Mawazo ya kimasikini hayo.Kwa kweli wakati Mama anasema wanajenga Samia complex nilishtuka, nikajikuta nimenyong’onyea sana! Bora hata asingesema kwenye public!
Kiufupi mabilioni yetu yanatafutiwa njia za kuyapiga na watu wachache!
Hiyo ikulu hata bajeti yake hawataki kuiweka wazi!!!
Wangeianika tuone maajabu!!
Weka ambacho unaona hujajibiwa.Soma neno kwa neno na hoja zijibu kwa mtiririko huo sio general kama ulivyo fanya ndugu
Wajenge viwanda, Hospitali n, shule na masoko hapo ikulu.Je, kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?
NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex. Kwanini iitwe Samia Complex?
- Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu.
- Ujenzi wa Viwanja vya Golf.
- Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000
Je, Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo? Kuna ulazima gani?
Je, nani mnufaika wa hayo yote?
Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
Jana Samia kaongea kuwa Ikulu bado kuna mambo yanafanyika ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia ya kurukia Ndege
Hii nchi haina viapumbeleNdege zenyewe zipi? Uwanja complicated wa msalato nao unasubiri, ni hizihizi kodi zetu au?
Well
Vipaumbele vya nchi yetu miaka ya karibuni ni vipi? Elimu ujinga na maradhi vimeisha?
Maana enzi za Mkee Mkapa kila mwisho wa mwezi tulikua tunakumbushwa na kupewa updates where are we heading to…
Hivyo vyote hata wewe unaweza kujenga, au ulikatazwa?Wajenge viwanda, Hospitali n, shule na masoko hapo ikulu.
Uwivu huoo hamtaki na sisi viongozi wenu tuanze kujifunza na kucheza golf ikulu..Je, kuna ulazima wa yafuatayo au ni kupoteza pesa za walipa kodi?
NB: Kama wanatimiliza Ndoto ya Nyerere kwanini Complex isiitwe Nyerere Complex au iitwe aliyeanzisha Ujenzi Magufuli Complex. Kwanini iitwe Samia Complex?
- Kujenga Njia ya Kuruka Ndege Ikulu.
- Ujenzi wa Viwanja vya Golf.
- Ujenzi wa Complex ya watu 2000-3000
Je, Watanzania tuna kodi kiasi hicho kujenga Ikulu ya namna hiyo? Kuna ulazima gani?
Je, nani mnufaika wa hayo yote?
Kwanini hizo pesa zisiende kwenye elimu ya awali na msingi maana huko ndo chanzo cha madudu ya huku juu?
CCM wenzio haoUsiposema samia complex utahalishaje upigaji wa fedha? Yaani hapo upigaji umehalishwa. Ni mwendo wa kula tu.
Huyu mama kwakweli anawaangusha sana wanawake wenzie kiuongozi.
Ukiona mtu yoyote katia neno kwanini pesa hizo zisiende kwenye elimu ujue mwisho wake wa kufikiri umeishia hapo. Ngoja nikujibu kwa urahisi tu, Ikulu ya nchi ni hazina ya nchi na itabaki hata vizazi vinayokuja ni muhimu kuwa na sehemu bora ya kufanya shughuli za serikali wala sio kupoteza pesa kwa mawazo yako maana ni kama kusema budget ya nchi 100% iende kwenye shule tu huu ni ujinga kila kitu kinapangwa kwa budget na elimu ina budget yake. Ukisema kodi kwani uliambiwa kodi yako inaongezake kulipia ujenzi? acheni gubu hata wewe unaweza kumuita mtoto wako Magufuli. Stand Magufuli, Mji wa serikali Magufuli na mpaka ikulu Magufuli imekuwa nini tena, Nyerere jina lake liko kila sehemu mimi naona tubadilishe nchi jina tu kutoka Repuclic of Tanzania to Republic of Nyerere au Magufuli
Kha!Hivyo vyote hata wewe unaweza kujenga, au ulikatazwa?
Uliambiwa kuna uhaba wa maeneo ya kulima?Kila mtu anataka jina lake liwepo hapo tena kwa kujipigia chepuo mwenyewe mara Zanzibar mara Nungwi golf courts.
Hivi mfano Nyerere aliacha vitu gani vikiitwa kwa jina lake alipokuwa madarakani? Barabara?
Vingi vimepewa jina lake na watu Baki akiwa mstaafu au marehemu.
JNIA yenyewe aliiacha ikiitwa DIA hadi 2005.
BTW:Eneo lenyewe wamehodhi kubwa mno ekari 8,473 zote za nini si heri wangewapa vijana wa maigizo ya kilimo ya BBT ya Bashe.
Kuna Ikulu duniani yenye uwanja wa ndege au wana taka wawe wa kwanzaHatari sana what for? Wangeweka tu kiwanja cha helicopter ingekuwa poa tu. Afrika tuna shida mahala viongozi wanataka kufanya mambo kama donor country tena unakuta donor country hata hawafanyi hivyo. Just imagine ni pesa kiasi gani itatumika kuitunza hiyo complex kwa kila mwezi?
Kifurushi cha bima ya watoto yenyewe wameshindwa. Kisha mmama mtu mzima wanayemuita rais anashangilia kujengwa kiwanja kwa golf sababu anajua wajukuu zake watatibiwa ulaya.
Wewe mpaka uambiwe?Uliambiwa kuna uhaba wa maeneo ya kulima?
Sasa wewe na akili zako zote unatufananisha na kile ki mkoa Rwanda? kweli tunawatu akili zao zina changamoto, leo hii sisi wakutuweka kundi moja na Rwanda ya Kagame kwa lipi haswa? Hii Tanzania na EA mtu wa kushindina naye ni Kenya. Halafu toka lini nchi tukaweka vipaumbele vyetu kwa kuangalia Kagame anafanya nini. Usitukoshee heshima kama nchi kutufananisha na nchi kama wilaya yetu. Hata kama unachuki zako na Mama Samia uko umeenda mbali. Nchi yoyote ni lazima uwe na airport nzuri, Immigration nzuri, ofisi za serikali nzuri na ikulu nzuri ndio sura ya nchi mengine yatakuja.Ikulu = hazina ya nchi?
Wenzetu hua mnatumia ubongo upi kutoa arguments kama hizi? Muulize Mzee Kagame Ikulu iko wapi? Unadhani hawezi kujenga ikulu ya maonyesho?