Ijue ‘ thamani ‘ ya ‘ PhD ‘ ya Ulaya ya Waziri Mwakyembe

PhD aliisahau mbeya
Nadhani sasa itungwe Sheria ya kwamba hawa ' Wakubwa ' wa Serikalini wawe wanatuwekea na Majina ya Vyuo Vikuu vyao walivyosoma huko Ulaya na kupata hizo ' Doctorate Degree ' zao ili nasi tujiridhishe kwani siyo Siri Mimi GENTAMYCINE kwa hii Elimu yangu tu ya Darasa la Saba naona nawazidi Wakubwa / Viongozi wengi mno na ambao ni ' Wasomi ' katika suala zima la Ujengaji Hoja na matumizi sahihi ya Akili tulizopewa bure na Mwenyezi Mungu.

Sasa nathibitisha rasmi kuwa nina ' Mashaka ' makubwa na ' PhD ' ya Waziri Mwakyembe na za Watu wengine kama Sita ( 6 ) hivi ila leo nawaweka ' Kiporo ' kwani haiwezekani na haiingii akilini Mtu mwenye Elimu Kubwa tena ya kuwa na Doctorate Degree / PhD lakini bado anawaza Kipopoma / Kipumbavu namna hii.
 
Akizungumza kwa ‘ Mikogo ‘ kama kawaida yake Bungeni leo alipokuwa akiwasilisha Bajeti ya Wizara yake Waziri mwenye dhamana na masuala ya Michezo nchini ‘ Msomi ‘ wa hali ya juu Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa sababu Kuu Tatu ambazo ndizo zimefanya Timu ya Taifa ya Vijana ya ‘ Serengeti Boys ‘ kufanya vibaya katika hii Michuano inayoendelea nchini.

Si vibaya tukizijua hizo sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Waziri ‘ Msomi ‘ wa ‘ PhD ‘ Mwakyembe alizozitoa leo Bungeni…..


Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Mawakala wa akina El Haji Diof na Samuel Eto walianza Kuwarubuni na Kuwaahidi Mipesa Kibao.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Wazazi wa hawa Wachezaji walishaanza Kuwakopa Watoto Wao Hela kwakuwa walishasikia kuwa Watoto Wao hao wanaenda kuwa Matajiri hivyo ikawaathiri Vijana Kisaikolojia.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa kuna Watanzania wengine baada ya kusikia hawa Vijana wameahidiwa Pesa nyingi hao Watanzania walianza kuwaonea Wivu / Kijicho hawa Vijana hali ambayo ilianza kuwawekea Nuksi na wakaharibu kabisa.

Shikamoo sana Waziri Dkt. Mwakyembe.

Nawasilisha.
KWA KWELI NASOMA, NATAFAKARI TOKA JUZI ALIPOSEMA HAYA HUYU MSOMI WETU SIJAELEWA NA BAYA ZAIDI SIONI MWELEKEO WA KUELEWA. WASOMI WETU NI MAJINIASI SANA INAFIKIA SISI WANYONGE HATUWAELEWI NADHANI.
 
Hata wewe yangekukuta yale yaliyomkuta ya ile sumu, ukurutu akilini na mwilini kisha ukawa waziri ungekuwa na hoja hizo hizo. Tatizo lililopo kwa watanzania wengi wanafikiri huyu ndugu alipona. wewe mwangalie tu uone kama dishi lake lipo vizuri. Ni kama huwa anaweweseka vile hata anapoongea. Nakupa kazi wewe msomaji utenge muda wa kumfuatilia huyu ndugu utapata jibu.
 
Tanzania ni ya ajabu sana. tunahimiza wawekezaji hadi kwenye sekta ya michezo na mawakala waje kuangalia vipaji tulivyonavyo na wawachukue wachezaji wengi wacheze nje ili kuimarisha Taifa Stars lakini viongozi wanawakebehi mawakala kiasi hiki! Hovyo kabisa
 
Mwakyembe ni mwanasheria mzuri lakini kwenye hili suala la Serengeti Boys ameingizwa chaka vibaya sana na walio chini yake.

Ile tu JPM kusema kuwa alikuwa akipigiwa simu na Mwakyembe halafu hapokei baada ya kufungwa na Lesotho inatosha kuonyesha namna ambavyo anashindwa kuondoa madudu ya ubabaishaji pale TFF.

Mkuu Karia hapatani na wachezaji wa zamani kina China na wakongwe wengine, huwezi kupata mafanikio endelevu iwapo wewe unayepewa dhamana ya soka hupatani na wanasoka waliocheza miaka ya nyuma.

Mwakyembe anapungukiwa aina fulani ya kuendana na watu wa soka la kibongo, siwezi kumlaumu huyu ni mtu wa hali ya juu sana hapa Tanzania, analazimika kujishusha lakini bado anakosa zile akili za fitina kama alizonazo Aden Rage na kina Kapuya.
 
Mwakyembe ni mwanasheria mzuri lakini kwenye hili suala la Serengeti Boys ameingizwa chaka vibaya sana na walio chini yake.

Ile tu JPM kusema kuwa alikuwa akipigiwa simu na Mwakyembe halafu hapokei baada ya kufungwa na Lesotho inatosha kuonyesha namna ambavyo anashindwa kuondoa madudu ya ubabaishaji pale TFF.

Mkuu Karia hapatani na wachezaji wa zamani kina China na wakongwe wengine, huwezi kupata mafanikio endelevu iwapo wewe unayepewa dhamana ya soka hupatani na wanasoka waliocheza miaka ya nyuma.


Mwakyembe anapungukiwa aina fulani ya kuendana na watu wa soka la kibongo, siwezi kumlaumu huyu ni mtu wa hali ya juu sana hapa Tanzania, analazimika kujishusha lakini bado anakosa zile akili za fitina kama alizonazo Aden Rage na kina Kapuya.

Kwahiyo Rais wa TFF Wallace Karia akiwa karibu na huyo Athumani Abdallah China ndiyo ' Serengeti Boys ' na ' Taifa Stars ' vitabeba ' Vikombe ' vyote vya CAF na FIFA? Hivi kuna Uongozi wa Soka wa nchi hii ambao ulikuwa jirani / karibu sana na hawa Wachezaji wako za Zamani kama Uongozi wa ' Libero ' Mzee Leodgar Chilla Tenga? Je Tanzania tulikuwa na ' Kiwango ' gani Kimpira na Kimataifa wakati wa Kipindi chake? Tanzania kama Tanzania ' tumeshalaanika ' tu kwa mambo mengi hivyo twendeni tu hivi hivi hadi pale dunia itakapopinduka au Kristo atakapokuja tena.
 
Akizungumza kwa ‘ Mikogo ‘ kama kawaida yake Bungeni leo alipokuwa akiwasilisha Bajeti ya Wizara yake Waziri mwenye dhamana na masuala ya Michezo nchini ‘ Msomi ‘ wa hali ya juu Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa sababu Kuu Tatu ambazo ndizo zimefanya Timu ya Taifa ya Vijana ya ‘ Serengeti Boys ‘ kufanya vibaya katika hii Michuano inayoendelea nchini.

Si vibaya tukizijua hizo sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Waziri ‘ Msomi ‘ wa ‘ PhD ‘ Mwakyembe alizozitoa leo Bungeni…..

Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Mawakala wa akina El Haji Diof na Samuel Eto walianza Kuwarubuni na Kuwaahidi Mipesa Kibao.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Wazazi wa hawa Wachezaji walishaanza Kuwakopa Watoto Wao Hela kwakuwa walishasikia kuwa Watoto Wao hao wanaenda kuwa Matajiri hivyo ikawaathiri Vijana Kisaikolojia.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa kuna Watanzania wengine baada ya kusikia hawa Vijana wameahidiwa Pesa nyingi hao Watanzania walianza kuwaonea Wivu / Kijicho hawa Vijana hali ambayo ilianza kuwawekea Nuksi na wakaharibu kabisa.

Shikamoo sana Waziri Dkt. Mwakyembe.

Nawasilisha.

Msamehe ni mgonjwa
 
Yaani kuna madokta na professor hapa tz hadi unajiuliza ..yawezekana ni rahisi sana kuwa na izo elimu

Aisee kwamba mtoto wa under 17 mzazi anamkopa rubbish..wakati pesa wangepewa baada ya kufuzu

Rubbish,rubbish
Hii ni fedheha kubwa kwa Wazazi pamoja na hawa Vijana kiujumla. Itawaathiri zaidi kisaikolojia kuliko kuwajenga..
 
Kwahiyo Rais wa TFF Wallace Karia akiwa karibu na huyo Athumani Abdallah China ndiyo ' Serengeti Boys ' na ' Taifa Stars ' vitabeba ' Vikombe ' vyote vya CAF na FIFA? Hivi kuna Uongozi wa Soka wa nchi hii ambao ulikuwa jirani / karibu sana na hawa Wachezaji wako za Zamani kama Uongozi wa ' Libero ' Mzee Leodgar Chilla Tenga? Je Tanzania tulikuwa na ' Kiwango ' gani Kimpira na Kimataifa wakati wa Kipindi chake? Tanzania kama Tanzania ' tumeshalaanika ' tu kwa mambo mengi hivyo twendeni tu hivi hivi hadi pale dunia itakapopinduka au Kristo atakapokuja tena.
Mkuu huwezi kulinganisha TFF ya Tenga na hii ya Karia, yapo mengi sana yenye tofauti.

Kalusha Bwalya ni sehemu muhimu ya mafanikio ya timu ya taifa ya Zambia mpaka ikabeba kombe la afrika mbele ya kina Drogba.

Kina Amunike na wengine wa kizazi chake ni sehemu muhimu ya mafanikio ya Super Eagles ya miaka ya karibuni.

Huwezi kuwakwepa kina Gary Neville na Beckham kama unaitakia mema three lions.

Karia anamlengesha pabaya Dr Mwakyembe.
 
Back
Top Bottom