In this Information Age, almost everybody is an ‘expert’ in ‘everything’.
So, if I had my druthers, this is what I would do:
Wale wote ambao kwao Rais Magufuli hana jema lolote lile, ningewapa fursa ya wao kuunda serikali nzima ya kuiongoza Tanzania halafu tuone kile ambacho wao wangekifanya kilicho bora zaidi na kilicho tofauti kabisa na afanyacho Rais kwa sasa.
Manake sasa naona na sisi kwenye hii Tanzania yetu tuna watu wanaosumbuliwa na Magufuli Derangement Syndrome.
Chochote afanyacho Rais, kuna watu hawatapenda tu, hata kama na wao ni wanufaika.
Chochote asemacho Rais, watu hawa wenye huu ugonjwa wa Magufuli Derangement Syndrome, watasema ni kibaya tu kwa vile kimesemwa na yeye. Lakini kitu hicho hicho kikisemwa na mwingine, watashangilia kwa kupiga makofi na vigeregere.
Watu hawa natamani sana wao ndo waunde serikali ili hatimaye tuone kama kweli wanaweza kufanya kinyume na vile ufanyavyo huu utawala wa sasa.
Manake isije tu kuwa ni kelele za kupitia kwenye keyboards zisizoambatana na substance yoyote ile kwenye uhalisia.
Anyway, that’s just a hope. And a hope without a plan is nothing more than a wish.....