I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

naona una kazi sana kumuelewa mwanakijiji

ulalamishi wa raia wa kawaida , wewe au mimini tofauti na mbunge yeyote yule

Mbunge anaweza

kuandaa mswaada na akaupeleka bungeni na ukajadiliwa na mawazo yatakayotoka pale itakuwa ni bunge limeamua
tangu mwaka jana hakuna jitihanda zozote zilizofanywa na mtu yeyote za kuifanya TBC ionyeshe matangazo! mbunge anatakiwa atumie nguvu lakini sio kulalamika kana kwamba ni HAKI wakati haijaandikwa mahali popote na mwenye nguvu ya kufanya iandikwe mahali ni huyo mlaamikaji!!

Mbowe na timu yake wanalalamika sawa kabisa na kapuku fulani mzururaji barabarani ja hakuna namna ya kisheria ku isukuma serikali ionyeshe?

Lakini pili, hakuna mbunge anayewza bunge kuwa na TV yake au na bajeti yake ili watafute chombo kingine cha habati mbali ya TBC na waonyeshe matangazo?? kumbuka kuna ulalamishi wa mhimili mmoja kuingilia mwingine

hauoni TBC kama chombo cha serikali kinashinikizwa na bunge na huu ni muhingiliano wa mihimili?

Neleze , niambie , kama umewahi kusikia, au kama limewahi kufanyika, je matangazo ya bunge kwa siku ni sh ngapi? na je bunge haliwezi kulipa? na kama hela haipo kuna jambo limefanyika kuipata hiyo hela??

nimewaza kama kwenye akili timamu zaidi ya wabunge wote wanaolalamika Bunge kutoonyeshwa live ambao wako CDM na CCM

umeelewa au ninatwanga maji kwenye kinu
Yaani....pamoja na ZITTO kumiliki chama lkn bado mnavinyongo na MBOWE unataka kutuambia mpinzani wa NCHI hii MBOWE peke yake?....ww kama mwananchi wakawaida umelidhika na kulishwa viporo vya mijadala ya Bunge?,,,,ikiwa hujalidhika kama Mwananch wa kawaida umesaidiaje ...kilipush jambo hili au nyie mpo kusubiri jamaa zenu wa Chadema watakosea wapi mjifanye wataalamu wa uchambuzi wa SIASA za Upinzani tz acheni haya Mambo Nchi hii niyetu sote Lazima tushirikiane kuijenga Visasi vya Siasa havisaidii
 
Ogopa kitu kinaitwa Internet&Servers. Ukitupia vitu humo ndani, kama huna access ya ku-delete na ku-demagnetise hiyo serving devise, basi iko siku uliyoyandika au ku-upload yatakurudi. Hili liwe somo na kwa wengine!

Kweli kabisa kaduguda; baada ya kaburi kufukuliwa nimemkuta ndugu yangu MMK wa 2013 akiwa hai. Lakini huyu MMK wa sasa wa kuanzia October 2015 mpaka leo siyo mwenyewe! wataalam wa uchawi watamtafutia jina lake nimepata tabu Sana!!!
 
MM akitumia kichwa kufikiri enzi hizo

Nadhani watu mnapata shida; kwa sababu labda kusoma ni kugumu au kuelewa ni kugumu. Hakuna ubaya wowote wa TV kuoneshwa "live". Sijawahi kusema "ni vibaya kuonesha TV" au ni "haipaswi watu kuona kinachoendelea Bungeni". Sababu iliyotolewa wakati ule ilikuwa ni sababu ya kipuuzi kutaka kuzuia kurusha TV "live", sababu iliyotolewa sasa hivi siyo ya wakati ule - sidhani kama watu wanaona tofauti. Lakini zaidi labda inabidi niendeleee kuwaelimisha wengine. Wanaodai hadi kususa waonekane kwenye TV wanazungumzia suala la haki yao kuonwa au kurusha matangazo live. Hii haki haipo.

Nadhani ipo haja ya kuchukua hatua ya lazima ya kuufunga huu mjadala tena.
 
Nadhani watu mnapata shida; kwa sababu labda kusoma ni kugumu au kuelewa ni kugumu. Hakuna ubaya wowote wa TV kuoneshwa "live". Sijawahi kusema "ni vibaya kuonesha TV" au ni "haipaswi watu kuona kinachoendelea Bungeni". Sababu iliyotolewa wakati ule ilikuwa ni sababu ya kipuuzi kutaka kuzuia kurusha TV "live", sababu iliyotolewa sasa hivi siyo ya wakati ule - sidhani kama watu wanaona tofauti. Lakini zaidi labda inabidi niendeleee kuwaelimisha wengine. Wanaodai hadi kususa waonekane kwenye TV wanazungumzia suala la haki yao kuonwa au kurusha matangazo live. Hii haki haipo.

Nadhani ipo haja ya kuchukua hatua ya lazima ya kuufunga huu mjadala tena.
Sababu iliyotolewa kipindi kile ni ipi na ya sasa hiyo "nzuri" ni ipi??


sidhani kama wabunge wanang'ang'ania "haki ya kuonekana kwenye Tv" bali "wananchi kupata habari"
 
Naona wengi humu ama mmeingia JF juzi ama mmeanza kusoma makala zinazoikosoa serikali majuzi tu. Tulioanza zamani tuligundua toka awali kabisa kwamba adui wa taifa hili ni CCM na wakati huo CCM haikuwa na mtu wa kumtupia lawama kwa sababu CCM ndio ilikuwa kila kitu...bunge, polisi, jeshi, mahakama n.k. Popote pale tulipojikuta, tulifikishwa na CCM pamoja na serikali yake, hawakuwepo wa kutupiwa lawama zaidi yao.

Tulipoanza kudai mfumo wa vyama vingi, kwa shinikizo kutoka ndani na nje, CCM kwa shingo upande ililazimika kuridhia lakini kwa masharti ambayo hayakuwekwa wazi. Baada ya kuona hatari iliyoletwa na mfumo huo, wajanja ndani ya CCM walikaa kitako na kutafakari ni vipi wataendelea kuaminiwa na wananchi. Kitu kimoja walichokiridhia ni kwamba sasa angalau wamepatikana alternatives wa kuwatupia lawama mambo yakienda kombo,upinzani.

Lakini hapo napo walikwaa kisiki, kwa hayati Mwalimu Julis Kambarage Nyerere, mwanzilishi, national icon, Baba wa Taifa na mwanachama namba moja wa Chama cha Mapinduzi. Mwalimu alikuwa kama LUKU kwa CCM na wengi waliotaka kwenda nje ya mstari hakuwamezea maneno, aliwapa kavu kavu. Alichosahau Mwalimu ni kwamba he had created a monster, a monster that would stop at nothing to get what it wanted at whatever cost.

Thus Mwalimu became the first victim of a product of his own creation, a monster out of control! Mwalimu aliwapiga stop Lowassa na Kikwete mara tu baada ya mfumo mpya wa vyama vingi...alikuwa ana sababu zake, alijua jinsi mizizi ya CCM ilivyojikita katika kila nyanja. Nia yake kubwa ilikuwa ni namna ya kukipunguzia nguvu hili zimwi kwa sababu alijua kwa nguvu ilizo nazo, CCM isingeweza kuachia madaraka hivi hivi kirahisi.

Alikuwa anatafuta namna na kulidhoofisha hili zimwi hadi kufikia hatua ya kutamani kuiona CCM ikipasuka vipande viwili angalau vijitokeze vyama viwili vyenye nguvu sawa. Baada ya kifo kilichogubikwa na utata, Mwalimu akatuacha Watanzania kama yatima na yasemekana (sina hakika) machozi yake kabla ya kukata roho yaliashiria vitu viwili...masikitiko na huruma kwa kutuacha Watanzania mikononi mwa manyang'au yasiyo na huruma.

Nikipata muda nitarudi niendeleee na hii makala na namna inavyowahusu wanafiki waliokuja kujitokeza baadaye kama Mzee Mwanakijiji, Mwakyembe, Shivji na wengineo...
 
Mnapata shida sana..ugomvi uko kwenye kudai kama haki...na pe lendekezo langu lina simama. Badala ya kususa i gepigwa kuwa wabunge waamue....

Kutokuidai kama haki itamaanisha kuomba kama hisani na itamaanisha kukubali watakaloamua, na tukiwakubalia manake tubong'oe mbele yao!!

Ushauri wa kupiga kura matokeo yanajulikana, walio wengi hawawezi kupinga watakalo wakubwa wao hata kama hawalipendi jambo lenyewe.

Baada ya matokeo ya kura itabidi kukubaliana nao, na tukiwakubalia inabidi tubong'oe mbele yao!!!

Je kiongozi uko tayari kubong'oa mbele yao???
 
Nadhani watu mnapata shida; kwa sababu labda kusoma ni kugumu au kuelewa ni kugumu. Hakuna ubaya wowote wa TV kuoneshwa "live". Sijawahi kusema "ni vibaya kuonesha TV" au ni "haipaswi watu kuona kinachoendelea Bungeni". Sababu iliyotolewa wakati ule ilikuwa ni sababu ya kipuuzi kutaka kuzuia kurusha TV "live", sababu iliyotolewa sasa hivi siyo ya wakati ule - sidhani kama watu wanaona tofauti. Lakini zaidi labda inabidi niendeleee kuwaelimisha wengine. Wanaodai hadi kususa waonekane kwenye TV wanazungumzia suala la haki yao kuonwa au kurusha matangazo live. Hii haki haipo.

Nadhani ipo haja ya kuchukua hatua ya lazima ya kuufunga huu mjadala tena.
Mzee umeshabong'oa tulia waliosimama nyuma yako wafanye yao.
 
Kijana hacha kujitoa ufahamu, wakati unajipinda kuandika hii nakala ndefu na vibwagizo vya kejeri hakufahamu kuwa unachodai si haki? Huu unafiki mpaka lini jamani yaani kijana mdogo kamawewe unajitoa ufahamu kwa ajiri ya tumbo lako..
Asante mkuu, hata mwanakijiji apindishe maneno haibadilishi ukweli kuwa sasa hivi amekuwa kinyonga. Heshima aliyokuwa nayo imepotezwa na unafiki.
 
Mnapata shida sana..ugomvi uko kwenye kudai kama haki...na pe lendekezo langu lina simama. Badala ya kususa i gepigwa kuwa wabunge waamue. Lakini huwezi kudai kuwa ni haki. Na inawezekana kweli wanataka kutuloga! ..suala ni suala la haki...Ni vizuri. Kuona mijadala lakini huwezi kudai kuona kama suala la haki. Mnaofikiri nimejigeuka ni kwa sababu hamnisomi. Sijasema mahali popote sasa hivi kuwa si nambo jema au haifai bunge kuoneshwa "live" napo wengine kutokana na kufikiri nimesema nini wanashindwa kuelewa nilichosema.
Loh!!!! Mzee Mwanakijiji leo unataka kura ipigwe bungeni kuamua hili jambo???

Ni wewe kweli ama kunamtu amehack account yako ya JF??


Ni wewe unakuwa na mawazo ya hivi kweli???


mimi bado siamini kama ni wewe
 
Duuhh!! Hii ni hatari kwa mtu mzima aisee!!

Kuna siku nilimpa makavu humu akaja na mitusi kibao (muone sura kama andazi lililoungua)..nadhani wengi mnakumbuka maana mlicheka sana humu na kutubeza tulioiona kweli!!! Humu kuna watu huwa hatukurupuki kuandika na ndio maana comments zetu ni chache ila zenye uhakika!!

Leo MM tukana tena kama unaweza....
Alitukana kabisaaaa???? Hiyo ilinipita aiseeee......
 
Mwanakijiji huwaga ananchekesha sana akikosa hoja.

anaishiaga tu kusema "hamuelewi ninachosema", etc - as if anatoka sayari ya Mars!

na ass-kissers wake akina Waberoya, etc just dance to the tune they can't even comprehend!!
 
Nadhani watu mnapata shida; kwa sababu labda kusoma ni kugumu au kuelewa ni kugumu. Hakuna ubaya wowote wa TV kuoneshwa "live". Sijawahi kusema "ni vibaya kuonesha TV" au ni "haipaswi watu kuona kinachoendelea Bungeni". Sababu iliyotolewa wakati ule ilikuwa ni sababu ya kipuuzi kutaka kuzuia kurusha TV "live", sababu iliyotolewa sasa hivi siyo ya wakati ule - sidhani kama watu wanaona tofauti. Lakini zaidi labda inabidi niendeleee kuwaelimisha wengine. Wanaodai hadi kususa waonekane kwenye TV wanazungumzia suala la haki yao kuonwa au kurusha matangazo live. Hii haki haipo.

Nadhani ipo haja ya kuchukua hatua ya lazima ya kuufunga huu mjadala tena.
Niliwaambia watu, subirini aje mtaona atakavyocheza na maneno, naamini wamekubali. No sir, mjadala haufungiki, tutaendelea kuupdate ili waliochelewa kukujua wakujue uzuri.
 
Mwanakijiji wakati huo alisema haya nanukuu:

Mtanisamehe - huu ni miongoni mwa maamuzi ya kipumbavu. Mtu mwenye akili akikushauri jambo la kijing akijua wewe nawe una akili halafu ukakubali atakudharau -alisema Baba wa Taifa. Wametuambia jambo la kijinga swali ni je tunajitambua na sisi tuna akili?

Leo anasema Wasidai kuonekana Laivu kwa kuwa siyo haki yao!.
Sasa anataka wakubaliane blindly huko si ndo kukubali ujinga?
 
Back
Top Bottom