Hongereni kwa ku-spin mambo!!! Hivi kujiunga CCM si hiari!!! Kama hukubaliani, si unakuwa nje kama mimi, sasa kuna haja gani ya Ku-spin.
Kila siku zinavyoenda hizi spinning strategy zinaendelea kuweka wazi kwamba kumbe CCM wako fiti zaidi.
Sasa ma-think tank wa Upinzani badala ya kuja na mambo yao... kueneza siasa zao wanapata shida na wanaCCM ambao wanabadilisha katiba yao kwa vikao... wanatoa matamko kwa vikao...
Mwalimu angekuwepo na kuona waliyoyafanya kina Mkapa, JK na ukimya wa vigogo wengine wa CCM, angerudisha kadi jangwani!! Hakuwa anajikomba kwa mtu yeyote ndani ya CCM.
Wewe kweli unampenda Nyerere...
Sitabishana tena na wewe kuhusu yeye...
Mkuu heshima mbele,
1. sasa ilikuwaje hakurudisha kadi kwenye uchaguzi wa visiwani, ambao sio siri CCM ilishindwa mwaka 1995?
2. NBC ilipouzwa na Mkapa, tena kwa bei poa na chaguo lake mbona hakurudisha kadi CCM?
3. Lowassa aliporudi cabinet, mbona hakurudisha kadi?
Akili yangu eti ina kutu, no way mkuu, katiba ya CCM ni reflcetion ya mawazo ya Mwalimu, tena ndio maana sasa CCm wamemua kumuenzi maana kuna sehemu wamegundua kuwa walikuwa wanakosea, that is my point na ninasema kuwa ili Tanzania tuendelee tunahitaji kuachana na hizo fikra za Mwalimu, huenda zilikuwa valid enzi hizo, lakini sasa hivi tunachohitaji na respect kwa the rule of law ya jamhuri yetu, sio katiba za vyama vya siasa.
Mwalimu, amefanya mengi mazuri kwa taifa letu, lakini the time has now come, tunahitaji kuachana na fikra zilizopitwa na wakati, maana kwa mfano, Mwalimu alijua kuwa Lowassa, ni mla rushwa na ushaidi alikuwa nao, lakini akamzuia tu asiwe rais, badala ya kumfikisha kwenye sheria, sasa cha ajabu ni kipi cha CCM ya sasa kurudia yale yale ya Mwalimu, ya kumruhusu Lowassa kujiuzulu tu? badala ya kwenda kwenye sheria ni kwa sababu bado wanafuata mawazo yale yale yaliyopitwa na wakati.
Kwa hiyo basi:-
(1) Sisi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa
pamoja wa TANU na ASP tuliokutana leo
tarehe 21 Januari, 1977 mjini Dar es Salaam,
chini ya uongozi wa pamoja wa Mwalimu Julius
K. Nyerere Rais wa TANU na Ndugu Aboud
Jumbe, Rais wa ASP, kwa kauli moja tunaamua
na kutamka rasmi kuvunjwa kwa Tanganika
African National Union (TANU) na Afro Shirazi
Party (ASP) ifikapo tarehe 5 Februari, 1977, na
wakati huo huo kuundwa kwa Chama kipya cha
pekee na chenye uwezo wa mwisho katika
mambo yote kwa mujibu wa Katiba.
hapa utakesha ndugu yangu! Mwanakijiji hasikii wala haambiwi la mtu kuhusu Nyerere. Ni bora tu mkubaliane kutokubaliana muendelee na mijadala mingine.
Sasa, kosa kubwa ambalo CCM watakuwa wamelifanya juzi Butiama na ambalo watalijutia ni kukusanya maandishi yote ya Nyerere na kuyatafsiri na kuyaweka pamoja. Bora wafanya baada ya uchaguzi wa 2010 kwani wakifanya kabla ya hapo itakuwa ni kutengeneza mafuta ya kuwakaangia.
hhahahaha nimecheka kweli.. ukweli ni kuwa siyo kumpenda Mwalimu bali kuupenda ukweli. Kama mtu akija na kutoa kauli za kuhukumu k.v "fulani alisema hivi" au "alifanya vile" ni jukumu la mtu yeyote mwenye akili timamu kuhoji je ni kweli fulani alisema au kufanya yanayosemwa?
Mtu ambaye hataki kufikiri atakubali mara moja na kusema "duh kumbe fulani alifanya hivi au vile" na kama ni jambo la chuki basi chuki hupandikizwa na kama ni jambo la mapenzi basi mapenzi hupandikizwa.
Kwenye suala la Mwalimu kuna mengi yanasemwa juu yake. Kuwa alisema hivi au alifanya vile; mwisho yanakuwa kama ya Hillary. Tatizo ni kuwa karibu kila kitu ambacho mwalimu alikisema hadharani kimeandikwa mahali (na hapa nina maana tangu aingie kwenye uongozi wa kisiasa wa nchi).
Hivyo mtu akisema Mwalimu alisema hivi mtu ana hiari ya kuamini au kukataa kwa sababu yaliyosemwa yanajulikana, yapo na yanaweza kuthibitishwa. Ndio maana uliposema Nyerere alisema "Bila CCM Tanzania itayumba" nilikukatilia kwa sababu sicho alichosema Nyerere lakini mtu mwingine anaweza kuamini ulichosema.
Sasa, kosa kubwa ambalo CCM watakuwa wamelifanya juzi Butiama na ambalo watalijutia ni kukusanya maandishi yote ya Nyerere na kuyatafsiri na kuyaweka pamoja. Bora wafanya baada ya uchaguzi wa 2010 kwani wakifanya kabla ya hapo itakuwa ni kutengeneza mafuta ya kuwakaangia. Believe me, it is not in the interest ya CCM kukusanya maandishi hayo na kuyafanya yapatikane kiurahisi. Itakuwa ni kama Martin Luther alipotafsiri Biblia kwenda Kijerumani na kusababisha reformation!
Majibu ya maswali yako hayo ni kuwa kama mtu huru alikuwa na haki ya kuamua kurudisha kadi au la kwa misingi yake yeye siyo kwa misingi ya wewe na mimi; kama wakati ule hakuona tayari kurudisha kadi ilikuwa ni haki yake. Tutajua siku moja kwanini hakujiengua CCM na kwanini alijaribu kuisahihisha sana baada ya 1995 ndio maana wakati wa kufa kwake pale London kauli yake ya kwaheri haikuwa "waambieni wanaCCM wangu niliwapenda"..Mkuu heshima mbele,
1. sasa ilikuwaje hakurudisha kadi kwenye uchaguzi wa visiwani, ambao sio siri CCM ilishindwa mwaka 1995?
2. NBC ilipouzwa na Mkapa, tena kwa bei poa na chaguo lake mbona hakurudisha kadi CCM?
3. Lowassa aliporudi cabinet, mbona hakurudisha kadi?
Akili yangu eti ina kutu, no way mkuu,
Mzee hii ni hoja tofauti kabisa na uliyotoa mwanzo; mwanzoni ulisema ni yeye aliyebuni na kuandika katiba hiyo? sijui kama unakumbuka lakini sasa unasema ni reflection? Of course ni reflection ya mawazo ya watu wengi akiwemo Nyerere; ni reflection ya wajumbe wa Mkutano mkuu uliounda CCM.katiba ya CCM ni reflcetion ya mawazo ya Mwalimu,
tena ndio maana sasa CCm wamemua kumuenzi maana kuna sehemu wamegundua kuwa walikuwa wanakosea,
that is my point na ninasema kuwa ili Tanzania tuendelee tunahitaji kuachana na hizo fikra za Mwalimu, huenda zilikuwa valid enzi hizo, lakini sasa hivi tunachohitaji na respect kwa the rule of law ya jamhuri yetu, sio katiba za vyama vya siasa.
Mwalimu, amefanya mengi mazuri kwa taifa letu, lakini the time has now come, tunahitaji kuachana na fikra zilizopitwa na wakati,
maana kwa mfano, Mwalimu alijua kuwa Lowassa, ni mla rushwa na ushaidi alikuwa nao, lakini akamzuia tu asiwe rais, badala ya kumfikisha kwenye sheria,
sasa cha ajabu ni kipi cha CCM ya sasa kurudia yale yale ya Mwalimu, ya kumruhusu Lowassa kujiuzulu tu? badala ya kwenda kwenye sheria ni kwa sababu bado wanafuata mawazo yale yale yaliyopitwa na wakati.
Mzee, tumeziacha fikra za Nyerere mbona miaka mingi iliyopita, mbona hatujaendelea?
Labda ni kile alichokisema yeye mwenyewe kuwa "kuwa jukumu la uongozi unaofuatia ni kuangalia sisi tumefanikiwa wapi na tumekosea wapi, hivyo kuacha yale tuliyokosea na kushikilia yale ya msingi; lakini nyinyi mmeacha siyo tu tuliyokosea sisi bali hata yale ya msingi!". (Mei Mosi 1995.
Mazuri gani aliyoyafanya Nyerere ambayo tuyaache? Ni fikra zipi za Mwalimua ambazo zimepitwa na wakati?
Kwamba maendeleo ni ya watu na siyo vitu ni fikra zilizopitwa na wakati; kwamba kujenga Taifa la watu walio huru na sawa ni fikra zilizopitwa na wakati?
Mzee usimbebeshe Nyerere ufisadi wa Lowassa. Yaani ni Nyerere tu aliyejua kuhusu hayo unayoyasema kuhusu Lowassa? Mbona hawa wengine wakampa uwaziri hadi uwaziri mkuu? Yaani sasa unamtaka Nyerere angekuwa Polisi, mwanasheria mkuu n.k Mimi nadhani wewe unampa Nyerere nguvu nyingi za kiungu na uwezo mkubwa karibu na wa malaika kiasi kwamba angeweza kufanya yote hayo na huwezi kuona limitations zake kama mwanadamu.
Yaani Rufiji unanishangaza. Unataka kusema Mwalimu aliaacha kujenga daraja lako miaka 24 yote aliyokuwa madarakani akisubiri alijenge wakati wa Mkapa? Na mbona hakulijenga wakati wa Mwinyi?
Kwa taarifa yako, Mwalimu hakujali kabisa usafiri wa Kusini. Na aliona Kusini ni kama jela, ndio maana alimsukumiza Kasanga Tumbo huko kwa miaka kumi, kama adhabu.
Unataka kusema Mwalimu aliacha tukose hata sabuni ya kuogea, akisubiri ajenge supermarkets wakati wa Mkapa? Mtu aliyesema kukosekana vitu madukani ni matokeo ya maendeleo unathubutu kumlinganisha na Mkapa? Unamkosea sana haki Mkapa.
Mwalimu alikataza watu wa Songea kuuza mahindi yao nje. Wakati huo huo akawanyima barabara ya kuyaleta Dar, yakabaki yanawaozea tu. Mkapa alikwenda huko akawaruhusu kuyauza kwa yoyote yule. Wewe utasema ni Mwalimu aliwakomboa? Usidanganye.
Mwalimu alipokea nchi iliyokuwa inatumia 20% ya bajeti kwenye Elimu. Alianza kubomoa Elimu kwa matendo, na kwa kuinyima fedha, na kufikia wakati anaondoka madarakani, alishashusha bajeti ya Elimu hadi kufikia asilimia 4.9 tu ya bajeti yote.
Mwalimu aliua shule nzuri kama St. Francis (Pugu), St. Andrew's (Minaki), Miriam College (Kilakala), Assumption College (Weru Weru), etc. Baya zaidi ni kwamba alikataza kabisa kuanzishwa kwa shule nyingine kama hizo.
Mwalimu huyo huyo ndiye aliwafundisha akina Malecela, na CCM kwa ujumla, naman ya kuiba kura. Hilo bado linatutesa.
Labda Mwalimu alikuwa na nia nzuri, lakini ukweli ni kwamba aliturudisha nyuma sana. Si haki useme kazi nzuri za Mkapa ni kazi za Mwalimu.
Uuuhuuuu! but wajibu wa pili ni..
Hapana mkuu, kuna maendeleo makubwa sana mkuu, kama freedom of speech, umiliki wa mali binafsi, tatizo ni kwamba maendeleo haya hawakupata wengi kama ambavyo tungetaka, hasa wananchi wa hali ya chini, lakini mabadiliko yapo mengi sana mkuuu, hivi mkuu huoni kuwa siku hizi wananchi tunakula luninga?
nia yake ingekuwa ni njema kwa taifa, basi angeyasema mwenyewe aliyoyakosea, na aliyeyakosea ni yeye binafsi maana viongozi wengine walikuwa wanafuata upepo tu! Lakini hata siku moja hakusema alikosea wapi, ndio maan sasa tunahangaika tuu hatujui pa kugusa?
Mambo ya maazimio ya Arusha, yamepitwa sana mambo ya maadili ya viongozi yamepitwa sana tunatakiwa kuheshimu sheria za jamhuri sio maadili ya CCM
Maendeleo ya watu mbona yeye mwenyewe yalimshinda kuya-implemment tikaishia kula yanga tu, huku wakubwa na wenye nguvu wakila unga mweupe, angalau sasa hata wanyonge tunapata angalau harufu maana ni hela yako tu, watu walio huru aliwajenga wapi mbona kina Seif Bakari, Seif Hamadi, na Jumbe walipojaribu kuwa huru aliwafukuza? Can you imagine Zitto na Salaa wangekuwepo enzi zile za Mwalimu, saaa hizi wangekuwa wapi?
Haya ndio baadhi ya maandishi ya Mwalimu, ninayosema kila wakati yalikuwa mazuri kusoma tu, ila kwa sasa yamepitwa na wakati tena sana!
Yaaani mkulu wangu MMJ, unaaamini hii mikenge ya Mwalimu? Kama kweli aliwashirikisha kwenye maamuzi muhimu namna hii matatizo ya muafaka yanatokea wapi mkuu?
Ninasema Mwalimu, was great ametufanyia mambo mengi mazuri as a nation, lakini mawazo yake mengi sasa yamepitwa na wakati, ni wakati wa sisi wa-Tanzania kuamua wapi tunataka kwenda, lakini cha muhimu tuanze na kuheshimu sheria zetuza taifa, badala ya mambo ya katiba za chama.
Mkuu again heshima mbele, sasa CCM watajikaaanga mara ngapi? Maana kama hawakujikaaanga kwenye mafisadi na bado ndio kwanza wanashinda kiteto, basi hata wakuyaweka maandishi yote ya Mwalimu haitasaidia kitu, au?
I like this one mkuu, maana Kasori mtu wa karibu sana na Mwalimu, ndiye anaweza kujibu hili, jinsi Mwalimu alivyomzuia Lowassa kuwa rais, na nguvu za ajabu alizokuwa nazo Mwalimu, mpaka kumuita Kawawa mjinga, unasema huyu mtu alikuwa na nguvu za kawaida?
naomba unisaidie ni mambo gani ambayo yalimfanya Mwalimu kuwa "great"? na naomba unipe kiasi kidogo tu cha "mambo mengi mazuri" kwa Taifa ambayo Nyerere aliyafanya.
Halafu ni mawazo yake yepi "mengi yamepitwa na wakati"?