Naona MM ameomalia "haki ya kuona bunge live". hatari moja ya msimamo wako ni kuonekana unatafuta "refuge" kwenye "semantics", unacheza na maneno, wakati zamani ulikuwa unaangalia "spirit". kuna ripoti ya Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, TLS, inayopatikana hapa :
http://tls.or.tz/wp-content/uploads/2015/07/FOI-Research-Report_Final-Version1.pdf
"
Kwa hali halisi kama ambavyo itafafanuliwa kwa kina katika tafiti hii, haki ya kupata taarifa Tanzania imekuwa si rahisi kupatikana kutokana na vikwazo kadha wa kadha ikiwemo kutokuwepo kwa mazingira wezeshi ya mfumo wa kisheria na urasimu katika taratibu za kiutawala ambazo huwa kisiki katika kupata haki ya taarifa. Kwa nyongeza, historia ya haki ya taarifa Tanzania inaeleza kwamba haki ya kupata taarifa imekuwa ikitafsiriwa mara kwa mara kama uwepo wa vyombo vya habari bila kutilia mkazo mantiki ya taarifa zinazosambazwa kwa umma.
Haki ya kupata taarifa ni moja ya msingi muhimu sana katika maendeleo. Haki hii imetafsiriwa na kujumuishwa katika mikataba ya kimataifa ya (kisheria na isiyo ya kisheria) ambayo Tanzania imetia saini. Pia ni moja wapo ya haki za binadamu ambazo zinalindwa kupitia kanuni za kimataifa na sheria za desturi za kimataifa (Mendel, 2007, Uk.1). Haki hii ipo katika mikataba mbali mbali ya kimataifa na kikanda kama vile:
i. Azimio la Kimataifa la Haki za Binadamu1948, Ibara ya 19;
ii. Mkataba wa kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa8 (ICCPR) chini ya Ibara ya 19 (2);
iii. Mkataba wa Aarhus (Mkataba wa haki ya kupata taarifa, ushiriki wa umma katika
kufanya maamuzi na ufikiaji wa haki katika mambo ya mazingira), Tume ya Uchumi
ya Umoja wa Mataifa wa Uchumi kwa ajili ya Ulaya, 25 Juni 1998;
iv. Mkataba wa Kupambana na Rushwa, Mkutano Mkuu-Azimio Na. 58/4 la Oktoba
31, 2003;
v. Maoni Na. 34, Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa, Septemba 12,
2011 ambayo inatafsiri Ibara ya 19 ya Mkataba wa Kimataifa wa Kiraia na Kisiasa
(ICCPR) wa mwaka 1966 juu ya uhuru wa maoni na kujieleza;
vi. Mkataba wa Afrika wa Watu na Haki za Binadamu, 1981 Ibara ya 9;
vii. Azimio la Uhuru wa Kujieleza Afrika, 2002, inayothibitisha Haki ya taarifa Afrika;
viii. Azimio la Afrika juu ya Demokrasia, Chaguzi na Utawala Bora, Januari 30, 2007;
ix. Azimio la Afrika juu ya Maadili na Kanuni za Utumishi wa Umma na Utawala, 2011
Ibara ya 6.
3.0.2 Mifumo ya Kisheria za Kitaifa
3.0.2.1 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Ibara ya 18 (kama ilivyorekebishwa mwaka 2005) inatoa haki ya kutafuta, kupokea na kusambaza habari bila kufungwa/kuzuiliwa na mipaka ya kitaifa (Katiba ya JMT, 1977).
Katiba inakataza kuingiliwa kwa mawasiliano binafsi na wakati huo huo ina vifungu vyenye kutoa haki ya kupewa taarifa kwa wakati wote katika matukio mbalimbali ya nchi na duniani kwa ujumla ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na jamii. (HakiElimu et al, 2005).
Ibara ya 189 inaeleza kuwa, kila mtu:
(a) Ana uhuru wa kutoa maoni na kueleza mawazo yake;
(b) Ana haki ya kutafuta, kupokea na kusambaza taarifa bila kujali mipaka ya kitaifa;
(c) Ana uhuru wa kuwasiliana na kupata ulinzi bila ya kuingiliwa mawasiliano yake;
na
(d) Ana haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu ya
maisha na shughuli za watu na pia masuala muhimu kwa jamii.
Hata hivyo, Katiba ya sasa haikutaja kwa vipengele kwamba haki na uhuru huo unaweza kutekelezwa kupitia vyombo vya habari kama ilivyoelezwa wazi katika ibara ya 18 (1)10 iliyopo katika toleo la awali. Kuondolewa huku katika katiba ya sasa imepelekea wadau wa vyombo vya habari kusema kuwa hakuna uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania (MCT, 2008).
Pamoja na hayo, ibara ya 30 (2) ya Katiba imeweka mipaka ya haki ya mtu mmoja kupata taarifa endapo inahatarisha haki za watu wengine au maslahi ya umma. Pia, katiba haitoi utaratibu wa kuhakikisha kwamba umma kwa ujumla na hasa watu walio katika mazingira ya vijijini na wasiojiweza kijamii na kiuchumi kuweza kupata taarifa muhimu, pia haitoi agizo la uwazi wa taarifa na adhabu dhidi ya mamlaka ambazo zitaficha taarifa au kukataa kutoa habari kwa umma".
Tuache kumung'unya maneno: watawala hawapendi mambo yao yajadiliwe waziwazi, hasa unapokuwa na vijana machachari ambao wanao uwezo wa kuyaweka wazi, na pia unao watu ambao wapo tayari kuwapa "data" hizo nyeti. inaaminika kwamba matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2015, ambayo yametoa ushindi mnono kwa wapinzani kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na huko nyuma, yamechangiwa na mambo kama haya ya kuonesha bunge live. lakini kwa data tu za utumbuaji majipu, inaonesha kweli hali ni mbaya sana. kwa hiyo serikali inataka kudhibiti "uozo" usianikwe mno, ili kupisha jitihada za Rais Magufuli kurudisha imani ya watu kwa serikali yao. Lakini mimi sidhani kama Serikali ina sababu ya kuogopa "kuvuliwa nguo". kama JK hakuogopa hayo yote, na hali ilikuwa namna ile, kwa nini Magufuli ahofie "uwazi", wakati anachapa kazi vizuri tu?