Kuwa mnyenyekevu siyo kuwa mnyonge. Kuwa mnyenyekevu maana yake ni kumheshimu mwenzako, kuheshimu mawazo yake, kuappreciate mawazo au jambo lake fulani, kumpa nafasi ya kutenda jambo, kama wewe umekosea kukubali kukosolewa, kama mwenzako ana pointi katika majadiliano yenu kukubali kwamba hoja zake zilikuwa nzito kuliko zako na kuchukua mwelekeo wa hoja zake, kutoakujikweza sana katika mambo fulani fulani, kama yeye kakosea basi umsahihishe kwa upole na mapendo bila kumng'akia na kumwonesha dharau. Wewe ukiwa na karama fulani au elimu au ujuzi fulani usijigambe au kuuringia kana kwamba ni wewe tu duniani. Hizo kwa kifupi ndio viashiria vya unyenyekevu.Pengine unisaidie zaidi hivi mwanamke kuwa mnyenyekevu ndo anatakiwa kuwaje. Na je hivi ukikuta pengine mwenzio alikuwa anakuambia pengine ana company then ukaja kufind out ni uongo unatakiwa u act vipi.
Swali lako la pili la company, samahani nimeshindwa kulielewa. Labda ulifafanue kwa uwazi zaidi. Pole sana.