I miss those days

I miss those days

I miss those days when we could actually tell the difference between 's' and 'x'. The days you could tell men from women, kids from grown-ups, OG from China-made.

Them amazing days when nothing was amaizing. Them days when a random beautiful mama would reply to your PM and what not. Them days when people could tell sarcasm. Oh! How I miss those days.
 
Tutake radhi ma engineer aisee ,ila hapo kwenye Khanga umenikumbusha mbali kinoma noma mana kademu kangu ka kwanza enzi hizo kalikuwa kanapenda kutupia hilo vazi la khanga nilikuwa sipati taabu kwenye kuiba muda
 
I Miss those days sikukuu usipovaa spesho hujatoka bado


I miss those days za kucheza kombolela sio noq m play station tu


I miss those days mtihani wa taifa ni taifa kweli ukimaliza la saba wapewa hongera mtaa na ndugu wote

I miss those days watu waliokuwa wananitongoza nilikuwa nawasemea kwa mama but now nakaushia tu au tunamalizana kiutuuzima lol
 
Dah.,i miss those days naangalia video za Hayati Mzee Rochereau na M'bilia Bel nadhania Congo booooonge moja la nchi!!...,kumbe wameshutia Paris!
Dah!
 
Habari za usiku huu,
Bila ya kuwa nafungana na upande wowote wa siasa ntawasalimu tena kwa mara ya pili. Na wapendwa.
BTT; I miss those days ambazo nilikuwa na fall au namzimikia au namdondokea au nampenda mkaka kwa kuangalia handwriting yake tuu. (Hapa wale wanao andika vibaya aka madaktari na engineers mtanisamehe maana ilikuwa ngumu kuwakubali khaa miandiko mibaya kama bata kapita hehee ...
Nilikuwa nikipata barua ya mtu niliyempenda kwa mwandiko wallah ntachana karatasi zote ila si barua yake.

I miss those days ukipata barua shurti unasubiria kuisoma usiku, yaani unamaliza kazi zote unaoga unapaka marashi kisha unapanda kitandani na kuanza kuisoma taratibu hadi maneno yanakaa moyoni.

I miss those days mdada ukienda gengeni umevaa gauni ndani na khanga ya kiunoni kwa juu wakaka wa mtaani utasikia psii psii hata kama huvutii utasikia psii psii ukirudi nyumbani lazima ujiangalie kwenye kioo na kuniambia kumbe nalipa eeh kumbe hamna lolote, maringo yanaanza sasa hapo kwa mschana.

I miss those days mschana huwezi fanya kazi nzito mbele ya mvulana. Utasikia subiri kwanza ngoja nikuoneshe basi utabebewa dumu la maji hadi karibu na nyumbani. Ilikuwa raha sana.

I miss those days kukiwa na timu ya mpira ya vijana wa mtaani halafu kuna mkaka unayempenda ameumizwa na wenzie katikati ya mechi unakosaje rahaa utasikia jamani msiniumizie.....

I miss those days magauni ya chirmen linavaliwa jumapili kanisani mguuni una utankoma saa nane hahahahahaa.

Now days vijana hawana art love hasa ya mwandiko maana ni full touch screen na ku type. Kama ni kazi mschana utapiga kazi hadi utoke kigimbi hakuna hata wa kukusaidia hata kama wapo wakaka 10 mbele yako.

I just miss those days......
Kasie aka ajuza bin kibibi.

Usikuuu mweeemaa.

Una umri mdogo lakini ni dhahiri umeanza ufigisu muda mrefu sana!
 
I Miss those days sikukuu usipovaa spesho hujatoka bado


I miss those days za kucheza kombolela sio noq m play station tu


I miss those days mtihani wa taifa ni taifa kweli ukimaliza la saba wapewa hongera mtaa na ndugu wote

I miss those days watu waliokuwa wananitongoza nilikuwa nawasemea kwa mama but now nakaushia tu au tunamalizana kiutuuzima lol


Mama yako angejua unavyomaliza kitu uzima akikumbuka ulivyo kuwa unamsumbua
angebaki mdomo wazi
 
Mama yako angejua unavyomaliza kitu uzima akikumbuka ulivyo kuwa unamsumbua
angebaki mdomo wazi
kuna umri ulifika nikajitambua kutongozwa nikawaida kwa binti ikawa nikajifunza alone mbinu za kuwakwepa mpaka nilipoanza dating
 
I miss wali wa zamani ulikuwa na kaharufu kazuri sana , lazima tuoge mapema sana siku hiyo .
I miss those days marehemu baba akija usiku katupia vitu vyake anaweka cassete ya kanda bongoman anatushindanisha kukata mauno watoto wote mshindi anapewa sh.20 mara nyingi nilishinda
 
I miss those days hakukuwa na kipindupindu na tulikuwa tunakula maji ya bombani, kila mwezi wanapita watu wa city kufanya fumigation kuua mazalia ya wadudu waletao magonjwa.
 
Umeona eej

Cc lara 1

I miss those days hapakuwa na wapambe. .. .. .

I miss those days ukumbi wa harusi unapambwa kwa toilet papers za pink na light blue.
 
Last edited by a moderator:
I miss wali wa zamani ulikuwa na kaharufu kazuri sana , lazima tuoge mapema sana siku hiyo .
I miss those days marehemu baba akija usiku katupia vitu vyake anaweka cassete ya kanda bongoman anatushindanisha kukata mauno watoto wote mshindi anapewa sh.20 mara nyingi nilishinda

Hehee kumbe baba yako alikugeuza Joyce wowowo?
 
Dah.,i miss those days naangalia video za Hayati Mzee Rochereau na M'bilia Bel nadhania Congo booooonge moja la nchi!!...,kumbe wameshutia Paris!
Dah!

Zamani Watanzania kila nchi tulijua imetupita kimaendeleo
watu walikuwa wanazamia hata Mozambique ...
 
Una umri mdogo lakini ni dhahiri umeanza ufigisu muda mrefu sana!

I miss those days huanzi darasa la kwanza hadi mkono wako upite juu ya kichwa na kushika sikio la upande mwingine.
 
Ha hahahahahaaaa looh

Mimi huwa namiss simu za kukoroga na zenye kufuli
na kabati la tv pia lina kufuli...au tv kukaa chumbani kwa wazazi
hadi wakague madaftari ndo waitoe sebuleni
 
I miss those days bibi harusi anatembea kwa miguu toka nyumbani kwao to Church na from church to husband's home.
I miss those days bibi harusi anakula keki na kushushia na chai ya moto.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom