Nashauri Doroth Gwajima arudi Wizara ya Afya na Ummy Mwalim aende Maendeleo ya jamii

El Roi

JF-Expert Member
May 29, 2020
263
502
Moja ya mawaziri wazuri wachapa kazi ktk awamu hii ni Dorothy Gwajima na Ummy Mwalimu.

Uchapakazi wao ni makini na wanaooneka wanapenda kazi. Yaani, wanaishi Ili wafanye kazi, na siyo wanafanya kazi Ili waishi. (They live to work and not work to live).

Kwa maana ya kuongezea thamani uchapakazi wao na hivyo kuongeza ufanisi katika wizara tajwa, yangefanyika mabadiliko, ya kiufundi kwa maana ya kubadilishana wizara.

Dorothy Gwajima ni daktari wa binadamu kitaaluma na juu ya hapo ni mahiri( specialist) kwenye masuala ya utawala wa afya (Masters in Public Healthy). Ukimuona huyu mama kwa maana ya taaluma, amesheheni Kila kitu kinachohitajiwa na wizara hii. Yaani utaalamu (expertise) wenyewe, na component ya utawala wa ki- tiba.

Na kwa haiba yake ya ukali kiasi na ufuatiliaji( Aggressiveness) angesaidia sana, wizara hii kufanya vizuri zaidi, maana anazijua corridor zote zilizoko kwenye "utabibu".

Na kwa kuwa ni mfuatiliaji na mkali kiasi, issue za uzembe, kujificha kwenye taaluma wakati unafanya makosa na vitendo vya rushwa,vingepungua kama siyo kuporomoka kwa kiwango kikubwa.

Kwa ajili ya ufanisi mkubwa huyu mama, ikimpendeza Rais basi apelekwe wizara hii.

Kwa Ummy Mwalimu, wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na watoto ilikuwa wizara hasa inayomfaa kwa maana ya anakotoka na utaalamu wake( background).

Huyu ni mwanasheria na mwanaharakati ambaye aligeuka kuwa mwanasiasa.

Kabla ya kuwa mwanasiasa alijihusisha sana na mambo ya utetezi wa jamii katika maeneo mbalimbali.

Kwa kuwa Kuna hitaji kubwa la kuwa na Sheria zinazoendana na wakati na hasa kwa kuifanya jamii kuwa sawa katika makundi mbalimbali ya jamii, component ya Sheria ambayo mama huyu anayo, ingeweza kusaidia sana.

Na kwa kuwa taaluma yake ni Sheria, kusukuma mambo katika wizara hii ingekuwa rahisi maana ana jicho tayari la kujua kinachopaswa kufanyika kwa sababu ya ujuzi wake wa Sheria.

Wakati huu Kuna uhitaji mkubwa wa haki za watu na utetezi wa makundi maalumu. Background yake ya uanaharakati (Activism) ungesaidia sana kusukuma mambo na hivyo kuifanya wizara hii iyafikie malengo yake haraka.

Nimuonavyo huyu mama akiwa kwenye uga anaouelewa vizuri kama hivi wa sheria na utetetezi wa haki za watu ataifanya kazi hiyo kwa raha.

Kuwabadilisha hawa akimama wachapa kazi Ili wakae kwenye wizara ambazo zinaendana na asili yao ya utaalamu ( expertise) ni kama kumchukua Samaki na kumrudisha majini. ( Utafanya aishi kwa raha na kujitanua).

Kama itawapendeza wenye mamlaka walione hili kwa jicho kama langu na hakika wizara hizi zitapaa sana na nchi itajengwa vema kwa maana hiyo.
 
Hakunaga cha uchapakazi kitu inatafutwa duniani ni pesa kupitia posho..hii ndo siri kubwa watu wengi wasiojua kazi zinafanywa na watendaji wa huku chini ila hawa watunga sera ni takataka tu huu ndio msimamo wangu mpaka nitakapokufa wanasiasa ni kikundi tu cha kuidhinisha pesa..hakuna kazi kwenye position ya uwaziri
 
Moja ya mawaziri wazuri wachapa kazi ktk awamu hii ni Dorothy Gwajima na Ummy Mwalimu.

Uchapakazi wao ni makini na wanaooneka wanapenda kazi. Yaani, wanaishi Ili wafanye kazi, na siyo wanafanya kazi Ili walione hili kwa jicho kama langu na hakika wizara hizi zitapaa sana na nchi itajengwa vema kwa maana hiyo.
Unbelievable na picha zao kabisa wengine hatuwafahamu ili tutoe majawabu kama kweli unayosema.
 
Moja ya mawaziri wazuri wachapa kazi ktk awamu hii ni Dorothy Gwajima na Ummy Mwalimu.

Uchapakazi wao ni makini na wanaooneka wanapenda kazi. Yaani, wanaishi Ili wafanye kazi, na siyo wanafanya kazi Ili waishi. (They live to work and not work to live).

Kwa maana ya kuongezea thamani uchapakazi wao na hivyo kuongeza ufanisi katika wizara tajwa, yangefanyika mabadiliko, ya kiufundi kwa maana ya kubadilishana wizara.
e hili kwa jicho kama langu na hakika wizara hizi zitapaa sana na nchi itajengwa vema kwa maana hiyo.
Hawa mademu naona wote ngoma droo. Hawana jipya japo nawapenda kwa kutojiruhusu kuwa chawa
 
Nakubaliana kabisa na pendekezo lako. Angalizo langu ni kwamba, Dorothy Gwajima hawezi kukubalika kwenye wizara ya Afya, na sababu zake hizo hizo sifa za kiutendaji ulizozitaja kwenye post yako:

Kuijua taaluma ya afya na hasa juu ya utawala, ni kumfanya awe tishio kwa mianya ya watu ya ulaji. Penye upigaji anajua, na kapigie kenyewe anakajua, kwa hiyo hawawezi kumdanganya kitu!

Aggressiveness ktk follow up maana yake ni mwisho wa yale mambo ya funika kombe mwanaharamu apite. Ukimdanganya kitu jua atafuatilia; watumishi wetu wengi hawataki kufuatiliwa. Tumejenga utamaduni wa "acha liende", kwa hiyo kupata kiongozi mfuatiliaji ni ataitwa mnoko.

Ukali na seriousness ya ufuatiliaji maana yake ni kutaka watu wafanye kazi kwa bidii na kwa ufanisi. Ni mtumishi gani nchi bado anataka kufanya kazi kwa bidii na Ufanisi? Positions walizonazo watu ni kwa ajili ya ulaji na upigaji tu.
 
Wote waliotajwa wanafanya kazi kwa kupitia vyombo vya habari.

Mtoa mada,utendaji kazi sio mpaka kiongozi atoe matamko mbele ya kamera na waandishi wa habari.

Wengi unaowaona kwenye kamera,ni mwendo wa kutengeneza kiki.

Kama ni kazi zinafanywa nà wataalamu,maelezo ya kitaalamu yanatakiwa kutolewa na wataalamu,lakini wanaoteuliwa wanaacha kwenda kwenda kwa wananchi,wanakimbilia vyombo vya habari,na wananchi wanafikiri kila wanachokiona kimesemwa na mwanasiasa kwamba ndio utendaji.
 
Hila Ummy leo nimemuona akijibu maswali ya ziara ya raisi India aisee huyu mwana Mama anajua tena anajua
 
Wako vizuri ili profile ya Dorothy imepoa sana ameamua kuwa low profile tofauti na zamani, Ummy inaonekana anajua kula vizuri na wenyewe Bora wawe mawaziri tu popote pale
 
Wizara ni katibu mkuu, waziri ataonekana mchapa kazi kama katibu mkuu wake yupo vizuri ..Dkt. Zainab Chaula, pale afya alikuwa yupo vizuri sana .. kuna kipindi alikuwa haelewani na Ummy hadi Magufuli akasema "sms zao anazisoma" Dkt. Zainab Chaula wizara ya afya ndio kwake hasa
 
Matatizo ya mawaziri wetu wengi, ni "reactive" katika utendaji wao, hususan Gwajima na Ummy.

Hqwwnw ubunifu kabisa, wapo stagnant na routine works na mapakw kitokee kitu ndiyo wakurup7ke.

Sijawahi kuona plan zao kama vile nnavyomuna Bashe na January.

Bashe na January wizara zao tumeona wana plan za miaka kadhaa ijayo.


Hawa mabinti, sifahamu ni malezi ya Kitanzania au ndiyo "cqpacity" zao zimeishia hapo. Kwa mtazamo wangu, wizara zào zinapwaya sana kwenye ubunifu.

Wizara zao zipo zipo tu kimazowea, ubunifu ni 0.
 
Matatizo ya mawaziri wetu wengi, ni "reactive" katika utendaji wao, hususan Gwajima na Ummy.

Hqwwnw ubunifu kabisa, wapo stagnant na routine works na mapakw kitokee kitu ndiyo wakurup7ke.

Sijawahi kuona plan zao kama vile nnavyomuna Bashe na January.

Bashe na January wizara zao tumeona wana plan za miaka kadhaa ijayo.


Hawa mabinti, sifahamu ni malezi ya Kitanzania au ndiyo "cqpacity" zao zimeishia hapo. Kwa mtazamo wangu, wizara zào zinapwaya sana kwenye ubunifu.

Wizara zao zipo zipo tu kimazowea, ubunifu ni 0.
We nae bibi una wivu tu.
Mbona Gwajima ni member humu na hujawahi kumuuliza haya yote ukaona kama anayo au la?
 
Back
Top Bottom