The Boss
JF-Expert Member
- Aug 18, 2009
- 49,320
- 117,611
Ebana eeeh hiyo ni kweli kabisa.
Nakumbuka kuna watu walikuwaga wanaenda Zaire kununua viatu na kuja kuviuza Dar.
Basi wengine tulikuwa tunaona Zaire imeendelea sana.
Mi nakumbuka kuna mjomba'angu mmoja hivi mjeda...aliendaga Msumbiji akarudi na nyanya za kwenye kopo [tomato paste] na corned beef za huko.
Basi nilikuwa naona jamaa wameendelea sana hadi wanatengeneza nyanya za kopo.
Hahahaa ujinga kitu kibaya sana.
Manake kigezo cha maendeleo tulichokuwa tunakitumia ni cha vitu na si watu.
Wakati maendeleo ya kweli ni ya watu na si vitu.
Na watu wakitoka Nairobi tunaenda kuwasalimia ha ha haa
haki ya Mungu hii nchi ilikuwa burudani...
Mtu akienda Ulaya ukoo wote mnaenda airport kumuaga...
Halafu kuna maeneo kupiga picha mnakamatwa na polisi....ha haa