiwango kikubwa na ni moja ya nchi zenye masikini wengi zaidi Africa (takribani milioni 28) meaning kila utafiti unaofanyika unaleta matokeo yaleyale
Halafu upande mwingine wa shillingi ni ajabu kwa kweli halafu moja ya nchi zenye utajiri mkubwa wa mali asili ni Tanzania.
Kwa nchi za Africa mashariki chukua Burundi,Rwanda,Kenya,Uganda,Tanzania sisi tunaongoza kwa rasilimali misitu,madini,mbuga za wanyama.
Ajabu ni masikini ukiiachia Burundi
Uganda wakianza kuchimba mafuta yao watatuzidi mbali sana.
Je sababu ni nini?
Siasa?
Baba wa taifa moja ya mistake aliyofanya ni kuleta ile siasa ya ujamaa na siasa nyingi sana.Hii imetu affect vizazi hadi vizazi tumeshaamka ila tumechelewa.
Sisi maneno ni mengi mno kuliko vitendo.
Tunatumia hela nyingi mno kwenye mambo ya chaguzi sisizo na mashiko kisa tu chama flani kisishinde.
Ndio maana watani jirani zetu Kenya wanapenda kututania kuwa wa TZ longo longo nyingi sana.
Askari wa Kenya akimkamata mtanzania hataki kubishana naye anajua atamshinda.
 
Back
Top Bottom