Serikali inakiuka Ibara ya 11(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wafungwa

Konseli Mkuu Andrew

JF-Expert Member
May 10, 2013
740
855
Salaam wakuu.

Ibara ya 11(2) ya Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, inatamka kama ifuatavyo;

"Kila mtu anayo haki ya kujielimisha, na kila raia
atakuwa huru kutafuta elimu katika fani anayopenda hadi kufikia
upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake"

Hali ni tofauti kwa wafungwa wanaotumikia vifungo katika magereza yetu hapa Tanzania, kwani hakuna fursa ya kutafuta elimu katika fani aipendayo hadi kufikia upeo wowote, inaonekana ukifungwa basi ndio unapoteza haki zote za kibanadamu kama vile kupiga kura katika chaguzi mbali mbali na haki ya kupata elimu.

Pia vipo vyuo hapa Tanzania ambavyo vipo chini ya usimamizi wa TCU ambavyo vina sheria ngumu kwa wanafunzi walikutwa na hatia na mahakama adhabu yao ni kufutiwa masomo.

Naishauri serikali sasa ianze kuwapa fursa wafungwa nao kupata haki ya kupata elimu katika viwango mbali mbali vya kielimu.Mfano unakuta mtu alikuwa yupo chuo kikuu mwaka wa nne na kwa bahati mbaya akifungwa kifungo hata cha miaka minne tuu , hapo ndio basi suala la shule linakuwa limeisha, kiasi kwamba akija kutoka anaanza upya na si wote wanaoweza kukabiliana na hali hiyo.

Pia kama ikiwapendeza naomba Ibara hii ya 11 iingine katika sehemu ya III ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inazungumzia Haki na Wajibu muhimu.

KUWA MFUNGWA KUSIMZUIE MTU KUPATA HAKI YA KIELIMU
 
kumptia fursa yakupata elimu ya ufundi stadi kunaweza msaidia anapo maliza kifungo chake kuja kujiajiri na kuajiri wengine na hatimae kupunguza uhalifu.
Kwanza magereza wangeweza kujiendesha kwa kufanya kazi zinazofanywa na TBA wao wangefanya, sahivi kuna ujenzi sijui wa bwawa na SGR wafungwa wangefanya hiyo kazi, magereza wangepata fedha na mfungwa angetoka na hela kidogo ya kuanzia maisha tofauti na sasa hata nauli sijui kama huwa wanapewa.
 
Hali ni tofauti kwa wafungwa wanaotumikia vifungo katika magereza yetu hapa Tanzania, kwani hakuna fursa ya kutafuta elimu katika fani aipendayo hadi kufikia upeo wowote, inaonekana ukifungwa basi ndio unapoteza haki zote za kibanadamu kama vile kupiga kura katika chaguzi mbali mbali na haki ya kupata elimu.
Kuna mfungwa alipata digri akiwa gerezani miaka ya 2007... kama sijakosea alisoma Laws OUT
 
Wafungwa wanatakiwa watumike katika kuendeleza na kukuza uchumi wa taifa letu. Yani ikiwezekana magereza ifanye kama vile JKT.

Wafungwa wazalishe bidhaa mbalimbali na waziuze kwa faida yao kwa kiasi na taasisi pia kwa kiasi kikubwa.


#NiMtazamo
 
Kuna mfungwa alipata digri akiwa gerezani miaka ya 2007... kama sijakosea alisoma Laws OUT
nataka kukupa ushaidi kuwa ni ngumu hapa Tanzania kujiendelezza kielimu ukiwa unatumikia kifungo.Mfano ByLaws za vyuo vingi mfano Mzumbe, na vyuo vingine vinatamka wazi wazi kuwa pingi mwanafunzi anaposhitakiwa katika kesi za jina basi atasimamishwa masomo na mahakama ikimkuta na hatia basi atafutiwa masomo yake.Huoni mfano huu wa sheria z vyuo vikuu vinawanyima wafungwa kujiendeleza?
 
Mbona kuna wafungwa waliopata digrii open university wakiwa magerezani.
nataka kukupa ushaidi kuwa ni ngumu hapa Tanzania kujiendelezza kielimu ukiwa unatumikia kifungo.Mfano ByLaws za vyuo vingi mfano Mzumbe, na vyuo vingine vinatamka wazi wazi kuwa pingi mwanafunzi anaposhitakiwa katika kesi za jina basi atasimamishwa masomo na mahakama ikimkuta na hatia basi atafutiwa masomo yake.Huoni mfano huu wa sheria z vyuo vikuu vinawanyima wafungwa kujiendeleza
 
Back
Top Bottom