Ikulu watakubali kunipa kibarua nilichoomba?

Kitu kikubwa ambacho Watanzania hatuwezi kukikubali ni kwamba hatujui tulikotoka,tuliko na tuendako, na hivyo basi hatujui tumejikwaa wapi,tumeangukia wapi na tutainukia wapi.
Tukijaribu kuangalia awamu nne ambazo zimetawala nchi hii,ni awamu ya JAKAYA KIKWETE ndiyo ambayo amekumbana na CHALLENGE nyingi na akaweza (kama sio kujaribu) kuzikabili kiungwana.
Nikianza na awamu ya MWALIMU,ambayo ilikuwa awamu ya kwanza,Yeye alikuwa na uzalendo wa kweli ambao kwa viwango vya binadamu wa sasa huwezi kuvikuta,aliishi maisha yale anayoyahubiri na aliamini katika haki ,ukweli,uzalendo na uchapakazi.na kupitia hayo,aliweza kujenga misingi imara sana katika nchi changa sana.Misingi ambayo Wabenzi wanajaribu kuibomoa lakini wameshindwa ingawa ki ukweli wanaitikisa.Aliiacha nchi ikiwa ina uchumi mzuri,utawala bora na kiwango cha chini kabisa cha rushwa kuliko kipindi chohote cha tawala nyingine.Nchi iliendeshwa kwa dira na mipango inayotekelezeka.
Sheikh,Alhaj ALLY HASSAN MWINYI,hakuwa na vission wala mission.alijaribu kuiga kama alivyotawala Mwalimu bila kujua mwalimu hakuwa binadamu wa kawaida katika zama hizi.mwishowe Mwinyi alivyoona hawezi akaamua kuacha Taifa lijipeleke vile litakavyo.Na hapo ndipo wale chui waliojivika ngozi ya kondoo ili kumuhadaa Kambarage,wakaamua kuvua ngozi zao na kuonyesha makucha yao.Na huu ndio ulikuwa mwanzo wa mparaganyiko tunaoushuhudia sasa.Uungwana na kutokuwa mkali katika mambo ya msingi akiwa kama Raisi kulisababishwa kuanza kujengeka kwa tabaka la mafisadi ambalo lilikuwa linaomba kila siku Mwalimu Kambarage aondoke duniani.
Ujio wa BEN WILLY MKAPA na kifo cha mwalimu Nyerere,kilifungua rasmi milango na kuondoa hofu toka kwa wale waliokuwa wakiitamani nafasi hiyo.Wakisaidiwa na Mkapa mwenyewe kama fisadi namba moja na mkuu wa nchi,walifanya kile ambacho kila mmoja wetu anakifahamu.Na kibaya za ni kitendo cha kushawishi na kufanikiwa kuliingiza Jeshi la wananchi wa tanzania(JWTZ) kushiriki katika uovu huo(rejea report ya mwanakijiji juu ya Meremeta).Jeshi lililokuwa likisifika kwa uzalendo,nidhamu na uchapakazi,likageuzwa kuwa ni tawi la mafisadi kufanya ufisadi wao.
Kama ni kujikwaa,basi hapo ndipo Nchi yetu ilipojikwaa,na lilikuwa ni pigokubwa kiasi ambacho,kuja kujipanga sawa itachukua muda mrefu sana ama tuwe tayari kujitolea damu zetu na wapendwa wetu kwa ajili ya kuiokoa nchi yetu.Ben Mkapa ana deni kubwa kwa nchi hii kiasi ambacho hata mbinguni hataweza kulilipa.Ule uchumi uliokuwa haujatengemaa vizuri tangu kipindi cha mwalimu,ukaja kusambaratika kipindi cha Mkapa,rasilimali zilizokuwa zikimilikiwa na serikali zikagawanywa katika kipindi hichohicho(naye akajigawanyia),Hata maliasili ambazo Mwalimu alisema hazitakuja oza hivyo zinaweza kusubiri,nazo ziligawanywa.
Uzalendo,undugu baina ya watanzania, na mapenzi kwa nchi vilifia hapo.na Mkapa alijua hilo na alifanya kwa makusudi.Mbaya zaidi alikuwa anajua nguvu ya KIKWETE katika CCM,na hivyo palikuwa hakuna uwezekano wa kumzuia kikwete kuchukua madaraka pindi muda ukifika.Ukijumlisha na uzalendo pamoja na record ya Jakaya katika utumishi wake,waliamua kutengeneza mazingira ambayo yatamuweka Jakaya katika nafasi ambayo hata yeye KIKWETE ataguswa endapo atataka kuwashuhulikia wahalifu.
Kikwete hakujua mkakati wa wanamtandao,mkakati wakum beba kikwete kwa kutumia fedha zao kutokana na urafiki baina yao.lakini kumbe wale vinara wa mtandao hawakuwa tayari kutoa fedha zao mfukoni bali ni kuunda makampuni hewa kwa maelekezo ya Mkapa ili fedha hizo zitumike kupigia kampeni Kikwete.Kitanzi kikawa kimeshaingia shingoni mwa Jakaya na kinamtesa hadi LEO.
Ninachomsikitikia ndugu yangu Kikwete ni kwamba,uzalendo anao,dhamira anayo na uwezo anao ila hana moyo wa kijasiri kupambana na hali hiyo au kuwatosa marafiki zake waliomfikisha hapo.Na hilo ndio anguko la raisi wetu.
Lakini ukiangalia sana,Jakaya hakuna kubwa alilolifanya la kumlamu zaidi ya kushindwa kuwachukulia hatua wahalifu wa serikali ya awamu ya tatu.Na huenda hilo ndio lilanalomuondolea sifa ya kuwa kiongozi bora na makini na hivyo kusababisha umaarufu wake uliomuingiza madarakani kwa kishindo kuporomoka.
Binafsi nayatazama mambo katika mtazamo huo,kuwa, tuliyumba awamu ya pili,tukajikwaa awamu ya tatu na sasa tumeanguka katika awamu ya nne.SASA JE! tujilaumu tulipojikwaa au tulipoangukia!!!
jibu kichwani mwako,
HATA UKIPEWA KAZI YA USHAURI KWA RAISI HUTAWEZA KUBADILISHA CHOCHOTE,Kwani raisi kama taasisi alishavikwa kitanzi ambacho asipokaka kimya,maadui wanavuta na kunyonga.hivyo usipoangalia utajikuta kazi yako ya ushauri utaona haithaminiwi nawe utageuka kuwa kama wao.

nawasilisha
 
Kuna matatu nayoweza kuchangia:-
1. Si kweli kwamba hajui what is right for his fellow Tanzanians
2. Unapopewa ushauri hulazimishwi kuufuata na
3. Hana hata hiyo nia ya kufanya chochote. kwangu yule ni failure 100%

Kwa kumalizia tu ni zile stori za pupils ku-count saa ngapi zimebaki kwenda break au kutoka shule regardless how much she/he gained from his/her attendance.
 
mwisho kabisa unatakiwa kumshauri hasirudi tena hiyo sehemu takatifu (Ikulu) Tutamwona kawajibika yeye binafsi na kufanya jambo la kiungwana
 
mimi nisingependa hii kazi upewe kwa sasa...JK hashauriki...kama kusoma hajui lakini hata picha haoni???? JK ni mnafiki na inawezekana anakubali kashindwa moyoni mwake....tumempatia madaraka, uwezo mkubwa sana lakini kwanini hawezi kuutumia kwa maslahi ya taifa...anachoremba ni nini??? Je hakushauriwa kwamba kuongoza nchi ni kazi kubwa......??
Mwanakijiji mimi naona kazi unayoifanya tayari inatosha...JK yote haya anayajua lakini hana uwezo...amejiweka pabaya...amezungukwa na wadhamini,mashemeji,washkaji ambao hawezi kuwaambia lolote...kama ni ushauri ushatoa wakutosha na umeonyesha muongozo wakati wote....kuomba kazi kwa JK si jambo jema....harakati ulizoanzisha nje zinatosha kuliko ukiingia kule ndani hatutajua umelishwa nini??? tupigane nje mpaka wafungue mlango tuwatoe tuingie wenyewe.....
 
Kitu kikubwa ambacho Watanzania hatuwezi kukikubali ni kwamba hatujui tulikotoka,tuliko na tuendako, na hivyo basi hatujui tumejikwaa wapi,tumeangukia wapi na tutainukia wapi.
Tukijaribu kuangalia awamu nne ambazo zimetawala nchi hii,ni awamu ya JAKAYA KIKWETE ndiyo ambayo amekumbana na CHALLENGEnyingi na akaweza (kama sio kujaribu) kuzikabili kiungwana.
Nikianza na awamu ya MWALIMU,ambayo ilikuwa awamu ya kwanza,Yeye alikuwa na uzalendo wa kweli ambao kwa viwango vya binadamu wa sasa huwezi kuvikuta,aliishi maisha yale anayoyahubiri na aliamini katika haki ,ukweli,uzalendo na uchapakazi.na kupitia hayo,aliweza kujenga misingi imara sana katika nchi changa sana.Misingi ambayo Wabenzi wanajaribu kuibomoa lakini wameshindwa ingawa ki ukweli wanaitikisa.Aliiacha nchi ikiwa ina uchumi mzuri,utawala bora na kiwango cha chini kabisa cha rushwa kuliko kipindi chohote cha tawala nyingine.Nchi iliendeshwa kwa dira na mipango inayotekelezeka.
Sheikh,Alhaj ALLY HASSAN MWINYI,hakuwa na vission wala mission.alijaribu kuiga kama alivyotawala Mwalimu bila kujua mwalimu hakuwa binadamu wa kawaida katika zama hizi.mwishowe Mwinyi alivyoona hawezi akaamua kuacha Taifa lijipeleke vile litakavyo.Na hapo ndipo wale chui waliojivika ngozi ya kondoo ili kumuhadaa Kambarage,wakaamua kuvua ngozi zao na kuonyesha makucha yao.Na huu ndio ulikuwa mwanzo wa mparaganyiko tunaoushuhudia sasa.Uungwana na kutokuwa mkali katika mambo ya msingi akiwa kama Raisi kulisababishwa kuanza kujengeka kwa tabaka la mafisadi ambalo lilikuwa linaomba kila siku Mwalimu Kambarage aondoke duniani.
Ujio wa BEN WILLY MKAPA na kifo cha mwalimu Nyerere,kilifungua rasmi milango na kuondoa hofu toka kwa wale waliokuwa wakiitamani nafasi hiyo.Wakisaidiwa na Mkapa mwenyewe kama fisadi namba moja na mkuu wa nchi,walifanya kile ambacho kila mmoja wetu anakifahamu.Na kibaya za ni kitendo cha kushawishi na kufanikiwa kuliingiza Jeshi la wananchi wa tanzania(JWTZ) kushiriki katika uovu huo(rejea report ya mwanakijiji juu ya Meremeta).Jeshi lililokuwa likisifika kwa uzalendo,nidhamu na uchapakazi,likageuzwa kuwa ni tawi la mafisadi kufanya ufisadi wao.
Kama ni kujikwaa,basi hapo ndipo Nchi yetu ilipojikwaa,na lilikuwa ni pigokubwa kiasi ambacho,kuja kujipanga sawa itachukua muda mrefu sana ama tuwe tayari kujitolea damu zetu na wapendwa wetu kwa ajili ya kuiokoa nchi yetu.Ben Mkapa ana deni kubwa kwa nchi hii kiasi ambacho hata mbinguni hataweza kulilipa.Ule uchumi uliokuwa haujatengemaa vizuri tangu kipindi cha mwalimu,ukaja kusambaratika kipindi cha Mkapa,rasilimali zilizokuwa zikimilikiwa na serikali zikagawanywa katika kipindi hichohicho(naye akajigawanyia),Hata maliasili ambazo Mwalimu alisema hazitakuja oza hivyo zinaweza kusubiri,nazo ziligawanywa.
Uzalendo,undugu baina ya watanzania, na mapenzi kwa nchi vilifia hapo.na Mkapa alijua hilo na alifanya kwa makusudi.Mbaya zaidi alikuwa anajua nguvu ya KIKWETE katika CCM,na hivyo palikuwa hakuna uwezekano wa kumzuia kikwete kuchukua madaraka pindi muda ukifika.Ukijumlisha na uzalendo pamoja na record ya Jakaya katika utumishi wake,waliamua kutengeneza mazingira ambayo yatamuweka Jakaya katika nafasi ambayo hata yeye KIKWETE ataguswa endapo atataka kuwashuhulikia wahalifu.
Kikwete hakujua mkakati wa wanamtandao,mkakati wakum beba kikwete kwa kutumia fedha zao kutokana na urafiki baina yao.lakini kumbe wale vinara wa mtandao hawakuwa tayari kutoa fedha zao mfukoni bali ni kuunda makampuni hewa kwa maelekezo ya Mkapa ili fedha hizo zitumike kupigia kampeni Kikwete.Kitanzi kikawa kimeshaingia shingoni mwa Jakaya na kinamtesa hadi LEO.
Ninachomsikitikia ndugu yangu Kikwete ni kwamba,uzalendo anao,dhamira anayo na uwezo anao ila hana moyo wa kijasiri kupambana na hali hiyo au kuwatosa marafiki zake waliomfikisha hapo.Na hilo ndio anguko la raisi wetu.
Lakini ukiangalia sana,Jakaya hakuna kubwa alilolifanya la kumlamu zaidi ya kushindwa kuwachukulia hatua wahalifu wa serikali ya awamu ya tatu.Na huenda hilo ndio lilanalomuondolea sifa ya kuwa kiongozi bora na makini na hivyo kusababisha umaarufu wake uliomuingiza madarakani kwa kishindo kuporomoka.
Binafsi nayatazama mambo katika mtazamo huo,kuwa, tuliyumba awamu ya pili,tukajikwaa awamu ya tatu na sasa tumeanguka katika awamu ya nne.SASA JE! tujilaumu tulipojikwaa au tulipoangukia!!!
jibu kichwani mwako,
HATA UKIPEWA KAZI YA USHAURI KWA RAISI HUTAWEZA KUBADILISHA CHOCHOTE,Kwani raisi kama taasisi alishavikwa kitanzi ambacho asipokaka kimya,maadui wanavuta na kunyonga.hivyo usipoangalia utajikuta kazi yako ya ushauri utaona haithaminiwi nawe utageuka kuwa kama wao.

nawasilisha

Notradammus,

Umeweka analysis nzuri sana hapo juu. Lakini hapo kny kipengele cha JK kukaa kimya ukumbuke Muomba kazi ikulu (MM) anasema katika hali kama hiyo angemshauri atumia kanuni ya LIWALO NA LIWE laiti kama atakubali kutumia kanuni hii, wananchi watakuwa nyuma yake....na hii nafikiri ni siraha nzuri sana kwa JK.....anapendwa na wengi hasa raia wa kawaida!

So to me kama JK kwa nafasi yake anaweza akafanya lolote lile kama raisi na hasa kwa manufaa ya nchi na akapata support ya Bunge na wananchi kwa ujumla.......!
 
KAzi hatokupa, msome Jenerali Ulimwengu:

Busara bandia, washauri bandia, maendeleo bandia

lC.gif
Jenerali Ulimwengu​
Agosti 5, 2009
rC.jpg

TUMEONA katika makala ya wiki jana jinsi kitoto kilichozaliwa katika familia ya mafisadi kinavyolelewa kifisadi, kinavyosomeshwa kifisadi, kinavyofanywa 'kifaulu' kifisadi, kinavyoajiriwa kifisadi, kinavyoozeshwa kifisadi na kinavyokuwa kitu kingine cha ufisadi katika mwendelezo wa utamaduni wa ufisadi kilimozaliwa.
Sidhani kwamba tunaweza kuwa na matumaini ya kupata lo lote la maana kutoka kitoto hicho kwa maana ya kuiendeleza nchi na kuwaendeleza watu wake. Watu wa aina ya kitoto hicho hawawezi kuijenga wala kuiongoza nchi, kwa sababu wao hawajajengwa wala kuongozwa katika misingi ya kujenga lo lote la maana isipokuwa kuendeleza utamaduni uliowazaa na kuwalea.
Kwa bahati mbaya, katika mazingira yetu, na katika mazingira ya nchi nyingi za Kiafrika, hawa ndio watu wanaoelekea kuchukua mikoba ya utawala kutoka kwa wazazi wao, katika mazingira ambamo mifumo ya utawala haiwaachii wananchi nafasi ya kuchagua viongozi wao.
Haya ni mazingira ambamo, kama nilivyoeleza katika makala zangu za nyuma, watawala wanaendesha nchi bila itikadi ya kimsingi inayowaelekeza na wanachofanya ni kila siku kuzuka na jipya lisilokuwa sehemu ya mwendelezo wa jambo jingine lo lote walilosimamia huko nyuma wala wanalotaraji kulisimamia siku za usoni.
Unakuwa ni uongozi wa kubabaisha, wa kila siku kuokoteza 'sound bite' za kauli-mbiu zisizodumu hata mwaka mmoja. Baada ya muda ukiwaangalia wanaonekana kama vile wamekwisha kusahau kauli-mbiu ya mwaka jana na sasa wanazindua nyingine.
Ni hali hii ndiyo inayojenga utegemezi wa kila aliye ndani ya utawala kwa 'busara' za Bwana Mkubwa, kwa maana ya kiongozi wa juu kabisa wa wakati huo, ambaye atakuwa na 'busara' kubwa sana ambazo hakuwahi kuwa nazo kabla hajaingia madarakani, na ambazo akiondoka madarakani anaziacha ofisini; anarudia kuwa mtu wa kawaida, wa akili kama zako na zangu.
Bila shaka hapa kuna tatizo: Waliomzunguka Bwana Mkubwa, kwa kukosa itikadi au mfumo wa fikra unaowaunganisha, na kwa kuhofia kupoteza 'kibarua' chao, wanajenga ukimya mkubwa na hatimaye hata uwezo wa kufikiri na kutamka kile wanachoamini unavia. Baada ya miongo michache katika hali hiyo hata yule aliyewahi kuwa mwalimu mzuri wa shule ya msingi hawezi tena kazi hiyo kwa kuwa kapoteza mazoea ya kufikiri, hata kwa kiwango hicho.
Papo hapo tunajua kwamba 'busara' za Bwana Mkubwa nazo hazina uhalisi wo wote kwa sababu zimetokana na sifa anazomwagiwa na waajiriwa wake na wapambe wengime. Sasa tukiunganisha 'busara' hizi feki na mazoea hafifu ya kutumia akili ya wasaidizi na wapambe wake, kinachozalishwa ni ombwe (vacuum) katika uongozi hata kama utawala unaweza kuwa na ufanisi wa kufanya menejimenti ya kilipo bila maendeleo.
Kwa kuwa maumbile hayapendi ombwe, Bwana Mkubwa na wapambe wake watajikuta wanafunikwa na itikadi kutoka kwingineko, kutoka nchi na asasi ambazo maslahi yake siyo lazima yasadifu na maslahi ya watu wetu. Mara nyingi haya maslahi ya pande mbili yanakuwa yanakinzana moja kwa moja, na vikali.
Yote hii ni kusema kwamba mazingira ambamo watawala wanaendesha utawala wao bila mfumo wa fikra, bila mtazamo wa kimkakati kuhusu mustakabali wa nchi yao na watu wao, katika mazingira hayo kitakachowaunganisha watawala hao ni ufisadi.. ufisadi wa ndani ya nchi ukisaidiana na kuelekezwa na ufisadi wa nje ya nchi.
Lile ombwe nililolitaja hapo juu linadhihirika hadi nje ya nchi, na wenye maslahi yao hawashindwi kulitambua hilo na kulifanyia kazi. Wanachofanya ni kuwapata mawakala wao katika nchi zetu watakaowatumikia. Malipo yao ni madaraka ya kisiasa, ambayo watawasaidia kuyapata katika gulio la kura pamoja na mapesa ya kuwapa ukwasi wa kuazima.
Hali ikiisha kuwa hivyo, hakuna linaloweza kufanyika kubadilisha fikra za watawala wa aina hii, kwa sababu ufinyu wao wa kufikiri na maslahi ya mabwana zao kutoka nje vinakuwa vimejenga ubia imara usiomsikia mtu wala jini. Mambo yao 'yanajipa' katika utaratibu tuliokuwa tukiujua kama Ubeberu lakini hivi sasa unatambulishwa kwa jina laini la Utandawazi.
Hii siyo hali ya kuruhusu, achilia mbali kuchochea, maendeleo. Maendeleo hayapatikani kutokana na mchakato unaoendeshwa na mawakala wa ndani wanaofanya kazi kwa kusimamiwa na kuelekezwa na maslahi ya kiuchumi ya Ubeberu. Hii ni hali ya kudumisha na kuimarisha uduni, udhaifu na umasikini wetu ndani ya kila aina ya neema tuliyopewa na maumbile na Mwenyezi Mungu.
Msomaji atakuwa amenielewa ni nini nataka kusema: kila kiongozi mwenye nia njema na watu wake na aliyedhamiria kuwaongoza ili waweze kujiletea (siyo kuwaletea) maendeleo ya kweli, hana budi kuwa na ubia katika uongozi wake. Kwanza atakuwa ameingia ubia na wananchi anaowaongoza; pili ataingia ubia na asasi anazozitumia katika malengo yake (tuseme chama, kwa mfano); tatu ndani ya asasi hizo ataunga ubia, atakula yamini, na viongozi wenzake wenye malengo kama yake.
Asipofanya hivyo, na akizidi kung'ang'ania kwamba uongozi wake hauna ubia, mtawala huyo anajidanganya, na wanaomwangalia na kumsikiliza watagundua baada ya muda si mrefu kwamba anao wabia ambao inamuwia vigumu kuwatangaza.
Hii si hali ya kuridhisha hata kidogo, na ni hali hiyo inayoifanya Afrika iendelee kumenyeka na umasikini wakati inao kila aina ya utajiri. Mojawapo ya mambo yanayoweza kuchochea maendeleo ni utawala bora, na utawala bora lazima uwe ni utawala wa pamoja, angalau kwa watu waliokula yamini ya pamoja ya kufanya mambo fulani ili kufanikisha malengo maalumu.
Kinyume cha hilo ni nini? Iko mifano lukuki, lakini mmoja ni wa hivi karibuni na unahusu maneno yaliyojaa masikioni hata wakati nikiandika makala hii. Imezinduliwa kampeni kubwa, na yenye kelele nyingi, inayoitwa 'Kilimo Kwanza.' Lengo lake la jumla ni kutoa kipaumbele kwa kilimo, ambalo ni jambo jema na sahihi.
Hata hivyo, wakuu wa Serikali wanajua kwamba ilikuwapo sera iliyoitwa 'Siasa ni Kilimo' iliyotangazwa mwaka 1972 kisha ikawekwa kabatini. Alipoondoka Mwalimu madarakani na sera hiyo ikaondoka, kwa sababu, kama ninavyosema, alijizungushia ukuta wa matarishi badala ya kujijengea wigo wa viongozi wenzake.
Baadaye sana, mmoja wa warithi wake, ambaye kwa hakika zamani alikuwa ni mmoja wa hao matarishi wake, aliulizwa ni jambo gani alidhani alikuwa amesahau kulishughulikia katika utawala wake wa miaka kumi. Jibu lake? Kilimo .
Tunashangaa nini? Katika 'uongozi' usiokuwa na ubia, ni nani katika watu waliokuwa wamemzunguka angethubutu kumwambia, Mzee, samahani sana kwa usumbufu wangu, lakini naona kama vile tumesahau kilimo? Tena, hata kwa kusema "tumesahau" ili aonekane naye anahusika katika uzembe huo.
Tunajua tayari kwamba watawala wa Kiafrika hawana washauri. Ofisi za 'washauri' ni vituo vya kuwazawadia wapambe waliotoa huduma kwa Bwana Mkubwa (aghalabu huduma chafu) wakati akisaka madaraka. Hakuna ushauri wo wote wanaotoa mbali na kumshangilia Bwana Mkubwa na kumwambia, Mzee ile hotuba yako ya leo, haijapata kutokea! na upuuzi mwingine kama huo. Hakuna washauri bali wamejaa wapiga debe, mashabiki, wapambe na washikaji, wote wakigharimu fedha nyingi mno za walipa kodi.
Sasa mawaziri ndio hao, na washauri ndio hao. Ni kwa nini hasa tunataraji kupata maendeleo? Nakumbushia tena: Kufanya jambo lile lile kila siku kwa njia ile ile, na kutaraji kupata matokeo tofauti, ni ishara mojawapo ya taahira ya akili.


Itaendelea
 
Kikwete yuko kama kwenye puto kubwa la aina fulani. Puto hilo linaenda naye mahali popote na wakati wowote na ndilo analitegemea kupata taarifa. Kwa miaka michache sasa nimefikia hitimisho kuwa ni kwa ajili manufaa ya puto hilo Kikwete hapewi taarifa sahihi, anafichwa mambo na anakuwa mtu wa mwisho kujua.

Nakumbuka wakati wa sakata la vijana Ukraine siku nimezungumza naye na kumuelezea alishangaa sana na hakuwa anajua na akabakia kusema "kama (wizara) wameshindwa wangeniambia" ili waone jinsi gani ya kushughulikia. Matokeo yake wale Puto wakawa wanatuma ujumbe kwa mtu yeyote ambaye alitaka kuwasaidia wale vijana kuwa akifanya hivyo atakuwa anaenda kinyume na Rais.

Ni yale yale kwenye masuala ya Mapanki ambapo kuna mtu alimwambia kuwa watanzania hawali mapanki na yeye akasimama kutamka hivyo hivyo; ni vile vile aliposimama na kusema kampuni ya BAE Systems (ya rada) inamilikiwa na serikali ya Uingereza na hivyo tutaidai Uingereza fedha yetu tuliyolipa ziada ya bei halisi; Na tumeliona tena kwenye suala la uchumi ambapo yeye aliwahakikishia wananachi kuwa uchumi wetu hautaathirika kwa kiasi kikubwa kwani hatujawa connected sana katika uchumi wa kimataifa halafu miezi michache baadaye anasema tumeathirika kwa sababu tuko connected katika uchumi huo wa kimataifa.

Yote ni dalili siyo ya mtu ambaye anaficha ukweli bali mtu ambaye hajui. Rais ni mtu anayetegemea Washauri wake sana kuliko kitu kingine na anatakiwa awe na washauri ambao watamuambia ukweli, watakaopingana kwa hoja na kumpatia taarifa sahihi (ziwe nzuri au mbaya) wakati wote ili kumsaidia kufanya maamuzi sahihi.

Bahati mbaya Rais wetu amezungukwa na puto ambalo linalenga kumpa taarifa zinazoonekana nzuri. Na ninaamini wakati mwingine wanampa taarifa za kumpotosha kwa makusudi. Ndio maana sitoshangaa hao washauri ndio wamemuambia kuwa hahusiki na Richmond na sitoshangaa hawakumuambia kabisa na hajui kuna taarifa imetolewa kuhusu yeye na Richmond.

Mara nyingi utaona kuwa Kikwete yuko ziarani mara nyingi sana na karibu Jumatano nyingi (siku ambazo magazeti mengi yanaandika habari za kisiasa) Kikwete anakuwa kwenye kaziara fulani nje ya nchi au mikoani. Na akirudi wanamfanya we busy sana kiasi kwamba hana muda wa kupata taarifa za ndani.

Ndio maana licha ya kuwa kuna tatizo la njaa linalokuja Kikwete yawezekana hajui kabisa hadi siku washauri watakapomuambia it is time to beg for more aid na yeye atatokea na kuzungumza na wafadhili kwa ajili ya msaada wa chakula.
 
Wangekuwa wanaisikiliza JF wangeongoza vizuri lakini sijui huwa hawaoni wanachoshauriwa maana kila uchao yanajirudia,haya 2010 hiyooooooooooooo.
 
Mzee Mwanakijiji,
Kikwete yuko kama kwenye puto kubwa la aina fulani. Puto hilo linaenda naye mahali popote na wakati wowote na ndilo analitegemea kupata taarifa. Kwa miaka michache sasa nimefikia hitimisho kuwa ni kwa ajili manufaa ya puto hilo Kikwete hapewi taarifa sahihi, anafichwa mambo na anakuwa mtu wa mwisho kujua.

Nakumbuka wakati wa sakata la vijana Ukraine siku nimezungumza naye na kumuelezea alishangaa sana na hakuwa anajua na akabakia kusema "kama (wizara) wameshindwa wangeniambia" ili waone jinsi gani ya kushughulikia. Matokeo yake wale Puto wakawa wanatuma ujumbe kwa mtu yeyote ambaye alitaka kuwasaidia wale vijana kuwa akifanya hivyo atakuwa anaenda kinyume na Rais.

Ni yale yale kwenye masuala ya Mapanki ambapo kuna mtu alimwambia kuwa watanzania hawali mapanki na yeye akasimama kutamka hivyo hivyo; ni vile vile aliposimama na kusema kampuni ya BAE Systems (ya rada) inamilikiwa na serikali ya Uingereza na hivyo tutaidai Uingereza fedha yetu tuliyolipa ziada ya bei halisi; Na tumeliona tena kwenye suala la uchumi ambapo yeye aliwahakikishia wananachi kuwa uchumi wetu hautaathirika kwa kiasi kikubwa kwani hatujawa connected sana katika uchumi wa kimataifa halafu miezi michache baadaye anasema tumeathirika kwa sababu tuko connected katika uchumi huo wa kimataifa.

Yote ni dalili siyo ya mtu ambaye anaficha ukweli bali mtu ambaye hajui. Rais ni mtu anayetegemea Washauri wake sana kuliko kitu kingine na anatakiwa awe na washauri ambao watamuambia ukweli, watakaopingana kwa hoja na kumpatia taarifa sahihi (ziwe nzuri au mbaya) wakati wote ili kumsaidia kufanya maamuzi sahihi.
Mkuu wangu nitarudia kusema kwamba JK sii mjinga kama unavyofikiria. Yote uloandika JK alikuwa na taarifa isipokuwa yeye ndio kakupiga goli..Jk mtoto wa mjini na mara zote kila jambo la kufumaniza linapoingizwa kwake ni lazima ijefanye halijui hata kama analijua fika, ili apate kujua wewe unaelewa nini..ukimtega kisogo tu anakung'onga!

Ni sawa na askari wanapokuja mlangoni kwako wakakuuliza kama wewe ni Mwanakijiji, jibu rahisi litakuwa sii mimi kwani Mwanakijiji kafanya nini?..ndio JK huyo babuu.

Sakata la Ukraine alilijua fika na kusema kweli kwake yeye kama rais aliliona dogo sana ambalo lingeshughulikiwa na waziri sio yeye..Na kwa lugha ya mjini tunasema matatizo ya wale vijana wakiwa mtoni huwezi kulinganisha na matattizo alokuwa akiletewa kila siku kuhusu wananchi wasiokuwa na maji, umeme na upungufu wa chakula nchini kutokana na ukame..After all yule ulokuwa ukimtaja -LOWASSA kumbuka kuwa wakati huo huyu mkulu ndio alikuwa kipenzi cha JK na akiendesha nchi ya wajinga.. JK akitesa na honeymoon ya Urais!
Swala la Mapanki, sii kweli JK hakufahamu kitu, laa sivyo asingefunga kiwanda cha wahindi walioshiriki ktk kutengeneza ile sinema na hata kuipiga marufuku kuonyeshwa nchini..iweje aipige marufuku wakati hajui kilichokuwemo ktk sinema ile!
Mzee wangu hivi kweli wewe unaamini Warusi waliweza kuingiza silaha nchini rais wa nchi hafahamu?.. tena ndege yenyewe ikilindwa na askari wetu usiku kucha.. sidhani kama Uwanja wa Taifa kuna ndege private zinalindwa hivyo.

Swala la BAE, hivi nikuulize wewe.. kama ungekuwa rais na unajua kilichofanyika na swali kama hilo limeulizwa wakati unataka kuwalinda wote waliohusika utasema kitu gani?.. ni kanyanga gani utawavika wakuondolee usiku!.. Ndio JK huyo mkuu wangu.

Kwa hiyo, JK anakwenda na mahesabu yake, ndio maana akaitwa muungwana kwa sababu anayajua madhambi yote lakini ytupo radhi atundikwe yeye lawama lakini watu wake waendelee kupeta..
Je, ni makosa anayofanya?.. inategemea wewe umesimama upande gani..kwa sababu Politics ni mchezo mchafu sana. Msikilize mzee Malecela kama wewe sii mwana CCM utachoka naye na sii kwamba hafahamu rafu zinazochezwa.

Kifupi kosa kubwa analofanya kama rais ni pale anapoachia watu binafsi wafanyabiashara kina Rostam na Lowassa kucheza siasa..Leo hii kuna mawaziri wakiwa namatatizo kiuongozi badala ya kwenda kwa rais wanakwenda kuwaona kina Lowassa hapo ndipo utaona JK kapoteza nguvu ya rais na binafsi sielewi strategy ipi anayotumia kama sii kujitia kitanzi yeye mwenyewe..unless anayo plan B kusubiuri uchaguzi ndio kesi zote zifumke, watu watiwe ndani hadi baada ya uchaguzi..

Kila siku hawa mafisadi wanazidi kupanda umaarufu na hakika uchaguzi ujao utakuwa baina ya JK na kundi la Lowassa! It won't suprise me if 2010, hawatajaribu kumwondoa (an atempt for his life!).
Waswahili wanasema Mjqnja ni yule anayejifanya hajui kumbe anajua, na mjinga ni yule anayejifanya kujua kumbe hajui!.
 
Last edited:
[/QUOTE]
Nakuhakikishia kuwa, bora amekaa kimyaaa kuliko kufikiria hatua dhidi ya wachezaji wenzake kwani mfumo wa CCM, huyo JK ni captain tu wa team nzima sii owner wala team coach...

Na akijaribu tu kufungua mdomo wake bila kutumia usanii atakombwa hadi yeye.......
 
Kuna matatu nayoweza kuchangia:-
1. Si kweli kwamba hajui what is right for his fellow Tanzanians
2. Unapopewa ushauri hulazimishwi kuufuata na
3. Hana hata hiyo nia ya kufanya chochote. kwangu yule ni failure 100%

Kwa kumalizia tu ni zile stori za pupils ku-count saa ngapi zimebaki kwenda break au kutoka shule regardless how much she/he gained from his/her attendance.

Hivi ni lini anatarajia kuachia hiyo ofisi? sooner or later?
 
Mzee MJJ hata ukipata kibarua cha kumshauri JK usitegemee atafuata ushauri wako kwa sababu hawezi kufuata ushauri wa kumwangamiza kutokana na madudu yote yaliyofanyika ya EPA,RICHMOND,MEREMETA,IPTL n.k. yeye pia ni mhusika mkuu, hivyo basi ushauri wangu kwa watanzania ni kupigania mabadiliko ya katiba ndilo suluhisho lililobaki kwetu na vizazi vijavyo.
 
Naam nimewapata.mwenyehoja kasema kikwete hana washauri wazalendo. wachangiaji wakaongezea haambiliki kwamba washauri anawapeleka puta,wengine kwamba he was the key player kwenye ufisadi kuchukuwa hatua ni kujifunga goli.wengine ni kwamba si mzalendo hana nia.wengine ni kwamba hana mamlaka ni coach (morinyo) na siyo abramovich.wengine ni kwamba tumpe tena nafasi KWA SHARTI MOJA, kipindi kijacho asitafute ufadhili kutoka kwa mafisadi.Sasa naomba ushauri uenda mambo yote ni sahihi.JE WENYE NCHI TUFANYE LIPI JEMA
 
Cheche imetema cheche baada ya cheche hizo sioni hatua za serikali kuzuia moto kwani mwazo wa moto ni cheche.Imekua kawaida kwa serikali na washauri wa Rais kukimbilia kumlinda rais katika mambo ya kipumbavu lakini ktk hili naona ni maji ya shingo bado hawana au bado watunga hadithi kuhusu swala hili.Shukurani kwa kazi yenu.Inabidi wabunge waombe majibu kuhusiana na kashfa hii.MUNGU USICHOKE KUIBARIKI TANZANA!
 
Mkuu wazo na ushauri mzuri lakini ulikuutuma siko.Washauri wa Rais hawako Ikulu hao walipo Ikulu ni vipaza sauti.Katika ushauri waka unautuma kwa mtengenezaji wa kipaza sauti ambae hawajibiki kwa vyoyote kwa kauli inayotoka katika kipaza sauti.Ushauri inabidi kuutuma kwa Rostam Aziz na mafisadi hawa dio marais wetu JK ni Rais kivuli.MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Hivi kweli JK kama yeye hana akili, utashi, udadisi, ung'amuzi, utambuzi na wala hashtuki, hasomi alama, nyakati au hawafahamu vizuri hao wanaomzunguka kuanzia mkewe, wanawe, ndugu, maswahiba, marafiki,....
URAIS umempunguzia uwezo wa kufikiri, kuamua, kutenda....
SIDHANI. Nchi inasonga mbele jamani. Baadhi yetu hatutaki kuyaona hata yale mazuri machache anayoyafanya! Tunataka afanye/aamue tunavyotaka sisi ambao si "MARAIS"!
 
Back
Top Bottom