If I had my druthers....

If I had my druthers....

Eti watu walikuwa wanapinga mashule na miundombinu 🤣🤣
Mkuu si maneno yangu, Ni KinaMusiba wa wakati huo.. KinaMusiba walikuwepo tangu kipindi cha Mkoloni 😂 😂
 
Nyie Chadema Mlikuwa na Mgombea?
Hahaha ccm ilikuwa na wagombea 40 walitumia mfumo gani kumpata Magufuli?! Unadhani wangejieleza mbele ya wajumne na kupigiwa kura, angeshinda?! Sasa kama hakupatikana kwa haki tangu chamani unadhani watampenda au wanaojipendekeza ni wale walionufaika naye yaani wateuliwa?! Mimi sijasema CHADEMA popote, nimeongelea Magufuli, hapendwi hilo liko wazi, angeruhusu wapinzani wafanye siasa aone kama kweli anapendwa, hata yeye anafahamu analazimisha wananchi kumkubali, ajipime kwa hao wanaompenda kwa kuruhusu ushindani wa haki na uwazi, hili lingemsaidia hata yeye kufahamu wanafiki ni kina nani miongoni mwa praise team.
 
Kingereza kiingi kwa kuchanganya na kiswahili, blabla kibao ... wana saikolojia wanasema huo ni mkwara wa kuonyesha ni jinsi gani ulihudhuria shule na kupata uelewa, na pia lengo hasa ni kutuonyesha kuwa hicho ulichokiandika ni cha kidarasani darasani ...

Bahati mbaya mkwara wako wa kishuleshule tumeustukia na kujikuta wengine tunaona umendika usichokielewa kwa sababu huko darasani ulipitwa/ulishindwa kuelewa kuwa uzuri/ubaya au ubora/udhaifu wa uongozi/kiongozi katika siasa hupimwa kwa mizani ya mazuri na mabaya yanayofanyika na si kwa kuhesabu kitu kimoja kimoja kilichofanyika kama ambavyo inafanyika sasa

Na hilo hutegeameana na uhusianoa wa moja kwa moja na furaha, upendo, mahusianoa mema, amani na utulivu wa wana nchi kwa ujumla ... Hivyo basi mizani ya Mfungwa mtarajiwa imezidi kwenye ubaya wa Mambo mabilimbali ikiwemo ukanadamizaji, dhulma, uonevu, unyimifu wa haki na hata udhalimu wa wazi ...

Ndio mana unaona nakusikia watu wakilalamika sana nawengine kufungwa midomo makusudi hivi nikuulize bro ni lini mtu atasifia bomberdia kwa gharama ya watu kutekwa nakupotezwa??? Kwani binadamu mmoja anauzwa shingapi??? Kwa kulinganisha na bei ya bombadia???

Kwani Kuna nini nyumaya ya hayo maendeleo mpaka uteke watu??? Hutaki watu waseme unataka useme wewe tu kwani we ni malaika kweli kama unavyojinasibu???
 
Wapingaji wa Magufuli wengi wanasumbuliwa na njaa ukifatilia wengi either maslahi yao yameminywa au wanapata mkate wa kila siku kwa kumpinga JPM.
Hivi unDHANI WATUMISHI WOTE WA KADA ZA CHINI WATAMKUBALI MAGUFULI? tangu ameingia madarakani hakuna kuongezewa mshahara
 
tena watafanya kinyume sana tuu! yaan ww unafurahia watu kuny’ang’anywa uhai wao. jema gan utawapatia watu zaid ya uhuru?? ukitaka kujua ubaya wa hii serikali kamuulize Erick kabendera! kakaa sero wiki nzima wanatafuta namna ya kumuumiza , walikua hawana plan b ikiferi ya kumpoteza. ndio maana walikaa naye muda woote huo. na kwa vile lengo lao ilikua ni kumnyamazisha milele na wameferi sasa wameona wampumzishe! je huu ndio utawala unaopigia upatuuu?????

elimu inatakiwa itukomboe kifikra na kimtizamo nje ya hapo hatuna tofaut mbumbu.

ukiishi kwa tajiri huku anakutesa na hatak ulalamike kisa unalala pazuri au unakula vizur huo ni ukichaa!

hakuna zuri dunian linaloweza kuwa mbadala ya uhai wa watu.
 
In this Information Age, almost everybody is an ‘expert’ in ‘everything’.

So, if I had my druthers, this is what I would do:

Wale wote ambao kwao Rais Magufuli hana jema lolote lile, ningewapa fursa ya wao kuunda serikali nzima ya kuiongoza Tanzania halafu tuone kile ambacho wao wangekifanya kilicho bora zaidi na kilicho tofauti kabisa na afanyacho Rais kwa sasa.

Manake sasa naona na sisi kwenye hii Tanzania yetu tuna watu wanaosumbuliwa na Magufuli Derangement Syndrome.

Chochote afanyacho Rais, kuna watu hawatapenda tu, hata kama na wao ni wanufaika.

Chochote asemacho Rais, watu hawa wenye huu ugonjwa wa Magufuli Derangement Syndrome, watasema ni kibaya tu kwa vile kimesemwa na yeye. Lakini kitu hicho hicho kikisemwa na mwingine, watashangilia kwa kupiga makofi na vigeregere.

Watu hawa natamani sana wao ndo waunde serikali ili hatimaye tuone kama kweli wanaweza kufanya kinyume na vile ufanyavyo huu utawala wa sasa.

Manake isije tu kuwa ni kelele za kupitia kwenye keyboards zisizoambatana na substance yoyote ile kwenye uhalisia.

Anyway, that’s just a hope. And a hope without a plan is nothing more than a wish.....
Freedom of expression inalindwa na katiba.Koma ku invade democratic space ya watanzania.
 
Hao waendelee tu kutumia latrine zao.. wanaboaaaaaaaa.. wengi wao wametenda mengi kabla sasa wanasaga meno.. no dezo dezo kwao na wanafamilia wao.
 
Yaani wewe jamaa ni kilaza.
Wewe unachojua ni kuandika kingereza tuu lakini kati ya vilaza wewe ni kiongozi.
Hamna unachokijua, mabandiko yako yamejaa ujinga tuu.

Mada kama hizi uwe unaacha watu wenye akili zao wazilete sio wewe akili imejaa matope tuu.
 
Yaani wewe jamaa ni kilaza.
Wewe unachojua ni kuandika kingereza tuu lakini kati ya vilaza wewe ni kiongozi.
Hamna unachokijua, mabandiko yako yamejaa ujinga tuu.

Mada kama hizi uwe unaacha watu wenye akili zao wazilete sio wewe akili imejaa matope tuu.

Ahsante kwa kuchangia ujinga.
 
Back
Top Bottom