I miss those days

I miss those days

Kwani jamani kitufe cha like kiko wapi? Nataka nitoe like
 
I miss wali wa zamani ulikuwa na kaharufu kazuri sana , lazima tuoge mapema sana siku hiyo .
I miss those days marehemu baba akija usiku katupia vitu vyake anaweka cassete ya kanda bongoman anatushindanisha kukata mauno watoto wote mshindi anapewa sh.20 mara nyingi nilishinda

Baba yenu alikuwa tajiri sana...Sh.20 ilikuwa ada ya primary school kwa mwaka mzima!
 
enzi za kusoma madeni China badala ya made in China

ubaguzi wa rangi wa Afrika kusini ulinipa shida kuelewa maana yake mimi nilijua wanabagua rangi za ukutani nikawa najiuliza hizo rangi za ukutani wanabaguaje na kwanini wanazibagua.
 
Those days t.v tunaangalia kwa jirani halafu tunaambiwa tukae chini tutamvurugia makochi.Kesi ya double dragon na the flingstones.Kumiliki kideo ilikuwa ishu mtaani.Enzi hizo Tabata full mikorosho na miembe daladala kupanda mpaka tabata relini.
 
Hahaaa enzi za Bruce Lee, Commando John, Michael (Ddcorf) wa kwenye American ninja, govindra, Ashantii yaani I miss those days looh
you really touched my heart, i miss them too, luckly i married the girl from those days, kasoma hii message kalia
 
Zamani Watanzania kila nchi tulijua imetupita kimaendeleo
watu walikuwa wanazamia hata Mozambique ...

The boss umeua ilikuwa hatari kila mishen town anataka kuzamia ilikuwa mtu akiwa amerudi toka south africa mtaani mzima unamshangaa
 
I Miss those days sikukuu usipovaa spesho hujatoka bado


I miss those days za kucheza kombolela sio noq m play station tu


I miss those days mtihani wa taifa ni taifa kweli ukimaliza la saba wapewa hongera mtaa na ndugu wote

I miss those days watu waliokuwa wananitongoza nilikuwa nawasemea kwa mama but now nakaushia tu au tunamalizana kiutuuzima lol

sirius nikikutongoza utakaushia hutamwambia hata rafiki yako?
 
Dah nimekumbuka mashati ya yekeyeke....
 
Na kurudi nyumbani kusikiliza mchezo wa mzee jangala...

ahhh...enzi hairudi! kina mzee Mundu,pwagu na pwaguzi!...halafu kipindi kingine kile cha RAHA LEO SHOW, Mama na Mwana na Bi Debora mwenda hapo hadithi za binti chura,ua jekundu daaah nilikuwa sing'oki kwenye radio ya NATIONAL (ya mbao) ya mzee wangu
 
I Miss those days sikukuu usipovaa spesho hujatoka bado


I miss those days za kucheza kombolela sio noq m play station tu


I miss those days mtihani wa taifa ni taifa kweli ukimaliza la saba wapewa hongera mtaa na ndugu wote

I miss those days watu waliokuwa wananitongoza nilikuwa nawasemea kwa mama but now nakaushia tu au tunamalizana kiutuuzima lol

tena basi ufaulu.....tena ufaulu shule ya bweni nje ya mkoa...daaah! yani ukitembea mtaani unajiona kama unaelea angani. tulipata heshima haswa...leo masikini,wanaofaulu hawajui hata kusoma
 
Mimi huwa namiss simu za kukoroga na zenye kufuli
na kabati la tv pia lina kufuli...au tv kukaa chumbani kwa wazazi
hadi wakague madaftari ndo waitoe sebuleni

umenikumbusha zamani simu mpaka ipite kwa operator,waweza ukapiga weeeee unasubiri uunganishwe na operator. operator aliweza kusikiliza kila mnachoongea.
kulikuwa pia na simu zile za reverse call(tuliziita RIVASKOO).Unapiga kwa operator kisha yeye anakuunganisha na simu unayotaka kupiga kisha makato yanakuwa sio kwako ila kule ulikopiga...hii ilikuwa maarufu sana kwa wanafunzi wa sekondari wa shule za bweni.....
Ahhh...enzi za benki ya posta na vile vitabu vya posta haha utadhani pasipoti ya kusafiria.
 
Unasingizia unaumwa usiende sunday school ili uangalie tamthilia ya shavo...
 
I miss those days tunacheza mziki wa Funk na Pop, mtu una slide kutoka mwanzo wa ukumbi mpaka mwisho.

I miss those days ukitaka kucheza muziki na msichana unaenda kuchagua kwa kuinama kidogo.
 
Yaani Enzo za kuvaa vitop, sketi za charanga nazikumbuka sana na pensi nyanya je unazikumbuka? Hahahahahaaa

Ha haa hapo kwenye pensi nyanya...
Umenikumbusha mbali mno
 
Mimi huwa namiss simu za kukoroga na zenye kufuli
na kabati la tv pia lina kufuli...au tv kukaa chumbani kwa wazazi
hadi wakague madaftari ndo waitoe sebuleni
Hahahahaaa The Boss you know where we have our lunch lunch and you know where to find me looh.

Umenichekesha na kunifurahisha sana. Let me say this... Hii ni experience ya kwetu......
Mshua wangu alienda nje ya Tanzania miaka hiyo kikazi na aliporudi Tz moja ya vitu alivyorudinavyo ni TV ambayo kwa miaka hiyo ilikuwa ni asset kubwa. Kuangalia TV ilikuwa ni ijumaa jioni jumamosi kuanzia mchana na jumapili kuanzia mchana hadi jioni kisha inarudishwa chumbani kwa baba na mama na inalala huko. Operators wa TV na deck walikuwa kaka zangu very sharp. Sasa itokee mmeiba kuangalia TV katikati ya wiki halafu itokee umeme ukatike na mkanda umekwamia kwenye deck, na mkanda wenyewe wa kuazima......nakwambia kila mtu anaanza kusali ili umeme urudi kabla hamjabambwa maana mtapitishiwa kipondo woote. Hahahaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom