Ianzishwe mikopo ya wahitimu na sharti la kuipata iwe vyeti na vitambulisho vyao

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
6,331
8,254
Vijana wanapenda kujiajiri ila wengi hawana mitaji anzisheni mikopo ya graduates ila kuipata mwaangalie vyeti tu na vitambulisho vyao ili wajiajiri wenyewe na kodi zitaongezeka.

Wazazi wamejinyima wamewasomesha watoto ili wapate ajira. Wazazi wengine hata nguo nzuri hawakununua, wala nyama na wali hawakula.

Walifanya kazi ngumu za kilimo cha jembe la mkono ili wapate fedha za ada. Lakini fedha zilizopatikana baada ya kuuza mazao yote hata laki 2 hazikufika. Wazazi wengine waliuza kila kitu nyumbani ili watoto wao waende shule.

Wazazi wengine walifanya kazi za hatari hata za kuuza gongo na pombe ili watoto wao waende shule.

Kiukweli mpaka mtoto anamaliza shule mzazi anakua amechoka haswa kiuchumi, kiafya na kiakili.

Sasa kama hali ndio hiyo mzazi anapata wapi nguvu ya kumsaidia mtoto wake kujiajiri.

Mngejitahidi kuwakopesha graduates mikopo, ukopaji uwe wa tofauti usiangalie kwamba mtu ana asset mwaangalie vyeti tu na vitambulisho vyao ili wajiajiri wenyewe na kodi zitaongezeka. Uzuri watafanya biashara na watalipa kodi.

Inakuaje bodaboda anakopeshwa alafu msomi hawezi kopeshwa? Inakuwaje mama ntilie anakopeshwa alafu msomi hawezi kopeshwa.

Kama kweli tunawapenda wasomi wenzetu na tunaumia kwasababu hawana ajira tutengeneze program ya kuwakopesha hao wasomi wote wanaohitimu vyuo wenye mawazo ya kufanya biashara.

Na mkopo huo utamke wazi mtu anayekopeshwa asiwe ameajiriwa.
 
Vijana wanapenda kujiajiri ila wengi hawana mitaji anzisheni mikopo ya graduates ila kuipata mwaangalie vyeti tu na vitambulisho vyao ili wajiajiri wenyewe na kodi zitaongezeka...
NAPENDA pia kutoa nyongeza vijana wapewe Elimu ya Kujitambua nadhani changamoto kubwa Ni kukosa Maarifa sahihi , mfano mtu yupo chuo simu yake imejaa namba za wanawake tupu.

Hata Mzazi akimtumia elfu kumi bado anajima kula ili aonge mademu watoto wa kike na wenyewe ndo vilevile wanawaza fashion na Maisha ya Tamthiliya hata Serikali wakiwapa mikopo Kama hawajitambui na hawana knowledge ni kazi bure tu

So Mimi naamini Elimu ya Kujitambua ndi kila kitu so tujikite katika Maarifa zaidi .

Kila Mtu akitimiza wajibu wake lazima tutapiga hatua trust me homie
 
NAPENDA pia kutoa nyongeza vijana wapewe Elimu ya Kujitambua nadhani changamoto kubwa Ni kukosa Maarifa sahihi , mfano mtu yupo chuo simu yake imejaa namba za wanawake tupu...
Umeharibu uzi, umeambiwa wenye mawazo. Mtu mwenye wazo la biashara hawezi kuwa hivyo ulivyo andika. Tuwe seriously, hii ni issue nyeti sana.
 
Nchi ya ovyo na ya kipumbavu kama hii usitegeme hili kutokea , nchi isiyovalue watu wenye elimu .

Ila kila mtu atapitia haya machungu na frustrations ambazo graduates wanapitia ,hata kama si yeye basi mtoto wake au ndugu yake wa karibu atapitia hilo tanuru la unemployment and lack of life's prospects ,tena Kwa economic stagnancy hii na overpopulation ilivyo nchi hii.

Hili suala linahitaji wide and deep implementation ya mitazamo mpaka sera na willing ya mabadiliko katika ngazi ya jamii mpaka serikali kuu .
 
Unajua ukiwa jobless kuna uwezekano mkubwa wa kumtupia kila MTU lawama kwa mambo ambayo hapo wazi kabisa,sasa kwa akili yako ni taasisi gani ya kifedha inaweza kutoa mikopo kwa guarantee ya cheti chako cha degree au form 4/6?

Hicho cheti chako cha karatasi kina thamani gani mpaka taasisi ya kifedha ikubali kama dhamana-unatumia akili kufikiri kweli?

Kama una wazo lako la kujiajiri au kufanya biashara kuna mikopo inatolewa na Serikalinza mitaa (Halmashauri) kwa Wanawawake,Vijana na walavu.tengenezeni kikundi cha watu 3-5 wasilisheni wazi lenu mtapewa fedha.

Acha akili mgando
 
Unajua ukiwa jobless kuna uwezekano mkubwa wa kumtupia kila MTU lawama kwa mambo ambayo hapo wazi kabisa,sasa kwa akili yako ni taasisi gani ya kifedha inaweza kutoa mikopo kwa guarantee ya cheti chako cha degree au form 4/6?

Hicho cheti chako cha karatasi kina thamani gani mpaka taasisi ya kifedha ikubali kama dhamana-unatumia akili kufikiri kweli?

Kama una wazo lako la kujiajiri au kufanya biashara kuna mikopo inatolewa na Serikalinza mitaa (Halmashauri) kwa Wanawawake,Vijana na walavu.tengenezeni kikundi cha watu 3-5 wasilisheni wazi lenu mtapewa fedha.

Acha akili mgando
Mimi ni mtetezi wa watanzania na wala sijamtupia mtu lawama.

Na huu uzi unamaana kubwa sana. Unawapa viongozi jambo la kufanya.

Kuwakopesha watu sio bure. You are investing your money, na baadaye unapata return na kodi.
Kukopesha watu sio adhabu it's a bussiness boss. Jitahidi sana kuficha hisia hasi tunapoweka mada za kuwashauri viongozi wetu.

Lakini si hivyo tu, sheria za ukopeshaji huwa zinatungwa na kubadilishwa. Mbona Kenya wanatoa mikopo bila dhamana yoyote, si wametunga tu sheria hapo.
 
Unajua ukiwa jobless kuna uwezekano mkubwa wa kumtupia kila MTU lawama kwa mambo ambayo hapo wazi kabisa,sasa kwa akili yako ni taasisi gani ya kifedha inaweza kutoa mikopo kwa guarantee ya cheti chako cha degree au form 4/6?

Hicho cheti chako cha karatasi kina thamani gani mpaka taasisi ya kifedha ikubali kama dhamana-unatumia akili kufikiri kweli?

Kama una wazo lako la kujiajiri au kufanya biashara kuna mikopo inatolewa na Serikalinza mitaa (Halmashauri) kwa Wanawawake,Vijana na walavu.tengenezeni kikundi cha watu 3-5 wasilisheni wazi lenu mtapewa fedha.

Acha akili mgando
The talk is cheap
 
Yahn pesa kwa makaratasi kwa jina la vyeti sasa usiporudsha mkopo makaratasi(vyeti) yatawasaidia nn
 
Kuna haja ya kuwawezesha vijana kupata Cha kufanya,ndani na nje ya nchi,Cha kwanza,inabidi mfumo wa uchumi ubadilishwe,sio huu ambao serikali inashika na kutawala njia za uchumi,tuwe na uwezo wa kuwa na wafanyabiashara kama Elon musk,ambao wanakuwa na uwezo mkubwa hata kuweza,kuibishia serikali(sio nchi),
Hapa kwetu ukiwa mbabe wa kiuchumi(kama alivyokuwa Mo),unatekwa!!
Inabidi nchi ibadilishe sera,tuvutie makampuni makubwa,kama google,Facebook,Tesla,wawekeze kwetu,
Mikopo ya Elimu ya juu,ifutwe kwa kozi za IT,computer,Hawa vijana waperekwe nje,wapige kazi,wapate uzoefu,waje nyumbani wawekeze,vijana walianzisha makampuni,wawezeshwe kupata tender hata nje ya mipaka
 
Elimu ya hivyo vyeti ingekuwa ni Elimu kweli kweli yenye kumsaidia mtu kukabiliana na changamoto za kujiajiri. Lakini ukiangalia kwa kina hiyo elimu waliyonayo graduates ni ya kuajiriwa. Sasa elimu ya kuajiriwa itakuwaje collateral ya kumdhamini mtu kupewa pesa??

Hili suala siyo la kukimbilia....graduates wengi wapo after job hunting na siyo self employment.
 
Mikopo sio tatizo je wanaelimu juu ya uzalishaji mali? Zaidi ya kuwaza ngono Hakuna cha ziada wanajua
 
Back
Top Bottom