Best Daddy
JF-Expert Member
- Apr 2, 2019
- 767
- 1,292
Tunamkumbuka Stephen King kwa maneno yake yenye busara hasa pale aliposema:
"Talent is cheaper than table salt. What separates the talented individual from the successful one is a lot of hard work."
Ila bwana Kevin Durant yeye akasema "” Hard work beats talent when talent fails to work hard” Kisha akaenda zake.
Ila katika msimu wa 2015/2016 baada ya fainali ya UCL vyombo vya habari kila kona ya dunia vilipambwa na vichwa vya habari vyenye maneno mepesi lakini yenye kufikirisha ndani yake kutoka kwa CR7 pale alipoweka wazi bila kung'ata ulimi , akisema;
"A talent without hardwork is NOTHING"
Yes, Yeye alisema Kipaji bila jitahada au kujituma kwake si chochote.
Wengi tulichagua kutomuelewa kwa kusema labda kwake, ila kwa Messi haipo hivyo. (Tuishie hapa tusije tukaingia kwenye mtego wa Team Messi vs CR7)"
Turudi hapa nyumbani sasa, Japo mifano yangu itajikita kwa vilabu vikubwa Simba, Yanga kidogo na Azam. (Huu sio upendeleo ila kama Club yako unataka izungumziwe basi ipambane kuja huku juu)
Chukua First Eleven ya Simba, Kisha Chukua ya Yanga, then Maliza na ya Azam. (Tulia kidogo).
Endapo mpira unachezwa kwenye karatasi kupitia vipaji vya wachezaji, basi Simba ni Bingwa, Azam na Yanga watachuana vikali sana kutafuta nafasi ya pili.
(Ukihisi kuna jambo halipo sawa kwa hiki nilichosema, think again).
Swali: Kuna timu ina vipaji kama SSC kwa sasa? Kuna timu ilisifiwa kwa usajili bora kama Azam? Kuna Timu ambayo ilionekana ipo nyuma nyuma wakati wa usajili kama Yanga? Sio kwa upigaji kelele angalia wachezaji waliokuwa wanasajiliwa.
Sasa kipi kinamfanya Yanga awe juu hadi sasa hasa katika perfomance?
Katika hizo timu mbili kuna mtu anatoa energy kama Mudathir? Kuna mtu anajituma kama Yao? Baka je? Vipi kuhusu Max, I think kwa mechi hizi mbili ikiwepo hii fainali jamaa anazunguka uwanja mzima? Sasa kwa hii Jitahada ya Max, Msimu huu Aziz Ki atakua na namba nzuri sana, wengi mtabeza ila kwa nature ya uchezaji wa Simba basi Chama ajiandae kisaikolojia. Huku pia namtabiria makubwa Pacome maana tayari viungo wa Yanga hasa Aucho, M. Yahya, Max wanafanya kazi kubwa, yeye wasubirie kutumia akili yake. I think ni moja ya wachezaji wenye akili kubwa pale Yanga.
Je Unaiona Pressing Ya Musonda au huyu dogo Mzize? Sijui wanamuona Job?....List inaendelea. Kila mchezaji anapambana. Kila mchezaji anatoka jasho.
Hii yanga ambayo ukicheza nayo unaweza piga magoti na kuomba refa amalize dakika 90, unafikiri ni vipaji pekee?
Hii Yanga ambayo ukikutana nayo inakutesa hadi maji unawezaita Mma? Haijalishi wewe ni nani? Unafikiri ni vipaji pekee? Nasema hivi, Sawa tumechukua Ngao mbele yake, lakini kama tukikutana naye kwenye ligi tukacheza slow hivi? Nasema hivi lazima tunaaibika. Wanaweza wakatengeneza record mpya katika mechi ya derby.
Jamani, mnaona lakini Yanga anavyotoa hii energy?
Sasa huu ndio mstari unaotofautisha Yanga na hivi vilabu viwili. Hao wengine hata hawapress, wakipoteza mpira wanatembea, mtu akipewa mpira anasimama, Robertintho atalaumiwa kila siku kwa Kumpanga Mzamiru na Kibu D lakini kiukweli hao ndio wanatoa energy inayotakiwa uwanjani. Ila Simba akitoa hata nusu ya energy ya Yanga uwanjani basi tutakuja kuzungumza mengine hapa. Naomba nisitafsirike vibaya, Sisemi Simba au Azam wacheze kama Yanga, hapana. Hapa nazungumzia kujituma tu.
NB: Timu kuwa na energy au kukosa energy inaweza kuwa ni sababu za kiufundi, ila mara nyingi hutokana na nature ya wachezaji unaosajili (Hii nitaizungumza vizuri wakati mwingine).
Ila kwa ufupi, upande wa Simba, imani yangu inaniambia Wachezaji hawamtaki Kocha, haiwezekani mchezaji professional unacheza hivi? Unataka Robertinho akufundishe kukaba endapo utapoteza mpira?
Na hapa sidhani kama ni wachezaji tu, maybe hata viongozi hawamtaki pia. Kwa hii picha inayoendelea, Robertinho ikiwezekana aachie ngazi tu, kabla hajakutana na aibu kubwa, akachafua CV yake. Maana tayari anaonekana amekosa sauti katika timu, yani timu haiwezi ikacheza hivi ni tofauti kabisa na falsafa ya Robertinho. Nasubiri kuona Mechi ya kuingia makundi dhidi ya Power Dynamos wanaweza wakamuangushia Jumba hapa au mechi ya ligi na Mtani, akikosekana hapo basi mechi na Azam.(Lazima wamtafute kwenye game kubwa ambayo ina hisia na attention kubwa kutoka kwa Mashabiki).
Pia, kuhusu nature ya wachezaji wa Simba(Nitakuja kuzungumzia) Ila hata mwenyewe jaribu kuangalia nature ya wachezaji wa Simba compare na Yanga taratibu unawezapata majibu. Angalia Umri, miili yao, Lifestyle yao, e.t.c. Hata aje kocha wa viungo kutoka Man City hawezi fanya wachezaji wazee wakimbie kama vijana. Jokes, but it is true.
Azam kwa kikosi walichonacho, I think wamekosa Mashabiki au uongozi wenye sauti ya kuipa pressure hii timu ipambane. Inacheza kama timu ya Baba. Ni changamoto kubwa sana kwa kocha yeyote mwenye malengo kufanikiwa akiwa Azam.
Kutokana na neno Hard kutafsirika vibaya, katika uzi huu "Hard work" is the act of dedicating oneself to achieving a goal through persistence, determination, discipline, and sacrifice
Muda ni Mwalimu mzuri sana.
"Talent is cheaper than table salt. What separates the talented individual from the successful one is a lot of hard work."
Ila bwana Kevin Durant yeye akasema "” Hard work beats talent when talent fails to work hard” Kisha akaenda zake.
Ila katika msimu wa 2015/2016 baada ya fainali ya UCL vyombo vya habari kila kona ya dunia vilipambwa na vichwa vya habari vyenye maneno mepesi lakini yenye kufikirisha ndani yake kutoka kwa CR7 pale alipoweka wazi bila kung'ata ulimi , akisema;
"A talent without hardwork is NOTHING"
Yes, Yeye alisema Kipaji bila jitahada au kujituma kwake si chochote.
Wengi tulichagua kutomuelewa kwa kusema labda kwake, ila kwa Messi haipo hivyo. (Tuishie hapa tusije tukaingia kwenye mtego wa Team Messi vs CR7)"
Turudi hapa nyumbani sasa, Japo mifano yangu itajikita kwa vilabu vikubwa Simba, Yanga kidogo na Azam. (Huu sio upendeleo ila kama Club yako unataka izungumziwe basi ipambane kuja huku juu)
Chukua First Eleven ya Simba, Kisha Chukua ya Yanga, then Maliza na ya Azam. (Tulia kidogo).
Endapo mpira unachezwa kwenye karatasi kupitia vipaji vya wachezaji, basi Simba ni Bingwa, Azam na Yanga watachuana vikali sana kutafuta nafasi ya pili.
(Ukihisi kuna jambo halipo sawa kwa hiki nilichosema, think again).
Swali: Kuna timu ina vipaji kama SSC kwa sasa? Kuna timu ilisifiwa kwa usajili bora kama Azam? Kuna Timu ambayo ilionekana ipo nyuma nyuma wakati wa usajili kama Yanga? Sio kwa upigaji kelele angalia wachezaji waliokuwa wanasajiliwa.
Sasa kipi kinamfanya Yanga awe juu hadi sasa hasa katika perfomance?
Katika hizo timu mbili kuna mtu anatoa energy kama Mudathir? Kuna mtu anajituma kama Yao? Baka je? Vipi kuhusu Max, I think kwa mechi hizi mbili ikiwepo hii fainali jamaa anazunguka uwanja mzima? Sasa kwa hii Jitahada ya Max, Msimu huu Aziz Ki atakua na namba nzuri sana, wengi mtabeza ila kwa nature ya uchezaji wa Simba basi Chama ajiandae kisaikolojia. Huku pia namtabiria makubwa Pacome maana tayari viungo wa Yanga hasa Aucho, M. Yahya, Max wanafanya kazi kubwa, yeye wasubirie kutumia akili yake. I think ni moja ya wachezaji wenye akili kubwa pale Yanga.
Je Unaiona Pressing Ya Musonda au huyu dogo Mzize? Sijui wanamuona Job?....List inaendelea. Kila mchezaji anapambana. Kila mchezaji anatoka jasho.
Hii yanga ambayo ukicheza nayo unaweza piga magoti na kuomba refa amalize dakika 90, unafikiri ni vipaji pekee?
Hii Yanga ambayo ukikutana nayo inakutesa hadi maji unawezaita Mma? Haijalishi wewe ni nani? Unafikiri ni vipaji pekee? Nasema hivi, Sawa tumechukua Ngao mbele yake, lakini kama tukikutana naye kwenye ligi tukacheza slow hivi? Nasema hivi lazima tunaaibika. Wanaweza wakatengeneza record mpya katika mechi ya derby.
Jamani, mnaona lakini Yanga anavyotoa hii energy?
Sasa huu ndio mstari unaotofautisha Yanga na hivi vilabu viwili. Hao wengine hata hawapress, wakipoteza mpira wanatembea, mtu akipewa mpira anasimama, Robertintho atalaumiwa kila siku kwa Kumpanga Mzamiru na Kibu D lakini kiukweli hao ndio wanatoa energy inayotakiwa uwanjani. Ila Simba akitoa hata nusu ya energy ya Yanga uwanjani basi tutakuja kuzungumza mengine hapa. Naomba nisitafsirike vibaya, Sisemi Simba au Azam wacheze kama Yanga, hapana. Hapa nazungumzia kujituma tu.
NB: Timu kuwa na energy au kukosa energy inaweza kuwa ni sababu za kiufundi, ila mara nyingi hutokana na nature ya wachezaji unaosajili (Hii nitaizungumza vizuri wakati mwingine).
Ila kwa ufupi, upande wa Simba, imani yangu inaniambia Wachezaji hawamtaki Kocha, haiwezekani mchezaji professional unacheza hivi? Unataka Robertinho akufundishe kukaba endapo utapoteza mpira?
Na hapa sidhani kama ni wachezaji tu, maybe hata viongozi hawamtaki pia. Kwa hii picha inayoendelea, Robertinho ikiwezekana aachie ngazi tu, kabla hajakutana na aibu kubwa, akachafua CV yake. Maana tayari anaonekana amekosa sauti katika timu, yani timu haiwezi ikacheza hivi ni tofauti kabisa na falsafa ya Robertinho. Nasubiri kuona Mechi ya kuingia makundi dhidi ya Power Dynamos wanaweza wakamuangushia Jumba hapa au mechi ya ligi na Mtani, akikosekana hapo basi mechi na Azam.(Lazima wamtafute kwenye game kubwa ambayo ina hisia na attention kubwa kutoka kwa Mashabiki).
Pia, kuhusu nature ya wachezaji wa Simba(Nitakuja kuzungumzia) Ila hata mwenyewe jaribu kuangalia nature ya wachezaji wa Simba compare na Yanga taratibu unawezapata majibu. Angalia Umri, miili yao, Lifestyle yao, e.t.c. Hata aje kocha wa viungo kutoka Man City hawezi fanya wachezaji wazee wakimbie kama vijana. Jokes, but it is true.
Azam kwa kikosi walichonacho, I think wamekosa Mashabiki au uongozi wenye sauti ya kuipa pressure hii timu ipambane. Inacheza kama timu ya Baba. Ni changamoto kubwa sana kwa kocha yeyote mwenye malengo kufanikiwa akiwa Azam.
Kutokana na neno Hard kutafsirika vibaya, katika uzi huu "Hard work" is the act of dedicating oneself to achieving a goal through persistence, determination, discipline, and sacrifice
Muda ni Mwalimu mzuri sana.