The Sunk Cost Fallacy
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 19,586
- 14,138
Yule ni mtendaji kwenye siasa mlimpeleka kufanya nini?Leo Mhe. Rais amesema ana mpango wa kugawa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili kuanzisha wizara mahsusi kwa ajili ya mambo ya jinsia(ilikiwepo kabla ya 2015), naamini itakuwa wizara ya Jinsia, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto. Kwanza Hongera kwa kuona ukubwa wa wizara hiyo.
Basi naona hiyo ni fursa ni kumuondoa Prof. Ndalichako kwenye elimu na kumpeleka kwenye hiyo wizara ambayo mimi naona itamfaa kuliko wizara nyeti ya elimu.
Katika wizara ya elimu ataeliwe mtu mwenye uthubutu, anayejiamini, mbunifu na mwenye commitment juu ya kazi yake.
Prof. Joyce hafanyi lolote kule. Amezidiwa hata na Mama Ummy na anasaidiwa sana na Ummy kwenye majukumu yake.
Kwa ufupi, hafai wizara ya elimu.
Atafutwe mtu mwenye commitment ya level au zaidi ya Lukuvi, Ummy na Mulamula katika field zao.
Tunahitaji kufanya kitu kwenye elimu.