I seems to be boring

I seems to be boring

Hello my dears Wana JF,
Napenda kuelimika katika hili swala, na hisi kuwa huwa na bore hubby kutokana sijui ni mazoea au sijui cha kuongea naye! Nifanye nini ili nisiwe na mbore, maana mimi nadhani nimkimya sana inaweza kupita masaa manne hatujaongea kitu, na sipendi kuongea pumba nikaonekana wa kuja. Msaada tafadhalini wandugu

  • ...akiongea usimkatishe...
  • ...akiongea msikilize (hata kama humwelewi/unaboreka)...
  • ...akiongea usimdharau...
  • ...akikuuliza mjibu vizuri, kama huna jibu mwambie utamjibu baadae..
  • ...akikusemesha itikia...nk
ukishajifunza hayo, itakuwa rahisi kwako kuongea kwa ufanisi...
 
Hi Mrs Mtaba.. Huyo mumeo yupo hivyo tangu mkiwa wachumba, mkaoana au ni tabia mpya ameianzisha? kama yuko hivyo basi ni tabia yake na tabia haina dawa try to understand him..lkn kama ni tabia mpya...kuna kitu hapo...
 
Jamani Mrs Mtaba nakumbuka kama kuna thread umewahi ileta hapa hapa kwenye ukurasa huu mwenye data jamani naomba mnikumbushe ili twendelee kumelimisha mwenzetu.
 
MRS MBATA!
BE WHAT YOU ARE BWANA!
halafu hebu tuwasiliane,huyo mumeo ni mtu wa nyumbani kabisa!wakina MBATA wamesettle maeneo fulani ya ikelu,lyamkena na kiumba!hawa watu hawana matatizo.jaribu kuni pm
 
Ndugu, yawezekana kuna sababu za hilo gap kati yako na mwenzio, anyway, nadhani haina maana sana kujua chanzo cha uhusiano wenu kwa sasa, lakini cha muhimu naamini mume wako au mke wako ndo mshikaji wako wa karibu saaaaana, ndo wa kucheka naye ukaonyesha jino la 33, kwa hiyo jiachie. Usione aibu kuchekwa ushamba au lolote, ni bora mara mia akucheke yeye kuliko watu baki, maana yeye atakurekebisha na maisha yatasonga mbele. Changamka! Kuwa wewe kama wewe na na sio kujifunza mapenzi ya kuiga! Kwani ukimpa huduma nzuri, msosi safi, malazi safi, heshima kwa kwenda mbele, what else....?
 
Hello my dears Wana JF,
Napenda kuelimika katika hili swala, na hisi kuwa huwa na bore hubby kutokana sijui ni mazoea au sijui cha kuongea naye! Nifanye nini ili nisiwe na mbore, maana mimi nadhani nimkimya sana inaweza kupita masaa manne hatujaongea kitu, na sipendi kuongea pumba nikaonekana wa kuja. Msaada tafadhalini wandugu

Mwenye tatizo ni wewe. Unajificha, hutaki kujionesha ulivyo. Unaonesha picha isiyo yako. Kumbe please, jitahidi kuwa mkweli, muwazi. Huna sababu ya kumwonea aibu mumeo. Unapaswa kuwa huru, kuwa "uchi" kwa kila jambo kwake. watu wa ndoa hawapaswa kuoneana aibu au kuogopana kwa chochote. Ni afadhali akujue udhaifu wako ndivyo anavyoweza kukusaidia. Katika maisha ya ndoa hakuna kitu "kuongea pumba". Yote yana maana kwa mahusiano. Kile unachofikiri ni pumba kumbe ndicho jamaa anachopenda kukisia. Kumbe usimpigie calculation katika mahusiano. Na pengine yeye naye anakuwa mkimya kwa sababu anaona unampigia mahesabu. Please be free! utaona maisha yenu yatabadilika. Huenda na jamaa akachangamka akaanza kuwa toafuti. Kumbuka nyie ni mume na mke. You share averything.
 
Hello my dears Wana JF,
Napenda kuelimika katika hili swala, na hisi kuwa huwa na bore hubby kutokana sijui ni mazoea au sijui cha kuongea naye! Nifanye nini ili nisiwe na mbore, maana mimi nadhani nimkimya sana inaweza kupita masaa manne hatujaongea kitu, na sipendi kuongea pumba nikaonekana wa kuja. Msaada tafadhalini wandugu

haki ya Mungu utaachwa! We ongea tu hata kama ni pumba. Laiti ungejua yanayozungumzwa na wapenzi wakiwa faragha
 
haki ya Mungu utaachwa! We ongea tu hata kama ni pumba. Laiti ungejua yanayozungumzwa na wapenzi wakiwa faragha

Mazee maisha sio faragha peke yake. Mdau hajasema kwamba anakosa la kuongea huko faragha (labda kama nahitaji ku-elaboreti), yeye kama nimempata anasema Mr. Right wake haoneshi kumuapreshiet anachoongea, yaani ndo kama vile yaani aaargh pumba flani ivi anaona anampotezea stimu..Sijui kama umenipata. Hiyo ni dalili mbaya sana kwa mawazo yangu.
 
Hili ndilo jibu nililotarajia...maana kibinadamu this is too much wajameni.

Duh..mama pole sana. Ndio hivo tena kubali matokeo na angalia ustaarabu mwingine hata kama sio kwa kuvunja ndoa au kukidhi haja za kingono, kuna vitu vingi vimeumbwa kumfurahisha binadamu..kuna marafiki, misosi fresh, vinywaji, kusafiri dunia, watoto kama unao etc vikazanie hivyo, sio kila ndoa itakuwa ideal..accept and move on.
 
Hili ndilo jibu nililotarajia...maana kibinadamu this is too much wajameni.

Pole sana dada, inaonyesha umekata sana tamaa, usikate tamaa kiasi hicho ni dhambi , bado una nafasi,
Kwanza mlikaa muda gani mpaka mkaamua kuoana?
Na kipindi cha uchumba alikuwa na tabia hizohizo?
na kama alikuwa na tabia hizo kwa nini ulikubali kuolewa naye? au ndo ulijua mkiingia nadania atabadilika
nijibu then nitakushauri.
 
Mazee maisha sio faragha peke yake. Mdau hajasema kwamba anakosa la kuongea huko faragha (labda kama nahitaji ku-elaboreti), yeye kama nimempata anasema Mr. Right wake haoneshi kumuapreshiet anachoongea, yaani ndo kama vile yaani aaargh pumba flani ivi anaona anampotezea stimu..Sijui kama umenipata. Hiyo ni dalili mbaya sana kwa mawazo yangu.
Exactly! yani ndugu yangu wewe umenipata na umenielewa vizuri sana katika hili swala...ni kweli kabisa niyaongeyao yanaonekana pumba kwake. Sio kwamba mimi sio muongeaji, tena ni mpiga soga ile mbaya.
 
Duh..mama pole sana. Ndio hivo tena kubali matokeo na angalia ustaarabu mwingine hata kama sio kwa kuvunja ndoa au kukidhi haja za kingono, kuna vitu vingi vimeumbwa kumfurahisha binadamu..kuna marafiki, misosi fresh, vinywaji, kusafiri dunia, watoto kama unao etc vikazanie hivyo, sio kila ndoa itakuwa ideal..accept and move on.
Yani asante sana kwa ushauri wako mzuri kaka, alafu nikimgusia hicho kipengela hapo juu, basi hata kama alikuwa hana pesa atakopa tuu ili uondoke, yani naona hujiskia fresh sana.
 
Yani asante sana kwa ushauri wako mzuri kaka, alafu nikimgusia hicho kipengela hapo juu, basi hata kama alikuwa hana pesa atakopa tuu ili uondoke, yani naona hujiskia fresh sana.

yaani anapenda wewe usafiri?
Ina maana hapendi uwepo wako? una uhakika anakupenda kweli? na kama una uhakika na hilo, kuna vitu gani anakufanyia mpaka unajua kweli ananipenda ukiacha hilo la kunyamaza, lazima kuna tatizo labda mapenzi yamepungua,
sijui embu jibu maswali yangu nikuambie zaidi.
 
Yani asante sana kwa ushauri wako mzuri kaka, alafu nikimgusia hicho kipengela hapo juu, basi hata kama alikuwa hana pesa atakopa tuu ili uondoke, yani naona hujiskia fresh sana.

Yawezekana unaongea mno kupita kiasi, na pengine unajifanya mwalimu wa kumfundisha kila jambo. Yaani unaonekana unajua kila kitu mbele yake. Wanaume wengine hawapendi wanawake wanajifanya kujua kila kitu au wanaozungumza mno kupita kiasi, kwani - mawazo yao - unatishia uanaume wao. Tena ona wewe mwenyewe unasema huwahupendi kuongea pumba. Kumbe kwa kila unachoongea unakuwa umekitafakari sana kiasi kwamba utakapoongea iwe point nzito mbele ya mumeo. Kumbe kama mlikuwa kwenye kujadili jambo ungependa point yako ipite. You are not cheap! Hiyo si nzuri mama. Jaribu kuwa mnyenyekevu. UKubali kukosolewa pia na kufundishwa na mwenzako. Kumbe mwenzako anakuona kero, na anaona akae kimya na kukushiti kana kwamba hujaongea kitu hata kama umeongea cha maana. Anataka kukuonesha kwamba wewe pengine si kitu sana kama unavyofikiri. Ukiomba likizo anakupa mara moja ili aondokane na "profesa" ndani ya nyumba. Nasema hivi nataka kusoma mawazo yenu. naweza nikawa nje, lakini yaweza kuwa sababu. Tafakari bila kujihurumia.
 
No Way!!! the strongest ever is the female of the species...
women are strong and not weak!!! gosh by golly wow!! you got it all wrong.
women are weak....period
Biblia na kuran tukufu vinaeleza kinaga ubaga......wanawake ni watu wa kukaa nyumbani kusaidia kazi ndogo ndogo za home.....hii ya siku hizi kupewa ubunge wa bure ni kinyujme na mafundisho ya Mwenyezi Mungu......

....najua lazima usema women are not weak....huko kwenu mnapigwa sana nasikia mnalalamika siku hizi.....ngoja tutawakodishia two kuryazi
 
Yawezekana unaongea mno kupita kiasi, na pengine unajifanya mwalimu wa kumfundisha kila jambo. Yaani unaonekana unajua kila kitu mbele yake. Wanaume wengine hawapendi wanawake wanajifanya kujua kila kitu au wanaozungumza mno kupita kiasi, kwani - mawazo yao - unatishia uanaume wao. Tena ona wewe mwenyewe unasema huwahupendi kuongea pumba. Kumbe kwa kila unachoongea unakuwa umekitafakari sana kiasi kwamba utakapoongea iwe point nzito mbele ya mumeo. Kumbe kama mlikuwa kwenye kujadili jambo ungependa point yako ipite. You are not cheap! Hiyo si nzuri mama. Jaribu kuwa mnyenyekevu. UKubali kukosolewa pia na kufundishwa na mwenzako. Kumbe mwenzako anakuona kero, na anaona akae kimya na kukushiti kana kwamba hujaongea kitu hata kama umeongea cha maana. Anataka kukuonesha kwamba wewe pengine si kitu sana kama unavyofikiri. Ukiomba likizo anakupa mara moja ili aondokane na "profesa" ndani ya nyumba. Nasema hivi nataka kusoma mawazo yenu. naweza nikawa nje, lakini yaweza kuwa sababu. Tafakari bila kujihurumia.
Pengine unisaidie zaidi hivi mwanamke kuwa mnyenyekevu ndo anatakiwa kuwaje. Na je hivi ukikuta pengine mwenzio alikuwa anakuambia pengine ana company then ukaja kufind out ni uongo unatakiwa u act vipi.
 
haki ya Mungu utaachwa! We ongea tu hata kama ni pumba. Laiti ungejua yanayozungumzwa na wapenzi wakiwa faragha

Huwezi kosa la kuongea nampenzi wako, hata ukimwambia neno nakupenda mara mia mia kidogo!, halafu penda kumsifia always na kumpongeza kwa anayo yafanya na kumtia moyo kwa anayo tegemea ama endelea kuyafanya

La mwisho ujue kwa mpenzi wako ndo pa kuongea pumba zako zoooote maishani! For your information pointi tupu kwenye mapenzi ni kuboa, kwani mtu anakuwa anatamani kuipumzisha akili yake na smart things, wewe unangangana na kurudisha smartness all the time!

so jimwage kwa kwenda mbele kwako ndo pumziko la mpenzi wako.. na utashangaa atakavo zifurahia hizo pumba zako! All the best.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom