ID zenu nyingine tunazijua

ID zenu nyingine tunazijua

97903b52-2770-47e9-8b83-c3be9d36a734.jpeg
 
Ila ID za JF..🙌🏿❗

Enzi za mada maalum ya nagari ikafikia mahali tukawa na group la WhatsApp la magari

Sasa yule mwana mmoja alikuwa active Sana JF na kwenye group.. Akasema yeye ni dereva wa IT na coaster za kukodi

Basi muda mwingi akawa ni mtu wa kupost matukio ya safari za usiku.. Hasa kupeleka misiba ama IT

Yani 24/7 yuko barabarani.. Sasa ikabidi watu waanze kuhoji anapumzika saa ngapi? Na anawezaje kupost JF na kwenye group wakati anaendesha?

Kidogo akapunguza ila akaja sasa kutupiga kipigo kitakatifu.. Akatutangazia msiba msiba wa mwanae pekee wa kike aliyekuwa Mombasa na mama wa jambo
Akatupiga fix mtoto kauliwa na huyo mama! Tukatumiwa na picha ya mtoto akiwa hai ..ILA
Picha za msiba hakuna
Picha za jeneza bilabila
Picha za kaburi bilabila🙌🏿🙆🏿‍♂😃
Kumbukeni hapo kwenye group tumeshamchangia sana na JF pia🤣

Alikuwa na watu wake wa kumtetea sana! Mmoja (mdada) alikuja kuomba radhi baadae baada ya jamaa kukaribishwa kwake akapewa pombe kidogo ndio vituko halisi vikajidhihiri😀
Baada ya ishu ya msiba feki wa mtoto kubumbuluka jamaa aliingia mitini na group likawa bye! Bye..!😀
 
Back
Top Bottom