Nostradamus
JF-Expert Member
- Jun 8, 2009
- 392
- 6
Kitu kikubwa ambacho Watanzania hatuwezi kukikubali ni kwamba hatujui tulikotoka,tuliko na tuendako, na hivyo basi hatujui tumejikwaa wapi,tumeangukia wapi na tutainukia wapi.
Tukijaribu kuangalia awamu nne ambazo zimetawala nchi hii,ni awamu ya JAKAYA KIKWETE ndiyo ambayo amekumbana na CHALLENGE nyingi na akaweza (kama sio kujaribu) kuzikabili kiungwana.
Nikianza na awamu ya MWALIMU,ambayo ilikuwa awamu ya kwanza,Yeye alikuwa na uzalendo wa kweli ambao kwa viwango vya binadamu wa sasa huwezi kuvikuta,aliishi maisha yale anayoyahubiri na aliamini katika haki ,ukweli,uzalendo na uchapakazi.na kupitia hayo,aliweza kujenga misingi imara sana katika nchi changa sana.Misingi ambayo Wabenzi wanajaribu kuibomoa lakini wameshindwa ingawa ki ukweli wanaitikisa.Aliiacha nchi ikiwa ina uchumi mzuri,utawala bora na kiwango cha chini kabisa cha rushwa kuliko kipindi chohote cha tawala nyingine.Nchi iliendeshwa kwa dira na mipango inayotekelezeka.
Sheikh,Alhaj ALLY HASSAN MWINYI,hakuwa na vission wala mission.alijaribu kuiga kama alivyotawala Mwalimu bila kujua mwalimu hakuwa binadamu wa kawaida katika zama hizi.mwishowe Mwinyi alivyoona hawezi akaamua kuacha Taifa lijipeleke vile litakavyo.Na hapo ndipo wale chui waliojivika ngozi ya kondoo ili kumuhadaa Kambarage,wakaamua kuvua ngozi zao na kuonyesha makucha yao.Na huu ndio ulikuwa mwanzo wa mparaganyiko tunaoushuhudia sasa.Uungwana na kutokuwa mkali katika mambo ya msingi akiwa kama Raisi kulisababishwa kuanza kujengeka kwa tabaka la mafisadi ambalo lilikuwa linaomba kila siku Mwalimu Kambarage aondoke duniani.
Ujio wa BEN WILLY MKAPA na kifo cha mwalimu Nyerere,kilifungua rasmi milango na kuondoa hofu toka kwa wale waliokuwa wakiitamani nafasi hiyo.Wakisaidiwa na Mkapa mwenyewe kama fisadi namba moja na mkuu wa nchi,walifanya kile ambacho kila mmoja wetu anakifahamu.Na kibaya za ni kitendo cha kushawishi na kufanikiwa kuliingiza Jeshi la wananchi wa tanzania(JWTZ) kushiriki katika uovu huo(rejea report ya mwanakijiji juu ya Meremeta).Jeshi lililokuwa likisifika kwa uzalendo,nidhamu na uchapakazi,likageuzwa kuwa ni tawi la mafisadi kufanya ufisadi wao.
Kama ni kujikwaa,basi hapo ndipo Nchi yetu ilipojikwaa,na lilikuwa ni pigokubwa kiasi ambacho,kuja kujipanga sawa itachukua muda mrefu sana ama tuwe tayari kujitolea damu zetu na wapendwa wetu kwa ajili ya kuiokoa nchi yetu.Ben Mkapa ana deni kubwa kwa nchi hii kiasi ambacho hata mbinguni hataweza kulilipa.Ule uchumi uliokuwa haujatengemaa vizuri tangu kipindi cha mwalimu,ukaja kusambaratika kipindi cha Mkapa,rasilimali zilizokuwa zikimilikiwa na serikali zikagawanywa katika kipindi hichohicho(naye akajigawanyia),Hata maliasili ambazo Mwalimu alisema hazitakuja oza hivyo zinaweza kusubiri,nazo ziligawanywa.
Uzalendo,undugu baina ya watanzania, na mapenzi kwa nchi vilifia hapo.na Mkapa alijua hilo na alifanya kwa makusudi.Mbaya zaidi alikuwa anajua nguvu ya KIKWETE katika CCM,na hivyo palikuwa hakuna uwezekano wa kumzuia kikwete kuchukua madaraka pindi muda ukifika.Ukijumlisha na uzalendo pamoja na record ya Jakaya katika utumishi wake,waliamua kutengeneza mazingira ambayo yatamuweka Jakaya katika nafasi ambayo hata yeye KIKWETE ataguswa endapo atataka kuwashuhulikia wahalifu.
Kikwete hakujua mkakati wa wanamtandao,mkakati wakum beba kikwete kwa kutumia fedha zao kutokana na urafiki baina yao.lakini kumbe wale vinara wa mtandao hawakuwa tayari kutoa fedha zao mfukoni bali ni kuunda makampuni hewa kwa maelekezo ya Mkapa ili fedha hizo zitumike kupigia kampeni Kikwete.Kitanzi kikawa kimeshaingia shingoni mwa Jakaya na kinamtesa hadi LEO.
Ninachomsikitikia ndugu yangu Kikwete ni kwamba,uzalendo anao,dhamira anayo na uwezo anao ila hana moyo wa kijasiri kupambana na hali hiyo au kuwatosa marafiki zake waliomfikisha hapo.Na hilo ndio anguko la raisi wetu.
Lakini ukiangalia sana,Jakaya hakuna kubwa alilolifanya la kumlamu zaidi ya kushindwa kuwachukulia hatua wahalifu wa serikali ya awamu ya tatu.Na huenda hilo ndio lilanalomuondolea sifa ya kuwa kiongozi bora na makini na hivyo kusababisha umaarufu wake uliomuingiza madarakani kwa kishindo kuporomoka.
Binafsi nayatazama mambo katika mtazamo huo,kuwa, tuliyumba awamu ya pili,tukajikwaa awamu ya tatu na sasa tumeanguka katika awamu ya nne.SASA JE! tujilaumu tulipojikwaa au tulipoangukia!!!
jibu kichwani mwako,
HATA UKIPEWA KAZI YA USHAURI KWA RAISI HUTAWEZA KUBADILISHA CHOCHOTE,Kwani raisi kama taasisi alishavikwa kitanzi ambacho asipokaka kimya,maadui wanavuta na kunyonga.hivyo usipoangalia utajikuta kazi yako ya ushauri utaona haithaminiwi nawe utageuka kuwa kama wao.
nawasilisha
Tukijaribu kuangalia awamu nne ambazo zimetawala nchi hii,ni awamu ya JAKAYA KIKWETE ndiyo ambayo amekumbana na CHALLENGE nyingi na akaweza (kama sio kujaribu) kuzikabili kiungwana.
Nikianza na awamu ya MWALIMU,ambayo ilikuwa awamu ya kwanza,Yeye alikuwa na uzalendo wa kweli ambao kwa viwango vya binadamu wa sasa huwezi kuvikuta,aliishi maisha yale anayoyahubiri na aliamini katika haki ,ukweli,uzalendo na uchapakazi.na kupitia hayo,aliweza kujenga misingi imara sana katika nchi changa sana.Misingi ambayo Wabenzi wanajaribu kuibomoa lakini wameshindwa ingawa ki ukweli wanaitikisa.Aliiacha nchi ikiwa ina uchumi mzuri,utawala bora na kiwango cha chini kabisa cha rushwa kuliko kipindi chohote cha tawala nyingine.Nchi iliendeshwa kwa dira na mipango inayotekelezeka.
Sheikh,Alhaj ALLY HASSAN MWINYI,hakuwa na vission wala mission.alijaribu kuiga kama alivyotawala Mwalimu bila kujua mwalimu hakuwa binadamu wa kawaida katika zama hizi.mwishowe Mwinyi alivyoona hawezi akaamua kuacha Taifa lijipeleke vile litakavyo.Na hapo ndipo wale chui waliojivika ngozi ya kondoo ili kumuhadaa Kambarage,wakaamua kuvua ngozi zao na kuonyesha makucha yao.Na huu ndio ulikuwa mwanzo wa mparaganyiko tunaoushuhudia sasa.Uungwana na kutokuwa mkali katika mambo ya msingi akiwa kama Raisi kulisababishwa kuanza kujengeka kwa tabaka la mafisadi ambalo lilikuwa linaomba kila siku Mwalimu Kambarage aondoke duniani.
Ujio wa BEN WILLY MKAPA na kifo cha mwalimu Nyerere,kilifungua rasmi milango na kuondoa hofu toka kwa wale waliokuwa wakiitamani nafasi hiyo.Wakisaidiwa na Mkapa mwenyewe kama fisadi namba moja na mkuu wa nchi,walifanya kile ambacho kila mmoja wetu anakifahamu.Na kibaya za ni kitendo cha kushawishi na kufanikiwa kuliingiza Jeshi la wananchi wa tanzania(JWTZ) kushiriki katika uovu huo(rejea report ya mwanakijiji juu ya Meremeta).Jeshi lililokuwa likisifika kwa uzalendo,nidhamu na uchapakazi,likageuzwa kuwa ni tawi la mafisadi kufanya ufisadi wao.
Kama ni kujikwaa,basi hapo ndipo Nchi yetu ilipojikwaa,na lilikuwa ni pigokubwa kiasi ambacho,kuja kujipanga sawa itachukua muda mrefu sana ama tuwe tayari kujitolea damu zetu na wapendwa wetu kwa ajili ya kuiokoa nchi yetu.Ben Mkapa ana deni kubwa kwa nchi hii kiasi ambacho hata mbinguni hataweza kulilipa.Ule uchumi uliokuwa haujatengemaa vizuri tangu kipindi cha mwalimu,ukaja kusambaratika kipindi cha Mkapa,rasilimali zilizokuwa zikimilikiwa na serikali zikagawanywa katika kipindi hichohicho(naye akajigawanyia),Hata maliasili ambazo Mwalimu alisema hazitakuja oza hivyo zinaweza kusubiri,nazo ziligawanywa.
Uzalendo,undugu baina ya watanzania, na mapenzi kwa nchi vilifia hapo.na Mkapa alijua hilo na alifanya kwa makusudi.Mbaya zaidi alikuwa anajua nguvu ya KIKWETE katika CCM,na hivyo palikuwa hakuna uwezekano wa kumzuia kikwete kuchukua madaraka pindi muda ukifika.Ukijumlisha na uzalendo pamoja na record ya Jakaya katika utumishi wake,waliamua kutengeneza mazingira ambayo yatamuweka Jakaya katika nafasi ambayo hata yeye KIKWETE ataguswa endapo atataka kuwashuhulikia wahalifu.
Kikwete hakujua mkakati wa wanamtandao,mkakati wakum beba kikwete kwa kutumia fedha zao kutokana na urafiki baina yao.lakini kumbe wale vinara wa mtandao hawakuwa tayari kutoa fedha zao mfukoni bali ni kuunda makampuni hewa kwa maelekezo ya Mkapa ili fedha hizo zitumike kupigia kampeni Kikwete.Kitanzi kikawa kimeshaingia shingoni mwa Jakaya na kinamtesa hadi LEO.
Ninachomsikitikia ndugu yangu Kikwete ni kwamba,uzalendo anao,dhamira anayo na uwezo anao ila hana moyo wa kijasiri kupambana na hali hiyo au kuwatosa marafiki zake waliomfikisha hapo.Na hilo ndio anguko la raisi wetu.
Lakini ukiangalia sana,Jakaya hakuna kubwa alilolifanya la kumlamu zaidi ya kushindwa kuwachukulia hatua wahalifu wa serikali ya awamu ya tatu.Na huenda hilo ndio lilanalomuondolea sifa ya kuwa kiongozi bora na makini na hivyo kusababisha umaarufu wake uliomuingiza madarakani kwa kishindo kuporomoka.
Binafsi nayatazama mambo katika mtazamo huo,kuwa, tuliyumba awamu ya pili,tukajikwaa awamu ya tatu na sasa tumeanguka katika awamu ya nne.SASA JE! tujilaumu tulipojikwaa au tulipoangukia!!!
jibu kichwani mwako,
HATA UKIPEWA KAZI YA USHAURI KWA RAISI HUTAWEZA KUBADILISHA CHOCHOTE,Kwani raisi kama taasisi alishavikwa kitanzi ambacho asipokaka kimya,maadui wanavuta na kunyonga.hivyo usipoangalia utajikuta kazi yako ya ushauri utaona haithaminiwi nawe utageuka kuwa kama wao.
nawasilisha