Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
MPENDWA msomaji, unafikiri Rais Jakaya Kikwete ana watu wanaomshauri juu ya mambo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa?
Unafikiri wapo watu wanaomshauri kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi?
Kwa kuangalia mambo mbalimbali yanayoendelea leo nchini unaweza kuamini kuwa kuna watu wanalipwa mamilioni kumshauri rais? Kwa kupima yale yanayofanywa na serikali unaweza kufikiria kuwa ushauri unaotolewa kwa rais ni mzuri?
Kama tukiweka kipimo cha uzuri na ubaya kati ya moja na kumi, moja ikiwa ni mbaya sana na kumi ni mzuri sana; utaupa namba gani ushauri anaopewa Kikwete kuhusu masuala mbalimbali ya nchi?
Ukiniuliza mimi maswali hayo, jibu langu ni jepesi; yeyote anayemshauri rais leo hii angekuwa hana kazi siku ya kwanza alipofungua mdomo wake. Sitanii.
Kuna mlolongo wa mambo ambayo yamefanywa na Ikulu ambayo kwa hakika yamenifanya nijihoji kama ninaota au nasinzia; mambo ambayo tukiyaangalia kwa karibu tutaona kuwa kuna mtu aidha hatoi ushauri mzuri au ushauri wake ni mbaya.
Ni kwa sababu basi, nimeamua kujitolea kwa mara nyingi kuwa mshauri wa bure wa rais na naahidi kumshauri vizuri na kwa manufaa ya taifa tu.
Sitampa ushauri wowote ule wa kumfanya aonekane mzuri au kufanya Ikulu ionekane vizuri. Nitampa ushauri ambao utamhakikishia mambo anayoyafanya na maamuzi anayochukua yote ni kwa masilahi ya taifa tu.
Ushauri huo nitautoa kwa uwazi na ukweli lakini vile vile kwa usiri mkubwa. Naahidi sitatoa siri za ushauri ninaompa rais na hivyo kumhakikishia mazungumzo yetu yanabakia kifuani mwangu daima.
Hivyo nimeamua kuomba kuwa mshauri wa bure wa rais. Ili kuonyesha kuwa ushauri wangu yawezekana ukawa ni bora kuliko ule uliotolewa hadi hivi nitatoa mifano michache ambayo ningemshauri rais tofauti na inavyoonekana alishauriwa hivi sasa.
Kuhusu uamuzi wa Bunge juu ya Richmond
Badala ya kumwachia waziri mkuu kuanzisha uchunguzi mwingine nje ya ule uliofanywa na Bunge, ningemshauri rais kuagiza kuwa uamuzi wote uliotolewa na Bunge uwe umetekelezwa ndani ya siku saba.
Ningemshauri kuwa kwa vile Bunge ndilo lina jukumu la kuisimamia serikali, basi uamuzi wowote wa waziri mkuu au mtu mwingine kuanzisha uchunguzi mwingine wa jambo lililochunguzwa na kuamuliwa na Bunge utakuwa ni uvunjaji wa katiba na dharau kwa Bunge.
Hivyo, ningemshauri rais kuwataka Johnson Mwanyika, Edward Hosea na wengine wote waliotakiwa kuwajibishwa kuwasilisha barua zao za kujiuzulu mara moja.
Kama angesikiliza ushauri huo, hili suala la Richmond lingekuwa limemalizwa mwezi Machi mwaka jana. Hivyo, ushauri wangu kwa rais ungekuwa wa kutii kwa kutekeleza uamuzi wa Bunge bila kusita (without reservation).
Kuhusu ufisadi Benki Kuu
Kwa vile mimi ndiye ningekuwa mshauri mkuu wa rais, basi jambo la kwanza ambalo ningemshauri kuhusu Benki Kuu ni kuwasimamisha mara moja watumishi wote wa umma pale ripoti ya Deloitte & Touche ilipotoka na mapendekezo ya kuanzisha uchunguzi.
Ningemshauri asipoteze muda kwa kuwavumilia, bali kufanya haraka na kwa wepesi uchunguzi huru na kuhakikisha wahusika wote wanashughulikiwa mara moja.
Hivyo, nisingemshauri kuunda kamati nyingine, bali kumshauri amuagize Mwendesha Mashitaka Mkuu kuleta mashitaka kwa wahusika wote, akipata ushirikiano wa kipelelezi kutoka Idara ya Upelelezi (CID).
Kwa vile suala la Benki Kuu ni nyeti na linahusu moyo hasa wa uchumi wa taifa letu, ningemshauri aialike taasisi kama Scotland Yard au SFO kuendesha uchunguzi wa suala zima la EPA na CIS na madudu mengine yote yanayodaiwa kuendelea Benki Kuu.
Kwa kufanya hivyo, rais angeonekana ni mwamuzi asiyesita (decisive) na angeonyesha amelipa uzito unaostahili jambo hilo. Kama angenisikiliza, basi mambo yote ya Benki Kuu yangekuwa yamefikia mahali patamu leo hii.
Kuhusu suala la Kagoda
Kwa vile suala la Kagoda katika EPA linaonekana kuwatatiza watendaji, ningemshauri atumie kanuni ya "liwalo na liwe". Kwamba haiwezekani kampuni moja ichote sh bilioni 40 halafu watu waendelee kuremburiana macho na kutomasana huku wakicheka cheka.
Ningemshauri kumwagiza Mwendesha Mashitaka kuleta mashitaka yanayostahili mara moja dhidi ya wale ambao tayari anajua wanahusika kwa namna moja au nyingine na suala la Kagoda.
Kama Mwendesha Mashitaka angesema kuwa anaogopa kuwakamata wahusika kwa sababu wataitikisa nchi, basi ningemshauri rais amwajibishe mara moja na kumweka mtu ambaye yuko tayari kuitii sheria kwa gharama yoyote na si mawazo yake.
Suala la Meremeta
Kwanza ningemshauri Rais amwambie Waziri Mkuu asiwaongopee wananchi. Ningemshauri amwambie Waziri Mkuu afute kauli yake kuwa suala la Meremeta ni suala la ulinzi na kama angekataa basi ningemshauri rais amwondoe waziri mkuu na kuunda baraza jipya la mawaziri.
Ningemshauri rais alihutubie taifa juu ya machafu ya Meremeta yaliyofanywa na utawala uliopita na kuliambia kuhusu uhusiano wa aibu ya serikali na watu ambao huko nyuma wamekuwa ni mamluki wa kivita kwenye machafuko ya Angola, Sierra Leone, DRC na Liberia.
Ningemshauri rais awaambie wananchi kuwa suala la Meremeta ni la aibu na kuwa viongozi waliopita waliruhusu mamluki kutumia ardhi yetu kuchota utajiri wetu ili kufadhili shughuli zao haramu!
Ningemshauri rais kuwaambia wananchi kuwa ule uwanja wa ndege ambao ulijengwa katika moja ya migodi yetu hapa nchini ulikuwa unatumika kwa shughuli za kusafirisha nje utajiri wetu kama watu hao hao walivyofanya huko Uganda.
Hivyo, ningemshauri kufuta makubaliano yoyote kati ya Tanzania na watu hawa au makampuni yao mengine ambayo leo yamepewa maeneo mengine ya kutafuta mafuta na dhahabu. Hii, ningemwambia ingeirudishia Tanzania heshima yake inayostahili.
Kuhusu Muungano
Suala la Muungano nisingemshauri lolote kwani sidhani kama ana nia, uwezo au uthubutu wa kulishughulikia kwa jinsi ambavyo naamini ingeweza kuulinda Muungano wetu, kudumisha udugu na kuhakikisha kuwa Bara wanafurahi, Zanzibar wanafurahi na Watanzania wote wanafurahia, na wakati huo huo kila mmoja anajijua kuna kitu amepungukiwa lakini wanakubali upungufu huo kwani katika kupungukiwa kwao wanaweza kuona haja ya umoja wao.
Kuhusu CCM
Sasa kwa vile nitakuwa mshauri wa rais nadhani haitakuwa vibaya kumshauri pia kuhusu chama chake. Kwa sababu utawala ulioko madarakani unatokana na chama chake, basi nitamtendea hisani nikimshauri jambo moja kubwa, nalo ni kuitisha mkutano mkuu maalumu wa CCM ili wafukuzane uanachama.
Kabla ya hapo, kwanza ningemshauri amshawishi Andrew Chenge, Rostam Aziz na wengine kujiuzulu nyadhifa zao. Tena, sasa hivi itakuwa vizuri kwani hakuna uchaguzi mdogo wowote unaoweza kufanyika hadi uchaguzi mkuu. Katika kufanya hivyo atajionyesha kuwa amekidhibiti chama na anaonyesha uongozi.
Kuhusu washauri wake wa sasa
Kwa jinsi walivyoboronga masuala mbalimbali, ningemshauri kabla hatujaenda mbali awatimue kwanza washauri wake wa sasa na wale wanaoitwa ‘wasemaji' wake. Kwa sababu kundi hilo linatia aibu katika fani nzima ya kuwa mzungumzaji wa ofisi ya juu kabisa nchini.
Wakati mwingine nafikiria hawa jamaa wanafanya makusudi ili kumuaibisha Rais au wamelewa ving'ora vya pale Ikulu kiasi kwamba wanafikiri wanaweza kusema lolote kwa jina la rais!
Nina mambo mengine mengi ya kuweza kumshauri. Najua kwa kufanya hivyo sasa tatizo litakuja, je, atakubali?
Unafikiri wapo watu wanaomshauri kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi?
Kwa kuangalia mambo mbalimbali yanayoendelea leo nchini unaweza kuamini kuwa kuna watu wanalipwa mamilioni kumshauri rais? Kwa kupima yale yanayofanywa na serikali unaweza kufikiria kuwa ushauri unaotolewa kwa rais ni mzuri?
Kama tukiweka kipimo cha uzuri na ubaya kati ya moja na kumi, moja ikiwa ni mbaya sana na kumi ni mzuri sana; utaupa namba gani ushauri anaopewa Kikwete kuhusu masuala mbalimbali ya nchi?
Ukiniuliza mimi maswali hayo, jibu langu ni jepesi; yeyote anayemshauri rais leo hii angekuwa hana kazi siku ya kwanza alipofungua mdomo wake. Sitanii.
Kuna mlolongo wa mambo ambayo yamefanywa na Ikulu ambayo kwa hakika yamenifanya nijihoji kama ninaota au nasinzia; mambo ambayo tukiyaangalia kwa karibu tutaona kuwa kuna mtu aidha hatoi ushauri mzuri au ushauri wake ni mbaya.
Ni kwa sababu basi, nimeamua kujitolea kwa mara nyingi kuwa mshauri wa bure wa rais na naahidi kumshauri vizuri na kwa manufaa ya taifa tu.
Sitampa ushauri wowote ule wa kumfanya aonekane mzuri au kufanya Ikulu ionekane vizuri. Nitampa ushauri ambao utamhakikishia mambo anayoyafanya na maamuzi anayochukua yote ni kwa masilahi ya taifa tu.
Ushauri huo nitautoa kwa uwazi na ukweli lakini vile vile kwa usiri mkubwa. Naahidi sitatoa siri za ushauri ninaompa rais na hivyo kumhakikishia mazungumzo yetu yanabakia kifuani mwangu daima.
Hivyo nimeamua kuomba kuwa mshauri wa bure wa rais. Ili kuonyesha kuwa ushauri wangu yawezekana ukawa ni bora kuliko ule uliotolewa hadi hivi nitatoa mifano michache ambayo ningemshauri rais tofauti na inavyoonekana alishauriwa hivi sasa.
Kuhusu uamuzi wa Bunge juu ya Richmond
Badala ya kumwachia waziri mkuu kuanzisha uchunguzi mwingine nje ya ule uliofanywa na Bunge, ningemshauri rais kuagiza kuwa uamuzi wote uliotolewa na Bunge uwe umetekelezwa ndani ya siku saba.
Ningemshauri kuwa kwa vile Bunge ndilo lina jukumu la kuisimamia serikali, basi uamuzi wowote wa waziri mkuu au mtu mwingine kuanzisha uchunguzi mwingine wa jambo lililochunguzwa na kuamuliwa na Bunge utakuwa ni uvunjaji wa katiba na dharau kwa Bunge.
Hivyo, ningemshauri rais kuwataka Johnson Mwanyika, Edward Hosea na wengine wote waliotakiwa kuwajibishwa kuwasilisha barua zao za kujiuzulu mara moja.
Kama angesikiliza ushauri huo, hili suala la Richmond lingekuwa limemalizwa mwezi Machi mwaka jana. Hivyo, ushauri wangu kwa rais ungekuwa wa kutii kwa kutekeleza uamuzi wa Bunge bila kusita (without reservation).
Kuhusu ufisadi Benki Kuu
Kwa vile mimi ndiye ningekuwa mshauri mkuu wa rais, basi jambo la kwanza ambalo ningemshauri kuhusu Benki Kuu ni kuwasimamisha mara moja watumishi wote wa umma pale ripoti ya Deloitte & Touche ilipotoka na mapendekezo ya kuanzisha uchunguzi.
Ningemshauri asipoteze muda kwa kuwavumilia, bali kufanya haraka na kwa wepesi uchunguzi huru na kuhakikisha wahusika wote wanashughulikiwa mara moja.
Hivyo, nisingemshauri kuunda kamati nyingine, bali kumshauri amuagize Mwendesha Mashitaka Mkuu kuleta mashitaka kwa wahusika wote, akipata ushirikiano wa kipelelezi kutoka Idara ya Upelelezi (CID).
Kwa vile suala la Benki Kuu ni nyeti na linahusu moyo hasa wa uchumi wa taifa letu, ningemshauri aialike taasisi kama Scotland Yard au SFO kuendesha uchunguzi wa suala zima la EPA na CIS na madudu mengine yote yanayodaiwa kuendelea Benki Kuu.
Kwa kufanya hivyo, rais angeonekana ni mwamuzi asiyesita (decisive) na angeonyesha amelipa uzito unaostahili jambo hilo. Kama angenisikiliza, basi mambo yote ya Benki Kuu yangekuwa yamefikia mahali patamu leo hii.
Kuhusu suala la Kagoda
Kwa vile suala la Kagoda katika EPA linaonekana kuwatatiza watendaji, ningemshauri atumie kanuni ya "liwalo na liwe". Kwamba haiwezekani kampuni moja ichote sh bilioni 40 halafu watu waendelee kuremburiana macho na kutomasana huku wakicheka cheka.
Ningemshauri kumwagiza Mwendesha Mashitaka kuleta mashitaka yanayostahili mara moja dhidi ya wale ambao tayari anajua wanahusika kwa namna moja au nyingine na suala la Kagoda.
Kama Mwendesha Mashitaka angesema kuwa anaogopa kuwakamata wahusika kwa sababu wataitikisa nchi, basi ningemshauri rais amwajibishe mara moja na kumweka mtu ambaye yuko tayari kuitii sheria kwa gharama yoyote na si mawazo yake.
Suala la Meremeta
Kwanza ningemshauri Rais amwambie Waziri Mkuu asiwaongopee wananchi. Ningemshauri amwambie Waziri Mkuu afute kauli yake kuwa suala la Meremeta ni suala la ulinzi na kama angekataa basi ningemshauri rais amwondoe waziri mkuu na kuunda baraza jipya la mawaziri.
Ningemshauri rais alihutubie taifa juu ya machafu ya Meremeta yaliyofanywa na utawala uliopita na kuliambia kuhusu uhusiano wa aibu ya serikali na watu ambao huko nyuma wamekuwa ni mamluki wa kivita kwenye machafuko ya Angola, Sierra Leone, DRC na Liberia.
Ningemshauri rais awaambie wananchi kuwa suala la Meremeta ni la aibu na kuwa viongozi waliopita waliruhusu mamluki kutumia ardhi yetu kuchota utajiri wetu ili kufadhili shughuli zao haramu!
Ningemshauri rais kuwaambia wananchi kuwa ule uwanja wa ndege ambao ulijengwa katika moja ya migodi yetu hapa nchini ulikuwa unatumika kwa shughuli za kusafirisha nje utajiri wetu kama watu hao hao walivyofanya huko Uganda.
Hivyo, ningemshauri kufuta makubaliano yoyote kati ya Tanzania na watu hawa au makampuni yao mengine ambayo leo yamepewa maeneo mengine ya kutafuta mafuta na dhahabu. Hii, ningemwambia ingeirudishia Tanzania heshima yake inayostahili.
Kuhusu Muungano
Suala la Muungano nisingemshauri lolote kwani sidhani kama ana nia, uwezo au uthubutu wa kulishughulikia kwa jinsi ambavyo naamini ingeweza kuulinda Muungano wetu, kudumisha udugu na kuhakikisha kuwa Bara wanafurahi, Zanzibar wanafurahi na Watanzania wote wanafurahia, na wakati huo huo kila mmoja anajijua kuna kitu amepungukiwa lakini wanakubali upungufu huo kwani katika kupungukiwa kwao wanaweza kuona haja ya umoja wao.
Kuhusu CCM
Sasa kwa vile nitakuwa mshauri wa rais nadhani haitakuwa vibaya kumshauri pia kuhusu chama chake. Kwa sababu utawala ulioko madarakani unatokana na chama chake, basi nitamtendea hisani nikimshauri jambo moja kubwa, nalo ni kuitisha mkutano mkuu maalumu wa CCM ili wafukuzane uanachama.
Kabla ya hapo, kwanza ningemshauri amshawishi Andrew Chenge, Rostam Aziz na wengine kujiuzulu nyadhifa zao. Tena, sasa hivi itakuwa vizuri kwani hakuna uchaguzi mdogo wowote unaoweza kufanyika hadi uchaguzi mkuu. Katika kufanya hivyo atajionyesha kuwa amekidhibiti chama na anaonyesha uongozi.
Kuhusu washauri wake wa sasa
Kwa jinsi walivyoboronga masuala mbalimbali, ningemshauri kabla hatujaenda mbali awatimue kwanza washauri wake wa sasa na wale wanaoitwa ‘wasemaji' wake. Kwa sababu kundi hilo linatia aibu katika fani nzima ya kuwa mzungumzaji wa ofisi ya juu kabisa nchini.
Wakati mwingine nafikiria hawa jamaa wanafanya makusudi ili kumuaibisha Rais au wamelewa ving'ora vya pale Ikulu kiasi kwamba wanafikiri wanaweza kusema lolote kwa jina la rais!
Nina mambo mengine mengi ya kuweza kumshauri. Najua kwa kufanya hivyo sasa tatizo litakuja, je, atakubali?